< Mwanzo 48 >

1 Ikawa baada ya mambo haya, mmojawapo akamwambia Yusufu, “Tazama, baba yako ni mgonjwa.” Hivyo akaondoka pamoja na wanawe wawili, Manase na Efrahimu.
And it came to pass after these things, that one said to Joseph, Lo! thy father, is sick. So he took his two sons with him, Manasseh and Ephraim.
2 Yakobo alipoambiwa, “Tazama, mwanao Yusufu amekuja kukuona,” Israeli akakusanya nguvu na kukaa juu ya kitanda.
And one told Jacob, and said—Lo! thy son Joseph, coming in unto thee. So Israel strengthened himself, and sat up on the couch.
3 Yakobo akamwambia Yusufu, Mungu Mwenyezi alinitokea huko Luzu katika nchi ya Kanaani. Akanibariki na
Then said Jacob unto Joseph, GOD Almighty, appeared unto me in Luz in the land of Canaan, —and blessed me;
4 kuniambia, 'Tazama, nitakupa uzao mwingi, na kukuzidisha. Nitakufanya kuwa kusanyiko la mataifa. Nitakupa nchi hii wewe na uzao wako kuwa milki ya milele.'
and said unto me—Behold me! about to make thee fruitful, so will I multiply thee, and give thee to become a multitude of peoples, —so will I give this land to thy seed after thee, as an age-abiding possession.
5 Na sasa wanao wawili, waliozaliwa kwako katika nchi ya Misri kabla sijaja Misri, ni wangu. Efrahimu na Manase watakuwa wangu, kama walivyo Rubeni na Simioni.
Now, therefore thy two sons who were born to thee in the land of Egypt, before I came in unto thee in Egypt, are mine! Ephraim and Manasseh, like Reuben and Simeon, shall be mine!
6 Watoto utakaowapata baada ya hapo ni wako; watahesabiwa katika majina ya ndugu zao katika urithi wao.
But thine offspring which thou hast begotten after them, thine own shall they be, —after the name of their brethren, shall they be called in their inheritance.
7 Lakini kwangu mimi, nilipokuja kutoka Padani, kwa uzuni yangu Raheli alikufa njiani katika nchi ya Kanaani, wakati kungalipo kitambo kwenda Efrathi. Nilimzika pale katika njia iendayo Efrathi” (ndio, Bethlehemu).
But, as for me, when I came in from Padan, Rachel died by me, in the land of Canaan, in the way, while yet there was a stretch of country to come into Ephrath, —so I buried her there in the way to Ephrath, the same, is Bethlehem.
8 Israeli alipowaona wana wa Yusufu, akasema, “Ni nani hawa?”
Then Israel saw Joseph’s sons, —and said—Who are these?
9 Yusufu akamwambia baba yake, “Hawa ni wanangu, Mungu alionipa hapa:” Israeli akasema, “Walete kwangu, kwamba niwabariki.”
And Joseph said unto his father, My sons, they are, whom God hath given me, in this place. And he said—Bring them, I pray thee, unto me, that I may bless them.
10 Basi macho ya Israeli yalikuwa yanashindwa kwa ajili ya umri wake, hivyo hakuweza kuona. Hivyo Yusufu akawasogeza karibu yake, na akawabusu na kuwakumbatia.
Now, the eyes of Israel, had become dim from old age, —he could not see, —so he drew them near unto him, and kissed them, and embraced them.
11 Israeli akamwambia Yusufu, “Sikutazamia kuuona uso wako tena, Lakini Mungu ameniruhusu kuwaona hata wanao.”
And Israel said unto Joseph, To see thine own face, had I not thought, —and lo! God hath caused me to see even thy seed!
12 Yusufu akawaondoa kati ya magoti ya Israeli, na kisha akainama na uso wake juu ya nchi.
And Joseph brought them out from beside his knees, and bowed himself down with his face towards the earth.
13 Yusufu akawachukua wote wawili, Efrahimu katika mkono wake wa kulia kuelekea mkono wa kushoto wa Israeli, na Manase katika mkono wake wa kulia kuelekea mkono wa kulia wa Israeli, na akawasogeza kwake.
And Joseph took them both, —Ephraim in his right hand on Israel’s left hand, and Manasseh in his left hand, on Israel’s right hand, and drew them near unto him.
14 Israeli akainua mkono wake wa kulia na kuuweka juu ya kichwa cha Efrahimu, aliyekuwa mdogo, na mkono wake wa kushoto juu ya kichwa cha Manase. Akaipishanisha mikono yake, kwani Manase ndiye alikuwa mzaliwa wa kwanza.
Then Israel put forth his right hand and laid it upon the head of Ephraim, though, he, was the younger, and his left hand upon the head of Manasseh, —crossing his hands, although, Manasseh, was the first-born.
15 Israeli akambariki Yusufu, akisema, Mungu ambaye mbele zake baba zangu Ibrahimu na Isaka walitembea, Mungu aliyenilinda hata leo,
Thus blessed he Joseph, and said, —God himself—before whom walked my fathers. Abraham and Isaac, God himself—who hath been my shepherd, since I came into being until this day; —
16 malaika walionilinda na madhara yote, awabariki vijana hawa. Jina langu na litajwe kwao, na majina ya baba zangu Ibrahimu na Isaka. Na wawe makutano ya watu juu ya nchi.”
The Messenger—who hath been my redeemer from all evil—bless the lads! And may there be called upon them, my name, and the name of my fathers. Abraham and Isaac; And may they swarm into a multitude, in the midst of the earth!
17 Yusufu alipoona baba yake ameweka mkono wake wa kulia juu ya kichwa cha Efrahimu, haikumpendeza. Akauchukuwa mkono wa baba yake auweke katika kichwa cha Manase.
And Joseph saw that his father had laid his right hand on the head of Ephraim and it was displeasing in his eyes, —so he took hold of his father’s hand to remove it from off the head of Ephraim, on to the head of Manasseh.
18 Yusufu akamwambia baba yake, “Sivyo babangu; kwani huyu ndiye mzaliwa wa kwanza. Uweke mkono wako juu ya kichwa chake.”
And Joseph said unto his father—Not so, my father! for, this, is the firstborn, lay thy right hand upon his head.
19 Baba yake akakataa na kusema, “Ninafahamu, mwanangu, nafahamu. Yeye naye atakuwa watu, naye pia atakuwa mkuu. Lakini mdogo wake atakuwa mkuu kuliko yeye, na uzao wake utakuwa wingi wa mataifa.”
And his father refused, and said—I know—my son, I know! He also, shall become a people, and he also, shall become great, —but nevertheless, his younger brother, shall become greater than he, and his seed, shall become a filling up of the nations.
20 Israeli akawabariki siku hiyo kwa maneno haya, “Watu wa Israeli watatamka baraka kwa majina yenu wakisema, Mungu na akufanye kama Efrahimu na kama Manase'. “Kwa njia hii, Israeli akamweka Efrahimu mbele ya Manase.
And he blessed them on that day, saying—In thee, let Israel bless himself saying, God set thee as Ephraim, and as Manasseh! So he set Ephraim before Manasseh.
21 Israeli akamwambia Yusufu, “Tazama, ninakaribia kufa, lakini Mungu atakuwa nanyi, na atawarudisha katika nchi ya baba zenu.
And Israel said unto Joseph: Lo! I, am about to die, —but it shall come to pass that, God will be with you, and will take you back into the land of your fathers.
22 Kwako wewe, kwa kuwa uko juu ya ndugu zako, ninakupa mtelemko wa mlima niliouchukuwa kutoka kwa Waamori kwa upanga wangu na upinde wangu.”
But, I, have given to thee one mountain-track above thy brethren, —which I took out of the hand of the Amorite, with my sword and with my bow.

< Mwanzo 48 >