< Mwanzo 4 >

1 Mwanume akalala na Hawa mke wake. Akabeba mimba na akamzaa Kaini. Akasema, “nimezaa mwanaume kwa msaada wa Yahwe.”
Adam je spoznal svojo ženo Evo in ta je spočela ter rodila Kajna in rekla: »Dobila sem človeka od Gospoda.«
2 Kisha akazaa ndugu yake Habili. Sasa Habili akawa mchungaji, lakini Kaini alilima udongo.
In ponovno je rodila njegovega brata Abela. In Abel je bil čuvaj ovc, toda Kajn je bil orač tal.
3 Ikawa kwamba baada ya muda Kaini alileta sehemu ya mazao ya ardhi kama sadaka kwa Yahwe.
Tekom časa se je pripetilo, da je Kajn od sadu tal prinesel daritev Gospodu.
4 Habili pia, alileta sehemu ya wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona. Yahwe akamkubali Habili pamoja na sadaka yake,
In tudi Abel je prinesel prvence od svojega tropa in od njihove tolšče. In Gospod je imel spoštovanje do Abela in njegove daritve,
5 lakini Kaini pamoja na sadaka yake Mungu hakuikubali. Kwa hiyo Kaini alikasirika sana, na uso wake ukakunjamana.
toda do Kajna in njegove daritve [pa] ni imel spoštovanja. In Kajn je bil zelo ogorčen in njegovo obličje je upadlo.
6 Yahwe akamwambia Kaini, “kwa nini umekasirika na kwa nini uso wako umekunjamana?
Gospod je rekel Kajnu: »Zakaj si ogorčen? In zakaj je tvoje obličje upadlo?
7 Kama ukifanya vema, je hutapata kibali? lakini kama hutafanya lilio jema, dhambi iko inakuotea mlangoni na inatamani kukutawala, lakini inakupasa uishinde.
Če delaš dobro ali ne boš sprejet? Če pa ne delaš dobro, greh leži pri vratih. Njegovo poželenje naj bo k tebi, ti pa boš vladal nad njim.«
8 Kaini akamwambia Habili ndugu yake. Hata wakati walipokuwa shambani, Kaini aliinuka dhidi ya Habili ndugu yake na akamuua. (Katika tafsiri za kale zinasema, Kaini alimwambia Habili ndugu yake, “twende mashambani.” Na wakati walipokuwa shambani, Kaini alimuinukia Habili ndugu yake na kumuua).
Kajn je govoril s svojim bratom Abelom, in ko sta bila na polju, se je pripetilo, da se je Kajn dvignil zoper svojega brata Abela in ga ubil.
9 Kisha Yahwe akamuuliza Kaini, “Ndugu yako Habili yuko wapi?” Akasema, “sijui. Je mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?”
Gospod je rekel Kajnu: »Kje je tvoj brat, Abel?« On pa je rekel: »Ne vem. Sem mar jaz čuvaj svojega brata?«
10 Yahwe akasema, “umefanya nini? damu ya ndugu yako inaniita mimi kutokea ardhini.
Rekel je: »Kaj si storil? Glas krvi tvojega brata iz tal vpije k meni.
11 Na sasa umelaaniwa wewe kutoka ardhi ambayo imefungua kinywa chake kupokea damu ya ndugu yako kutoka mikononi mwako.
Sedaj si preklet pred zemljo, ki je odprla svoja usta, da iz tvoje roke sprejme kri tvojega brata.
12 Utakapo ilima ardhi, kuanzia sasa na kuendelea haita kuzalia wewe nguvu yake. Utakuwa mkimbizi na mtu asiye na makao duniani.”
Ko boš oral tla, ti odslej ne bodo obrodila svoje moči; na zemlji boš ubežnik in potepuh.«
13 Kaini akamwambia Yahwe, “Adhabu yangu ni kubwa kuliko uwezo wangu wa kustahimili.
Kajn je Gospodu rekel: »Moja kazen je večja, kakor jo lahko prenesem.
14 Kwa hakika umenifukuza siku hii ya leo kutoka kwenye ardhi hii, na sitaonekana mbele ya uso wako. Nitakuwa mkimbizi na mtu nisiye na makao katika dunia, na yeyote atakaye niona ataniua.”
Glej, danes si me napodil izpred obličja zemlje, in skrit bom pred tvojim obličjem, in na zemlji bom ubežnik ter potepuh; in zgodilo se bo, da me bo ubil vsak, kdor me najde.«
15 Yahwe akamwambia, “ikiwa mtuyeyote atamuua Kaini, kisasi kitakuwa juu yake mara saba.” Kisha Yahwe akaweka alama juu ya Kaini, ili kwamba kama mtu awayeyote akimuona, mtu huyo asimshambulie.
Gospod mu je rekel: »Zatorej kdorkoli ubije Kajna, bo nanj nadeto sedemkratno maščevanje.« In Gospod je na Kajna namestil znamenje, da kdorkoli ga najde, ga ne bi ubil.
16 Kwa hiyo Kaini akatoka mbele ya uwepo wa Yahwe na akaishi katika nchi ya Nodi, mashariki mwa Edeni.
Kajn je odšel izpred Gospodove prisotnosti in prebival v deželi Nod, vzhodno od Edena.
17 Kaini akamjua mke wake na akapata mimba. Akamzaa Henoko. Akajenga mji na akauita kwa jina la mwanae Henoko.
Kajn je spoznal svojo ženo in ta je spočela ter rodila Henoha. Ta je zgradil mesto in ime mesta imenoval Henoh, po imenu svojega sina.
18 Kwa Henoko akazaliwa Iradi. Iradi akamzaa Mehuyaeli. Mehuyaeli akamzaa Methushaeli. Methushaeli akamzaa Lameki.
Henohu se je rodil Irád, in Irád je zaplodil Mehujaéla, in Mehujaél je zaplodil Metušaéla, in Metušaél je zaplodil Lameha.
19 Lameki akajitwalia wake wawili: jinala mmoja alikuwa Ada, na jina la yule mwingine alikuwa Sila.
Lameh si je vzel dve ženi: ime prve je bilo Ada, ime druge pa Cila.
20 Ada akamzaa Yabali. Huyu ndiye alikuwa baba yao na wale walioishi hemani ambao wanafuga wanyama.
Ada je rodila Jabála; ta je bil oče teh, ki prebivajo v šotorih in teh, ki imajo živino.
21 Ndugu yake aliitwa Yubali. Huyu alikuwa baba yao na wale wapigao kinubi na filimbi.
Ime njegovega brata je bilo Jubál; bil je oče vseh teh, ki prijemajo harfo in piščal.
22 Sila naye akamzaa Tubal Kaini, mfua vyombo vya shaba na chuma. Dada yake na Tubal Kaini alikuwa Naama.
Cila pa je rodila tudi Tubál Kajina, učitelja vsakega rokodelca z bronom in železom, in Tubál Kajinova sestra je bila Naáma.
23 Lameki akawaambia wake zake, Ada na Sila, sikieni sauti yangu; ninyi wake wa Lameki, sikilizeni nisemacho. Kwa kuwa nimemuua mtu kwa kunijeruhi, kijana kwa kunichubua.
Lameh je rekel svojima ženama, Adi in Cili: »Poslušajta moj glas, vidve, Lamehovi ženi, prisluhnita mojemu govoru, kajti umoril sem človeka, ki mi prizadeva rane in mladeniča, za mojo rano.
24 Ikiwa Kaini atalipiwa kisasi mara saba, ndipo Lameki atalipiwa kisasi mara sabini na saba.”
Če bo Kajn sedemkrat maščevan, resnično, Lameh [pa] sedeminsedemdesetkrat.«
25 Adam akamjua mke wake tena, na akazaa mtoto mwanaume. Akamuita jina lake Sethi na akasema, “Mungu amenipatia mtoto mwingine wa kiume kwa nafasi ya Habili, kwa kuwa Kaini alimuuwa.”
Adam je spet spoznal svojo ženo in rodila je sina in njegovo ime je imenovala Set. »Kajti Bog, « je rekla, »mi je določil drugega potomca namesto Abela, ki ga je ubil Kajn.«
26 Mtoto wa kiume alizaliwa kwa Sethi na akamuita jina lake Enoshi. Wakati huo watu walianza kuliitia jina la Yahwe.
In Setu, tudi njemu se je rodil sin, in njegovo ime je imenoval Enóš. Potem so ljudje začeli klicati Gospodovo ime.

< Mwanzo 4 >