< Mwanzo 45 >

1 Ndipo Yusufu hakuweza kujizuia mwenyewe mbele ya watumishi waliosimama kando yake. Akasema kwa sauti, “Kila mtu aondoke.” Hivyo hakuna mtumishi aliyesimama kando yake wakati Yusufu alipojitambulisha kwa ndugu zake.
And not he was able Joseph to restrain himself to all those standing with him and he called out send out every man from with me and not he stood anyone with him when made himself known Joseph to brothers his.
2 Akalia kwa sauti, Wamisri wakasikia, na nyumba ya Farao wakasikia kuhusu hilo.
And he gave voice his in weeping and they heard Egypt and it heard [the] household of Pharaoh.
3 Yusufu akawambia ndugu zake, “Mimi ni Yusufu. Je baba yangu ni mzima bado? Ndugu zake hawakuweza kumjibu, kwani walitishwa na uwepo wake.
And he said Joseph to brothers his I [am] Joseph ¿ still [is] father my living and not they were able brothers his to answer him for they were terrified of him.
4 Kisha Yusufu akawambia ndugu zake, “Nikaribieni, tafadhari.” Nao wakasogea. Akawambia, “Mimi ni Yusufu ndugu yenu, mliyemwuza Misri.
And he said Joseph to brothers his draw near please to me and they drew near and he said I [am] Joseph brother your whom you sold me Egypt towards.
5 Lakini sasa msihuzunike au kukasirika miongoni mwenu kwamba mliniuza huku, kwani Mungu alinituma mbele yenu ili kutunza uhai.
And now - may not you be grieved and may not it burn in view your that you sold me hither for for preservation of life he sent me God before you.
6 Maana ni miaka miwili njaa imekuwa katika nchi, na bado kuna miaka mitano ambayo hakutakuwa na kulima wala kuvuna.
For this two years the famine [has been] in [the] midst of the land and still five years when there not [will be] plowing and harvest.
7 Mungu alinituma mbele yenu kuwahifadhi kama masalia duniani, na kuwaweka hai kwa ukombozi mkuu.
And he sent me God before you to make for you a remnant on the earth and to preserve alive for you a deliverance great.
8 Hivyo si ninyi mlionipeleka huku bali ni Mungu, na amenifanya baba kwa Farao, bwana wa nyumba yake yote, na mtawala wa nchi yote ya Misri.
And therefore not you you sent me hither for God and he has appointed me to a father of Pharaoh and to lord of all household his and ruler over all [the] land of Egypt.
9 Fanyeni haraka mwende kwa baba yangu na mmwambie, 'Hivi ndivyo asemavyo Yusufu mwanao, “Mungu amenifanya bwana kwa Wamisri wote. Shuka kwangu, usikawie.
Hurry and go up to father my and you will say to him thus he says son your Joseph he has appointed me God to lord of all Egypt come down! to me may not you delay.
10 Utaishi katika nchi ya Gosheni, nawe utakuwa karibu nami, wewe na watoto wako na watoto wa watoto wako, na kondoo wako na mbuzi wako, na yote uliyonayo.
And you will dwell in [the] land of Goshen and you will be near to me you and children your and [the] children of children your and sheep your and cattle your and all that [belongs] to you.
11 Nami nitakuhudumia pale, kwa maana bado kuna miaka mitano ya njaa, hivyo usije ukaingia katika uhitaji, wewe, nyumba yako, na yote uliyonayo.”
And I will provide for you there for still [will be] five years famine lest you should become impoverished you and household your and all that [belongs] to you.
12 Tazama, macho yenu yanaona, na macho ya Benjamini ndugu yangu, kwamba ni kinywa changu kinachoongea nanyi.
And there! eyes your [are] seeing and [the] eyes of brother my Benjamin that mouth my [is] the [one which] speaks to you.
13 Mtamwambia baba yangu juu ya heshima yangu yote huku Misri na yote mliyoyaona. Mtaharakisha na kumleta baba yangu huku.”
And you will tell to father my all honor my in Egypt and all that you saw and you will hurry and you will bring down father my hither.
14 Akaikumbatia shingo ya Benjamini ndugu yake na kulia, na Benjamini akalia shongoni mwake.
And he fell on [the] neck of Benjamin brother his and he wept and Benjamin he wept on neck his.
15 Akawabusu ndugu zake wote na kulia kwa ajili yao. Baada ya hayo ndugu zake wakaongea naye.
And he kissed all brothers his and he wept over them and after thus they spoke brothers his with him.
16 Habari ya jambo hili ikasemwa katika nyumba ya Farao: “Ndugu zake Yusufu wamekuja.” Ikampendeza sana Farao na watumishi wake.
And the sound it was heard [the] house of Pharaoh saying they have come [the] brothers of Joseph and it was good in [the] eyes of Pharaoh and in [the] eyes of servants his.
17 Farao akamwambia Yusufu, “Wambie ndugu zako, 'Fanyeni hivi: Wapakieni wanyama wenu na mwende katika nchi ya Kanaani.
And he said Pharaoh to Joseph say to brothers your this do load animal[s] your and go go [the] land of towards Canaan.
18 Mchukueni baba yenu na nyumba zenu mnijie. Nami nitawapa mema ya nchi ya Misri, nanyi mtakula unono wa nchi.'
And fetch father your and households your and come to me so let me give to you [the] good thing[s] of [the] land of Egypt and eat [the] fat of the land.
19 Basi mmeamriwa, 'Fanyeni hivi, chukueni mikokoteni kutoka Misri kwa ajili ya watoto wenu na kwa ajili ya wake zenu. Mchukueni baba yenu na kuja.
And you you are commanded this do take for yourselves from [the] land of Egypt carts for little one[s] your and for wives your and you will carry father your and you will come.
20 Msijari kuhusu mali zenu, kwani mema yote ya nchi ya Misri ni yenu.”
And eye your may not it look with regret on things your for [the] good thing[s] of all [the] land of Egypt [will belong] to you it.
21 Wana wa Israeli wakafanya hivyo. Yusufu akawapa mikokoteni, kwa kadili ya agizo la Farao, na akawapa mahitaji ya safari.
And they did thus [the] sons of Israel and he gave to them Joseph carts on [the] mouth of Pharaoh and he gave to them provision[s] for the journey.
22 Akawapa wote mavazi ya kubadilisha, lakini akampa Benjamini vipande mia tatu vya fedha na mavazi matano ya kubadilisha.
To all of them he gave to each changes of clothes and to Benjamin he gave three of hundred silver and five changes of clothes.
23 Akampelekea baba yake: punda kumi waliobeba mema ya Misri, punda majike kumi wamebeba nafaka, mikate, na mahitaji mengine kwa baba yake kwa ajili ya safari.
And to father his he sent according to this ten donkeys carrying some of [the] good thing[s] of Egypt and ten female donkeys carrying grain and food and food for father his for the journey.
24 Hivyo akawaruhusu ndugu zake nao wakaondoka. Akawambia, “Angalieni msijemkagombana njiani.”
And he sent off brothers his and they went and he said to them may not you stir up on the way.
25 Wakapanda kutoka Misri na kuja katika nchi ya Kanaani, kwa Yakobo baba yao.
And they went up from Egypt and they came [the] land of Canaan to Jacob father their.
26 Wakamwambia “Yusufu bado yu hai, na ndiye mtawala juu ya nchi yote ya Misri.” Na moyo wake ulishikwa na ushangao, kwani hakuwaamini.
And they told to him saying still Joseph [is] alive and that he [is] ruling over all [the] land of Egypt and it grew numb heart his for not he believed them.
27 Wakamwambia maneno yote ya Yusufu aliyokuwa amewambia. Yakobo alipoona mikokoteni Yusufu aliyokuwa amepeleka kuwabeba, roho ya Yakobo baba yao ikafufuka.
And they spoke to him all [the] words of Joseph which he had spoken to them and he saw the carts which he had sent Joseph to carry him and it lived [the] spirit of Jacob father their.
28 Israeli akasema, “Inatosha. Yusufu mwanangu yu hai. Nitakwenda nikamwone kabla sijafa.”
And he said Israel enough still Joseph son my [is] alive I will go so I may see him before I will die.

< Mwanzo 45 >