< Mwanzo 35 >
1 Mungu akamwambia Yakobo, “Inuka, panda kwenda Betheli, na ukae pale. Unijengee madhabahu pale, niliyekutokea pale ulipomkimbia Esau kaka yako.”
Then said God unto Jacob, Arise, go up to Bethel, and dwell there, —and make there an altar, to the GOD who appeared unto thee, when thou fleddest from the face of Esau thy brother.
2 Kisha Yakobo akawambia nyumba yake na wote aliokuwa nao, “Wekeni mbali miungu yote ya kigeni iliyo kati yenu, jitakaseni wenyewe, na kubadili mavazi yenu.
And Jacob said unto his house, and unto all who were with him, —Put away the gods of the alien which are in your midst, and purify yourselves, and change your garments;
3 Kisha tuondoke na kwenda Betheli. Nitajenga pale madhabahu kwa Mungu, aliyenijibu katika siku ya shida yangu, naye amekuwa pamoja nami kila nilikokwenda.
And let us arise, and go up to Beth-el, —that I may make there an altar to the GOD who answered me in the day of my distress, and was with me in the way that I went.
4 Hivyo wakampa Yakobo miungu yote ya kigeni iliyokuwa mikononi mwao, na heleni zilizokuwa katika masikio yao. Yakobo akazifukia chini ya mwaloni uliokuwa karibu na Shekemu.
So they gave unto Jacob all the gods of the alien which were in their hand, and the earrings which were in their ears, —and Jacob hid them under the oak, which was by Shechem.
5 Kwa kadili walivyo safiri, Mungu akaifanya miji yote iliyokuwa karibu nao kuhofu, hivyo watu hao hawakuwafuatia wana wa Yakobo.
And they brake up, —and it came to pass that the terror of God, was on the cities which were round about them, so that they pursued not after the sons of Jacob.
6 Hivyo Yakobo akafika Luzu(ndiyo Betheli), ulioko katika nchi ya Kanaani, yeye na watu wote aliokuwa nao.
And Jacob came in towards Luz, which was in the land of Canaan, the same, is Beth-el, —he and all the people who were with him.
7 Alijenge madhabahu na kuliita eneo hilo El Betheli, kwa sababu Mungu alikuwa amejifunua kwake, alipokuwa akimkimbia ndugu yake.
And he built there an altar, and called the place El-Beth-el, —because, there, God revealed himself unto him, when he fled from the face of his brother,
8 Debora, mlezi wa Rebeka, akafa. Akazikwa chini kutoka Betheli chini ya mwaloni, hivyo ikaitwa Aloni Bakuthi.
And Deborah, Rebekah’s nurse died, and was buried below Beth-el, under the oak, —so the name thereof was called, Allon-bacuth.
9 Yakobo alipokuja kutoka Padani Aramu, Mungu akamtokea tena na kumbariki.
And God appeared unto Jacob again, when he came in from Padan-aram, —and blessed him.
10 Mungu akamwambia, “Jina lako ni Yakobo, lakini jina lako halitakuwa Yakobo tena. Jina lako litakuwa Israeli.” Hivyo Mungu akamwita jina lake Israeli.
And God said to him, Thy name, is Jacob, —Thy name shall no longer be called Jacob But, Israel, shall be thy name. So he called his name, Israel.
11 Mungu akamwambia, “Mimi ni Mungu Mwenyezi, Uwe mwenye kuzaa na kuongezeka. Taifa na wingi wa mataifa watakujia, na wafalme watatoka miongoni mwa uzao wako.
And God said to him—I, am GOD Almighty! Be fruitful and multiply, A nation, and a multitude of nations shall spring from thee, —And, kings, from thy loins, shall come forth;
12 Nchi ambayo nilimpa Ibrahimu na Isaka, nitakupa wewe. Nami nitaupa pia uzao wako baada yako nchi hii.”
And, the land which I gave to Abraham and to Isaac, To thee, will I give it, —And to thy seed after thee, will I give the land.
13 Mungu akapanda kutoka mahali alipoongea naye.
And God went up from him at the place where he had spoken with him.
14 Yakobo akaweka nguzo katika eneo ambalo Mungu alikuwa ameongea naye, nguzo ya jiwe. Akamimina juu yake sadaka ya kinywaji na akamimina mafuta juu yake.
And Jacob set up a pillar in the place where he had spoken with him, a pillar of stone, —and he poured out thereon a drink-offering, and poured thereon oil.
15 Yakobo akaiita sehemu Mungu aliyoongea naye, Betheli
And Jacob called the name of the place where God had spoken with him, Beth-el.
16 Wakaendelea na safari kutoka Betheli. Walipokuwa kitambo kabla ya kufika Efrathi, Raheli akashikwa na uchungu.
Then brake they up from Beth-el, and it came to pass when there was yet a stretch of country, to enter into Ephrath, that Rachel was in childbirth, and had hard-labour in her child-birth.
17 Akawa na utungu mzito. Alipokuwa katika utungu mzito zaidi, mkunga akamwambia, “Usiogope, kwani sasa utapata mtoto mwingine wa kiume.”
So it came to pass when she was in hard-labour in her child-birth, that the midwife said to her—Do not fear, for this also of thine, is, a son.
18 Hata alipokaribia kufa, kwa pumzi yake ya mwisho akamwita jina lake Benoni, lakini baba yake akamwita jina lake Benjamini.
And it came to pass when her soul was going forth—for she died, that she called his name Ben-oni, —but, his father, called him, Ben-jamin.
19 Raheli akafa na kuzikwa katika njia iendayo Efrathi (ndio Bethlehemu).
So Rachel died, —and was buried on the way to Ephrath, the same, is Bethlehem.
20 Yakobo akaweka nguzo katika kaburi lake. Ndiyo alama ya kaburi la Raheli hata leo.
And Jacob set up a pillar, over her grave, —the same, is—The Pillar of the Grave of Rachel until this day.
21 Israeli akaendelea na safari na akaweka hema yake kuvuka mnara wa walinzi wa kondoo.
Then Israel brake up, —and spread his tent at a distance from Migdal Eder.
22 Yakobo alipokuwa akiishi katika nchi hiyo, Rubeni akalala na Bilha suria wa baba yake, na Israeli akasikia kuhusu hilo. Basi Yakobo alikuwa na wana kumi na mbili.
And it came to pass while Israel inhabited that land, that Reuben went and lay with Bilhah his father’s concubine; and Israel heard of it. And so the Sons of Israel came to be Twelve.
23 Wanawe kwa Lea walikuwa Rubeni, mzaliwa wa kwanza wa Yakobo, na Simoni, Lawi, Yuda, Isakari, na Zabuloni.
The sons of Leah, the firstborn of Jacob, Reuben, —And Simeon and Levi and Judah, and Issachar and Zebulon:
24 Wanawe kwa Raheli walikuwa Yusufu na Benjamini.
The sons of Rachel, Joseph and Benjamin:
25 Wanawe kwa Bilha, mjakazi wa Raheli walikuwa Dani na Naftali.
And the sons of Bilhah, handmaid of Rachel, Dan, and Naphtali:
26 Wana wa Zilpa, mjakazi wa Lea, walikuwa Gadi na Asheri. Hawa wote walikuwa wana wa Yakobo waliozaliwa kwake huko Padani Aramu.
And the sons of Zilpah, handmaid of Leah, Gad and Asher: These, are the sons of Jacob, who were born to him, in Padan-aram.
27 Yakobo akaja kwa Isaka, baba yake, huko Mamre katika Kiriathi Arba (jina sawa na Hebroni), alipoishi Ibrahimu na Isaka.
Then came Jacob unto Isaac his father, to Mamre, the city of Arba, —the same, is Hebron, where had sojourned Abraham and Isaac.
28 Isaka akaishi miaka mia moja na themanini.
And the days of Isaac came to be—a hundred and eighty years.
29 Isaka akapumua pumzi yake ya mwisho na akafa, na akakusanywa kwa wahenga wake, na mtu mzee amejaa siku. Esau na Yakobo, wanawe, wakamzika.
And Isaac breathed his last, and died and was added unto his people, old, and satisfied with days, —and Esau and Jacob his sons buried him.