< Mwanzo 47 >

1 Kisha Yusufu akaingia kwa Farao na kumwambia, “Baba yangu na ndugu zangu, kondoo wao, mbuzi wao, na yote waliyonayo, wamefika kutoka katika nchi ya Kanaani. Tazama, wapo katika nchi ya Gosheni.”
And he went Joseph and he told to Pharaoh and he said father my and brothers my and flock[s] their and herd[s] their and all that [belongs] to them they have come from [the] land of Canaan and there they [are] in [the] land of Goshen.
2 Akawachukua watano katika ndugu zake na kuwatambulisha kwa Farao.
And from [the] end of brothers his he took five men and he presented them before Pharaoh.
3 Farao akawambia ndugu zake, “Kazi yenu ni nini?” Wakamwambia Farao, “Watumishi wako ni wafugaji, kama mababu zetu.”
And he said Pharaoh to brothers his what? [are] work your and they said to Pharaoh [are] herder[s] of sheep servants your both we as well as fathers our.
4 Kisha wakamwambia Farao, “Tumekuja kukaa kwa muda katika nchi. Hakuna malisho kwa ajili ya makundi ya watumishi wako, kwa maana njaa ni kali sana katika nchi ya Kanaani. Hivyo, tafadhari waache watumishi wako wakae katika nchi ya Gosheni.”
And they said to Pharaoh to sojourn in the land we have come for there not [is] pasture for the sheep which [belongs] to servants your for [was] heavy the famine in [the] land of Canaan and therefore let them dwell please servants your in [the] land of Goshen.
5 Kisha Farao akamwambia Yusufu, kusema, “Baba yako na ndugu zako wamekuja kwako.
And he said Pharaoh to Joseph saying father your and brothers your they have come to you.
6 Nchi ya Misri iko mbele yako. Mkalishe baba yako na ndugu zako katika eneo zuri, nchi ya Gosheni. Ikiwa unafahamu watu wenye uwezo miongoni mwao, uwaweke kuwatunza wanyama wangu.”
[the] land of Egypt [is] before you it in [the] best of the land cause to dwell father your and brothers your let them dwell in [the] land of Goshen and if you know and there among them [are] men of ability and you will appoint them overseers of livestock over [that] which [belongs] to me.
7 Kisha Yusufu akamwingiza Yakobo baba yake na kumweka mbele ya Farao. Yakobo akambariki Farao.
And he brought Joseph Jacob father his and he made stand him before Pharaoh and he blessed Jacob Pharaoh.
8 Farao akamwambia Yakobo, “Umeishi kwa muda gani?”
And he said Pharaoh to Jacob how many? [are] [the] days of [the] years of life your.
9 Yakobo akamwambia Farao, “Miaka ya safari zangu ni mia moja na thelathini. Miaka ya maisha yangu imekuwa mifupi na ya maumivu. Siyo kama miaka ya baba zangu.”
And he said Jacob to Pharaoh [the] days of [the] years of sojournings my [are] thirty and one hundred year[s] few and displeasing they have been [the] days of [the] years of life my and not they have reached [the] days of [the] years of [the] lives of ancestors my in [the] days of sojournings their.
10 Kisha Yakobo akambariki Farao na kuondoka mbele zake.
And he blessed Jacob Pharaoh and he went out from to before Pharaoh.
11 Kisha Yusufu akamweka baba yake na ndugu zake. Akawapa eneo katika nchi ya Misri, sehemu nzuri sana ya nchi, katika eneo la Ramesesi, kama Farao alivyokuwa ameagiza.
And he caused to dwell Joseph father his and brothers his and he gave to them a possession in [the] land of Egypt in [the] best of the land in [the] land of Rameses just as he had commanded Pharaoh.
12 Yusufu akamhudumia baba yake kwa chakula, ndugu zake, na nyumba yote ya baba yake, kulingana na hesabu ya wahitaji wao.
And he provided for Joseph father his and brothers his and all [the] household of father his food to [the] mouth of the little one[s].
13 Basi hakukuwa na chakula katika nchi yote; kwani njaa ilikuwa kali sana. Nchi ya Misri na nchi ya Kanaani ikaharibika kwa sababu ya njaa.
And [was] food there not in all the land for [was] heavy the famine very and it languished [the] land of Egypt and [the] land of Canaan because of the famine.
14 Yusufu akakusanya pesa yote iliyokuwa katika nchi ya Misri na nchi ya Kanaani, kwa kuwauzia wakaaji wake chakula. Kisha Yusufu akaleta ile pesa katika kasri la Farao.
And he gathered up Joseph all the money which was found in [the] land of Egypt and in [the] land of Canaan for the grain which they [were] buying grain and he brought Joseph the money [the] house of towards Pharaoh.
15 Pesa yote ya nchi za Misri na Kanaani ilipokwisha, Wamisri wote wakaja kwa Yusufu wakisema, “Tupe chakula! Kwa nini tufe mbele zako kwa maana pesa yetu imekwisha?”
And it was finished the money from [the] land of Egypt and from [the] land of Canaan and they came all Egypt to Joseph saying give! to us food and why? will we die before you for it has come to an end money.
16 Yusufu akasema, “Ikiwa pesa yenu imekwisha, leteni wanyama wenu nami nitawapa chakula badala ya wanyama wenu.”
And he said Joseph give livestock your so let me give [it] to you for livestock your if it has come to an end money.
17 Hivyo wakaleta wanyama wao kwa Yusufu. Yusufu akawapa chakula kwa kubadilishana na farasi, kondoo, mbuzi na kwa punda. Akawalisha kwa mkate kwa kubadilisha na wanyama wao mwaka ule.
And they brought livestock their to Joseph and he gave to them Joseph food for the horses and for [the] livestock of the flock[s] and for [the] livestock of the herd[s] and for the donkeys and he refreshed them with food for all livestock their in the year that.
18 Mwaka ule ulipokwisha, wakaja kwake mwaka uliofuata na kumwambia, “Hatutaficha kwa bwana wangu kwamba pesa yetu yote imekwisha, na wanyama ni wa bwana wangu. Hakuna kilichobaki mbele za bwana wangu, isipokuwa miili yetu na nchi yetu.
And it was finished the year that and they came to him in the year second and they said to him not we will hide from lord my that except it has been finished the money and [the] livestock of the cattle [is] to lord my not it is left before lord my except body our and land our.
19 Kwa nini tufe mbele za macho yake, sisi na nchi yetu? Utununue sisi na nchi yetu badala ya chakula, na sisi na nchi yetu tutakuwa watumishi wa Farao. Tupe mbegu ili kwamba tuishi na tusife, na kwamba nchi isiwe tupu bila watu.
Why? will we die to eyes your both we as well as land our buy us and land our for food so we may be we and land our slaves of Pharaoh and give seed so we may live and not we will die and the land not it will be desolate.
20 Hivyo Yusufu akamnunulia Farao nchi yote ya Misri. Kwani kila Mmisri akauza shamba lake, kwa sababu njaa ilikuwa kali sana. Kwa njia hii, nchi ikawa mali ya Farao.
And he bought Joseph all [the] land of Egypt to Pharaoh for they sold Egypt everyone field his for it was severe on them the famine and it be[longed] the land to Pharaoh.
21 Na watu, akawafanya kuwa watumwa kutoka mpaka mmoja wa Misri hata mkapa mwingine.
And the people he brought in it to the cities from [the] end of [the] territory of Egypt and to end its.
22 Ilikuwa ni nchi ya makuhani pekee ambayo Yusufu hakuinunua, kwa maana makuhani walikuwa wakipewa posho. Walikula katika sehemu aliyowapa Farao. Kwa hiyo hawakuuza nchi yao.
Only [the] land of the priests not he bought for an allowance [belonged] to the priests from with Pharaoh and they eat allowance their which he gave to them Pharaoh there-fore not they sold land their.
23 Kisha Yusufu akawambia watu, “Tazama, nimewanunua ninyi na nchi yenu leo kwa ajili ya Farao. Basi mbegu hii hapa kwa ajili yenu, nanyi mtapanda katika nchi.
And he said Joseph to the people here! I have bought you this day and land your for Pharaoh here! for you [is] seed and you will sow the land.
24 Wakati wa mavuno, mtampa Farao sehemu ya tano, na sehemu nne zitakuwa zenu, kwa mbegu za shamba na kwa chakula cha nyumba zenu na watoto wenu.”
And it will be at the harvest and you will give a fifth to Pharaoh and [the] four the hands it will be[long] to you to [the] seed of the field and to food your and for [those] who [are] in households your and to eat for little one[s] your.
25 Wakasema, “Umeokoa maisha yetu. Na tupate kibali machoni pako. Tutakuwa watumishi wa Farao.”
And they said you have preserved alive us may we find favor in [the] eyes of lord my and we will be slaves of Pharaoh.
26 Hivyo Yusufu akaifanya kuwa sheria inayofanya kazi hata leo katika nchi ya Misri, kwamba moja ya tano ni ya Farao. Eneo la makuhani peke yake ndo halikufanywa kuwa la Farao.
And he established it Joseph to a statute until the day this on [the] land of Egypt [belongs] to Pharaoh to the fifth part only [the] land of the priests to alone them not it belonged to Pharaoh.
27 Hivyo Israeli akaishi katika nchi ya Misri, katika eneo la Gosheni. Watu wake wakapata umiliki pale. Walikuwa wenye kuzaa na kuongezeka sana.
And he dwelt Israel in [the] land of Egypt in [the] land of Goshen and they had possessions in it and they were fruitful and they multiplied exceedingly.
28 Yakobo akaishi katika nchi ya Misri miaka kumi na saba, kwa hiyo miaka ya maisha ya Yakobo ilikuwa miaka mia moja arobaini na saba.
And he lived Jacob in [the] land of Egypt seven-teen year[s] and it was [the] days of Jacob [the] years of life his seven years and forty and one hundred year[s].
29 Wakati wa kufa kwake Yakobo ulipokaribia, alimwita Yusufu mwanaye na kumwambia, “Ikiwa nimepata kibali mbele zako, weka mkono wako chini ya paja langu, na unitendee kwa uaminifu na kweli. Tafadhari usinizike Misri.
And they drew near [the] days of Israel to die and he summoned - son his Joseph and he said to him if please I have found favor in view your put please hand your under thigh my and you will do with me loyalty and faithfulness may not please you bury me in Egypt.
30 Nitakapolala na baba zangu, utanitoa Misri na kunizika katika eneo la kuzikia la baba zangu.” Yusufu akasema, “Nitafanya kama ulivyosema.”
And I will lie down with ancestors my and you will carry me from Egypt and you will bury me in grave their and he said I I will do according to word your.
31 Israeli akasema, “Niapie,” na Yusufu akamwapia. Kisha Israeli akainama chini mbele ya kitanda chake.
And he said swear an oath! to me and he swore an oath to him and he bowed down Israel on [the] head of the bed.

< Mwanzo 47 >