< Mwanzo 44 >

1 Yusufu akamwamru msimamizi wa nyumba yake, akisema, “Jaza magunia ya watu hawa kwa chakula, kiasi wawezacho kubeba, na uweke pesa ya kila mtu katika mdomo wa gunia lake.
Il donna cet ordre à l'intendant de sa maison: « Remplissez de nourriture les sacs des hommes, autant qu'ils peuvent en porter, et mettez l'argent de chacun dans l'ouverture de son sac.
2 Uweke kikombe changu, cha fedha, katika mdomo wa gunia la mdogo, na pesa yake ya chakula pia.” Msimamizi akafanya kama Yusufu alivyosema.
Mets ma coupe, la coupe d'argent, dans l'ouverture du sac du plus jeune, avec son argent. » Il fit selon la parole que Joseph avait dite.
3 Kukapambazuka asubuhi, na wale watu wakaruhusiwa kuondoka, wao na punda zao.
Dès que le matin se leva, les hommes partirent, eux et leurs ânes.
4 Walipokuwa wametoka mjini lakini hawajafika mbali, Yusufu akamwambia msimamizi wa nyumba yake, “Inuka, uwafuatie wale watu, na utakapowapata, wambie, 'Kwa nini mmelipa uovu badala ya mema?
Lorsqu'ils sortirent de la ville et qu'ils ne furent pas encore loin, Joseph dit à son intendant: « Monte, suis les hommes. Quand tu les auras rattrapés, demande-leur: Pourquoi avez-vous rendu le mal pour le bien?
5 Je hiki siyo kikombe ambacho bwana wangu hukinywea, na kikombe akitumiacho kwa uaguzi? Mmefanya vibaya, kwa jambo hili mlilolifanya.”
N'est-ce pas là ce que boit mon seigneur et ce par quoi il devine? Vous avez fait le mal en agissant ainsi ».
6 Msimamizi wa nyumba akawapata na kuwambia maneno haya.
Il les rattrapa et leur adressa ces paroles.
7 Wakasema, “Kwa nini bwana wetu anasema maneno kama haya? Na iwe mbali na watumishi wako kwamba wanaweza kufanya jambo hili.
Ils lui dirent: « Pourquoi mon seigneur tient-il de tels propos? Loin de tes serviteurs l'idée de faire une telle chose!
8 Tazama, pesa tulizozikuta katika midomo ya magunia yetu, tulizileta kwako kutoka katika nchi ya Kanaani. Ni kwa jinsi gani basi tunaweza kuiba katika nyumba ya bwana wako fedha au dhahabu?
Voici, l'argent que nous avons trouvé dans la bouche de nos sacs, nous te l'avons rapporté du pays de Canaan. Comment donc voler de l'argent ou de l'or dans la maison de ton seigneur?
9 Yeyote kitakayeonekana kwake miongoni mwa watumishi wako, atakufa, nasi sote tutakuwa watumwa wa bwana wangu.”
Chez celui de tes serviteurs chez qui on le trouvera, qu'il meure, et nous aussi nous serons les esclaves de mon seigneur. »
10 Msimamizi akasema, “Basi na iwe kwa kadili ya maneno yenu. Yeye ambaye kikombe kitaonekana kwake atakuwa mtumwa wangu, nanyi wengine mtakuwa bila hatia.”
Il dit: « Qu'il en soit maintenant ainsi selon vos paroles. Celui chez qui elle sera trouvée sera mon esclave; et toi, tu seras irréprochable. »
11 Kisha kila mtu akaharakisha na kulishusha gunia lake chini. na kila mtu akalifungua gunia lake.
Ils se hâtèrent alors de descendre leur sac à terre, et chacun ouvrit son sac.
12 Msimamizi akatafuta. akaanza na mkubwa wa wote na kumaliza kwa mdogo wa wote, na kikombe kikaonekana katika gunia la Benjamini.
Il chercha, en commençant par le plus âgé et en terminant par le plus jeune. La coupe fut trouvée dans le sac de Benjamin.
13 Wakararua mavazi yao. Kila mtu akapakia juu ya punda wake nao wakarudi mjini.
Puis ils déchirèrent leurs vêtements, chargèrent chacun leur âne et retournèrent à la ville.
14 Yuda na ndugu zake wakaja katika nyumba ya Yusufu. Bado alikuwepo pale, nao wakainama mbele zake hata chini.
Juda et ses frères arrivèrent à la maison de Joseph, et il était encore là. Ils se jetèrent à terre devant lui.
15 Yusufu akawambia, “Je ni nini hili mlilolifanya? Je hamjui kwamba mtu kama mimi anafanya uaguzi.
Joseph leur dit: « Quelle est cette action que vous avez commise? Ne savez-vous pas qu'un homme tel que moi peut effectivement faire de la divination? ».
16 Yuda akasema, “Je tunaweza kumwambia nini bwana wangu? Tuseme nini? au ni jinsi gani twaweza kujithibitisha wenyewe? Mungu ameona uovu wa watumishi wako. Tazama, sisi ni watumwa wa bwana wangu, wote sisi na yule ambaye kikombe kimeonekana mkononi mwake.”
Juda dit: « Que dirons-nous à mon seigneur? Que dirons-nous? Comment allons-nous nous disculper? Dieu a découvert l'iniquité de tes serviteurs. Voici, nous sommes les esclaves de mon seigneur, nous et celui dans la main duquel se trouve la coupe. »
17 Yusufu akasema, “Na iwe mbali nami kwamba naweza kufanya hivyo. Mtu ambaye kikombe kimeonekana mkononi mwake, huyu ndiye atakuwa mtumwa wangu, lakini ninyi wengine, nendeni kwa amani kwa baba yenu.”
Il répondit: « Loin de moi l'idée de faire cela. L'homme dans la main duquel se trouve la coupe sera mon esclave; quant à toi, monte en paix vers ton père. »
18 Ndipo Yuda alipomkaribia na kusema, “Bwana wangu, tafadhari mwache mtumishi wako aseme neno katika masikio ya bwana wangu, na usiziache hasira zako kuwaka dhidi ya mtumishi wako, kwani wewe ni kama Farao.
Alors Juda s'approcha de lui, et dit: « Oh, mon seigneur, permets à ton serviteur de dire une parole aux oreilles de mon seigneur, et ne laisse pas ta colère s'enflammer contre ton serviteur, car tu es comme Pharaon.
19 Bwana wangu aliwauliza watumishi wake, kusema, Je mnaye baba au ndugu?'
Mon seigneur a demandé à ses serviteurs: « Avez-vous un père ou un frère? »
20 Nasi tukamwambia bwana wangu, 'Tunaye baba, ni mzee, na mwana wa uzee wake, ni mdogo. Na ndugu yake alishakufa, na yeye peke yake ndiye amebaki kwa mama yake, na baba yake anampenda.'
Nous avons répondu à mon seigneur: « Nous avons un père, un vieillard, et un enfant de sa vieillesse, un petit garçon; son frère est mort, et il reste seul de sa mère; et son père l'aime.
21 Nawe ukawambia matumishi wako, 'Mleteni ili nimwone.'
Tu as dit à tes serviteurs: « Faites-le descendre vers moi, afin que je pose mes yeux sur lui.
22 Nasi tukamwambia bwana wangu, 'Kijana hawezi kumwacha babaye. Kwani akimwacha babaye baba yake angekufa.'
Nous avons dit à mon seigneur: « Le garçon ne peut pas quitter son père, car s'il le quittait, son père mourrait. »
23 Na ukawambia watumishi wako, 'Mdogo wenu asipokuja pamoja nanyi, hamtauona uso wangu tena.'
Tu as dit à tes serviteurs: « Si ton plus jeune frère ne descend pas avec vous, vous ne verrez plus ma face.
24 Na ikawa tulipokwenda kwa mtumishi wako baba yangu, tulimwambia maneno ya bwana wangu.
Lorsque nous sommes montés vers ton serviteur, mon père, nous lui avons rapporté les paroles de mon seigneur.
25 Na baba yetu akasema, Nendeni tena, mkatununulie chakula.'
Notre père nous dit: « Retourne acheter un peu de nourriture.
26 Nasi tukasema, “Hatuwezi kushuka. Ikiwa mdogo wetu atakuwa nasi, ndipo tutakaposhuka, kwani hatuwezi kuuona uso wa mtu yule mdogo wetu asipokuwa pamoja nasi.'
Nous avons répondu: « Nous ne pouvons pas descendre. Si notre plus jeune frère est avec nous, nous descendrons, car nous ne verrons peut-être pas le visage de cet homme, à moins que notre plus jeune frère ne soit avec nous.
27 Mtumishi wako baba yetu akatwambia, 'Mnajua kwamba mke wangu alinizalia wana wawili.
Ton serviteur, mon père, nous a dit: « Vous savez que ma femme m'a enfanté deux fils.
28 Na mmoja akatoka kwangu nami nikasema, “Bila shaka ameraruliwa vipande, na tangu hapo sijamwona.”
L'un d'eux est sorti de chez moi, et j'ai dit: « Certainement, il est déchiré en morceaux »; et je ne l'ai pas revu depuis.
29 Nanyi mkimchukua huyu naye kutoka kwangu mabaya yanaweza kumpata, mtashusha mvi zangu kwa kaburini kwa huzuni. (Sheol h7585)
Si tu m'enlèves aussi celui-ci, et qu'il lui arrive malheur, tu feras descendre mes cheveux blancs avec tristesse au séjour des morts'. (Sheol h7585)
30 Kwa hiyo, basi, nitapokuja kwa mtumishi wako baba yangu, na kijana hayupo nasi, kwa kuwa uhai wake umefungamanishwa katika uhai wa kijana,
Maintenant, quand j'arriverai chez ton serviteur, mon père, et que le garçon ne sera pas avec nous, puisque sa vie est liée à celle du garçon,
31 itakuwa, atakapoona kwamba kijana hayupo nasi atakufa. Na watumishi wako watazishusha mvi za mtumishi wako baba yetu kaburini kwa masikitiko. (Sheol h7585)
il arrivera, quand il verra que le garçon n'est plus, qu'il mourra. Tes serviteurs feront descendre avec douleur au séjour des morts les cheveux blancs de ton serviteur, notre père. (Sheol h7585)
32 Kwani mtumishi wako alikuwa mdhamini wa kijana kwa baba yangu na alisema, 'Ikiwa sitamleta kwako, ndipo nitakapokuwa mwenye hatia kwa baba yangu daima.”
Car ton serviteur s'est porté garant de l'enfant auprès de mon père, en disant: « Si je ne te l'amène pas, c'est moi qui en porterai la responsabilité auprès de mon père pour toujours ».
33 Kwa hiyo sasa, tafadhari mwache mtumishi wake akae kama mtumwa kwa bwana wangu badala ya kijana, na umwache kijana aende na ndugu zake.
Maintenant donc, que ton serviteur reste à la place du garçon, esclave de mon seigneur, et que le garçon monte avec ses frères.
34 Kwa maana nitakwenda jinsi gani kwa baba yangu ikiwa kijana hayupo nami? Ninaogopa kuona mabaya yatakayompata baba yangu.”
Car comment monterai-je vers mon père, si le garçon n'est pas avec moi? de peur que je ne voie le malheur qui frappera mon père. »

< Mwanzo 44 >