< Mwanzo 37 >

1 Yakobo akaishi katika nchi aliyokaa babaye, katika nchi ya Kanaani.
And Jacob dwelt in the land in which his father was a stranger, in the land of Canaan.
2 Haya ndiyo matukio yaliyomhusu Yakobo. Yusufu, aliyekuwa kijana wa miaka kumi na saba, alikuwa akilichunga kundi pamoja na ndugu zake. Alikuwa pamoja na wana wa Bilha na pamoja na wana wa Zilpa, wake wa baba yake. Yusufu akaleta taarifa yao mbaya kwa baba yao.
These are the generations of Jacob. Joseph, being seventeen years old, was feeding the flock with his brethren; and the lad was with the sons of Bilhah, and with the sons of Zilpah, his father’s wives: and Joseph brought to his father their bad report.
3 Basi Israeli akampenda Yusufu kuliko wanawe wote kwa sababu alikuwa mwana wa uzee wake. Akamshonea vazi zuri.
Now Israel loved Joseph more than all his children, because he was the son of his old age: and he made him a coat of many colours.
4 Ndugu zake wakaona kwamba baba yao alimpenda sana kuliko ndugu zake wote. Wakamchukia na hawakuongea naye vema.
And when his brethren saw that their father loved him more than all his brethren, they hated him, and could not speak peaceably to him.
5 Yusufu akaota ndoto, na akawambia ndugu zake. Wakamchukia zaidi.
And Joseph dreamed a dream, and he told it to his brethren: and they hated him yet the more.
6 Aliwambia, “Tafadhari sikilizeni ndoto hii niliyoiota.
And he said to them, Hear, I pray you, this dream which I have dreamed:
7 Tazama, tulikuwa tukifunga miganda ya nafaka shambani na tazama, mganda wangu ukainuka na kusimama wima, na tazama, miganda yenu ikasogea na kuuinamia mganda wangu”
For, behold, we were binding sheaves in the field, and, lo, my sheaf arose, and also stood upright; and, behold, your sheaves stood around, and made obeisance to my sheaf.
8 Ndugu zake wakamwambia, “Je ni kweli utatutawala? Je utatutawala juu yetu? Hata wakamchukia zaidi kwa ajili ya ndoto zake na maneno yake.
And his brethren said to him, Shalt thou indeed reign over us? or shalt thou indeed have dominion over us? And they hated him yet the more for his dreams, and for his words.
9 Akaota ndoto nyingine na kuwasimulia ndugu zake. Alisema, “Tazama, nimeota ndoto nyingine: Jua na mwezi na nyota kumi na moja ziliniinamia.”
And he dreamed yet another dream, and told it to his brethren, and said, Behold, I have dreamed a dream more; and, behold, the sun and the moon and the eleven stars made obeisance to me.
10 Akamwambia baba yake vile vile alivyowambia ndugu zake, na baba yake akamkemea. Akamwambia, Je umeota ndoto ya namna gani hii? Je mama yako na mimi na ndugu zako kweli tutakuja kukuinamia mpaka chini?”
And he told it to his father, and to his brethren: and his father rebuked him, and said to him, What is this dream that thou hast dreamed? Shall I and thy mother and thy brethren indeed come to bow down ourselves to thee to the earth?
11 Ndugu zake wakamwonea wivu, lakini baba yake akaliwema jambo hilo moyoni.
And his brethren envied him; but his father observed the saying.
12 Ndugu zake wakaenda kulichunga kundi la baba yao huko Shekemu.
And his brethren went to feed their father’s flock in Shechem.
13 Israeli akamwambia Yusufu, 'Je ndugu zako hawalichungi kundi huko Shekemu? Njoo, nami nitakutuma kwao.” Yusufu akamwambia, “nipo tayari.”
And Israel said to Joseph, Do not thy brethren feed the flock in Shechem? come, and I will send thee to them. And he said to him, Here am I.
14 Akamwambia, “Basi nenda, uwaone ndugu zako na kundi wanaendeleaje, na uniletee neno.” Hivyo Yakobo akamtuma kutoka katika bonde la Hebroni, na Yusufu akaenda Shekemu.
And he said to him, Go, I pray thee, see whether it is well with thy brethren, and well with the flocks; and bring me word again. So he sent him from the vale of Hebron, and he came to Shechem.
15 Mtu mmoja akamwona Yusufu. Tazama, Yusufu alikuwa akizunguka kondeni. Yule mtu akamwuliza, “Unatafuta nini?”
And a certain man found him, and, behold, he was wandering in the field: and the man asked him, saying, What seekest thou?
16 Yusufu akamwambia, “Nawatafuta ndugu zangu. Tafadhari, niambie, wananalichunga wapi kundi.”
And he said, I seek my brethren: tell me, I pray thee, where they feed their flocks.
17 Yule mtu akasema, “Waliondoka mahali hapa, kwa maana niliwasikia wakisema, 'Haya twende Dothani.” Yusufu akawafuata ndugu zake na kuwaona huko Dothani.
And the man said, They have departed from here; for I heard them say, Let us go to Dothan. And Joseph went after his brethren, and found them in Dothan.
18 Wakamwona kutokea mbali, na kabla hajawakaribia, wakapanga njama ya kumwua.
And when they saw him afar off, even before he came near to them, they conspired against him to slay him.
19 Ndugu zake wakaambiana wao kwa wao, “Tazama, mwotaji anakaribia.
And they said one to another, Behold, this dreamer is coming.
20 Njoni sasa, na tumwue na kumtupa katika mojawapo ya mashimo haya. Nasi tutasema, 'Mnyama mkali amemrarua.' Nasi tutaona ndoto zake zitakuwaje.”
Come now therefore, and let us slay him, and cast him into some pit, and we will say, Some evil beast hath devoured him: and we shall see what will become of his dreams.
21 Rubeni alilisikia hilo na kumwokoa kutoka katika mikono yao. Alisema, “Tusiuondoe uhai wake.”
And Reuben heard it, and he delivered him from their hands; and said, Let us not kill him.
22 Rubeni aliwambia, “Msimwage damu. Mtupeni katika shimo hili lililopo nyikani, lakini msiweke mikono yenu juu yake” - ili kwamba aweze kumwokoa katika mikono yao na kumrudisha kwa baba yake.
And Reuben said to them, Shed no blood, cast him into this pit that is in the wilderness, and lay no hand upon him; that he might deliver him from their hands, to bring him back to his father.
23 Ikawa Yusufu alipowafikia ndugu zake, walimvua vazi lake zuri.
And it came to pass, when Joseph had come to his brethren, that they stripped Joseph of his coat, his coat of many colours that was on him;
24 Wakamchukua na kumtupa shimoni. Shimo lilikuwa tupu bila maji.
And they took him, and cast him into a pit: and the pit was empty, there was no water in it.
25 Wakakaa chini kula mkate. Walipoinua macho yao na kuangalia, na, tazama, msafara wa Waishmaeli ulikuwa ukija kutoka Gileadi, pamoja na ngamia wao waliochukua viungo, malhamu na manemane. Walikuwa wakisafiri kuvichukua kuelekea Misri.
And they sat down to eat bread: and they lifted up their eyes and looked, and, behold, a company of Ishmaelites came from Gilead with their camels bearing spicery and balm and myrrh, going to carry them down to Egypt.
26 Yuda akawambia ndugu zake, “Ni faida gani kama tutamwua ndugu yetu na kufunika damu yake?
And Judah said to his brethren, What profit is it if we slay our brother, and conceal his blood?
27 Haya, na tumwuze kwa Waishmaeli na wala tusiweke mikono yetu juu yake. Kwani yeye ni ndugu yetu, nyama yetu.” Ndugu zake wakamsikiliza.
Come, and let us sell him to the Ishmaelites, and let not our hand be upon him; for he is our brother our flesh. And his brethren were content.
28 Wafanyabiashara wa Kimidiani wakapita. Ndugu zake wakamwinua na kumtoa Yusufu shimoni. Wakamwuza Yusufu kwa Waishmaeli kwa vipande ishirini vya fedha. Waishmaeli wakamchukua Yusufu mpaka Misri.
Then there passed by Midianites merchants; and they drew and lifted Joseph out of the pit, and sold Joseph to the Ishmaelites for twenty pieces of silver: and they brought Joseph into Egypt.
29 Rubeni akarudi kwenye shimo, na, tazama, Yusufu hakuwemo shimoni. Akararua mavazi yake.
And Reuben returned to the pit; and, behold, Joseph was not in the pit; and he tore his clothes.
30 Akarudi kwa ndugu zake na kusema, “Kijana yuko wapi? Na mimi, je niende wapi?”
And he returned to his brethren, and said, The child is not; and I, where shall I go?
31 Wakachinja mbuzi na kisha wakalichukua vazi la Yusufu na kulichovya katika damu.
And they took Joseph’s coat, and killed a kid of the goats, and dipped the coat in the blood;
32 Kisha wakalipeleka kwa baba yao na kusema, “Tumeiona hii. Tafadhari angalia kwamba ni vazi la mwanao au hapana.”
And they sent the coat of many colours, and they brought it to their father; and said, This have we found: know now whether it is thy son’s coat or not.
33 “Yakobo akaitambua na kusema, “Ni nguo ya mwanangu. Mnyama wa mwitu amemrarua. Bila shaka Yusufu ameraruliwa katika vipande.
And he knew it, and said, It is my son’s coat; an evil beast hath devoured him; Joseph is without doubt torn in pieces.
34 Yakobo akararua mavazi yake na kuvaa mavazi ya magunia katika viuno vyake. Akaomboleza kwa ajili ya mwanawe siku nyingi.
And Jacob tore his clothes, and put sackcloth on his loins, and mourned for his son many days.
35 Wanawe na binti zake wote wakainuka na kumfariji, lakini alikataa kufarijiwa. Akasema, “Hakika nitashuka kuzimu nikimwombolezea mwanangu.” Babaye akamlilia. (Sheol h7585)
And all his sons and all his daughters rose up to comfort him; but he refused to be comforted; and he said, For I will go down into the grave to my son mourning. Thus his father wept for him. (Sheol h7585)
36 Wamidiani wakamwuza huko Misri kwa Potifa, afisa wa Farao, kepteni wa walinzi.
And the Midianites sold him into Egypt to Potiphar, an officer of Pharaoh’s, and captain of the guard.

< Mwanzo 37 >