< Mwanzo 45 >
1 Ndipo Yusufu hakuweza kujizuia mwenyewe mbele ya watumishi waliosimama kando yake. Akasema kwa sauti, “Kila mtu aondoke.” Hivyo hakuna mtumishi aliyesimama kando yake wakati Yusufu alipojitambulisha kwa ndugu zake.
Joseph could no longer refrain himself before many that stood by: whereupon he commanded that all should go out, and no stranger be present at their knowing one another.
2 Akalia kwa sauti, Wamisri wakasikia, na nyumba ya Farao wakasikia kuhusu hilo.
And he lifted up his voice with weeping, which the Egyptians and all the house of Pharao heard.
3 Yusufu akawambia ndugu zake, “Mimi ni Yusufu. Je baba yangu ni mzima bado? Ndugu zake hawakuweza kumjibu, kwani walitishwa na uwepo wake.
And he said to his brethren: I am Joseph: is my father yet living? His brethren could not answer him, being struck with exceeding great fear.
4 Kisha Yusufu akawambia ndugu zake, “Nikaribieni, tafadhari.” Nao wakasogea. Akawambia, “Mimi ni Yusufu ndugu yenu, mliyemwuza Misri.
And he said mildly to them: Come nearer to me. And when they were come near him, he said: I am Joseph, your brother, whom you sold into Egypt.
5 Lakini sasa msihuzunike au kukasirika miongoni mwenu kwamba mliniuza huku, kwani Mungu alinituma mbele yenu ili kutunza uhai.
Be not afraid, and let it not seem to you a hard case that you sold me into these countries: for God sent me before you into Egypt for your preservation.
6 Maana ni miaka miwili njaa imekuwa katika nchi, na bado kuna miaka mitano ambayo hakutakuwa na kulima wala kuvuna.
For it is two years since the famine began to be upon the land, and five years more remain, wherein there can be neither ploughing nor reaping.
7 Mungu alinituma mbele yenu kuwahifadhi kama masalia duniani, na kuwaweka hai kwa ukombozi mkuu.
And God sent me before, that you may be preserved upon the earth, and may have food to live.
8 Hivyo si ninyi mlionipeleka huku bali ni Mungu, na amenifanya baba kwa Farao, bwana wa nyumba yake yote, na mtawala wa nchi yote ya Misri.
Not by your counsel was I sent hither, but by the will of God: who hath made me as it were a father to Pharao, and lord of his whole house, and governor in all the land of Egypt.
9 Fanyeni haraka mwende kwa baba yangu na mmwambie, 'Hivi ndivyo asemavyo Yusufu mwanao, “Mungu amenifanya bwana kwa Wamisri wote. Shuka kwangu, usikawie.
Make haste, and go ye up to my father, and say to him: Thus saith thy son Joseph: God hath made me lord of the whole land of Egypt: come down to me, linger not.
10 Utaishi katika nchi ya Gosheni, nawe utakuwa karibu nami, wewe na watoto wako na watoto wa watoto wako, na kondoo wako na mbuzi wako, na yote uliyonayo.
And thou shalt dwell in the land of Gessen: and thou shalt be near me, thou and thy sons, and thy sons’ sons, thy sheep, and thy herds, and all things that thou hast.
11 Nami nitakuhudumia pale, kwa maana bado kuna miaka mitano ya njaa, hivyo usije ukaingia katika uhitaji, wewe, nyumba yako, na yote uliyonayo.”
And there I will feed thee, (for there are yet five years of famine remaining), lest both thou perish, and thy house, and all things that thou hast.
12 Tazama, macho yenu yanaona, na macho ya Benjamini ndugu yangu, kwamba ni kinywa changu kinachoongea nanyi.
Behold, your eyes, and the eyes of my brother Benjamin see that it is my mouth that speaketh to you.
13 Mtamwambia baba yangu juu ya heshima yangu yote huku Misri na yote mliyoyaona. Mtaharakisha na kumleta baba yangu huku.”
You shall tell my father of all my glory, and all things that you have seen in Egypt: make haste and bring him to me.
14 Akaikumbatia shingo ya Benjamini ndugu yake na kulia, na Benjamini akalia shongoni mwake.
And falling upon the neck of his brother Benjamin, he embraced him and wept: and Benjamin in like manner wept also on his neck.
15 Akawabusu ndugu zake wote na kulia kwa ajili yao. Baada ya hayo ndugu zake wakaongea naye.
And Joseph kissed all his brethren, and wept upon every one of them: after which they were emboldened to speak to him.
16 Habari ya jambo hili ikasemwa katika nyumba ya Farao: “Ndugu zake Yusufu wamekuja.” Ikampendeza sana Farao na watumishi wake.
And it was heard, and the fame was abroad in the king’s court: The brethren of Joseph are come: and Pharao with all his family was glad.
17 Farao akamwambia Yusufu, “Wambie ndugu zako, 'Fanyeni hivi: Wapakieni wanyama wenu na mwende katika nchi ya Kanaani.
And he spoke to Joseph that he should give orders to his brethren, saying: Load your beasts, and go into the land of Chanaan.
18 Mchukueni baba yenu na nyumba zenu mnijie. Nami nitawapa mema ya nchi ya Misri, nanyi mtakula unono wa nchi.'
And bring away from thence your father and kindred, and come to me: and I will give you all the good things of Egypt, that you may eat the marrow of the land.
19 Basi mmeamriwa, 'Fanyeni hivi, chukueni mikokoteni kutoka Misri kwa ajili ya watoto wenu na kwa ajili ya wake zenu. Mchukueni baba yenu na kuja.
Give orders also that they take wagons out of the land of Egypt, for the carriage of their children and their wives: and say: Take up your father, and make haste to come with all speed:
20 Msijari kuhusu mali zenu, kwani mema yote ya nchi ya Misri ni yenu.”
And leave nothing of your household stuff: for all the riches of Egypt shall be yours.
21 Wana wa Israeli wakafanya hivyo. Yusufu akawapa mikokoteni, kwa kadili ya agizo la Farao, na akawapa mahitaji ya safari.
And the sons of Israel did as they were bid. And Joseph gave them wagons according to Pharao’s commandment: and provisions for the way.
22 Akawapa wote mavazi ya kubadilisha, lakini akampa Benjamini vipande mia tatu vya fedha na mavazi matano ya kubadilisha.
He ordered also to be brought out for every one of them two robes: but to Benjamin he gave three hundred pieces of silver with five robes of the best:
23 Akampelekea baba yake: punda kumi waliobeba mema ya Misri, punda majike kumi wamebeba nafaka, mikate, na mahitaji mengine kwa baba yake kwa ajili ya safari.
Sending to his father as much money and raiment, adding besides ten he asses to carry off all the riches of Egypt, and as many she asses, carrying wheat and bread for the journey.
24 Hivyo akawaruhusu ndugu zake nao wakaondoka. Akawambia, “Angalieni msijemkagombana njiani.”
So he sent away his brethren, and at their departing said to them: Be not angry in the way.
25 Wakapanda kutoka Misri na kuja katika nchi ya Kanaani, kwa Yakobo baba yao.
And they went up out of Egypt, and came into the land of Chanaan to their father Jacob.
26 Wakamwambia “Yusufu bado yu hai, na ndiye mtawala juu ya nchi yote ya Misri.” Na moyo wake ulishikwa na ushangao, kwani hakuwaamini.
And they told him, saying: Joseph thy son is living: and he is ruler in all the land of Egypt. Which when Jacob heard, he awaked as it were out of a deep sleep, yet did not believe them.
27 Wakamwambia maneno yote ya Yusufu aliyokuwa amewambia. Yakobo alipoona mikokoteni Yusufu aliyokuwa amepeleka kuwabeba, roho ya Yakobo baba yao ikafufuka.
They, on the other side, told the whole order of the thing. And when he saw the wagons and all that he had sent his spirit revived,
28 Israeli akasema, “Inatosha. Yusufu mwanangu yu hai. Nitakwenda nikamwone kabla sijafa.”
And he said: It is enough for me, if Joseph my son be yet living: I will go and see him before I die.