< Mwanzo 48 >
1 Ikawa baada ya mambo haya, mmojawapo akamwambia Yusufu, “Tazama, baba yako ni mgonjwa.” Hivyo akaondoka pamoja na wanawe wawili, Manase na Efrahimu.
Poslije nekog vremena jave Josipu: “Eno ti je otac obolio.” Nato on uzme sa sobom svoja dva sina, Manašea i Efrajima.
2 Yakobo alipoambiwa, “Tazama, mwanao Yusufu amekuja kukuona,” Israeli akakusanya nguvu na kukaa juu ya kitanda.
Kad Jakovu rekoše: “Evo ti je došao sin Josip”, Izrael skupi svoje snage i sjede na postelju.
3 Yakobo akamwambia Yusufu, Mungu Mwenyezi alinitokea huko Luzu katika nchi ya Kanaani. Akanibariki na
Reče Jakov Josipu: “Bog Svemožni, El Šadaj, objavi mi se u Luzu, u zemlji kanaanskoj; blagoslov mi dade,
4 kuniambia, 'Tazama, nitakupa uzao mwingi, na kukuzidisha. Nitakufanya kuwa kusanyiko la mataifa. Nitakupa nchi hii wewe na uzao wako kuwa milki ya milele.'
a potom mi reče: 'Učinit ću te rodnim i mnogobrojnim, učinit ću da postaneš skup naroda, a tvome potomstvu poslije tebe dat ću ovu zemlju u posjed zauvijek.'
5 Na sasa wanao wawili, waliozaliwa kwako katika nchi ya Misri kabla sijaja Misri, ni wangu. Efrahimu na Manase watakuwa wangu, kama walivyo Rubeni na Simioni.
Sad, oba tvoja sina što su ti se rodila u zemlji egipatskoj, prije nego sam ja stigao k tebi u Egipat, neka budu moji - Efrajim i Manaše neka budu moji kao i Ruben i Šimun!
6 Watoto utakaowapata baada ya hapo ni wako; watahesabiwa katika majina ya ndugu zao katika urithi wao.
A djeca što su ti se rodila poslije njih neka ostanu tvoja; a u svom nasljedstvu neka se zovu po imenu svoje braće.
7 Lakini kwangu mimi, nilipokuja kutoka Padani, kwa uzuni yangu Raheli alikufa njiani katika nchi ya Kanaani, wakati kungalipo kitambo kwenda Efrathi. Nilimzika pale katika njia iendayo Efrathi” (ndio, Bethlehemu).
Kad sam se, naime, vraćao iz Padana, na moju žalost, tvoja majka Rahela umrije na putovanju u kanaansku zemlju, tek u maloj udaljenosti od Efrate. Sahranio sam je ondje uz put u Efratu, sadašnji Betlehem.”
8 Israeli alipowaona wana wa Yusufu, akasema, “Ni nani hawa?”
Opazivši Izrael Josipove sinove, zapita: “Tko su ovi?”
9 Yusufu akamwambia baba yake, “Hawa ni wanangu, Mungu alionipa hapa:” Israeli akasema, “Walete kwangu, kwamba niwabariki.”
Josip odgovori svome ocu: “Sinovi su to moji koje mi je Bog dao ovdje.” “Dovedi mi ih da ih blagoslovim”, reče.
10 Basi macho ya Israeli yalikuwa yanashindwa kwa ajili ya umri wake, hivyo hakuweza kuona. Hivyo Yusufu akawasogeza karibu yake, na akawabusu na kuwakumbatia.
Izraelu oči oslabile od starosti, nije vidio. Zato mu privede sinove, a on ih poljubi i zagrli.
11 Israeli akamwambia Yusufu, “Sikutazamia kuuona uso wako tena, Lakini Mungu ameniruhusu kuwaona hata wanao.”
Potom Izrael reče Josipu: “Nisam očekivao da ću još ikada vidjeti tvoje lice; kad, evo, Bog mi dade da vidim i tvoje potomke.”
12 Yusufu akawaondoa kati ya magoti ya Israeli, na kisha akainama na uso wake juu ya nchi.
Josip ih tada skine s njegovih koljena i duboko se, sve do zemlje, nakloni.
13 Yusufu akawachukua wote wawili, Efrahimu katika mkono wake wa kulia kuelekea mkono wa kushoto wa Israeli, na Manase katika mkono wake wa kulia kuelekea mkono wa kulia wa Israeli, na akawasogeza kwake.
Nato ih uze Josip obojicu - Efrajima svojom desnicom, Izraelu nalijevo, a Manašea svojom ljevicom, Izraelu nadesno - te ih k njemu primače.
14 Israeli akainua mkono wake wa kulia na kuuweka juu ya kichwa cha Efrahimu, aliyekuwa mdogo, na mkono wake wa kushoto juu ya kichwa cha Manase. Akaipishanisha mikono yake, kwani Manase ndiye alikuwa mzaliwa wa kwanza.
Ali Izrael ispruži svoju desnicu i stavi je na Efrajimovu glavu, premda je bio mlađi, a svoju ljevicu na glavu Manašeovu - tako je držao ruke unakrst - iako je Manaše bio prvorođenac.
15 Israeli akambariki Yusufu, akisema, Mungu ambaye mbele zake baba zangu Ibrahimu na Isaka walitembea, Mungu aliyenilinda hata leo,
Tako je davao svoj blagoslov Josipu govoreći: “Bog, čijim su putovima hodili oci moji Abraham i Izak, Bog, koji mi je pastir bio otkako postah pa do danas,
16 malaika walionilinda na madhara yote, awabariki vijana hawa. Jina langu na litajwe kwao, na majina ya baba zangu Ibrahimu na Isaka. Na wawe makutano ya watu juu ya nchi.”
anđeo koji me od svakog zla izbavljao - djecu ovu neka blagoslovi! Neka se ime moje i mojih pređa Abrahama i Izaka po njima spominje! U mnoštva se mnogobrojna po zemlji razmnožili!”
17 Yusufu alipoona baba yake ameweka mkono wake wa kulia juu ya kichwa cha Efrahimu, haikumpendeza. Akauchukuwa mkono wa baba yake auweke katika kichwa cha Manase.
Kad je Josip vidio da je njegov otac položio desnicu na Efrajimovu glavu, njegovim se očima to učini krivo; zato posegne za rukom svoga oca da je pomakne s Efrajimove glave na glavu Manašeovu.
18 Yusufu akamwambia baba yake, “Sivyo babangu; kwani huyu ndiye mzaliwa wa kwanza. Uweke mkono wako juu ya kichwa chake.”
“Ne tako, oče moj,” reče Josip svome ocu, “jer ovo je prvorođenac; zato stavi desnicu na njegovu glavu!”
19 Baba yake akakataa na kusema, “Ninafahamu, mwanangu, nafahamu. Yeye naye atakuwa watu, naye pia atakuwa mkuu. Lakini mdogo wake atakuwa mkuu kuliko yeye, na uzao wake utakuwa wingi wa mataifa.”
Ali njegov otac to odbije rekavši: “Znam ja, sine moj, znam; i od njega će postati narod i bit će velik. Ali njegov mlađi brat bit će veći od njega, a njegovo će potomstvo biti mnoštvo.”
20 Israeli akawabariki siku hiyo kwa maneno haya, “Watu wa Israeli watatamka baraka kwa majina yenu wakisema, Mungu na akufanye kama Efrahimu na kama Manase'. “Kwa njia hii, Israeli akamweka Efrahimu mbele ya Manase.
Onoga ih, dakle, dana blagoslovi rekavši: “Vama nek' se Izrael blagoslivlja govoreći: Kao što je Efrajimu i Manašeu, nek' i tebi Bog učini!” Tako stavi Efrajima pred Manašea.
21 Israeli akamwambia Yusufu, “Tazama, ninakaribia kufa, lakini Mungu atakuwa nanyi, na atawarudisha katika nchi ya baba zenu.
Poslije Izrael reče Josipu: “Ja ću, evo, naskoro umrijeti; no Bog će biti s vama i opet vas dovesti u zemlju vaših otaca.
22 Kwako wewe, kwa kuwa uko juu ya ndugu zako, ninakupa mtelemko wa mlima niliouchukuwa kutoka kwa Waamori kwa upanga wangu na upinde wangu.”
A tebi ostavljam Šekem, nešto više nego tvojoj braći, što sam ga svojim mačem i lukom osvojio od Amorejaca.”