< Mwanzo 36 >

1 Hivi ndivyo vizazi vya Esau (aliyeitwa pia Edom).
Detta är Esaus slägte, som kallas Edom.
2 Esau akachukua wakeze kutoka kwa Wakanaani. Hawa walikuwa wake zake: Ada binti Eloni Mhiti; Oholibama binti Ana, mjukuu wa Zibeoni Mhivi; na
Esau tog hustrur af Canaans döttrar: Ada Elons Hetheens dotter, och Aholibama Anas dotter, Zibeons Heveens dotters.
3 Basemathi, binti Ishmaeli, dada wa Nebayothi.
Och Basmath Ismaels dotter, Nebajoths syster.
4 Ada akamzaa Elifazi kwa Esau, na Basemathi akamzaa Reueli.
Och Ada födde Esau Eliphas. Men Basmath födde Reguel.
5 Oholibama akamzaa Yeushi, Yalamu, na Kora. Hawa walikuwa wana wa Esau waliozaliwa kwake katika nchi ya Kananaani.
Aholibama födde Jeus, Jaelam och Korah. Desse äro Esaus barn, som honom födde voro i Canaans lande.
6 Esau akawachukua wakeze, wanawe, binti zake, na watu wote wa nyumba yake, mifugo wake - wanyama wake wote, na mali yake yote, aliyokuwa amekusanya katika nchi ya Kanaani, na akaenda katika nchi iliyoko mbali kutoka kwa Yakobo nduguye.
Och Esau tog sina hustrur, söner och döttrar, och alla sins huses själar; sina håfvor, och allan boskapen med alla ägodelar, som han förvärfvat hade i Canaans lande: Och for uti ett land, ifrå sin broder Jacob.
7 Alifanya hivi kwa sababu mali zao zilikuwa nyingi sana kwa wao kuishi pamoja. Nchi waliyokuwa wamekaa isingeweza kuwafaa kwa mifugo yao.
Förty deras ägodelar voro så stora, att de kunde icke bo med hvarannan: Och landet, der de uti främlingar voro, kunde icke fördraga dem, för deras stora ägodelars skull.
8 Hivyo Esau, aliyejulikana pia kama Edomu, akakaa katika nchi ya kilima Seiri.
Så bodde då Esau på Seirs berg: Och denne Esau är Edom.
9 Hivi ndivyo vizazi vya Esau, babu wa Waedomu katika nchi ya mlima Seiri.
Detta är Esaus slägte, af hvilkom de Edomeer komne äro på Seirs berg.
10 Haya yalikuwa majina ya wana wa Esau: Elifazi mwana wa Ada, mkewe Esau; Reueli mwana wa Basemathi, mkewe Esau.
Och så heta Esaus barn: Eliphas Ada son, Esaus hustrus; Reguel Basmaths son, Esaus hustrus.
11 Wana wa Elifazi walikuwa Temani, Omari, Zefo, Gatamu, na Kenazi.
Men Eliphas söner voro desse: Theman, Omar, Zepho, Gatham och Kenas.
12 Timna, suria wa Elifazi, mwana wa Esau, akamzaa Amaleki. Hawa walikuwa wajukuu wa Ada, mkewe Esau.
Och Thimna var Eliphas Esau sons frilla; hon födde Amalek. Desse äro de barn af Ada, Esaus hustru.
13 Hawa walikuwa wana wa Reueli: Nahathi, Zera, Shama, na Miza. Hawa walikuwa wajukuu wa Basemathi, mkewe Esau.
Men Reguels barn äro desse: Nahath, Serah, Samma, Missa. Desse äro de barn af Basmath, Esaus hustru.
14 Hawa walikuwa wana wa Oholibama, mkewe Esau, aliyekuwa binti Ana na mjukuu wa Zibeoni. Alimzalia Esau Yeushi, Yalamu, na Kora.
Men de barn af Aholibama, Esaus hustru, Anas dotter, Zibeons dotters, äro desse, dem hon födde Esau: Jeus, Jaelam och Korah.
15 Hizi zilikuwa koo kati ya vizazi vya Esau: uzao wa Elifazi, mzaliwa wa kwanza wa Esau: Temani, Omari, Zefo, Kenazi, Kora,
Desse äro de Förstar ibland Esaus barn: Eliphas barn, den första Esaus sons, voro desse: den Försten Theman, den Försten Omar, den Försten Zepho, den Försten Kenas,
16 Gatamu, na Amaleki. Hivi vilikuwa vizazi vya koo kutoka kwa Elifazi katika nchi ya Edomu. Walikuwa wajukuu wa Ada.
Den Försten Korah, den Försten Gatham, den Försten Amalek. Desse äro de Förstar af Eliphas i Edoms lande; och äro barn af Ada.
17 Hizi zilikuwa koo kutoka kwa Reueli, mwana wa Esau: Nahathi, Zera, Shama, Miza. Hizi zilikuwa koo kutoka kwa Reueli katika nchi ya Edomu. Walikuwa wajukuu wa Basemathi, mkewe Esau.
Och desse äro Reguels barn, Esau sons: Den Försten Nahath, den Försten Serah, den Försten Samma, den Försten Missa. Desse äro de Förstar af Reguel uti de Edomeers lande; och äro barn af Basmath, Esaus hustru.
18 Hizi zilikuwa koo za Oholibama, mkewe Esau: Yeushi, Yalamu, Kora. Hizi ni koo zilizotoka kwa Oholibama mkewe Esau, binti Ana.
Desse äro barn af Aholibama, Esaus hustru: Den Försten Jeus, den Försten Jaelam, den Försten Korah. Desse äro de Förstar af Aholibama Anas dotter, Esaus hustru.
19 Hawa walikuwa wana wa Esau na koo zao.
Desse äro Esaus barn, och deras Förstar; han är Edom.
20 Hawa walikuwa wana wa Seiri Mhori, wenyeji wa nchi hiyo: Lotani, Shobali, Zibeoni, Ana,
Men de barn af Seir den Horeen, som i landena bodde, äro desse: Lotan, Sobal, Zibeon, Ana,
21 Dishoni, Ezeri, na Dishani. Hizi zilikuwa koo the Wahori, wenyeji wa Seiri katika nchi ya Edomu.
Dison, Ezer och Disan. Desse äro de Förstar ibland de Horeer, alle Seirs barn i Edoms lande.
22 Wana wa Lotani walikuwa Hori na Hemani, na Timna alikuwa dada wa Lotani.
Men Lotans barn voro desse: Hori och Hemam; och Lotans syster het Thimna.
23 Hawa walikuwa wana wa Shobali: Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo, na Onamu.
Sobals barn voro desse: Alvan, Manahat, Ebal, Sepho och Onam.
24 Hawa walikuwa wana wa Zibeoni: Aia na Ana. Huyu ndiye Ana aliyeona chemichemi za moto nyikani, alipokuwa akichunga punda wa Zibeoni babaye.
Zibeons barn voro: Aja och Ana: Denne är den Ana, som i öknene påfann mular, då han vaktade sins faders Zibeons åsnar.
25 Hawa walikuwa watoto wa Ana: Dishoni na Oholibama, binti Ana.
Men Anas barn voro: Dison och Aholibama, det är Anas dotter.
26 Hawa walikuwa wana wa Dishoni: Hemdani, Eshbani, Ithrani, na Kerani.
Disons barn voro: Hemdan, Esban, Jithran och Cheran.
27 Hawa walikuwa wana wa Ezeri: Bilhani, Zaavani, na Akani.
Ezers barn voro: Bilhan, Saavan och Akan.
28 Hawa walikuwa wana wa Dishani: Uzi na Arani.
Disans barn voro: Uz och Aran.
29 Hizi zilikuwa koo za Wahori: Lotani, Shobali, Zibeoni, na Ana,
Desse äro de Förstar ibland de Horeer: Den Försten Lotan, den Försten Sobal, den Försten Zibeon, den Försten Ana.
30 Dishoni, Ezeri, Dishani: hizi zilikuwa koo za Wahori, kulingana na ukoo ulivyoorodheshwa katika nchi ya Seiri.
Den Försten Dison, den Försten Ezer, den Försten Disan. Desse äro de Förstar ibland de Horeer, de som regerade i Seirs lande.
31 Hawa walikuwa wafalme waliomiliki katika nchi ya Edomu kabla ya mfalme yeyote kumilika juu ya Waisraeli:
Men de Konungar, som i Edoms lande regerade, förra än Israels barn Konungar hade, äro desse:
32 Bela mwana wa Beori, alitawala huko Edomu, na jina la mji wake lilikuwa Dinhaba.
Bela var Konung i Edom, Beors son; och hans stad het Dinhaba.
33 Bela alipofariki, kisha Yobabu mwana wa Zera kutoka Bozra, akatawala mahali pake.
Och då Bela blef död, vardt Jobab Konung i hans stad, Seras son af Bozra.
34 Yobabu alipofariki, Hushamu aliyekuwa wa nchi ya Watemani, akatawala mahali pake.
Då Jobab blef död, vardt Husam utaf de Themaneers lande Konung i hans stad.
35 Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi aliyewashinda Wamidiani katika nchi ya Moabu, akatawala mahali pake. Jina la mji wake lilikuwa Avithi.
Då Husam blef död, vardt Konung i hans stad Hadad Bedads son, den som slog de Midianiter på de Moabiters mark; och hans stad het Avith.
36 Hadadi alipofariki, kisha Samla wa Masreka akatawala mahali pake.
Då Hadad blef död, vardt Samla af Masreka Konung i hans stad.
37 Samla alipofariki, kisha Shauli wa Rehobothi kando ya mto alitawala mahali pake.
Då Samla blef död, vardt Konung i hans stad Saul af Rehoboth vid älfvena.
38 Shauli alipofariki, kisha Baali Hanani mwana wa Akbori akatawala mahali pake.
Då Saul blef död, vardt Baalhanan Achbors son Konung i hans stad.
39 Baali Hanani mwana wa Akbori, alipokufa, kisha Hadari akatawala mahali pake. Jina la mji wake lilikuwa Pau. Jina la mkewe lilikuwa Mehetabeli, binti Matredi, mjukuu wa Me Zahabu.
Då Baalhanan Achbors son blef död, vardt Hadar Konung i hans stad: Och hans stad het Pagu; och hans hustru het Mehetabeel, Matreds dotter, och Mesahabs dotter.
40 Haya ndiyo yalikuwa majina ya wakuu wa koo kutoka uzao wa Esau, kwa kufuata koo zao na maeneo yao, kwa majina yao: Timna, Alva, Yethethi,
Alltså heta de Förstar af Esau i deras slägter, rummom och namnom: Den Försten Thimna, den Försten Alva, den Försten Jetheth,
41 Oholibama, Ela, Pinoni,
Den Försten Aholibama, den Försten Ela, den Försten Pinon,
42 Kenazi, Temani, Mbza,
Den Försten Kenas, den Försten Theman, den Försten Mibzar,
43 Magdieli, na Iramu. Hawa walikuwa wakuu wa ukoo wa Edomu, kwa kufuata makao yao katika nchi waliyomiliki. Nao ni Esau, baba wa Waedomu.
Den Försten Magdiel, den Försten Iram. Desse äro de Förstar i Edom, såsom de bott hafva uti deras arfvelande. Och Esau är fadren till de Edomeer.

< Mwanzo 36 >