< Mwanzo 47 >
1 Kisha Yusufu akaingia kwa Farao na kumwambia, “Baba yangu na ndugu zangu, kondoo wao, mbuzi wao, na yote waliyonayo, wamefika kutoka katika nchi ya Kanaani. Tazama, wapo katika nchi ya Gosheni.”
Then came Ioseph and tolde Pharaoh, and sayde, My father, and my brethren, and their sheepe, and their cattell, and all that they haue, are come out of the land of Canaan, and behold, they are in the land of Goshen.
2 Akawachukua watano katika ndugu zake na kuwatambulisha kwa Farao.
And Ioseph tooke part of his brethren, euen fiue men, and presented them vnto Pharaoh.
3 Farao akawambia ndugu zake, “Kazi yenu ni nini?” Wakamwambia Farao, “Watumishi wako ni wafugaji, kama mababu zetu.”
Then Pharaoh said vnto his brethren, What is your trade? And they answered Pharaoh, Thy seruants are shepheards, both we and our fathers.
4 Kisha wakamwambia Farao, “Tumekuja kukaa kwa muda katika nchi. Hakuna malisho kwa ajili ya makundi ya watumishi wako, kwa maana njaa ni kali sana katika nchi ya Kanaani. Hivyo, tafadhari waache watumishi wako wakae katika nchi ya Gosheni.”
They sayde moreouer vnto Pharaoh, For to soiourne in ye lande are we come: for thy seruants haue no pasture for their sheepe, so sore is ye famine in the lande of Canaan. Nowe therefore, we pray thee, let thy seruants dwel in the land of Goshen.
5 Kisha Farao akamwambia Yusufu, kusema, “Baba yako na ndugu zako wamekuja kwako.
Then spake Pharaoh to Ioseph, saying, Thy father and thy brethren are come vnto thee.
6 Nchi ya Misri iko mbele yako. Mkalishe baba yako na ndugu zako katika eneo zuri, nchi ya Gosheni. Ikiwa unafahamu watu wenye uwezo miongoni mwao, uwaweke kuwatunza wanyama wangu.”
The lande of Egypt is before thee: in the best place of the land make thy father and thy brethren dwel: let the dwel in the land of Goshen: and if thou knowest that there be men of actiuitie among them, make them rulers ouer my cattell.
7 Kisha Yusufu akamwingiza Yakobo baba yake na kumweka mbele ya Farao. Yakobo akambariki Farao.
Ioseph also brought Iaakob his father, and set him before Pharaoh. And Iaakob saluted Pharaoh.
8 Farao akamwambia Yakobo, “Umeishi kwa muda gani?”
Then Pharaoh sayde vnto Iaakob, Howe olde art thou?
9 Yakobo akamwambia Farao, “Miaka ya safari zangu ni mia moja na thelathini. Miaka ya maisha yangu imekuwa mifupi na ya maumivu. Siyo kama miaka ya baba zangu.”
And Iaakob sayd vnto Pharaoh, The whole time of my pilgrimage is an hundreth and thirty yeeres: fewe and euill haue the dayes of my life bene, and I haue not attayned vnto the yeeres of the life of my fathers, in the dayes of their pilgrimages.
10 Kisha Yakobo akambariki Farao na kuondoka mbele zake.
And Iaakob tooke leaue of Pharaoh, and departed from the presence of Pharaoh.
11 Kisha Yusufu akamweka baba yake na ndugu zake. Akawapa eneo katika nchi ya Misri, sehemu nzuri sana ya nchi, katika eneo la Ramesesi, kama Farao alivyokuwa ameagiza.
And Ioseph placed his father, and his brethren, and gaue them possession in the lande of Egypt, in the best of the land, euen in the lande of Rameses, as Pharaoh had commanded.
12 Yusufu akamhudumia baba yake kwa chakula, ndugu zake, na nyumba yote ya baba yake, kulingana na hesabu ya wahitaji wao.
And Ioseph nourished his father, and his brethren, and all his fathers houshold with bread, euen to the yong children.
13 Basi hakukuwa na chakula katika nchi yote; kwani njaa ilikuwa kali sana. Nchi ya Misri na nchi ya Kanaani ikaharibika kwa sababu ya njaa.
Now there was no bread in all the land: for the famine was exceeding sore: so that the land of Egypt, and the land of Canaan were famished by reason of the famine.
14 Yusufu akakusanya pesa yote iliyokuwa katika nchi ya Misri na nchi ya Kanaani, kwa kuwauzia wakaaji wake chakula. Kisha Yusufu akaleta ile pesa katika kasri la Farao.
And Ioseph gathered all the money, that was found in the land of Egypt, and in the land of Canaan, for the corne which they bought, and Ioseph layd vp the money in Pharaohs house.
15 Pesa yote ya nchi za Misri na Kanaani ilipokwisha, Wamisri wote wakaja kwa Yusufu wakisema, “Tupe chakula! Kwa nini tufe mbele zako kwa maana pesa yetu imekwisha?”
So when money fayled in the lande of Egypt, and in the lande of Canaan, then all the Egyptians came vnto Ioseph, and sayde, Giue vs bread: for why should we dye before thee? for our money is spent.
16 Yusufu akasema, “Ikiwa pesa yenu imekwisha, leteni wanyama wenu nami nitawapa chakula badala ya wanyama wenu.”
Then saide Ioseph, Bring your cattell, and I will giue you for your cattell, if your money be spent.
17 Hivyo wakaleta wanyama wao kwa Yusufu. Yusufu akawapa chakula kwa kubadilishana na farasi, kondoo, mbuzi na kwa punda. Akawalisha kwa mkate kwa kubadilisha na wanyama wao mwaka ule.
So they brought their cattell vnto Ioseph, and Ioseph gaue them bread for the horses, and for the flockes of sheepe, and for the heards of cattel, and for the asses: so he fed them with bread for all their cattell that yeere.
18 Mwaka ule ulipokwisha, wakaja kwake mwaka uliofuata na kumwambia, “Hatutaficha kwa bwana wangu kwamba pesa yetu yote imekwisha, na wanyama ni wa bwana wangu. Hakuna kilichobaki mbele za bwana wangu, isipokuwa miili yetu na nchi yetu.
But when the yeere was ended, they came vnto him the next yeere, and sayd vnto him, We will not hide from my lord, that since our money is spent, and my lord hath the heards of the cattel, there is nothing left in the sight of my lorde, but our bodies and our ground.
19 Kwa nini tufe mbele za macho yake, sisi na nchi yetu? Utununue sisi na nchi yetu badala ya chakula, na sisi na nchi yetu tutakuwa watumishi wa Farao. Tupe mbegu ili kwamba tuishi na tusife, na kwamba nchi isiwe tupu bila watu.
Why shall we perish in thy sight, both we, and our land? bye vs and our land for bread, and we and our land will be bonde to Pharaoh: therefore giue vs seede, that we may liue and not dye, and that the land go not to waste.
20 Hivyo Yusufu akamnunulia Farao nchi yote ya Misri. Kwani kila Mmisri akauza shamba lake, kwa sababu njaa ilikuwa kali sana. Kwa njia hii, nchi ikawa mali ya Farao.
So Ioseph bought all the lande of Egypt for Pharaoh: for the Egyptians solde euery man his ground because the famine was sore vpon the: so the land became Pharaohs.
21 Na watu, akawafanya kuwa watumwa kutoka mpaka mmoja wa Misri hata mkapa mwingine.
And he remoued the people vnto the cities, from one side of Egypt euen to the other.
22 Ilikuwa ni nchi ya makuhani pekee ambayo Yusufu hakuinunua, kwa maana makuhani walikuwa wakipewa posho. Walikula katika sehemu aliyowapa Farao. Kwa hiyo hawakuuza nchi yao.
Onely the lande of the Priestes bought he not: for the Priestes had an ordinarie of Pharaoh, and they did eate their ordinarie, which Pharaoh gaue them: wherefore they solde not their grounde.
23 Kisha Yusufu akawambia watu, “Tazama, nimewanunua ninyi na nchi yenu leo kwa ajili ya Farao. Basi mbegu hii hapa kwa ajili yenu, nanyi mtapanda katika nchi.
Then Ioseph sayd vnto the people, Behold, I haue bought you this daye, and your lande for Pharaoh: lo, here is seede for you: sowe therefore the grounde.
24 Wakati wa mavuno, mtampa Farao sehemu ya tano, na sehemu nne zitakuwa zenu, kwa mbegu za shamba na kwa chakula cha nyumba zenu na watoto wenu.”
And of the encrease ye shall giue the fifth part vnto Pharaoh, and foure partes shalbe yours for the seede of the fielde, and for your meate, and for them of your housholdes, and for your children to eate.
25 Wakasema, “Umeokoa maisha yetu. Na tupate kibali machoni pako. Tutakuwa watumishi wa Farao.”
Then they answered, Thou hast saued our liues: let vs finde grace in the sight of my Lord, and we will be Pharaohs seruants.
26 Hivyo Yusufu akaifanya kuwa sheria inayofanya kazi hata leo katika nchi ya Misri, kwamba moja ya tano ni ya Farao. Eneo la makuhani peke yake ndo halikufanywa kuwa la Farao.
Then Ioseph made it a lawe ouer the land of Egypt vnto this day, that Pharaoh should haue the fift part, except the land of the priests only, which was not Pharaohs.
27 Hivyo Israeli akaishi katika nchi ya Misri, katika eneo la Gosheni. Watu wake wakapata umiliki pale. Walikuwa wenye kuzaa na kuongezeka sana.
And Israel dwelt in the lande of Egypt, in the countrey of Goshen: and they had their possessions therein, and grewe and multiplied exceedingly.
28 Yakobo akaishi katika nchi ya Misri miaka kumi na saba, kwa hiyo miaka ya maisha ya Yakobo ilikuwa miaka mia moja arobaini na saba.
Moreouer, Iaakob liued in the lande of Egypt seuenteene yeeres, so that the whole age of Iaakob was an hundreth fourtie and seuen yeere.
29 Wakati wa kufa kwake Yakobo ulipokaribia, alimwita Yusufu mwanaye na kumwambia, “Ikiwa nimepata kibali mbele zako, weka mkono wako chini ya paja langu, na unitendee kwa uaminifu na kweli. Tafadhari usinizike Misri.
Now when the time drewe neere that Israel must dye, he called his sonne Ioseph, and sayde vnto him, If I haue nowe founde grace in thy sight, put thine hand nowe vnder my thigh, and deale mercifully and truely with me: burie me not, I pray thee, in Egypt.
30 Nitakapolala na baba zangu, utanitoa Misri na kunizika katika eneo la kuzikia la baba zangu.” Yusufu akasema, “Nitafanya kama ulivyosema.”
But when I shall sleepe with my fathers, thou shalt carry me out of Egypt, and bury mee in their buryall. And he answered, I will doe as thou hast sayde.
31 Israeli akasema, “Niapie,” na Yusufu akamwapia. Kisha Israeli akainama chini mbele ya kitanda chake.
The he said, Sweare vnto me. And he sware vnto him. And Israel worshipped towardes the beds head.