< Mwanzo 39 >
1 Yusufu akaletwa Misri. Potifa, aliyekuwa afisa wa Farao mkuu wa walinzi na Mmisri, akamnunua kutoka kwa Waishmaeli, waliokuwa wamempeleka pale.
And Joseph he had been brought down Egypt towards and he bought him Potiphar [the] official of Pharaoh [the] commander of the bodyguards a man an Egyptian from [the] hand of the Ishmaelites who they had brought down him there towards.
2 Yahwe alikuwa pamoja na Yusufu na akawa mtu aliyefanikiwa. Aliishi katika nyumba ya Mmisri bwana wake.
And he was Yahweh with Joseph and he was a man successful and he was in [the] house of master his the Egyptian.
3 Bwana wake akaona kwamba Yahwe alikuwa pamoja naye na kwamba Yahwe alifanikisha kila kitu alichokifanya.
And he saw master his that Yahweh [was] with him and all that he [was] doing Yahweh [was] making successful in hand his.
4 Yusufu akapata kibali mbele zake. Akamtumikia Potifa. Potifa akamfanya msimamizi juu ya nyumba yake, na kila alichokimiliki, akakiweka chini ya uangalizi wake.
And he found Joseph favor in view his and he served him and he appointed him over household his and all [that] there [belonged] to him he gave in hand his.
5 Ikawa alipomfanya msimamizi juu ya nyumba yake na juu ya kila kitu alichomiliki, Yahwe akaibariki nyumba ya Mmisri kwa sababu ya Yusufu. Baraka za Yahwe zilikuwa juu ya kila kitu alichokuwa nacho Potifa nyumbani na shambani.
And it was from then he appointed him in household his and over all that there [belonged] to him and he blessed Yahweh [the] household of the Egyptian on account of Joseph and it was [the] blessing of Yahweh on all that there [belonged] to him in the house and in the field.
6 Potifa akaweka kila alichokuwa nacho chini ya uangalizi wa Yusufu. Hakuwa na haja ya kufikiri juu ya lolote isipokuwa chakula alichokula tu. Basi Yusufu alikuwa kijana mzuri na wa kuvutia.
And he left all that [belonged] to him in [the] hand of Joseph and not he knew with him anything that except the food which he [was] eating and he was Joseph handsome of form and handsome of appearance.
7 Ikawa baada ya hayo mke wa bwana wake akamtamani Yusufu. Akamwambia, “Lala nami.”
And it was after the things these and she lifted up [the] wife of master his eyes her to Joseph and she said lie! with me.
8 Lakini yeye alikataa na kumwambia mke wa bwana wake, “Tazama, bwana wangu haangalii chochote nikifanyacho nyumbani, na ameweka kila kitu anachokimiliki chini ya uangalizi wangu.
And he refused - and he said to [the] wife of master his here! lord my not he knows with me what? [is] in the house and all that there [belongs] to him he has given in hand my.
9 Hakuna mtu aliye mkuu katika nyumba hii kuliko mimi. Hajanidhuiria chochote isipokuwa wewe, kwa sababu wewe ni mkewe. Ni kwa namna gani basi naweza kufanya uovu mkuu namna hii na kumtenda dhambi Mungu?
Not [is] he great in the household this more than me and not he has withheld from me anything that except you in that you [are] wife his and how? will I do the evil great this and I will sin to God.
10 Akamwambia Yusufu siku baada ya siku, lakini yeye akakataa kulala naye wala kuwa naye.
And it was when spoke she to Joseph day - day and not he listened to her to lie beside her to be with her.
11 Ikawa siku moja aliingia ndani kufanya kazi yake. Hakuna mtu yeyote wa nyumbani aliyekuwepo pale ndani.
And it was when the day this and he went the house towards to do work his and not anyone from [the] men of the house [was] there in the house.
12 Akashika nguo zake na kusema, “Lala nami.” Akaacha nguo zake mikononi mwake, akakimbia, na kutoka nje.
And she seized him by clothing his saying lie! with me and he left clothing his in hand her and he fled and he went out the outside towards.
13 Ikawa, alipoona kwamba ameziacha nguo zake mikononi mwake na kwamba amekimbia nje,
And it was when saw she that he had left clothing his in hand her and he had fled the outside towards.
14 akawaita watu wa nyumbani mwake na kuwambia, “Tazama, Potifa ameleta Mwebrania huyu kutudhihaki. Aliingia kulala nami, na nikapiga kelele.
And she called out to [the] men of household her and she said to them saying see he has brought to us a man a Hebrew to mock us he came to me to lie with me and I called out with a voice great.
15 Ikawa aliponisikia nikipiga kelele, akaniacha na nguo yake, akakimbia, na kutoka nje.”
And it was when heard he that I raised voice my and I called out and he left clothing his beside me and he fled and he went out the outside towards.
16 Akaweka nguo zake karibu naye hata bwana yake alipokuja nyumbani.
And she placed clothing his beside her until came master his to house his.
17 Akamwambia maelelezo haya, “Yule mtumishi Mwebrania uliyemleta kwetu, aliingia kunidhihaki.
And she spoke to him according to the words these saying he came to me the servant the Hebrew whom you brought to us to mock me.
18 Ikawa nilipopiga kelele, akaacha nguo yake kwangu akakimbia nje.”
And it was when raised I voice my and I called out and he left clothing his beside me and he fled the outside towards.
19 Ikawa, bwana wake aliposikia maelezo aliyoambiwa na mkewe, “Hivi ndivyo mtumishi wako alivyonitenda,” alikasirika sana.
And it was when heard master his [the] words of wife his which she spoke to him saying according to the things these he did to me servant your and it burned anger his.
20 Bwana wa Yusufu akamchukua na kumweka gerezani, mahali walipowekwa wafungwa wa mfalme. Akawa pale kifungoni.
And he took [the] master of Joseph him and he put him into [the] house of the prison [the] place where ([the] prisoners of *Q(K)*) the king [were] imprisoned and he was there in [the] house of the prison.
21 Lakini Yahwe alikuwa pamoja na Yusufu na kumwonyesha uaminifu wa agano. Akampa kibali mbele ya mlinzi wa gereza.
And he was Yahweh with Joseph and he extended to him covenant loyalty and he gave favor his in [the] eyes of [the] commander of [the] house of the prison.
22 Mlinzi wa gereza akawaweka mikononi mwa Yusufu wafungwa wote waliokuwa gerezani. Chochote walichokifanya, kilikuwa chini ya uangalizi wa Yusufu.
And he gave [the] commander of [the] house of the prison in [the] hand of Joseph all the prisoners who [were] in [the] house of the prison and all that [they were] doing there he he was doing.
23 Mlinzi wa gereza hakuwa na wasiwasi juu ya chochote kilichokuwa mkononi mwake, kwa sababu Yahwe alikuwa pamoja naye. Yahwe akafanikisha kila alichokifanya.
Not - [the] commander of [the] house of the prison [was] seeing all anything in hand his in that Yahweh [was] with him and [that] which he [was] doing Yahweh [was] making successful.