< Mwanzo 47 >

1 Kisha Yusufu akaingia kwa Farao na kumwambia, “Baba yangu na ndugu zangu, kondoo wao, mbuzi wao, na yote waliyonayo, wamefika kutoka katika nchi ya Kanaani. Tazama, wapo katika nchi ya Gosheni.”
Joseph entra et fit un rapport à Pharaon, en disant: « Mon père et mes frères, avec leurs brebis, leurs bœufs et tout ce qui leur appartient, sont sortis du pays de Canaan; et voici, ils sont dans le pays de Gosen. »
2 Akawachukua watano katika ndugu zake na kuwatambulisha kwa Farao.
Il prit cinq hommes parmi ses frères, et les présenta à Pharaon.
3 Farao akawambia ndugu zake, “Kazi yenu ni nini?” Wakamwambia Farao, “Watumishi wako ni wafugaji, kama mababu zetu.”
Pharaon dit à ses frères: « Quelle est votre profession? » Ils dirent à Pharaon: « Tes serviteurs sont des bergers, nous et nos pères. »
4 Kisha wakamwambia Farao, “Tumekuja kukaa kwa muda katika nchi. Hakuna malisho kwa ajili ya makundi ya watumishi wako, kwa maana njaa ni kali sana katika nchi ya Kanaani. Hivyo, tafadhari waache watumishi wako wakae katika nchi ya Gosheni.”
Ils dirent aussi à Pharaon: « Nous sommes venus vivre comme des étrangers dans le pays, car il n'y a pas de pâturage pour les troupeaux de tes serviteurs. Car la famine sévit dans le pays de Canaan. Laisse donc tes serviteurs habiter dans le pays de Gosen. »
5 Kisha Farao akamwambia Yusufu, kusema, “Baba yako na ndugu zako wamekuja kwako.
Pharaon parla à Joseph, et dit: Ton père et tes frères sont venus vers toi.
6 Nchi ya Misri iko mbele yako. Mkalishe baba yako na ndugu zako katika eneo zuri, nchi ya Gosheni. Ikiwa unafahamu watu wenye uwezo miongoni mwao, uwaweke kuwatunza wanyama wangu.”
Le pays d'Égypte est devant toi. Fais habiter ton père et tes frères dans le meilleur du pays. Qu'ils habitent dans le pays de Gosen. Si tu connais parmi eux des hommes capables, confie-leur la garde de mon bétail. »
7 Kisha Yusufu akamwingiza Yakobo baba yake na kumweka mbele ya Farao. Yakobo akambariki Farao.
Joseph fit venir Jacob, son père, et le plaça devant Pharaon; et Jacob bénit Pharaon.
8 Farao akamwambia Yakobo, “Umeishi kwa muda gani?”
Pharaon dit à Jacob: « Quel âge as-tu? »
9 Yakobo akamwambia Farao, “Miaka ya safari zangu ni mia moja na thelathini. Miaka ya maisha yangu imekuwa mifupi na ya maumivu. Siyo kama miaka ya baba zangu.”
Jacob dit à Pharaon: « Les années de mon pèlerinage sont de cent trente ans. Les jours des années de ma vie ont été peu nombreux et mauvais. Ils n'ont pas atteint les jours des années de la vie de mes pères, aux jours de leur pèlerinage. »
10 Kisha Yakobo akambariki Farao na kuondoka mbele zake.
Jacob bénit Pharaon, et sortit de la présence de Pharaon.
11 Kisha Yusufu akamweka baba yake na ndugu zake. Akawapa eneo katika nchi ya Misri, sehemu nzuri sana ya nchi, katika eneo la Ramesesi, kama Farao alivyokuwa ameagiza.
Joseph plaça son père et ses frères, et leur donna une possession au pays d'Égypte, dans le meilleur du pays, au pays de Ramsès, comme Pharaon l'avait ordonné.
12 Yusufu akamhudumia baba yake kwa chakula, ndugu zake, na nyumba yote ya baba yake, kulingana na hesabu ya wahitaji wao.
Joseph fournit du pain à son père, à ses frères et à toute la famille de son père, selon la taille de leurs familles.
13 Basi hakukuwa na chakula katika nchi yote; kwani njaa ilikuwa kali sana. Nchi ya Misri na nchi ya Kanaani ikaharibika kwa sababu ya njaa.
Il n'y avait pas de pain dans tout le pays, car la famine était très forte, de sorte que le pays d'Égypte et le pays de Canaan s'éteignirent à cause de la famine.
14 Yusufu akakusanya pesa yote iliyokuwa katika nchi ya Misri na nchi ya Kanaani, kwa kuwauzia wakaaji wake chakula. Kisha Yusufu akaleta ile pesa katika kasri la Farao.
Joseph rassembla tout l'argent qui se trouvait dans le pays d'Égypte et dans le pays de Canaan, pour le blé qu'on achetait, et il apporta l'argent dans la maison de Pharaon.
15 Pesa yote ya nchi za Misri na Kanaani ilipokwisha, Wamisri wote wakaja kwa Yusufu wakisema, “Tupe chakula! Kwa nini tufe mbele zako kwa maana pesa yetu imekwisha?”
Lorsque tout l'argent fut dépensé dans le pays d'Égypte et dans le pays de Canaan, tous les Égyptiens vinrent trouver Joseph et dirent: « Donne-nous du pain, car pourquoi mourrions-nous en ta présence? Car notre argent manque. »
16 Yusufu akasema, “Ikiwa pesa yenu imekwisha, leteni wanyama wenu nami nitawapa chakula badala ya wanyama wenu.”
Joseph dit: « Donne-moi ton bétail, et je te donnerai de la nourriture pour ton bétail, si ton argent a disparu. »
17 Hivyo wakaleta wanyama wao kwa Yusufu. Yusufu akawapa chakula kwa kubadilishana na farasi, kondoo, mbuzi na kwa punda. Akawalisha kwa mkate kwa kubadilisha na wanyama wao mwaka ule.
Ils amenèrent leur bétail à Joseph, qui leur donna du pain en échange des chevaux, des troupeaux, des bœufs et des ânes, et il les nourrit de pain en échange de tout leur bétail pour cette année-là.
18 Mwaka ule ulipokwisha, wakaja kwake mwaka uliofuata na kumwambia, “Hatutaficha kwa bwana wangu kwamba pesa yetu yote imekwisha, na wanyama ni wa bwana wangu. Hakuna kilichobaki mbele za bwana wangu, isipokuwa miili yetu na nchi yetu.
Lorsque cette année fut terminée, ils vinrent le trouver la deuxième année et lui dirent: « Nous ne cacherons pas à mon seigneur que tout notre argent est dépensé, et que les troupeaux de bétail appartiennent à mon seigneur. Il ne reste plus aux yeux de mon seigneur que nos corps et nos terres.
19 Kwa nini tufe mbele za macho yake, sisi na nchi yetu? Utununue sisi na nchi yetu badala ya chakula, na sisi na nchi yetu tutakuwa watumishi wa Farao. Tupe mbegu ili kwamba tuishi na tusife, na kwamba nchi isiwe tupu bila watu.
Pourquoi mourrions-nous sous tes yeux, nous et nos terres? Achète-nous du pain, nous et nos terres, et nous serons, nous et nos terres, les serviteurs de Pharaon. Donne-nous de la semence, afin que nous vivions et ne mourions pas, et que le pays ne soit pas dévasté. »
20 Hivyo Yusufu akamnunulia Farao nchi yote ya Misri. Kwani kila Mmisri akauza shamba lake, kwa sababu njaa ilikuwa kali sana. Kwa njia hii, nchi ikawa mali ya Farao.
Joseph acheta tout le pays d'Égypte pour Pharaon, car chacun des Égyptiens vendit son champ, car la famine les frappait, et le pays devint la propriété de Pharaon.
21 Na watu, akawafanya kuwa watumwa kutoka mpaka mmoja wa Misri hata mkapa mwingine.
Quant au peuple, il le déplaça dans les villes, d'un bout à l'autre de la frontière de l'Égypte.
22 Ilikuwa ni nchi ya makuhani pekee ambayo Yusufu hakuinunua, kwa maana makuhani walikuwa wakipewa posho. Walikula katika sehemu aliyowapa Farao. Kwa hiyo hawakuuza nchi yao.
Mais il n'acheta pas les terres des prêtres, car les prêtres avaient une part de Pharaon et mangeaient la part que Pharaon leur donnait. C'est pourquoi ils n'ont pas vendu leurs terres.
23 Kisha Yusufu akawambia watu, “Tazama, nimewanunua ninyi na nchi yenu leo kwa ajili ya Farao. Basi mbegu hii hapa kwa ajili yenu, nanyi mtapanda katika nchi.
Joseph dit alors au peuple: « Voici que je vous ai achetés aujourd'hui, vous et vos terres, pour Pharaon. Voici de la semence pour vous, et vous ensemencerez la terre.
24 Wakati wa mavuno, mtampa Farao sehemu ya tano, na sehemu nne zitakuwa zenu, kwa mbegu za shamba na kwa chakula cha nyumba zenu na watoto wenu.”
Aux récoltes, vous donnerez un cinquième à Pharaon, et quatre parts vous appartiendront, pour la semence des champs, pour votre nourriture, pour celle de vos familles et pour celle de vos petits enfants. »
25 Wakasema, “Umeokoa maisha yetu. Na tupate kibali machoni pako. Tutakuwa watumishi wa Farao.”
Ils dirent: « Tu nous as sauvé la vie! Que nous trouvions grâce aux yeux de mon seigneur, et nous serons les serviteurs de Pharaon. »
26 Hivyo Yusufu akaifanya kuwa sheria inayofanya kazi hata leo katika nchi ya Misri, kwamba moja ya tano ni ya Farao. Eneo la makuhani peke yake ndo halikufanywa kuwa la Farao.
Joseph fit une loi sur le pays d'Égypte, jusqu'à ce jour, pour que Pharaon ait le cinquième. Seule la terre des prêtres ne devint pas la propriété de Pharaon.
27 Hivyo Israeli akaishi katika nchi ya Misri, katika eneo la Gosheni. Watu wake wakapata umiliki pale. Walikuwa wenye kuzaa na kuongezeka sana.
Israël habita au pays d'Égypte, dans le pays de Gosen; ils y acquirent des biens, furent féconds et multiplièrent beaucoup.
28 Yakobo akaishi katika nchi ya Misri miaka kumi na saba, kwa hiyo miaka ya maisha ya Yakobo ilikuwa miaka mia moja arobaini na saba.
Jacob vécut dix-sept ans au pays d'Égypte. Les jours de Jacob, les années de sa vie, furent donc de cent quarante-sept ans.
29 Wakati wa kufa kwake Yakobo ulipokaribia, alimwita Yusufu mwanaye na kumwambia, “Ikiwa nimepata kibali mbele zako, weka mkono wako chini ya paja langu, na unitendee kwa uaminifu na kweli. Tafadhari usinizike Misri.
Le temps où Israël devait mourir approchait. Il appela son fils Joseph et lui dit: « Si j'ai trouvé grâce à tes yeux, mets ta main sous ma cuisse et traite-moi avec bonté et sincérité. Ne m'enterre pas en Égypte,
30 Nitakapolala na baba zangu, utanitoa Misri na kunizika katika eneo la kuzikia la baba zangu.” Yusufu akasema, “Nitafanya kama ulivyosema.”
mais quand je dormirai avec mes pères, tu me transporteras hors d'Égypte et tu m'enterreras dans leur sépulture. » Joseph a dit: « Je ferai ce que vous avez dit. »
31 Israeli akasema, “Niapie,” na Yusufu akamwapia. Kisha Israeli akainama chini mbele ya kitanda chake.
Israël dit: « Jure-le-moi », et il le lui jura. Puis Israël se prosterna sur la tête du lit.

< Mwanzo 47 >