< Mwanzo 35 >
1 Mungu akamwambia Yakobo, “Inuka, panda kwenda Betheli, na ukae pale. Unijengee madhabahu pale, niliyekutokea pale ulipomkimbia Esau kaka yako.”
And God sayd vnto Iacob aryse ad get the vp to Bethell and dwell there. And make there an aulter vnto God that apeared vnto the when thou fleddest from Esau thy brother.
2 Kisha Yakobo akawambia nyumba yake na wote aliokuwa nao, “Wekeni mbali miungu yote ya kigeni iliyo kati yenu, jitakaseni wenyewe, na kubadili mavazi yenu.
Than sayd Iacob vnto his housholde and to all yt were with him put away the strauge goddes that are amonge you and make youre selues cleane and chaunge youre garmetes
3 Kisha tuondoke na kwenda Betheli. Nitajenga pale madhabahu kwa Mungu, aliyenijibu katika siku ya shida yangu, naye amekuwa pamoja nami kila nilikokwenda.
and let vs aryse and goo vp to Bethell yt I maye make an aulter there vnto God which herde me in the daye of my tribulatio and was wyth me in the waye which I went.
4 Hivyo wakampa Yakobo miungu yote ya kigeni iliyokuwa mikononi mwao, na heleni zilizokuwa katika masikio yao. Yakobo akazifukia chini ya mwaloni uliokuwa karibu na Shekemu.
And they gaue vnto Iacob all the straunge goddes which were vnder their handes ad all their earynges which were in their eares and Iacob hyd them vnder an ooke at Sichem.
5 Kwa kadili walivyo safiri, Mungu akaifanya miji yote iliyokuwa karibu nao kuhofu, hivyo watu hao hawakuwafuatia wana wa Yakobo.
And they departed. And the feare of God fell vpon the cyties that were rounde aboute them that they durst not folowe after the sonnes of Iacob.
6 Hivyo Yakobo akafika Luzu(ndiyo Betheli), ulioko katika nchi ya Kanaani, yeye na watu wote aliokuwa nao.
So came Iacob to Lus in the lande of Canaan otherwise called Bethell with all the people that was with him.
7 Alijenge madhabahu na kuliita eneo hilo El Betheli, kwa sababu Mungu alikuwa amejifunua kwake, alipokuwa akimkimbia ndugu yake.
And he buylded there an aulter and called the place Elbethell: because that God appered vnto him there when he fled from his brother.
8 Debora, mlezi wa Rebeka, akafa. Akazikwa chini kutoka Betheli chini ya mwaloni, hivyo ikaitwa Aloni Bakuthi.
Than dyed Deborr Rebeccas norse and was buryed benethe Bethell vnder an ooke. And the name of it was called the ooke of lamentation.
9 Yakobo alipokuja kutoka Padani Aramu, Mungu akamtokea tena na kumbariki.
And God appeared vnto Iacob agayne after he came out of Mesopotamia and blessed him
10 Mungu akamwambia, “Jina lako ni Yakobo, lakini jina lako halitakuwa Yakobo tena. Jina lako litakuwa Israeli.” Hivyo Mungu akamwita jina lake Israeli.
and sayde vnto him: thy name is Iacob. Notwithstondynge thou shalt be nomore called Iacob but Israel shalbe thy name. And so was his name called Israell.
11 Mungu akamwambia, “Mimi ni Mungu Mwenyezi, Uwe mwenye kuzaa na kuongezeka. Taifa na wingi wa mataifa watakujia, na wafalme watatoka miongoni mwa uzao wako.
And God sayde vnto him: I am God allmightie growe and multiplye: for people and a multitude of people shall sprynge of the yee ad kynges shall come out of they loynes.
12 Nchi ambayo nilimpa Ibrahimu na Isaka, nitakupa wewe. Nami nitaupa pia uzao wako baada yako nchi hii.”
And the lande which I gaue Abraha and Isaac will I geue vnto the and vnto thi seed after the will I geue it also.
13 Mungu akapanda kutoka mahali alipoongea naye.
And god departed fro him in the place where he talked with him.
14 Yakobo akaweka nguzo katika eneo ambalo Mungu alikuwa ameongea naye, nguzo ya jiwe. Akamimina juu yake sadaka ya kinywaji na akamimina mafuta juu yake.
And Iacob set vp a marke in the place where he talked with him: euen a pilloure of stone and powred drynkeoffringe theron and powred also oyle theron
15 Yakobo akaiita sehemu Mungu aliyoongea naye, Betheli
and called the name of the place where God spake with him Bethell.
16 Wakaendelea na safari kutoka Betheli. Walipokuwa kitambo kabla ya kufika Efrathi, Raheli akashikwa na uchungu.
And they departed from Bethel and when he was but a feld brede from Ephrath Rahel began to trauell. And in travelynge she was in perell.
17 Akawa na utungu mzito. Alipokuwa katika utungu mzito zaidi, mkunga akamwambia, “Usiogope, kwani sasa utapata mtoto mwingine wa kiume.”
And as she was in paynes of hir laboure the mydwyfe sayde vnto her: feare not for thou shalt haue this sonne also.
18 Hata alipokaribia kufa, kwa pumzi yake ya mwisho akamwita jina lake Benoni, lakini baba yake akamwita jina lake Benjamini.
Then as hir soule was a departinge that she must dye: she called his name Ben Oni. But his father called him Ben Iamin.
19 Raheli akafa na kuzikwa katika njia iendayo Efrathi (ndio Bethlehemu).
And thus dyed Rahel ad was buryed in the waye to Ephrath which now is called Bethlehem.
20 Yakobo akaweka nguzo katika kaburi lake. Ndiyo alama ya kaburi la Raheli hata leo.
And Iacob sett vp a piller apon hir graue which is called Rahels graue piller vnto this daye.
21 Israeli akaendelea na safari na akaweka hema yake kuvuka mnara wa walinzi wa kondoo.
And Israell went thece and pitched vp his tent beyonde the toure of Eder.
22 Yakobo alipokuwa akiishi katika nchi hiyo, Rubeni akalala na Bilha suria wa baba yake, na Israeli akasikia kuhusu hilo. Basi Yakobo alikuwa na wana kumi na mbili.
And it chaunced as Israel dwelt in that lande that Ruben went and laye with Bilha his fathers concubyne and it came to Israels eare. The sonnes of Iacob were. xij. in nombre.
23 Wanawe kwa Lea walikuwa Rubeni, mzaliwa wa kwanza wa Yakobo, na Simoni, Lawi, Yuda, Isakari, na Zabuloni.
The sonnes of Lea. Ruben Iacobs eldest sonne and Simeo Leui Iuda Isachar and Zabulon
24 Wanawe kwa Raheli walikuwa Yusufu na Benjamini.
The sonnes of Rahel: Ioseph and Ben Iamin.
25 Wanawe kwa Bilha, mjakazi wa Raheli walikuwa Dani na Naftali.
The sonnes of Bilha Rahels mayde: Dan and Nepthali.
26 Wana wa Zilpa, mjakazi wa Lea, walikuwa Gadi na Asheri. Hawa wote walikuwa wana wa Yakobo waliozaliwa kwake huko Padani Aramu.
The sonnes of Zilpha Leas mayde Gad and Aser. Thes are the sones of Iacob which were borne him in Mesopotamia.
27 Yakobo akaja kwa Isaka, baba yake, huko Mamre katika Kiriathi Arba (jina sawa na Hebroni), alipoishi Ibrahimu na Isaka.
Then Iacob went vnto Isaac his father to Mamre a pricipall cyte otherwise called Hebron: where Abraha and Isaac sogeorned as straungers.
28 Isaka akaishi miaka mia moja na themanini.
And the dayes of Isaac were an hundred and. lxxx. yeres:
29 Isaka akapumua pumzi yake ya mwisho na akafa, na akakusanywa kwa wahenga wake, na mtu mzee amejaa siku. Esau na Yakobo, wanawe, wakamzika.
and than fell he seke and dyed ad was put vnto his people: beynge olde and full of dayes. And his sonnes Esau ad Iacob buried him.