< Mwanzo 45 >

1 Ndipo Yusufu hakuweza kujizuia mwenyewe mbele ya watumishi waliosimama kando yake. Akasema kwa sauti, “Kila mtu aondoke.” Hivyo hakuna mtumishi aliyesimama kando yake wakati Yusufu alipojitambulisha kwa ndugu zake.
Joseph was unable to restrain himself any longer, standing before so many. Therefore, he instructed that all should go outside, and that no stranger should be among them as they recognized one another.
2 Akalia kwa sauti, Wamisri wakasikia, na nyumba ya Farao wakasikia kuhusu hilo.
And he lifted up his voice with weeping, which the Egyptians heard, along with the entire house of Pharaoh.
3 Yusufu akawambia ndugu zake, “Mimi ni Yusufu. Je baba yangu ni mzima bado? Ndugu zake hawakuweza kumjibu, kwani walitishwa na uwepo wake.
And he said to his brothers: “I am Joseph. Is my father still alive?” His brothers were unable to respond, being terrified by a very great fear.
4 Kisha Yusufu akawambia ndugu zake, “Nikaribieni, tafadhari.” Nao wakasogea. Akawambia, “Mimi ni Yusufu ndugu yenu, mliyemwuza Misri.
And he said to them mildly, “Approach toward me.” And when they had approached close by, he said: “I am Joseph, your brother, whom you sold into Egypt.
5 Lakini sasa msihuzunike au kukasirika miongoni mwenu kwamba mliniuza huku, kwani Mungu alinituma mbele yenu ili kutunza uhai.
Do not be afraid, and let it not seem to you to be a hardship that you sold me into these regions. For God sent me before you into Egypt for your salvation.
6 Maana ni miaka miwili njaa imekuwa katika nchi, na bado kuna miaka mitano ambayo hakutakuwa na kulima wala kuvuna.
For it is two years since the famine began to be upon the land, and five years more remain, in which there can be neither plowing, nor reaping.
7 Mungu alinituma mbele yenu kuwahifadhi kama masalia duniani, na kuwaweka hai kwa ukombozi mkuu.
And God sent me ahead, so that you may be preserved upon the earth, and so that you would be able to have food in order to live.
8 Hivyo si ninyi mlionipeleka huku bali ni Mungu, na amenifanya baba kwa Farao, bwana wa nyumba yake yote, na mtawala wa nchi yote ya Misri.
I was sent here, not by your counsel, but by the will of God. He has caused me to be like a father to Pharaoh, and to be the lord of his entire house, as well as governor throughout all the land of Egypt.
9 Fanyeni haraka mwende kwa baba yangu na mmwambie, 'Hivi ndivyo asemavyo Yusufu mwanao, “Mungu amenifanya bwana kwa Wamisri wote. Shuka kwangu, usikawie.
Hurry, and go up to my father, and say to him: ‘Your son Joseph commands this: God has caused me to be lord of the entire land of Egypt. Come down to me, do not delay,
10 Utaishi katika nchi ya Gosheni, nawe utakuwa karibu nami, wewe na watoto wako na watoto wa watoto wako, na kondoo wako na mbuzi wako, na yote uliyonayo.
and you will live in the land of Goshen. And you will be next to me, you and your sons and the sons of your sons, your sheep and your herds, and all that you possess.
11 Nami nitakuhudumia pale, kwa maana bado kuna miaka mitano ya njaa, hivyo usije ukaingia katika uhitaji, wewe, nyumba yako, na yote uliyonayo.”
And there I will pasture you, (for there are still five years of famine remaining) lest both you and your house perish, along with all that you possess.’
12 Tazama, macho yenu yanaona, na macho ya Benjamini ndugu yangu, kwamba ni kinywa changu kinachoongea nanyi.
Behold, your eyes and the eyes of my brother Benjamin can see that it is my mouth speaking to you.
13 Mtamwambia baba yangu juu ya heshima yangu yote huku Misri na yote mliyoyaona. Mtaharakisha na kumleta baba yangu huku.”
You will report to my father about all my glory, and about all that you have seen in Egypt. Hurry, and bring him to me.”
14 Akaikumbatia shingo ya Benjamini ndugu yake na kulia, na Benjamini akalia shongoni mwake.
And then falling upon the neck of his brother Benjamin, he embraced him and wept. And likewise, Benjamin wept at the same time on his neck.
15 Akawabusu ndugu zake wote na kulia kwa ajili yao. Baada ya hayo ndugu zake wakaongea naye.
And Joseph kissed all his brothers, and he cried over each one. After this, they were emboldened to speak to him.
16 Habari ya jambo hili ikasemwa katika nyumba ya Farao: “Ndugu zake Yusufu wamekuja.” Ikampendeza sana Farao na watumishi wake.
And it was overheard, and the news spread by word throughout the king’s court. The brothers of Joseph had arrived, and Pharaoh was gladdened along with all his family.
17 Farao akamwambia Yusufu, “Wambie ndugu zako, 'Fanyeni hivi: Wapakieni wanyama wenu na mwende katika nchi ya Kanaani.
And he told Joseph that he should command his brothers, saying: “‘Burden your beasts, and go into the land of Canaan,
18 Mchukueni baba yenu na nyumba zenu mnijie. Nami nitawapa mema ya nchi ya Misri, nanyi mtakula unono wa nchi.'
and take from there your father and kindred, and come to me. And I will give you all the good things of Egypt, so that you may eat from the marrow of the land.’”
19 Basi mmeamriwa, 'Fanyeni hivi, chukueni mikokoteni kutoka Misri kwa ajili ya watoto wenu na kwa ajili ya wake zenu. Mchukueni baba yenu na kuja.
“And you may even instruct that they take wagons from the land of Egypt, in order to transport their little ones as well as their wives. And say: ‘Take your father, and come quickly, as soon as possible.
20 Msijari kuhusu mali zenu, kwani mema yote ya nchi ya Misri ni yenu.”
You need not give up anything from your household, for all the riches of Egypt will be yours.’”
21 Wana wa Israeli wakafanya hivyo. Yusufu akawapa mikokoteni, kwa kadili ya agizo la Farao, na akawapa mahitaji ya safari.
And the sons of Israel did just as they were commanded. And Joseph gave them wagons, according to the command of Pharaoh, and provisions for the journey.
22 Akawapa wote mavazi ya kubadilisha, lakini akampa Benjamini vipande mia tatu vya fedha na mavazi matano ya kubadilisha.
Likewise, he ordered two robes for each of them to be brought. Yet truly, to Benjamin he gave three hundred pieces of silver along with five of the best robes.
23 Akampelekea baba yake: punda kumi waliobeba mema ya Misri, punda majike kumi wamebeba nafaka, mikate, na mahitaji mengine kwa baba yake kwa ajili ya safari.
And he sent just as much money and clothing to his father, adding also ten male donkeys, with which to transport all the riches of Egypt, and as many female donkeys, carrying wheat and bread for the journey.
24 Hivyo akawaruhusu ndugu zake nao wakaondoka. Akawambia, “Angalieni msijemkagombana njiani.”
Thus he sent away his brothers, and as they set out he said, “Do not become angry on the way.”
25 Wakapanda kutoka Misri na kuja katika nchi ya Kanaani, kwa Yakobo baba yao.
And they ascended out of Egypt, and they arrived in the land of Canaan, to their father Jacob.
26 Wakamwambia “Yusufu bado yu hai, na ndiye mtawala juu ya nchi yote ya Misri.” Na moyo wake ulishikwa na ushangao, kwani hakuwaamini.
And they reported to him, saying: “Your son Joseph is alive, and he is ruler throughout all the land of Egypt. When Jacob heard this, he was stirred up, as if from a deep sleep, yet he did not believe them.
27 Wakamwambia maneno yote ya Yusufu aliyokuwa amewambia. Yakobo alipoona mikokoteni Yusufu aliyokuwa amepeleka kuwabeba, roho ya Yakobo baba yao ikafufuka.
To the contrary, they explained the entire matter in order. And when he had seen the wagons, and all that he had sent, his spirit revived,
28 Israeli akasema, “Inatosha. Yusufu mwanangu yu hai. Nitakwenda nikamwone kabla sijafa.”
and he said: “It is enough for me, if my son Joseph is still alive. I will go and see him before I die.”

< Mwanzo 45 >