< Mwanzo 46 >
1 Israeli akasafiri na yote aliyokuwa nayo na akaja Beersheba. Pale akatoa sadaka kwa Mungu wa Isaka baba yake.
and to set out Israel and all which to/for him and to come (in): come Beersheba [to] Beersheba and to sacrifice sacrifice to/for God father his Isaac
2 Mungu akamwambia Israeli katika ndoto usiku, akisema, “Yakobo, Yakobo.”
and to say God to/for Israel in/on/with vision [the] night and to say Jacob Jacob and to say behold I
3 Akasema, “Mimi hapa.” Akasema, “Mimi ni Mungu, Mungu wa baba yako. Usiogope kushuka Misri, kwa maana nitakufanya taifa kubwa huko.
and to say I [the] God God father your not to fear from to go down Egypt [to] for to/for nation great: large to set: make you there
4 Nitakwenda pamoja nawe huko Misri, Nami nitakupandisha huku tena bila shaka. Na Yusufu akayafunika macho yako kwa mikono wake.”
I to go down with you Egypt [to] and I to ascend: establish you also to ascend: establish and Joseph to set: put hand: power his upon eye your
5 Yakobo akainuka kutoka Beersheba. Wana wa Israeli wakamsafirisha Yakobo baba yao, watoto wao, na wake wao, katika mikokotene ambayo Farao alikuwa ameipeleka kuwachukua.
and to arise: rise Jacob from Beersheba Beersheba and to lift: bear son: child Israel [obj] Jacob father their and [obj] child their and [obj] woman: wife their in/on/with cart which to send: depart Pharaoh to/for to lift: bear [obj] him
6 Wakachukua mifugo yao na mali zao walizokuwa wamezipata katika nchi ya Kanaani. Wakaja Misri, Yakobo na uzao wake wote pamoja naye.
and to take: take [obj] livestock their and [obj] property their which to gather in/on/with land: country/planet Canaan and to come (in): come Egypt [to] Jacob and all seed: children his with him
7 Akaja Misri pamoja na wanawe na wana wa wanawe, binti zake na wana wa binti zake, na uzao wake wote.
son: child his and son: child son: child his with him daughter his and daughter son: child his and all seed: children his to come (in): bring with him Egypt [to]
8 Haya ni majina ya watoto wa Israeli waliokuja Misri, Yakobo na wanawe: Rubeni, mzaliwa wa kwanza wa Yakobo;
and these name son: descendant/people Israel [the] to come (in): come Egypt [to] Jacob and son: child his firstborn Jacob Reuben
9 wana wa Rubeni Hanoki na Palu na Hezroni na Karmi;
and son: child Reuben Hanoch and Pallu and Hezron and Carmi
10 wana wa Simoni, Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Zohari, na Shauli, wana wa mwanamke Mkanaani;
and son: child Simeon Jemuel and Jamin and Ohad and Jachin and Zohar and Shaul son: child [the] Canaanitess
11 wana wa Lawi Gershoni, Kohathi, na Merari.
and son: child Levi Gershon Kohath and Merari
12 Wana wa Yuda: Eri, Shela, Peresi, na Zera, (Lakini Eri na Onani walikufa katika nchi ya Kanaani). Na wana wa Peresi walikuwa Hezroni na Hamuli.
and son: child Judah Er and Onan and Shelah and Perez and Zerah and to die Er and Onan in/on/with land: country/planet Canaan and to be son: child Perez Hezron and Hamul
13 Wana wa Isakari walikuwa Tola, Puva, Lobu, na Shimroni;
and son: child Issachar Tola and Puah and Yob and Shimron
14 Wana wa Zabuloni walikuwa Seredi, Eloni, na Yahleeli
and son: child Zebulun Sered and Elon and Jahleel
15 Hawa walikuwa wana wa Lea aliomzalia Yakobo huko Padani Aramu, pamoja na na Dina binti yake. Wanawe na binti zake walikuwa thelathini na watatu.
these son: child Leah which to beget to/for Jacob in/on/with Paddan (Paddan)-aram and with Dinah daughter his all soul: person son: child his and daughter his thirty and three
16 Wana wa Gadi walikuwa Zifioni, Hagi, Shuni, Ezboni, Eri, Arodi, na Areli.
and son: child Gad Ziphion and Haggi Shuni and Ezbon Eri and Arodi and Areli
17 Wana wa Asheri walikuwa Imna, Ishva, Ishvi, na Beria; na Sera alikuwa dada yao. Wana wa Beria walikuwa Heberi na Malkieli.
and son: child Asher Imnah and Ishvah and Ishvi and Beriah and Serah sister their and son: child Beriah Heber and Malchiel
18 Hawa walikuwa wana wa Zilpa, ambaye Labani alikuwa amempa Lea binti yake. Wana aliomzalia Yakobo wote walikuwa kumi na sita.
these son: child Zilpah which to give: give Laban to/for Leah daughter his and to beget [obj] these to/for Jacob six ten soul: person
19 Wana wa Raheli mkewe Yakobo walikuwa Yusufu na Benjamini.
son: child Rachel woman: wife Jacob Joseph and Benjamin
20 Huko Misri Manase na Efraimu walizaliwa kwa Yusufu na Asenathi, binti Potifera kuhani wa Oni.
and to beget to/for Joseph in/on/with land: country/planet Egypt which to beget to/for him Asenath daughter Potiphera Potiphera priest On [obj] Manasseh and [obj] Ephraim
21 Wana wa Benjamini walikuwa Bela, Bekeri, Ashbeli, Gera, Naamani, Ehi, Roshi, Mupimu, Hupimu, na Ardi.
and son: child Benjamin Bela and Becher and Ashbel Gera and Naaman Ehi and Rosh Muppim and Huppim and Ard
22 Hawa walikuwa wana wa Raheli waliozaliwa kwa Yakobo - jumla yao kumi na wanne.
these son: child Rachel which to beget to/for Jacob all soul: person four ten
23 Mwana wa Dani alikuwa Hushimu.
and son: child Dan Hushim
24 Wana wa Naftali walikuwa Yahzeeli, Guni, Yezeri, na Shilemi.
and son: child Naphtali Jahzeel and Guni and Jezer and Shillem
25 Hawa walikuwa wana Bilha aliomzalia Yakobo, ambaye Labani alimpa Raheli binti yake - wote walikuwa saba.
these son: child Bilhah which to give: give Laban to/for Rachel daughter his and to beget [obj] these to/for Jacob all soul: person seven
26 Wate waliokwenda na Yakobo, waliokuwa uzao wake, bila kuhesabu wake wa wana wa Yakobo walikuwa sitini na sita.
all [the] soul: person [the] to come (in): come to/for Jacob Egypt [to] to come out: produce thigh his from to/for alone: besides woman: wife son: child Jacob all soul: person sixty and six
27 Pamoja na wana wawili wa Yusufu waliozaliwa kwake huko Misri, watu wa familia yake waliokwenda Misri walikuwa sabini jumla yao.
and son: child Joseph which to beget to/for him in/on/with Egypt soul: person two all [the] soul: person to/for house: household Jacob [the] to come (in): come Egypt [to] seventy
28 Yakobo akamtuma Yuda kuwatangulia mbele kwa Yusufu kuonesha njia mbele yake kwenda Gosheni, nao wakaja katika eneo la Gosheni.
and [obj] Judah to send: depart to/for face: before his to(wards) Joseph to/for to show to/for face: before his Goshen [to] and to come (in): come land: country/planet [to] Goshen
29 Yusufu akaandaa kibandawazi chake na akaenda kumlaki baba yake huko Gosheni. Akamwona, akaikumbatia shingo yake, na akalia shingoni mwake kwa kitambo.
and to bind Joseph chariot his and to ascend: rise to/for to encounter: meet Israel father his Goshen [to] and to see: see to(wards) him and to fall: fall upon neck his and to weep upon neck his still
30 Israeli akamwambia Yusufu, “Basi na nife sasa, kwa kuwa nimeuona uso wako, kwamba bado uko hai.”
and to say Israel to(wards) Joseph to die [the] beat after to see: see I [obj] face your for still you alive
31 Yusufu akawambia ndungu zake na nyumba ya baba yake, “Nitakwenda na kumwambia Farao, kusema, 'Ndugu zangu na nyumba ya baba yangu, waliokuwa katika nchi ya Kanaani, wamenijia.
and to say Joseph to(wards) brother: male-sibling his and to(wards) house: household father his to ascend: rise and to tell to/for Pharaoh and to say to(wards) him brother: male-sibling my and house: household father my which in/on/with land: country/planet Canaan to come (in): come to(wards) me
32 Watu hawa ni wafugaji, kwani wamekuwa watunza wanyama. Wamekuja na makundi yao ya kondoo, na mbuzi, na vyote walivyonavyo.'
and [the] human to pasture flock for human livestock to be and flock their and cattle their and all which to/for them to come (in): bring
33 Itakuwa, Farao atakapowaita na kuwauliza, 'Kazi yenu ni ipi?'
and to be for to call: call to to/for you Pharaoh and to say what? deed: work your
34 mwambieni, 'Watumishi wako wamekuwa watunza wanyama tangu ujana wetu mpaka sasa, sisi, na baba zetu.' Fanyeni hivyo ili mweze kuishi katika nchi ya Gosheni, kwani kila mfugaji ni chukizo kwa Wamisri.”
and to say human livestock to be servant/slave your from youth our and till now also we also father our in/on/with for the sake of to dwell in/on/with land: country/planet Goshen for abomination Egyptian all to pasture flock