< Mwanzo 4 >
1 Mwanume akalala na Hawa mke wake. Akabeba mimba na akamzaa Kaini. Akasema, “nimezaa mwanaume kwa msaada wa Yahwe.”
Ja Adam tunsi emäntänsä Hevan, ja hän tuli raskaaksi, ja synnytti Kainin, ja sanoi: minulla on mies Herra.
2 Kisha akazaa ndugu yake Habili. Sasa Habili akawa mchungaji, lakini Kaini alilima udongo.
Ja taas hän synnytti hänen veljensä Habelin. Ja Habel tuli lampuriksi, mutta Kain peltomieheksi.
3 Ikawa kwamba baada ya muda Kaini alileta sehemu ya mazao ya ardhi kama sadaka kwa Yahwe.
Ja tapahtui muutamain päiväin perästä, että Kain uhrasi Herralle lahjan maan hedelmistä.
4 Habili pia, alileta sehemu ya wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona. Yahwe akamkubali Habili pamoja na sadaka yake,
Ja Habel myös uhrasi laumansa esikoisista, ja heidän lihavuudestansa. Ja Herra katsoi (leppyisesti) Habelin ja hänen uhrinsa puoleen.
5 lakini Kaini pamoja na sadaka yake Mungu hakuikubali. Kwa hiyo Kaini alikasirika sana, na uso wake ukakunjamana.
Mutta Kainin ja hänen uhrinsa puoleen ei hän (leppyisesti) katsonut: silloin Kain vihastui sangen kovin, ja hänen hahmonsa muuttui.
6 Yahwe akamwambia Kaini, “kwa nini umekasirika na kwa nini uso wako umekunjamana?
Niin Herra sanoi Kainille: miksis olet vihainen? Ja miksi hahmos muuttuu?
7 Kama ukifanya vema, je hutapata kibali? lakini kama hutafanya lilio jema, dhambi iko inakuotea mlangoni na inatamani kukutawala, lakini inakupasa uishinde.
Eikö se niin ole? jos hyvin teet niin syntis anteeksi annetaan; ja jolles hyvin tee, niin synti väijyy oven edessä, ja hänen himonsa on sinun tykös, vaan hallitse sinä häntä.
8 Kaini akamwambia Habili ndugu yake. Hata wakati walipokuwa shambani, Kaini aliinuka dhidi ya Habili ndugu yake na akamuua. (Katika tafsiri za kale zinasema, Kaini alimwambia Habili ndugu yake, “twende mashambani.” Na wakati walipokuwa shambani, Kaini alimuinukia Habili ndugu yake na kumuua).
Ja Kain puhui veljensä Habelin kanssa. Ja tapahtui heidän kedolla ollessansa, että Kain karkasi veljensä Habelin päälle, ja tappoi hänen.
9 Kisha Yahwe akamuuliza Kaini, “Ndugu yako Habili yuko wapi?” Akasema, “sijui. Je mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?”
Niin Herra sanoi Kainille: kussa on Habel sinun veljes? hän vastasi: en minä tiedä: olenko minä veljeni vartia?
10 Yahwe akasema, “umefanya nini? damu ya ndugu yako inaniita mimi kutokea ardhini.
Ja hän sanoi: mitäs tehnyt olet? veljes veren ääni huutaa minun tyköni maasta.
11 Na sasa umelaaniwa wewe kutoka ardhi ambayo imefungua kinywa chake kupokea damu ya ndugu yako kutoka mikononi mwako.
Ja nyt kirottu ole sinä: (kirottu) maan päältä, joka avasi suunsa ottamaan veljes verta sinun kädestäs.
12 Utakapo ilima ardhi, kuanzia sasa na kuendelea haita kuzalia wewe nguvu yake. Utakuwa mkimbizi na mtu asiye na makao duniani.”
Koskas maata viljelet, niin ei pidä sen tästedes sinulle väkeänsä antaman; kulkian ja pakenevaisen pitää sinun oleman maan päällä.
13 Kaini akamwambia Yahwe, “Adhabu yangu ni kubwa kuliko uwezo wangu wa kustahimili.
Ja Kain sanoi Herralle: minun rangaistukseni on suurempi, kuin että se on kannettava.
14 Kwa hakika umenifukuza siku hii ya leo kutoka kwenye ardhi hii, na sitaonekana mbele ya uso wako. Nitakuwa mkimbizi na mtu nisiye na makao katika dunia, na yeyote atakaye niona ataniua.”
Katsos, sinä ajat minun pois tänäpäivänä maalta, ja minun pitää sinun kasvois edestä lymymän ja tulen kulkiaksi ja pakenevaiseksi maan päällä. Ja niin minun käy, kuka ikänänsä minun löytää, se tappaa minun.
15 Yahwe akamwambia, “ikiwa mtuyeyote atamuua Kaini, kisasi kitakuwa juu yake mara saba.” Kisha Yahwe akaweka alama juu ya Kaini, ili kwamba kama mtu awayeyote akimuona, mtu huyo asimshambulie.
Mutta Herra sanoi hänelle: Sentähden, kuka ikänänsä Kainin tappaa, se pitää seitsemän kertaisesti kostettaman. Ja Herra pani merkin Kainiin, ettei kenkään häntä tappaisi, joka hänen löytäisi.
16 Kwa hiyo Kaini akatoka mbele ya uwepo wa Yahwe na akaishi katika nchi ya Nodi, mashariki mwa Edeni.
Ja niin Kain läksi Herran kasvoin edestä, ja asui Nodin maalla, itään päin Edenistä.
17 Kaini akamjua mke wake na akapata mimba. Akamzaa Henoko. Akajenga mji na akauita kwa jina la mwanae Henoko.
Ja Kain tunsi emäntänsä, joka tuli raskaaksi, ja synnytti Hanokin. Ja hän rakensi kaupungin, jonka hän kutsui poikansa nimellä Hanok.
18 Kwa Henoko akazaliwa Iradi. Iradi akamzaa Mehuyaeli. Mehuyaeli akamzaa Methushaeli. Methushaeli akamzaa Lameki.
Mutta Hanok siitti Iradin. Irad siitti Mahujaelin. Mahujael siitti Metusaelin. Metusael siitti Lamekin.
19 Lameki akajitwalia wake wawili: jinala mmoja alikuwa Ada, na jina la yule mwingine alikuwa Sila.
Mutta Lamek otti kaksi emäntää, yhden nimi oli Ada, ja toisen nimi Zilla.
20 Ada akamzaa Yabali. Huyu ndiye alikuwa baba yao na wale walioishi hemani ambao wanafuga wanyama.
Ja Ada synnytti Jabalin, joka oli niiden isä, jotka majoissa asuivat, ja karjaa kasvattivat.
21 Ndugu yake aliitwa Yubali. Huyu alikuwa baba yao na wale wapigao kinubi na filimbi.
Ja hänen veljensä nimi oli Jubal, josta kantelein ja huiluin soittajat tulivat.
22 Sila naye akamzaa Tubal Kaini, mfua vyombo vya shaba na chuma. Dada yake na Tubal Kaini alikuwa Naama.
Zilla myös synnytti TubalKainin, joka oli taitava kaikkinaisissa vaski-ja rautatöissä, ja Tubalkainin sisar oli Naema.
23 Lameki akawaambia wake zake, Ada na Sila, sikieni sauti yangu; ninyi wake wa Lameki, sikilizeni nisemacho. Kwa kuwa nimemuua mtu kwa kunijeruhi, kijana kwa kunichubua.
Ja Lamek sanoi emännillensä, Adalle ja Zillalle: te Lamekin emännät, kuulkaat minun ääntäni, ja vaari ottakaat siitä kuin minä sanon: minä olen miehen tappanut minulleni haavaksi, ja nuorukaisen minulleni sinimarjaksi:
24 Ikiwa Kaini atalipiwa kisasi mara saba, ndipo Lameki atalipiwa kisasi mara sabini na saba.”
Kain kostetaan seitsemän kertaisesti, mutta Lamek seitsemän ja seitsemänkymmenen kertaisesti.
25 Adam akamjua mke wake tena, na akazaa mtoto mwanaume. Akamuita jina lake Sethi na akasema, “Mungu amenipatia mtoto mwingine wa kiume kwa nafasi ya Habili, kwa kuwa Kaini alimuuwa.”
Ja Adam taas tunsi emäntänsä, ja hän synnytti pojan, ja kutsui hänen nimensä Set, sanoen: Jumala on minulle toisen siemenen antanut Habelin edestä, jonka Kain tappoi.
26 Mtoto wa kiume alizaliwa kwa Sethi na akamuita jina lake Enoshi. Wakati huo watu walianza kuliitia jina la Yahwe.
Ja Set myös siitti pojan, ja kutsui hänen Enos. Silloin ruvettiin saarnaamaan Herran nimestä.