< Mwanzo 36 >
1 Hivi ndivyo vizazi vya Esau (aliyeitwa pia Edom).
Estas son las generaciones de Esaú, es decir, Edom.
2 Esau akachukua wakeze kutoka kwa Wakanaani. Hawa walikuwa wake zake: Ada binti Eloni Mhiti; Oholibama binti Ana, mjukuu wa Zibeoni Mhivi; na
Las mujeres de Esaú eran mujeres de Canaán: Ada, la hija de Elón el hitita, y Aholibama, hija de Aná, hija de Zibeón el heveo,
3 Basemathi, binti Ishmaeli, dada wa Nebayothi.
Y Basemat, hija de Ismael, hermana de Nebaiot.
4 Ada akamzaa Elifazi kwa Esau, na Basemathi akamzaa Reueli.
Ada tenía un hijo Elifaz; y Basemat era la madre de Reuel;
5 Oholibama akamzaa Yeushi, Yalamu, na Kora. Hawa walikuwa wana wa Esau waliozaliwa kwake katika nchi ya Kananaani.
Aholibama era la madre de Jeús, Jaalam y Coré; estos son los hijos de Esaú, cuyo nacimiento tuvo lugar en la tierra de Canaán.
6 Esau akawachukua wakeze, wanawe, binti zake, na watu wote wa nyumba yake, mifugo wake - wanyama wake wote, na mali yake yote, aliyokuwa amekusanya katika nchi ya Kanaani, na akaenda katika nchi iliyoko mbali kutoka kwa Yakobo nduguye.
Esaú tomó sus mujeres, sus hijos, sus hijas, y todo el pueblo de su casa, y sus bestias, y sus ganados, y todos sus bienes que había juntado en la tierra de Canaán, y se fue a la tierra de Seir, lejos de su hermano Jacob.
7 Alifanya hivi kwa sababu mali zao zilikuwa nyingi sana kwa wao kuishi pamoja. Nchi waliyokuwa wamekaa isingeweza kuwafaa kwa mifugo yao.
porque su riqueza era tan grande que la tierra no era lo suficientemente amplia para ellos dos y todo su ganado.
8 Hivyo Esau, aliyejulikana pia kama Edomu, akakaa katika nchi ya kilima Seiri.
Así edificó Esaú su lugar de residencia en la región montañosa de Seir (Esaú es Edom).
9 Hivi ndivyo vizazi vya Esau, babu wa Waedomu katika nchi ya mlima Seiri.
Y estas son las generaciones de Esaú, el padre de los edomitas en el monte de Seir:
10 Haya yalikuwa majina ya wana wa Esau: Elifazi mwana wa Ada, mkewe Esau; Reueli mwana wa Basemathi, mkewe Esau.
Estos son los nombres de los hijos de Esaú: Elifaz, hijo de la mujer de Esaú, Ada, y Reuel, hijo de Basemath, la mujer de Esaú.
11 Wana wa Elifazi walikuwa Temani, Omari, Zefo, Gatamu, na Kenazi.
Los hijos de Elifaz fueron Temán, Omar, Zefo, Gatam y Cenaz.
12 Timna, suria wa Elifazi, mwana wa Esau, akamzaa Amaleki. Hawa walikuwa wajukuu wa Ada, mkewe Esau.
Y Elifaz, hijo de Esaú, tuvo una relación con una mujer llamada Timna, que dio a luz a Amalec; todos estos fueron hijos de Ada, la mujer de Esaú.
13 Hawa walikuwa wana wa Reueli: Nahathi, Zera, Shama, na Miza. Hawa walikuwa wajukuu wa Basemathi, mkewe Esau.
Y estos son los hijos de Reuel: Nahat, Zera, Sama, y Miza; fueron hijos de la mujer de Esaú, Basemat.
14 Hawa walikuwa wana wa Oholibama, mkewe Esau, aliyekuwa binti Ana na mjukuu wa Zibeoni. Alimzalia Esau Yeushi, Yalamu, na Kora.
Y estos son los hijos de Aholibama, hija de Aná, hija de Zibeón, que fué madre de Jeús, Jalam y Coré.
15 Hizi zilikuwa koo kati ya vizazi vya Esau: uzao wa Elifazi, mzaliwa wa kwanza wa Esau: Temani, Omari, Zefo, Kenazi, Kora,
Estos fueron los jefes entre los hijos de Esaú: los hijos de Elifaz, el primer hijo de Esaú: Temán, Omar, Zefo, Cenaz,
16 Gatamu, na Amaleki. Hivi vilikuwa vizazi vya koo kutoka kwa Elifazi katika nchi ya Edomu. Walikuwa wajukuu wa Ada.
Coré, Gatam, Amalec: todos estos fueron los jefes en la tierra de Edom, los hijos de Elifaz, la simiente de Ada.
17 Hizi zilikuwa koo kutoka kwa Reueli, mwana wa Esau: Nahathi, Zera, Shama, Miza. Hizi zilikuwa koo kutoka kwa Reueli katika nchi ya Edomu. Walikuwa wajukuu wa Basemathi, mkewe Esau.
Y estos son los hijos de Reuel, hijo de Esaú: Nahat, Zera, Sama, Miza; estos fueron los jefes de Reuel en la tierra de Edom, los hijos de Basemat, la mujer de Esaú.
18 Hizi zilikuwa koo za Oholibama, mkewe Esau: Yeushi, Yalamu, Kora. Hizi ni koo zilizotoka kwa Oholibama mkewe Esau, binti Ana.
Y estos son los hijos de Aholibama, la mujer de Esaú: Jeús, Jalam y Coré: estos fueron los jefes que vinieron de la mujer de Esaú, Aholibama, hija de Ana.
19 Hawa walikuwa wana wa Esau na koo zao.
Estos fueron los hijos de Esaú (es decir, Edom), y éstos fueron sus jefes.
20 Hawa walikuwa wana wa Seiri Mhori, wenyeji wa nchi hiyo: Lotani, Shobali, Zibeoni, Ana,
Estos son los hijos de Seir el horeo que vivían en ese país; Lotán, Sobal, Zibeon, Ana,
21 Dishoni, Ezeri, na Dishani. Hizi zilikuwa koo the Wahori, wenyeji wa Seiri katika nchi ya Edomu.
Disón, Ezer y Disán: estos son los jefes de los horeos, hijos de Seir, en la tierra de Edom.
22 Wana wa Lotani walikuwa Hori na Hemani, na Timna alikuwa dada wa Lotani.
Los hijos de Lotán fueron Hori y Hemam; La hermana de Lotan era Timna.
23 Hawa walikuwa wana wa Shobali: Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo, na Onamu.
Y estos son los hijos de Sobal: Alvan, Manahat, Ebal, Sefo y Onam.
24 Hawa walikuwa wana wa Zibeoni: Aia na Ana. Huyu ndiye Ana aliyeona chemichemi za moto nyikani, alipokuwa akichunga punda wa Zibeoni babaye.
Y estos son los hijos de Zibeón: Aja y Aná; el mismo Ana que hizo el descubrimiento de los manantiales en la tierra baldía, cuando estaba cuidando los asnos de su padre Zibeon.
25 Hawa walikuwa watoto wa Ana: Dishoni na Oholibama, binti Ana.
Y estos son los hijos de Aná: Disón y Aholibama su hija.
26 Hawa walikuwa wana wa Dishoni: Hemdani, Eshbani, Ithrani, na Kerani.
Estos son los hijos de Disón: Hemdan, Esban, Itran y Queran.
27 Hawa walikuwa wana wa Ezeri: Bilhani, Zaavani, na Akani.
Estos son los hijos de Ezer: Bilhan, Zaavan y Acan.
28 Hawa walikuwa wana wa Dishani: Uzi na Arani.
Estos son los hijos de Disán: Uz y Arán.
29 Hizi zilikuwa koo za Wahori: Lotani, Shobali, Zibeoni, na Ana,
Estos fueron los jefes de los horeos: Lotán, Sobal, Zibeón, Aná,
30 Dishoni, Ezeri, Dishani: hizi zilikuwa koo za Wahori, kulingana na ukoo ulivyoorodheshwa katika nchi ya Seiri.
Disón, Ezer y Disán. Tales fueron los jefes horeos en su orden en la tierra de Seir.
31 Hawa walikuwa wafalme waliomiliki katika nchi ya Edomu kabla ya mfalme yeyote kumilika juu ya Waisraeli:
Y estos son los reyes que gobernaban en la tierra de Edom antes que hubiera rey sobre los hijos de Israel.
32 Bela mwana wa Beori, alitawala huko Edomu, na jina la mji wake lilikuwa Dinhaba.
Bela, hijo de Beor, fue rey en Edom, y el nombre de su ciudad principal fue Dinaba.
33 Bela alipofariki, kisha Yobabu mwana wa Zera kutoka Bozra, akatawala mahali pake.
En su muerte, Jobab, hijo de Zera de Bosra, fue rey en su lugar.
34 Yobabu alipofariki, Hushamu aliyekuwa wa nchi ya Watemani, akatawala mahali pake.
Y a la muerte de Jobab, Husam, de la tierra de los temanitas, llegó a ser rey en su lugar.
35 Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi aliyewashinda Wamidiani katika nchi ya Moabu, akatawala mahali pake. Jina la mji wake lilikuwa Avithi.
Y a la muerte de Husam, Hadad, hijo de Bedad, que venció a los madianitas en el campo de Moab, llegó a ser rey; su ciudad principal fue llamada Avit.
36 Hadadi alipofariki, kisha Samla wa Masreka akatawala mahali pake.
Y a la muerte de Hadad, Samlat de Masreca se convirtió en rey.
37 Samla alipofariki, kisha Shauli wa Rehobothi kando ya mto alitawala mahali pake.
Y a la muerte de Samla, Saúl de Rehobot junto al río se hizo rey en su lugar.
38 Shauli alipofariki, kisha Baali Hanani mwana wa Akbori akatawala mahali pake.
Y a la muerte de Saúl, Baal-hanán, hijo de Acbor, se hizo rey.
39 Baali Hanani mwana wa Akbori, alipokufa, kisha Hadari akatawala mahali pake. Jina la mji wake lilikuwa Pau. Jina la mkewe lilikuwa Mehetabeli, binti Matredi, mjukuu wa Me Zahabu.
Y en la muerte de Baal-hanan, Hadar se hizo rey en su lugar; su ciudad principal se llamaba Pau, y el nombre de su esposa era Mehetabel; ella era la hija de Matred, la hija de Mezaab.
40 Haya ndiyo yalikuwa majina ya wakuu wa koo kutoka uzao wa Esau, kwa kufuata koo zao na maeneo yao, kwa majina yao: Timna, Alva, Yethethi,
Estos son los nombres de los jefes de Esaú por orden de sus familias y sus lugares: Timna, Alva, Jetet,
41 Oholibama, Ela, Pinoni,
Aholibama, Elah, Pinón,
43 Magdieli, na Iramu. Hawa walikuwa wakuu wa ukoo wa Edomu, kwa kufuata makao yao katika nchi waliyomiliki. Nao ni Esau, baba wa Waedomu.
Magdiel, Iram; estos son los jefes edomitas, en sus lugares en su herencia; este es Esaú, el padre de los edomitas.