< Mwanzo 45 >

1 Ndipo Yusufu hakuweza kujizuia mwenyewe mbele ya watumishi waliosimama kando yake. Akasema kwa sauti, “Kila mtu aondoke.” Hivyo hakuna mtumishi aliyesimama kando yake wakati Yusufu alipojitambulisha kwa ndugu zake.
And Joseph could not restrain himself before all who were stationed near him, so he cried out—Have forth every man from me! And there stood no man with him, when Joseph made himself known unto his brethren,
2 Akalia kwa sauti, Wamisri wakasikia, na nyumba ya Farao wakasikia kuhusu hilo.
Then gave he forth his voice in weeping, —and the Egyptians heard, and the house of Pharaoh heard.
3 Yusufu akawambia ndugu zake, “Mimi ni Yusufu. Je baba yangu ni mzima bado? Ndugu zake hawakuweza kumjibu, kwani walitishwa na uwepo wake.
Then said Joseph unto his brethren: I, am Joseph, is my father yet alive? But his brethren could not answer him, for they were terrified because of him.
4 Kisha Yusufu akawambia ndugu zake, “Nikaribieni, tafadhari.” Nao wakasogea. Akawambia, “Mimi ni Yusufu ndugu yenu, mliyemwuza Misri.
Then said Joseph unto his brethren—Draw near I pray you, unto me. And they drew near. And he said—I, am Joseph your brother, whom ye sold into Egypt.
5 Lakini sasa msihuzunike au kukasirika miongoni mwenu kwamba mliniuza huku, kwani Mungu alinituma mbele yenu ili kutunza uhai.
But, now, do not grieve, neither let it be vexing in your eyes, that ye sold me hither, —for, to save life, did God send me before you.
6 Maana ni miaka miwili njaa imekuwa katika nchi, na bado kuna miaka mitano ambayo hakutakuwa na kulima wala kuvuna.
For these two years, hath the famine been in the midst of the land, —and, yet five years, are there, in which there shall be neither ploughing, nor harvest.
7 Mungu alinituma mbele yenu kuwahifadhi kama masalia duniani, na kuwaweka hai kwa ukombozi mkuu.
So then God sent me before you, to plant for you a remainder in the earth, —and to save you alive, by a great deliverance,
8 Hivyo si ninyi mlionipeleka huku bali ni Mungu, na amenifanya baba kwa Farao, bwana wa nyumba yake yote, na mtawala wa nchi yote ya Misri.
Now, therefore it was not ye, who sent me hither, but, God, himself, —who also appointed me to be a father to Pharaoh, and a lord to all his house, and a ruler over all the land of Egypt.
9 Fanyeni haraka mwende kwa baba yangu na mmwambie, 'Hivi ndivyo asemavyo Yusufu mwanao, “Mungu amenifanya bwana kwa Wamisri wote. Shuka kwangu, usikawie.
Haste ye and go up unto my father, then shall ye say unto him—Thus saith thy son Joseph, God hath appointed me lord to all Egypt, —come down unto me do not delay;
10 Utaishi katika nchi ya Gosheni, nawe utakuwa karibu nami, wewe na watoto wako na watoto wa watoto wako, na kondoo wako na mbuzi wako, na yote uliyonayo.
so shalt thou dwell in the land of Goshen, and shalt be near unto me, thou, and thy sons, and thy sons’ sons, —and thy flocks and thy herds and all that is thine;
11 Nami nitakuhudumia pale, kwa maana bado kuna miaka mitano ya njaa, hivyo usije ukaingia katika uhitaji, wewe, nyumba yako, na yote uliyonayo.”
so will I sustain thee, there, for there are yet five years of famine, —lest thou come to poverty—thou and thy house and all who are thine.
12 Tazama, macho yenu yanaona, na macho ya Benjamini ndugu yangu, kwamba ni kinywa changu kinachoongea nanyi.
Now lo! your own eyes do see, and the eyes of my brother Benjamin, —that it is my own mouth, that doth speak unto you.
13 Mtamwambia baba yangu juu ya heshima yangu yote huku Misri na yote mliyoyaona. Mtaharakisha na kumleta baba yangu huku.”
As soon as ye have told my father all my honour in Egypt, and all that ye have seen, so soon shall ye hasten and bring down my father hither.
14 Akaikumbatia shingo ya Benjamini ndugu yake na kulia, na Benjamini akalia shongoni mwake.
Then fell he upon the neck of Benjamin his brother, and wept, —and Benjamin wept on his neck.
15 Akawabusu ndugu zake wote na kulia kwa ajili yao. Baada ya hayo ndugu zake wakaongea naye.
Then kissed he all his brethren, and wept upon them, —and, thereafter, his brethren spake with him.
16 Habari ya jambo hili ikasemwa katika nyumba ya Farao: “Ndugu zake Yusufu wamekuja.” Ikampendeza sana Farao na watumishi wake.
Now, the report, was heard by the house of Pharaoh, saying, The brethren of Joseph have come in, And it was good in the eyes of Pharaoh, and in the eyes of all his servants.
17 Farao akamwambia Yusufu, “Wambie ndugu zako, 'Fanyeni hivi: Wapakieni wanyama wenu na mwende katika nchi ya Kanaani.
So then Pharaoh said unto Joseph—Say unto thy brethren This, do, —lade your asses, and go enter into the land of Canaan;
18 Mchukueni baba yenu na nyumba zenu mnijie. Nami nitawapa mema ya nchi ya Misri, nanyi mtakula unono wa nchi.'
and fetch your father and your households and come in unto me, —that I may give you the best of the land of Egypt, and eat ye the fat of the land.
19 Basi mmeamriwa, 'Fanyeni hivi, chukueni mikokoteni kutoka Misri kwa ajili ya watoto wenu na kwa ajili ya wake zenu. Mchukueni baba yenu na kuja.
Thou, therefore command them, This, do ye, —Take you out of the land of Egypt, waggons for your little ones and for your wives, so shall ye bring your father and come in.
20 Msijari kuhusu mali zenu, kwani mema yote ya nchi ya Misri ni yenu.”
Your eye, moreover, let it not look with pity upon your goods, —for, the best of all the land of Egypt, is, yours.
21 Wana wa Israeli wakafanya hivyo. Yusufu akawapa mikokoteni, kwa kadili ya agizo la Farao, na akawapa mahitaji ya safari.
And the sons of Israel did so, and Joseph gave them waggons, at the bidding of Pharaoh, —and gave them provisions for the way:
22 Akawapa wote mavazi ya kubadilisha, lakini akampa Benjamini vipande mia tatu vya fedha na mavazi matano ya kubadilisha.
to all of them, gave he to each man changes of raiment, —but, to Benjamin, he gave three hundred pieces of silver, and five changes of raiment.
23 Akampelekea baba yake: punda kumi waliobeba mema ya Misri, punda majike kumi wamebeba nafaka, mikate, na mahitaji mengine kwa baba yake kwa ajili ya safari.
Moreover, to his father, sent he as followeth—ten he-asses, laden from the best of Egypt, —and ten she-asses laden with corn and bread and nourishing food for his father for the way.
24 Hivyo akawaruhusu ndugu zake nao wakaondoka. Akawambia, “Angalieni msijemkagombana njiani.”
Thus sent he forth his brethren and they departed, —and he said unto them, Do not fall out by the way.
25 Wakapanda kutoka Misri na kuja katika nchi ya Kanaani, kwa Yakobo baba yao.
And they went up out of Egypt, —and came into the land of Canaan, unto Jacob their father.
26 Wakamwambia “Yusufu bado yu hai, na ndiye mtawala juu ya nchi yote ya Misri.” Na moyo wake ulishikwa na ushangao, kwani hakuwaamini.
And they told him saying—Joseph: is, yet alive, yea, indeed, he, is ruler in all the land of Egypt. And his heart became faint, for he believed them not.
27 Wakamwambia maneno yote ya Yusufu aliyokuwa amewambia. Yakobo alipoona mikokoteni Yusufu aliyokuwa amepeleka kuwabeba, roho ya Yakobo baba yao ikafufuka.
So they spake unto him all the words of Joseph which he had spoken unto them h then saw he the waggons, which Joseph had sent to carry him, —and the spirit of Jacob their father revived.
28 Israeli akasema, “Inatosha. Yusufu mwanangu yu hai. Nitakwenda nikamwone kabla sijafa.”
And Israel said, Enough! Joseph my son is, yet alive, I must go and see him before I die!

< Mwanzo 45 >