< Mwanzo 43 >
1 Njaa ilikuwa kali katika nchi.
La famine s’appesantissait sur le pays.
2 Ikawa walipokuwa wametumia chakula chote walichokitoa Misri, baba yao akawambia, “Nendeni tena; mtununulie chakula.”
Quand ils eurent fini de manger le blé qu’ils avaient apporté d’Égypte, leur père leur dit: « Retournez nous acheter un peu de vivres. »
3 Yuda akamwambia, “Yule mtu alituonya kwa ukali, 'Hamtauona uso wangu ndugu yenu asipokuwa nanyi.'
Juda lui répondit: « Cet homme nous a fait cette déclaration formelle: Vous ne verrez point ma face que votre frère ne soit avec vous.
4 Ikiwa utamtuma ndugu yetu pamoja nasi, tutashuka na kuwanunulia chakula.
Si donc tu laisses venir notre frère avec nous, nous descendrons et nous t’achèterons des vivres.
5 Lakini usipompeleka, hatutashuka. Kwa maana yule mtu alitwambia, 'Hamtauona uso wangu ndugu yenu asipokuwa nanyi.”
Mais si tu ne le laisses pas venir, nous ne descendrons point; car cet homme nous a dit: Vous ne verrez pas ma face que votre frère ne soit avec vous. »
6 Israeli akawambia, “Kwa nini mlinitendea mimi vibaya hivyo kwa kumwambia mtu huyo kwamba mnaye ndugu mwingine?”
Et Israël dit: « Pourquoi m’avez-vous causé cette peine, de dire à cet homme que vous aviez encore un frère? »
7 Wakasema, “Yule mtu alituuliza habari zetu na familia yetu kwa kina. Akasema, 'Je baba yenu bado yuko hai? Je mnaye ndugu mwingine?'Tukamjibu kulingana na maswali haya. Tungejuaje kwamba angetwambia, 'Mleteni ndugu yenu?”
Ils dirent: « Cet homme nous a adressé beaucoup de questions sur nous et sur notre famille, en disant: Votre père vit-il encore? Avez-vous un autre frère? Et nous avons répondu selon ces questions. Pouvions-nous savoir qu’il dirait: Faites descendre votre frère? »
8 Yuda akamwambia Israeli baba yake, “Mtume kijana pamoja nami. Tutainuka na kwenda ili kwamba tuishi tusife, wote sisi, wewe, na hata watoto wetu.
Et Juda dit à Israël, son père: « Laisse partir l’enfant avec moi, afin que nous nous levions et nous mettions en route, et nous vivrons et ne mourrons point, nous, toi et nos petits enfants.
9 Mimi nitakuwa mdhamini wake. Utaniwajibisha mimi. Kama nisipomleta na kumweka mbele yako, basi nibebe lawama daima.
C’est moi qui réponds de lui, tu le redemanderas de ma main. Si je ne le ramène pas auprès de toi, si je ne le mets pas devant toi, je serai coupable envers toi à tout jamais.
10 Kwani kama tusingekawia, bila shaka hata sasa tungekuwa tumekwisha rudi mara ya pili.”
Car si nous n’avions pas tant tardé, nous serions maintenant deux fois de retour. »
11 Israeli baba yao akawambia, “Kama ni hivyo, basi fanyeni hivi. Chukueni baadhi ya mazao mazuri ya nchi katika mifuko yenu. Mchukulieni yule mtu zawadi: baadhi ya malhamu, asali, viungo na manemane, jozi na lozi.
Israël, leur père, leur dit: « Eh bien, puisqu’il le faut, faites ceci: Prenez dans vos vaisseaux des meilleures productions du pays et portez à cet homme un présent: un peu de baume et un peu de miel, de l’astragale, du ladanum, des pistaches et des amandes.
12 Chukueni pesa mara mbili mikononi mwenu. Pesa iliyorudishwa katika magunia yenu, muichukue tena katika mikono yenu. Pengine walikosea.
Prenez dans vos mains de l’argent en double, et reportez celui qui a été mis à l’entrée de vos sacs, peut-être par erreur.
13 Mchukueni ndugu yenu pia. Inukeni na mwende tena kwa mtu yule.
Prenez votre frère, levez-vous et retournez vers cet homme.
14 Mungu Mwenyezi na awape kuona rehema mbele ya huyo mtu, hivyo kwamba awafungulie ndugu yenu mwingine na Benjamini. Kama nikipotelewa na watoto, nimepotelewa.”
Que le Dieu tout-puissant vous fasse trouver grâce devant cet homme, afin qu’il laisse revenir avec vous votre autre frère, ainsi que Benjamin! Pour moi, si je dois être privé de mes enfants, que j’en sois privé! »
15 Watu wale wakachukua zawadi hii, na katika mikono yao wakachukua mara mbili ya kiasi cha pesa, pamoja na Benjamini. Wakaamka na kushuka Misri na kusimama mbele ya Yusufu.
Les hommes prirent ce présent, et ils prirent dans leurs mains de l’argent au double, ainsi que Benjamin; et, s’étant levés, ils descendirent en Égypte et se présentèrent devant Joseph.
16 Yusufu alipomwona Benjamini akiwa nao, akamwambia mtunzaji wa nyumba yake, “Walete watu hao ndani ya nyumba, chinja mnyama na umwandae, kwani watu hawa watakula chakula cha mchana pamoja nami.”
Dès que Joseph vit Benjamin avec eux, il dit à son intendant: « Fais entrer ces gens dans la maison, tue des victimes et apprête un repas, car ces gens mangeront avec moi à midi. »
17 Mtunzaji wa nyumba akafanya kama Yusufu alivyosema. Akawaleta wale watu nyumbani kwa Yusufu.
Cet homme fit ce que Joseph avait ordonné, et il conduisit ces gens dans la maison de Joseph.
18 Wale ndugu wakaogopa kwa vile walivyoletwa katika nyumba ya Yusufu. Wakasema, “Ni kwa sababu ya pesa iliyorudishwa katika magunia yetu mara ya kwanza tulipoletwa ndani, kwamba atafute nafasi kinyume chetu. Kwamba aweze kutukamata na kutuchukua kama watumwa, na kuchukua punda wetu.” Wakamsogelea mtunzaji wa nyumba ya Yusufu,
Pendant qu’on les conduisait à la maison de Joseph, les hommes eurent peur, et ils dirent: « C’est à cause de l’argent rapporté l’autre fois dans nos sacs qu’on nous emmène; c’est pour nous assaillir, tomber sur nous, nous prendre comme esclaves avec nos ânes. »
19 nao wakaongea naye mlangoni mwa nyumba,
S’étant approchés de l’intendant de la maison de Joseph, ils lui adressèrent la parole, à l’entrée de la maison,
20 wakisema, “Bwana wangu, tulikuja mara ya kwanza kununua chakula.
en disant: « Pardon, mon seigneur. Nous sommes déjà descendus une fois pour acheter des vivres.
21 Ikawa, tulipofika katika eneo la kupumzikia, tukafungua magunia yetu, na, tazama, pesa ya kila mtu ilikuwa katika gunia lake, pesa yetu kwa kiasi kamili. Tumeileta katika mikono yetu.
Au retour, quand nous arrivâmes à l’endroit où nous devions passer la nuit, nous avons ouvert nos sacs, et voici, l’argent de chacun était à l’entrée de son sac, notre argent selon son poids: nous le rapportons avec nous;
22 Tumekuja na pesa nyingine pia mikonon mwetu ili kununua chakula. Hatujui aliyeziweka pesa katika magunia yetu.”
et en même temps nous avons apporté d’autre argent pour acheter des vivres. Nous ne savons pas qui a mis notre argent dans nos sacs. »
23 Mtunzaji wa nyumba akasema, “Amani iwe kwenu, msiogope. Mungu wenu na Mungu wa baba yenu ndiye aliyeweka pesa katika magunia yenu. Nilipokea pesa yenu.” Kisha mtunzaji wa nyumba akamleta Simoni kwao.
Il leur dit: « Que la paix soit avec vous! Ne craignez rien. C’est votre Dieu, le Dieu de votre père, qui vous a donné un trésor dans vos sacs. Votre argent m’a été remis. » Et il leur amena Siméon.
24 Msimamizi wa nyumba akawapeleka watu hao katika nyumba ya Yusufu. Akawapa maji, nao wakaosha miguu yao. Akawalisha punda wao.
Cet homme, les ayant fait entrer dans la maison de Joseph, leur donna de l’eau et ils se lavèrent les pieds; il donna aussi du fourrage à leurs ânes.
25 Wakaandaa zawadi kwa ajili ya Yusufu aliyekuwa akija mchana, kwani walikuwa wamesikia kwamba watakula pale.
Ils préparèrent leur présent, en attendant que Joseph vint à midi; car on leur avait annoncé qu’ils mangeraient chez lui.
26 Yusufu alipokuja nyumbani, wakaleta nyumbani zawadi iliyokuwa mikononi mwao, nao wakainama mbele yake hata chini.
Quand Joseph fut arrivé chez lui, ils lui apportèrent dans la maison le présent qu’ils avaient dans la main, et se prosternèrent par terre devant lui.
27 Akawauliza juu ya hali zao na kusema,”Je baba yenu hajambo, yule mzee mliyemnena? Je bado yu hai?”
Il leur demanda comment ils se portaient, puis il dit: « Votre vieux père, dont vous avez parlé, est-il en bonne santé? vit-il encore? »
28 Wakasema, “Mtumishi wako baba yetu hajambo. Na bado yu hai” Wakajinyenyekeza na kuinama chini.
Ils répondirent: « Ton serviteur, notre père, est en bonne santé; il vit encore »; et ils s’inclinèrent et se prosternèrent.
29 Alipoinua macho yake akamwona Benjamini ndugu yake, mwana wa mamaye, naye akasema, “Je huyu ndiye mdogo wenu mliyemsema?” Na kisha akasema, “Mungu na awe mwenye neema kwako, mwanangu.”
Joseph leva les yeux, et il vit Benjamin, son frère, fils de sa mère; il dit: « Est-ce là votre jeune frère dont vous m’avez parlé? » Et il dit: « Que Dieu te soit favorable, mon fils! »
30 Yusufu akaharakisha kutoka chumbani, kwani aliguswa sana kuhusu nduguye. Akatafuta mahali pa kulia. Akaingia chumbani mwake na kulia umo.
Alors, en toute hâte, car ses entrailles étaient émues pour son frère, Joseph chercha un endroit pour pleurer; il entra dans sa chambre et il y pleura.
31 Akaosha uso wake na kutoka nje. Akajizuia mwenyewe, akasema, “karibuni chakula.”
Après s’être lavé le visage, il sortit et, faisant des efforts pour se contenir, il dit: « Servez à manger. »
32 Watumishi wakamhudumia Yusufu peke yake na wale ndugu peke yao. Wamisri pale wakala pamoja naye peke yao kwa sababu Wamisri hawakuweza kula mkate na Waebrania, kwani hilo ni chukizo kwa Wamisri.
On le servit à part, et ses frères à part, à part aussi les Égyptiens qui mangeaient avec lui, car les Égyptiens ne peuvent prendre leurs repas avec les Hébreux: c’est une abomination pour les Égyptiens.
33 Wale ndugu wakakaa mbele yake, mzaliwa wa kwanza kwa kulingana na haki yake ya uzaliwa, na mdogo kulingana na ujana wake. Wale watu wakashangaa wote.
Les frères de Joseph s’assirent devant lui, le premier-né selon son droit d’aînesse, et le plus jeune selon son âge; et ils se regardaient les uns les autres avec étonnement.
34 Yusufu akapeleka sehemu kwao kutoka katika chakula kilichokuwa mbele yake. Lakini sehemu ya Benjamini ilikuwa mara tano zaidi ya kila ndugu zake. Wakanywa na wakamfurahia.
Il leur fit porter des portions de devant lui, et la portion de Benjamin était cinq fois plus forte que les portions d’eux tous. Ils burent joyeusement avec lui.