< Mwanzo 39 >

1 Yusufu akaletwa Misri. Potifa, aliyekuwa afisa wa Farao mkuu wa walinzi na Mmisri, akamnunua kutoka kwa Waishmaeli, waliokuwa wamempeleka pale.
and Joseph to go down Egypt [to] and to buy him Potiphar eunuch Pharaoh ruler [the] guard man Egyptian from hand: to [the] Ishmaelite which to go down him there [to]
2 Yahwe alikuwa pamoja na Yusufu na akawa mtu aliyefanikiwa. Aliishi katika nyumba ya Mmisri bwana wake.
and to be LORD with Joseph and to be man to prosper and to be in/on/with house: household lord his [the] Egyptian
3 Bwana wake akaona kwamba Yahwe alikuwa pamoja naye na kwamba Yahwe alifanikisha kila kitu alichokifanya.
and to see: see lord his for LORD with him and all which he/she/it to make: do LORD to prosper in/on/with hand his
4 Yusufu akapata kibali mbele zake. Akamtumikia Potifa. Potifa akamfanya msimamizi juu ya nyumba yake, na kila alichokimiliki, akakiweka chini ya uangalizi wake.
and to find Joseph favor in/on/with eye: seeing his and to minister [obj] him and to reckon: overseer him upon house: household his and all there to/for him to give: put in/on/with hand: power his
5 Ikawa alipomfanya msimamizi juu ya nyumba yake na juu ya kila kitu alichomiliki, Yahwe akaibariki nyumba ya Mmisri kwa sababu ya Yusufu. Baraka za Yahwe zilikuwa juu ya kila kitu alichokuwa nacho Potifa nyumbani na shambani.
and to be from the past to reckon: overseer [obj] him in/on/with house: household his and upon all which there to/for him and to bless LORD [obj] house: household [the] Egyptian in/on/with because of Joseph and to be blessing LORD in/on/with all which there to/for him in/on/with house: home and in/on/with land: country
6 Potifa akaweka kila alichokuwa nacho chini ya uangalizi wa Yusufu. Hakuwa na haja ya kufikiri juu ya lolote isipokuwa chakula alichokula tu. Basi Yusufu alikuwa kijana mzuri na wa kuvutia.
and to leave: forsake all which to/for him in/on/with hand: power Joseph and not to know with him anything that if: except if: except [the] food which he/she/it to eat and to be Joseph beautiful appearance and beautiful appearance
7 Ikawa baada ya hayo mke wa bwana wake akamtamani Yusufu. Akamwambia, “Lala nami.”
and to be after [the] word: thing [the] these and to lift: bear woman: wife lord his [obj] eye her to(wards) Joseph and to say to lie down: have sex [emph?] with me
8 Lakini yeye alikataa na kumwambia mke wa bwana wake, “Tazama, bwana wangu haangalii chochote nikifanyacho nyumbani, na ameweka kila kitu anachokimiliki chini ya uangalizi wangu.
and to refuse and to say to(wards) woman: wife lord his look! lord my not to know with me what? in/on/with house: household and all which there to/for him to give: put in/on/with hand: power my
9 Hakuna mtu aliye mkuu katika nyumba hii kuliko mimi. Hajanidhuiria chochote isipokuwa wewe, kwa sababu wewe ni mkewe. Ni kwa namna gani basi naweza kufanya uovu mkuu namna hii na kumtenda dhambi Mungu?
nothing he great: large in/on/with house: household [the] this from me and not to withhold from me anything that if: except if: except [obj] you in/on/with in which you(f. s.) woman: wife his and how? to make: do [the] distress: evil [the] great: large [the] this and to sin to/for God
10 Akamwambia Yusufu siku baada ya siku, lakini yeye akakataa kulala naye wala kuwa naye.
and to be like/as to speak: speak she to(wards) Joseph day: daily day: daily and not to hear: hear to(wards) her to/for to lie down: have sex beside her to/for to be with her
11 Ikawa siku moja aliingia ndani kufanya kazi yake. Hakuna mtu yeyote wa nyumbani aliyekuwepo pale ndani.
and to be like/as [the] day [the] this and to come (in): come [the] house: home [to] to/for to make: do work his and nothing man: anyone from human [the] house: home there in/on/with house: home
12 Akashika nguo zake na kusema, “Lala nami.” Akaacha nguo zake mikononi mwake, akakimbia, na kutoka nje.
and to capture him in/on/with garment his to/for to say to lie down: have sex [emph?] with me and to leave: forsake garment his in/on/with hand: power her and to flee and to come out: come [the] outside [to]
13 Ikawa, alipoona kwamba ameziacha nguo zake mikononi mwake na kwamba amekimbia nje,
and to be like/as to see: see she for to leave: forsake garment his in/on/with hand her and to flee [the] outside [to]
14 akawaita watu wa nyumbani mwake na kuwambia, “Tazama, Potifa ameleta Mwebrania huyu kutudhihaki. Aliingia kulala nami, na nikapiga kelele.
and to call: call out to/for human house: household her and to say to/for them to/for to say to see: behold! to come (in): bring to/for us man Hebrew to/for to laugh in/on/with us to come (in): come to(wards) me to/for to lie down: have sex with me and to call: call out in/on/with voice great: large
15 Ikawa aliponisikia nikipiga kelele, akaniacha na nguo yake, akakimbia, na kutoka nje.”
and to be like/as to hear: hear he for to exalt voice my and to call: call out and to leave: forsake garment his beside me and to flee and to come out: come [the] outside [to]
16 Akaweka nguo zake karibu naye hata bwana yake alipokuja nyumbani.
and to rest garment his beside her till to come (in): come lord his to(wards) house: home his
17 Akamwambia maelelezo haya, “Yule mtumishi Mwebrania uliyemleta kwetu, aliingia kunidhihaki.
and to speak: speak to(wards) him like/as word [the] these to/for to say to come (in): come to(wards) me [the] servant/slave [the] Hebrew which to come (in): bring to/for us to/for to laugh in/on/with me
18 Ikawa nilipopiga kelele, akaacha nguo yake kwangu akakimbia nje.”
and to be like/as to exalt I voice my and to call: call out and to leave: forsake garment his beside me and to flee [the] outside [to]
19 Ikawa, bwana wake aliposikia maelezo aliyoambiwa na mkewe, “Hivi ndivyo mtumishi wako alivyonitenda,” alikasirika sana.
and to be like/as to hear: hear lord his [obj] word woman: wife his which to speak: speak to(wards) him to/for to say like/as Chronicles [the] these to make: do to/for me servant/slave your and to be incensed face: anger his
20 Bwana wa Yusufu akamchukua na kumweka gerezani, mahali walipowekwa wafungwa wa mfalme. Akawa pale kifungoni.
and to take: take lord Joseph [obj] him and to give: put him to(wards) house: home [the] prison place which (prisoner *Q(K)*) [the] king to bind and to be there in/on/with house: home [the] prison
21 Lakini Yahwe alikuwa pamoja na Yusufu na kumwonyesha uaminifu wa agano. Akampa kibali mbele ya mlinzi wa gereza.
and to be LORD with Joseph and to stretch to(wards) him kindness and to give: give favor his in/on/with eye: seeing ruler house: home [the] prison
22 Mlinzi wa gereza akawaweka mikononi mwa Yusufu wafungwa wote waliokuwa gerezani. Chochote walichokifanya, kilikuwa chini ya uangalizi wa Yusufu.
and to give: put ruler house: home [the] prison in/on/with hand: power Joseph [obj] all [the] prisoner which in/on/with house: home [the] prison and [obj] all which to make: do there he/she/it to be to make: do
23 Mlinzi wa gereza hakuwa na wasiwasi juu ya chochote kilichokuwa mkononi mwake, kwa sababu Yahwe alikuwa pamoja naye. Yahwe akafanikisha kila alichokifanya.
nothing ruler house: home [the] prison to see: see [obj] all anything in/on/with hand: power his in/on/with in which LORD with him and which he/she/it to make: do LORD to prosper

< Mwanzo 39 >