< Mwanzo 4 >

1 Mwanume akalala na Hawa mke wake. Akabeba mimba na akamzaa Kaini. Akasema, “nimezaa mwanaume kwa msaada wa Yahwe.”
Truly, Adam knew his wife Eve, who conceived and gave birth to Cain, saying, “I have obtained a man through God.”
2 Kisha akazaa ndugu yake Habili. Sasa Habili akawa mchungaji, lakini Kaini alilima udongo.
And again she gave birth to his brother Abel. But Abel was a pastor of sheep, and Cain was a farmer.
3 Ikawa kwamba baada ya muda Kaini alileta sehemu ya mazao ya ardhi kama sadaka kwa Yahwe.
Then it happened, after many days, that Cain offered gifts to the Lord, from the fruits of the earth.
4 Habili pia, alileta sehemu ya wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona. Yahwe akamkubali Habili pamoja na sadaka yake,
Abel likewise offered from the firstborn of his flock, and from their fat. And the Lord looked with favor on Abel and his gifts.
5 lakini Kaini pamoja na sadaka yake Mungu hakuikubali. Kwa hiyo Kaini alikasirika sana, na uso wake ukakunjamana.
Yet in truth, he did not look with favor on Cain and his gifts. And Cain was vehemently angry, and his countenance fell.
6 Yahwe akamwambia Kaini, “kwa nini umekasirika na kwa nini uso wako umekunjamana?
And the Lord said to him: “Why are you angry? And why is your face fallen?
7 Kama ukifanya vema, je hutapata kibali? lakini kama hutafanya lilio jema, dhambi iko inakuotea mlangoni na inatamani kukutawala, lakini inakupasa uishinde.
If you behave well, will you not receive? But if you behave badly, will not sin at once be present at the door? And so its desire will be within you, and you will be dominated by it.”
8 Kaini akamwambia Habili ndugu yake. Hata wakati walipokuwa shambani, Kaini aliinuka dhidi ya Habili ndugu yake na akamuua. (Katika tafsiri za kale zinasema, Kaini alimwambia Habili ndugu yake, “twende mashambani.” Na wakati walipokuwa shambani, Kaini alimuinukia Habili ndugu yake na kumuua).
And Cain said to his brother Abel, “Let us go outside.” And when they were in the field, Cain rose up against his brother Abel, and he put him to death.
9 Kisha Yahwe akamuuliza Kaini, “Ndugu yako Habili yuko wapi?” Akasema, “sijui. Je mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?”
And the Lord said to Cain, “Where is your brother Abel?” And he responded: “I do not know. Am I my brother’s keeper?”
10 Yahwe akasema, “umefanya nini? damu ya ndugu yako inaniita mimi kutokea ardhini.
And he said to him: “What have you done? The voice of your brother’s blood cries out to me from the land.
11 Na sasa umelaaniwa wewe kutoka ardhi ambayo imefungua kinywa chake kupokea damu ya ndugu yako kutoka mikononi mwako.
Now, therefore, you will be cursed upon the land, which opened its mouth and received the blood of your brother at your hand.
12 Utakapo ilima ardhi, kuanzia sasa na kuendelea haita kuzalia wewe nguvu yake. Utakuwa mkimbizi na mtu asiye na makao duniani.”
When you work it, it will not give you its fruit; a vagrant and a fugitive shall you be upon the land.”
13 Kaini akamwambia Yahwe, “Adhabu yangu ni kubwa kuliko uwezo wangu wa kustahimili.
And Cain said to the Lord: “My iniquity is too great to deserve kindness.
14 Kwa hakika umenifukuza siku hii ya leo kutoka kwenye ardhi hii, na sitaonekana mbele ya uso wako. Nitakuwa mkimbizi na mtu nisiye na makao katika dunia, na yeyote atakaye niona ataniua.”
Behold, you have cast me out this day before the face of the earth, and from your face I will be hidden; and I will be a vagrant and a fugitive on the earth. Therefore, anyone who finds me will kill me.”
15 Yahwe akamwambia, “ikiwa mtuyeyote atamuua Kaini, kisasi kitakuwa juu yake mara saba.” Kisha Yahwe akaweka alama juu ya Kaini, ili kwamba kama mtu awayeyote akimuona, mtu huyo asimshambulie.
And the Lord said to him: “By no means will it be so; rather, whoever would kill Cain, will be punished sevenfold.” And the Lord placed a seal upon Cain, so that anyone who found him would not put him to death.
16 Kwa hiyo Kaini akatoka mbele ya uwepo wa Yahwe na akaishi katika nchi ya Nodi, mashariki mwa Edeni.
And so Cain, departing from the face of the Lord, lived as a fugitive on the earth, toward the eastern region of Eden.
17 Kaini akamjua mke wake na akapata mimba. Akamzaa Henoko. Akajenga mji na akauita kwa jina la mwanae Henoko.
Then Cain knew his wife, and she conceived and gave birth to Enoch. And he built a city, and he called its name by the name of his son, Enoch.
18 Kwa Henoko akazaliwa Iradi. Iradi akamzaa Mehuyaeli. Mehuyaeli akamzaa Methushaeli. Methushaeli akamzaa Lameki.
Thereafter, Enoch conceived Irad, and Irad conceived Mahujael, and Mahujael conceived Mathusael, and Mathusael conceived Lamech.
19 Lameki akajitwalia wake wawili: jinala mmoja alikuwa Ada, na jina la yule mwingine alikuwa Sila.
Lamech took two wives: the name of one was Adah, and the name of the other was Zillah.
20 Ada akamzaa Yabali. Huyu ndiye alikuwa baba yao na wale walioishi hemani ambao wanafuga wanyama.
And Adah conceived Jabel, who was the father of those who live in tents and are shepherds.
21 Ndugu yake aliitwa Yubali. Huyu alikuwa baba yao na wale wapigao kinubi na filimbi.
And the name of his brother was Jubal; he was the father of those who sing to the harp and the organ.
22 Sila naye akamzaa Tubal Kaini, mfua vyombo vya shaba na chuma. Dada yake na Tubal Kaini alikuwa Naama.
Zillah also conceived Tubalcain, who was a hammerer and artisan in every work of brass and iron. In fact, the sister of Tubalcain was Noema.
23 Lameki akawaambia wake zake, Ada na Sila, sikieni sauti yangu; ninyi wake wa Lameki, sikilizeni nisemacho. Kwa kuwa nimemuua mtu kwa kunijeruhi, kijana kwa kunichubua.
And Lamech said to his wives Adah and Zillah: “Listen to my voice, you wives of Lamech, pay attention to my speech. For I have killed a man to my own harm, and an adolescent to my own bruising.
24 Ikiwa Kaini atalipiwa kisasi mara saba, ndipo Lameki atalipiwa kisasi mara sabini na saba.”
Sevenfold vengeance will be given for Cain, but for Lamech, seventy-seven times.”
25 Adam akamjua mke wake tena, na akazaa mtoto mwanaume. Akamuita jina lake Sethi na akasema, “Mungu amenipatia mtoto mwingine wa kiume kwa nafasi ya Habili, kwa kuwa Kaini alimuuwa.”
Adam also knew his wife again, and she gave birth to a son, and she called his name Seth, saying, “God has given me another offspring, in place of Abel, whom Cain killed.”
26 Mtoto wa kiume alizaliwa kwa Sethi na akamuita jina lake Enoshi. Wakati huo watu walianza kuliitia jina la Yahwe.
But to Seth also was born a son, whom he called Enos. This one began to invoke the name of the Lord.

< Mwanzo 4 >