< Mwanzo 36 >
1 Hivi ndivyo vizazi vya Esau (aliyeitwa pia Edom).
hae sunt autem generationes Esau ipse est Edom
2 Esau akachukua wakeze kutoka kwa Wakanaani. Hawa walikuwa wake zake: Ada binti Eloni Mhiti; Oholibama binti Ana, mjukuu wa Zibeoni Mhivi; na
Esau accepit uxores de filiabus Chanaan Ada filiam Elom Hetthei et Oolibama filiam Anae filiae Sebeon Evei
3 Basemathi, binti Ishmaeli, dada wa Nebayothi.
Basemath quoque filiam Ismahel sororem Nabaioth
4 Ada akamzaa Elifazi kwa Esau, na Basemathi akamzaa Reueli.
peperit autem Ada Eliphaz Basemath genuit Rauhel
5 Oholibama akamzaa Yeushi, Yalamu, na Kora. Hawa walikuwa wana wa Esau waliozaliwa kwake katika nchi ya Kananaani.
Oolibama edidit Hieus et Hielom et Core hii filii Esau qui nati sunt ei in terra Chanaan
6 Esau akawachukua wakeze, wanawe, binti zake, na watu wote wa nyumba yake, mifugo wake - wanyama wake wote, na mali yake yote, aliyokuwa amekusanya katika nchi ya Kanaani, na akaenda katika nchi iliyoko mbali kutoka kwa Yakobo nduguye.
tulit autem Esau uxores suas et filios et filias et omnem animam domus suae et substantiam et pecora et cuncta quae habere poterat in terra Chanaan et abiit in alteram regionem recessitque a fratre suo Iacob
7 Alifanya hivi kwa sababu mali zao zilikuwa nyingi sana kwa wao kuishi pamoja. Nchi waliyokuwa wamekaa isingeweza kuwafaa kwa mifugo yao.
divites enim erant valde et simul habitare non poterant nec sustinebat eos terra peregrinationis eorum prae multitudine gregum
8 Hivyo Esau, aliyejulikana pia kama Edomu, akakaa katika nchi ya kilima Seiri.
habitavitque Esau in monte Seir ipse est Edom
9 Hivi ndivyo vizazi vya Esau, babu wa Waedomu katika nchi ya mlima Seiri.
hae sunt generationes Esau patris Edom in monte Seir
10 Haya yalikuwa majina ya wana wa Esau: Elifazi mwana wa Ada, mkewe Esau; Reueli mwana wa Basemathi, mkewe Esau.
et haec nomina filiorum eius Eliphaz filius Ada uxoris Esau Rauhel quoque filius Basemath uxoris eius
11 Wana wa Elifazi walikuwa Temani, Omari, Zefo, Gatamu, na Kenazi.
fueruntque filii Eliphaz Theman Omar Sephu et Gatham et Cenez
12 Timna, suria wa Elifazi, mwana wa Esau, akamzaa Amaleki. Hawa walikuwa wajukuu wa Ada, mkewe Esau.
erat autem Thamna concubina Eliphaz filii Esau quae peperit ei Amalech hii sunt filii Adae uxoris Esau
13 Hawa walikuwa wana wa Reueli: Nahathi, Zera, Shama, na Miza. Hawa walikuwa wajukuu wa Basemathi, mkewe Esau.
filii autem Rauhel Naath et Zara Semma et Meza hii filii Basemath uxoris Esau
14 Hawa walikuwa wana wa Oholibama, mkewe Esau, aliyekuwa binti Ana na mjukuu wa Zibeoni. Alimzalia Esau Yeushi, Yalamu, na Kora.
isti quoque erant filii Oolibama filiae Ana filiae Sebeon uxoris Esau quos genuit ei Hieus et Hielom et Core
15 Hizi zilikuwa koo kati ya vizazi vya Esau: uzao wa Elifazi, mzaliwa wa kwanza wa Esau: Temani, Omari, Zefo, Kenazi, Kora,
hii duces filiorum Esau filii Eliphaz primogeniti Esau dux Theman dux Omar dux Sephu dux Cenez
16 Gatamu, na Amaleki. Hivi vilikuwa vizazi vya koo kutoka kwa Elifazi katika nchi ya Edomu. Walikuwa wajukuu wa Ada.
dux Core dux Gatham dux Amalech hii filii Eliphaz in terra Edom et hii filii Adae
17 Hizi zilikuwa koo kutoka kwa Reueli, mwana wa Esau: Nahathi, Zera, Shama, Miza. Hizi zilikuwa koo kutoka kwa Reueli katika nchi ya Edomu. Walikuwa wajukuu wa Basemathi, mkewe Esau.
hii quoque filii Rauhel filii Esau dux Naath dux Zara dux Semma dux Meza hii duces Rauhel in terra Edom isti filii Basemath uxoris Esau
18 Hizi zilikuwa koo za Oholibama, mkewe Esau: Yeushi, Yalamu, Kora. Hizi ni koo zilizotoka kwa Oholibama mkewe Esau, binti Ana.
hii autem filii Oolibama uxoris Esau dux Hieus dux Hielom dux Core hii duces Oolibama filiae Ana uxoris Esau
19 Hawa walikuwa wana wa Esau na koo zao.
isti filii Esau et hii duces eorum ipse est Edom
20 Hawa walikuwa wana wa Seiri Mhori, wenyeji wa nchi hiyo: Lotani, Shobali, Zibeoni, Ana,
isti filii Seir Horrei habitatores terrae Lotham et Sobal et Sebeon et Anan
21 Dishoni, Ezeri, na Dishani. Hizi zilikuwa koo the Wahori, wenyeji wa Seiri katika nchi ya Edomu.
Dison et Eser et Disan hii duces Horrei filii Seir in terra Edom
22 Wana wa Lotani walikuwa Hori na Hemani, na Timna alikuwa dada wa Lotani.
facti sunt autem filii Lotham Horrei et Heman erat autem soror Lotham Thamna
23 Hawa walikuwa wana wa Shobali: Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo, na Onamu.
et isti filii Sobal Alvam et Maneeth et Hebal Sephi et Onam
24 Hawa walikuwa wana wa Zibeoni: Aia na Ana. Huyu ndiye Ana aliyeona chemichemi za moto nyikani, alipokuwa akichunga punda wa Zibeoni babaye.
et hii filii Sebeon Ahaia et Anam iste est Ana qui invenit aquas calidas in solitudine cum pasceret asinos Sebeon patris sui
25 Hawa walikuwa watoto wa Ana: Dishoni na Oholibama, binti Ana.
habuitque filium Disan et filiam Oolibama
26 Hawa walikuwa wana wa Dishoni: Hemdani, Eshbani, Ithrani, na Kerani.
et isti filii Disan Amdan et Esban et Iethran et Charan
27 Hawa walikuwa wana wa Ezeri: Bilhani, Zaavani, na Akani.
hii quoque filii Eser Balaan et Zevan et Acham
28 Hawa walikuwa wana wa Dishani: Uzi na Arani.
habuit autem filios Disan Hus et Aran
29 Hizi zilikuwa koo za Wahori: Lotani, Shobali, Zibeoni, na Ana,
isti duces Horreorum dux Lothan dux Sobal dux Sebeon dux Ana
30 Dishoni, Ezeri, Dishani: hizi zilikuwa koo za Wahori, kulingana na ukoo ulivyoorodheshwa katika nchi ya Seiri.
dux Dison dux Eser dux Disan isti duces Horreorum qui imperaverunt in terra Seir
31 Hawa walikuwa wafalme waliomiliki katika nchi ya Edomu kabla ya mfalme yeyote kumilika juu ya Waisraeli:
reges autem qui regnaverunt in terra Edom antequam haberent regem filii Israhel fuerunt hii
32 Bela mwana wa Beori, alitawala huko Edomu, na jina la mji wake lilikuwa Dinhaba.
Bale filius Beor nomenque urbis eius Denaba
33 Bela alipofariki, kisha Yobabu mwana wa Zera kutoka Bozra, akatawala mahali pake.
mortuus est autem Bale et regnavit pro eo Iobab filius Zare de Bosra
34 Yobabu alipofariki, Hushamu aliyekuwa wa nchi ya Watemani, akatawala mahali pake.
cumque mortuus esset Iobab regnavit pro eo Husan de terra Themanorum
35 Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi aliyewashinda Wamidiani katika nchi ya Moabu, akatawala mahali pake. Jina la mji wake lilikuwa Avithi.
hoc quoque mortuo regnavit pro eo Adad filius Badadi qui percussit Madian in regione Moab et nomen urbis eius Ahuith
36 Hadadi alipofariki, kisha Samla wa Masreka akatawala mahali pake.
cumque mortuus esset Adad regnavit pro eo Semla de Maserecha
37 Samla alipofariki, kisha Shauli wa Rehobothi kando ya mto alitawala mahali pake.
hoc quoque mortuo regnavit pro eo Saul de fluvio Rooboth
38 Shauli alipofariki, kisha Baali Hanani mwana wa Akbori akatawala mahali pake.
cumque et hic obisset successit in regnum Baalanam filius Achobor
39 Baali Hanani mwana wa Akbori, alipokufa, kisha Hadari akatawala mahali pake. Jina la mji wake lilikuwa Pau. Jina la mkewe lilikuwa Mehetabeli, binti Matredi, mjukuu wa Me Zahabu.
isto quoque mortuo regnavit pro eo Adad nomenque urbis eius Phau et appellabatur uxor illius Meezabel filia Matred filiae Mizaab
40 Haya ndiyo yalikuwa majina ya wakuu wa koo kutoka uzao wa Esau, kwa kufuata koo zao na maeneo yao, kwa majina yao: Timna, Alva, Yethethi,
haec ergo nomina Esau in cognationibus et locis et vocabulis suis dux Thamna dux Alva dux Ietheth
41 Oholibama, Ela, Pinoni,
dux Oolibama dux Ela dux Phinon
dux Cenez dux Theman dux Mabsar
43 Magdieli, na Iramu. Hawa walikuwa wakuu wa ukoo wa Edomu, kwa kufuata makao yao katika nchi waliyomiliki. Nao ni Esau, baba wa Waedomu.
dux Mabdiel dux Iram hii duces Edom habitantes in terra imperii sui ipse est Esau pater Idumeorum