< Mwanzo 46 >

1 Israeli akasafiri na yote aliyokuwa nayo na akaja Beersheba. Pale akatoa sadaka kwa Mungu wa Isaka baba yake.
Then Israel tooke his iourney with all that he had, and came to Beer-sheba, and offered sacrifice vnto the God of his father Izhak.
2 Mungu akamwambia Israeli katika ndoto usiku, akisema, “Yakobo, Yakobo.”
And God spake vnto Israel in a vision by night, saying, Iaakob, Iaakob. Who answered, I am here.
3 Akasema, “Mimi hapa.” Akasema, “Mimi ni Mungu, Mungu wa baba yako. Usiogope kushuka Misri, kwa maana nitakufanya taifa kubwa huko.
Then hee sayde, I am God, the God of thy father, feare not to goe downe into Egypt: for I will there make of thee a great nation.
4 Nitakwenda pamoja nawe huko Misri, Nami nitakupandisha huku tena bila shaka. Na Yusufu akayafunika macho yako kwa mikono wake.”
I wil go downe with thee into Egypt, and I will also bring thee vp againe, and Ioseph shall put his hand vpon thine eyes.
5 Yakobo akainuka kutoka Beersheba. Wana wa Israeli wakamsafirisha Yakobo baba yao, watoto wao, na wake wao, katika mikokotene ambayo Farao alikuwa ameipeleka kuwachukua.
Then Iaakob rose vp from Beer-sheba: and the sonnes of Israel caried Iaakob their father, and their children, and their wiues in the charets, which Pharaoh had sent to cary him.
6 Wakachukua mifugo yao na mali zao walizokuwa wamezipata katika nchi ya Kanaani. Wakaja Misri, Yakobo na uzao wake wote pamoja naye.
And they tooke their cattell and their goods, which they had gotten in the lande of Canaan, and came into Egypt, both Iaakob and all his seede with him,
7 Akaja Misri pamoja na wanawe na wana wa wanawe, binti zake na wana wa binti zake, na uzao wake wote.
His sonnes and his sonnes sonnes with him, his daughters and his sonnes daughters, and al his seede brought he with him into Egypt.
8 Haya ni majina ya watoto wa Israeli waliokuja Misri, Yakobo na wanawe: Rubeni, mzaliwa wa kwanza wa Yakobo;
And these are the names of the children of Israel, which came into Egypt, euen Iaakob and his sonnes: Reuben, Iaakobs first borne.
9 wana wa Rubeni Hanoki na Palu na Hezroni na Karmi;
And the sonnes of Reuben: Hanoch, and Phallu, and Hezron, and Carmi.
10 wana wa Simoni, Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Zohari, na Shauli, wana wa mwanamke Mkanaani;
And the sonnes of Simeon: Iemuel, and Iamin, and Ohad, and Iachin, and Zohar; and Shaul the sonne of a Canaanitish woman.
11 wana wa Lawi Gershoni, Kohathi, na Merari.
Also the sonnes of Leui: Gershon, Kohath, and Merari.
12 Wana wa Yuda: Eri, Shela, Peresi, na Zera, (Lakini Eri na Onani walikufa katika nchi ya Kanaani). Na wana wa Peresi walikuwa Hezroni na Hamuli.
Also the sonnes of Iudah: Er, and Onan, and Shelah, and Pharez, and Zerah: (but Er and Onan died in ye land of Canaan) And the sonnes of Pharez were Hezron and Hamul.
13 Wana wa Isakari walikuwa Tola, Puva, Lobu, na Shimroni;
Also the sonnes of Issachar: Tola, and Phuuah, and Iob, and Shimron.
14 Wana wa Zabuloni walikuwa Seredi, Eloni, na Yahleeli
Also the sonnes of Zebulun: Sered, and Elon, and Iahleel.
15 Hawa walikuwa wana wa Lea aliomzalia Yakobo huko Padani Aramu, pamoja na na Dina binti yake. Wanawe na binti zake walikuwa thelathini na watatu.
These bee the sonnes of Leah, which shee bare vnto Iaakob in Padan Aram, with his daughter Dinah. All the soules of his sonnes and his daughters were thirtie and three.
16 Wana wa Gadi walikuwa Zifioni, Hagi, Shuni, Ezboni, Eri, Arodi, na Areli.
Also the sonnes of Gad: Ziphion, and Haggi, Shuni, and Ezbon, Eri, and Arodi, and Areli.
17 Wana wa Asheri walikuwa Imna, Ishva, Ishvi, na Beria; na Sera alikuwa dada yao. Wana wa Beria walikuwa Heberi na Malkieli.
Also the sonnes of Asher: Iimnah, and Ishuah, and Isui, and Beriah, and Serah their sister. And the sonnes of Beriah: Heber, and Malchiel.
18 Hawa walikuwa wana wa Zilpa, ambaye Labani alikuwa amempa Lea binti yake. Wana aliomzalia Yakobo wote walikuwa kumi na sita.
These are the children of Zilpah, whome Laban gaue to Leah his daughter: and these shee bare vnto Iaakob, euen sixtene soules.
19 Wana wa Raheli mkewe Yakobo walikuwa Yusufu na Benjamini.
The sonnes of Rahel Iaakobs wife were Ioseph and Beniamin.
20 Huko Misri Manase na Efraimu walizaliwa kwa Yusufu na Asenathi, binti Potifera kuhani wa Oni.
And vnto Ioseph in the lande of Egypt were borne Manasseh, and Ephraim, which Asenath the daughter of Poti-pherah prince of On bare vnto him.
21 Wana wa Benjamini walikuwa Bela, Bekeri, Ashbeli, Gera, Naamani, Ehi, Roshi, Mupimu, Hupimu, na Ardi.
Also the sonnes of Beniamin: Belah, and Becher, and Ashbel, Gera, and Naaman, Ehi, and Rosh, Muppim, and Huppim, and Ard.
22 Hawa walikuwa wana wa Raheli waliozaliwa kwa Yakobo - jumla yao kumi na wanne.
These are the sonnes of Rahel, which were borne vnto Iaakob, fourteene soules in all.
23 Mwana wa Dani alikuwa Hushimu.
Also the sonnes of Dan: Hushim.
24 Wana wa Naftali walikuwa Yahzeeli, Guni, Yezeri, na Shilemi.
Also the sonnes of Naphtali: Iahzeel, and Guni, and Iezer, and Shillem.
25 Hawa walikuwa wana Bilha aliomzalia Yakobo, ambaye Labani alimpa Raheli binti yake - wote walikuwa saba.
These are the sonnes of Bilhah, which Laban gaue vnto Rahel his daughter, and shee bare these to Iaakob, in all, seuen soules.
26 Wate waliokwenda na Yakobo, waliokuwa uzao wake, bila kuhesabu wake wa wana wa Yakobo walikuwa sitini na sita.
Al the soules, that came with Iaakob into Egypt, which came out of his loynes (beside Iaakobs sonnes wiues) were in the whole, three score and sixe soules.
27 Pamoja na wana wawili wa Yusufu waliozaliwa kwake huko Misri, watu wa familia yake waliokwenda Misri walikuwa sabini jumla yao.
Also the sonnes of Ioseph, which were borne him in Egypt, were two soules: so that al the soules of the house of Iaakob, which came into Egypt, are seuentie.
28 Yakobo akamtuma Yuda kuwatangulia mbele kwa Yusufu kuonesha njia mbele yake kwenda Gosheni, nao wakaja katika eneo la Gosheni.
The he sent Iudah before him vnto Ioseph, to direct his way vnto Goshen, and they came into the land of Goshen.
29 Yusufu akaandaa kibandawazi chake na akaenda kumlaki baba yake huko Gosheni. Akamwona, akaikumbatia shingo yake, na akalia shingoni mwake kwa kitambo.
Then Ioseph made ready his charet and went vp to Goshen to meete Israel his father, and presented himselfe vnto him and fel on his necke, and wept vpon his necke a good while.
30 Israeli akamwambia Yusufu, “Basi na nife sasa, kwa kuwa nimeuona uso wako, kwamba bado uko hai.”
And Israel sayde vnto Ioseph, Now let me die, since I haue seene thy face, and that thou art yet aliue.
31 Yusufu akawambia ndungu zake na nyumba ya baba yake, “Nitakwenda na kumwambia Farao, kusema, 'Ndugu zangu na nyumba ya baba yangu, waliokuwa katika nchi ya Kanaani, wamenijia.
Then Ioseph said to his brethren, and to his fathers house, I wil go vp and shew Pharaoh, and tell him, My brethren and my fathers house, which were in the land of Canaan, are come vnto me,
32 Watu hawa ni wafugaji, kwani wamekuwa watunza wanyama. Wamekuja na makundi yao ya kondoo, na mbuzi, na vyote walivyonavyo.'
And the men are shepheardes, and because they are shepheardes, they haue brought their sheepe and their cattell, and all that they haue.
33 Itakuwa, Farao atakapowaita na kuwauliza, 'Kazi yenu ni ipi?'
And if Pharaoh call you, and aske you, What is your trade?
34 mwambieni, 'Watumishi wako wamekuwa watunza wanyama tangu ujana wetu mpaka sasa, sisi, na baba zetu.' Fanyeni hivyo ili mweze kuishi katika nchi ya Gosheni, kwani kila mfugaji ni chukizo kwa Wamisri.”
Then ye shall say, Thy seruants are men occupied about cattell, from our childehood euen vnto this time, both we and our fathers: that yee may dwell in the lande of Goshen: for euery sheepe keeper is an abomination vnto the Egyptians.

< Mwanzo 46 >