< Mwanzo 34 >

1 Basi Dina, Binti wa Lea aliyemzalia Yakobo, akaenda kuwaona wasichana wa nchi.
Then Dinah the daughter of Leah, which she bare vnto Iaakob, went out to see the daughters of that countrey.
2 Shekemu mwana wa Hamori Mhivi, mwana mfalme wa nchi, akamwona na akamkamata kwa nguvu na kulala naye.
Whome when Shechem the sonne of Hamor the Hiuite lorde of that countrey sawe, hee tooke her, and lay with her, and defiled her.
3 Akavutiwa na Dina, binti Yakobo. Akampenda msichana na kuongea naye kwa upole.
So his heart claue vnto Dinah the daughter of Iaakob: and he loued the maide, and spake kindely vnto the maide.
4 Shekemu akamwambia Hamori baba yeke, kusema, “Nipe msichana huyu kuwa mke wangu.”
Then said Shechem to his father Hamor, saying, Get me this maide to wife.
5 Basi Yakobo akasikia kwamba alikuwa amemchafua Dina binti yake. Wanawe walikuwa pamoja na wanyama uwandani, hivyo Yakaobo akawangoja hata walipokuja.
(Nowe Iaakob heard that he had defiled Dinah his daughter, and his sonnes were with his cattell in the fielde: therefore Iaakob helde his peace, vntill they were come.)
6 Hamori baba wa Shekemu akaenda kuongea na Yakobo.
Then Hamor the father of Shechem went out vnto Iaakob to commune with him.
7 Wana wa Yakobo waliposikia neno hili wakaja kutoka uwandani. Watu hawa walichukizwa sana. Walikasirika sana kwa sababu alikuwa amemwaibisha Israeli kwa kumlazimisha binti wa Yakobo, kwa maana jambo kama hilo halikupasa kutendeka.
And whe the sonnes of Iaakob were come out of the fielde and heard it, it grieued the men, and they were very angry, because he had wrought villenie in Israel, in that he had lyen with Iaakobs daughter: which thing ought not to be done.
8 Hamori akaongea nao, akisema, “Shekemu mwanangu anampenda binti yenu. Tafadhari mpeni kuwa mke wake.
And Hamor communed with them, saying, the soule of my sonne Shechem longeth for your daughter: giue her him to wife, I pray you.
9 Mwoane nasi, tupeni binti zenu, na mjichukulie binti zetu kwa ajili yenu wenyewe.
So make affinitie with vs: giue your daughters vnto vs, and take our daughters vnto you,
10 Mtaishi nasi, na nchi itakuwa wazi kwa ajili yenu kufanya biashara humo, na kupata mali.”
And ye shall dwell with vs, and the lande shalbe before you: dwell, and doe your businesse in it, and haue your possessions therein.
11 Shekemu akamwambia baba yake na ndugu zake, “Na nione kibari machoni penu, na chochote mtakachoniambia nitatoa.
Shechem also said vnto her father and vnto her brethren, Let me finde fauour in your eyes, and I will giue whatsoeuer ye shall appoint me.
12 Niambieni kiasi kikubwa chochote cha mahari na zawadi kama mtakavyo, nami nitatoa chochote msemacho, lakini mnipe msichana kuwa mke wangu.”
Aske of me abundantly both dowrie and giftes, and I will giue as ye appoint me, so that ye giue me the maide to wife.
13 Wana wa Yakobo wakamjibu Shekemu na Hamori baba yake kwa hila, kwa sababu Shekemu alikuwa amemnajisi Dina dada yao.
Then the sonnes of Iaakob answered Shechem and Hamor his father, talking deceitfully, because he had defiled Dinah their sister,
14 Wakawambia, “Hatuwezi kufanya jambo hili, kumpa dada yetu mtu yeyote ambaye hajatailiwa; kwani hiyo ni aibu kwetu.
And they said vnto them, We can not do this thing, to giue our sister to an vncircumcised man: for that were a reproofe vnto vs.
15 Kwa sharti hili peke yake tutakubaliana nanyi: iwapo mtatailiwa kama sisi, ikiwa kila mtu mme miongoni mwenu atatailiwa.
But in this will we consent vnto you, if ye will be as we are, that euery man childe among you be circumcised:
16 Ndipo tutakapowapa binti zetu, nasi tutachukua binti zenu kwetu sisi wenyewe, na tutaishi nanyi na kuwa wamoja.
Then will we giue our daughters to you, and we will take your daughters to vs, and will dwell with you, and be one people.
17 Lakini kama hamtusikilizi na kutailiwa, ndipo tutakapomchukua dada yetu na kuondoka.
But if ye will not hearken vnto vs to be circumcised, then will we take our daughter and depart.
18 Maneno yao yakawafurahisha Hamori na Shekemu mwanaye.
Nowe their wordes pleased Hamor, and Shechem Hamors sonne.
19 Kijana hakukawia kufanya walichokisema, kwa maana alipendezwa na binti Yakobo, na kwa sababu alikuwa mtu aliyeheshimiwa sana katika nyumba ya babaye.
And the yong man deferd not to doe the thing because he loued Iaakobs daughter: he was also the most set by of all his fathers house.
20 Hamori na Shekemu mwanaye wakaenda katika lango la mji wao na kuongea na watu wa mji, kusema,
Then Hamor and Shechem his Sonne went vnto the gate of their citie, and communed with the men of their citie, saying,
21 “Watu hawa wanaamani nasi, hivyo na waishi katika nchi na kufanya biashara humo kwa maana, kweli, nchi ni kubwa ya kuwatosha. Haya na tuwachukue binti zao kuwa wake, nasi tuwape binti zetu.
These men are peaceable with vs: and that they may dwell in the land, and doe their affaires therin (for behold, the land hath roume ynough for them) let vs take their daughters to wiues, and giue them our daughters.
22 Kwa shariti hili pekee watu hawa wanakubali kuishi nasi na kuwa wamoja: ikiwa kila mwanamme miongoni mwetu atatailiwa, kama wao.
Onely herein will the men consent vnto vs for to dwell with vs, and to be one people, if all the men children among vs be circumcised as they are circumcised.
23 Je wanyama wao na vitu vyao - wanyama wao wote kuwa wetu? Haya na tukubaliane nao, nao wataishi kati yetu.”
Shall not their flockes and their substance and all their cattell be ours? onely let vs consent herein vnto them, and they will dwell with vs.
24 Watu wote wa mji wakamsikiliza Hamori na Shekemu, mwanaye. Kila mwanamme akatailiwa.
And vnto Hamor, and Shechem his sonne hearkened all that went out of the gate of his citie: and all the men children were circumcised, euen all that went out of the gate of his citie.
25 Katika siku ya tatu, walipokuwa katika maumivu bado, wawili wa wana wa Yakobo (Simoni na Lawi, kaka zake Dina), wakachukua kila mmoja upanga wake na kuushambulia mji ambao ulikuwa na uhakika wa ulinzi wake, nao wakauwa wanamme wote.
And on the thirde day (when they were sore) two of the sonnes of Iaakob, Simeon and Leui, Dinahs brethren tooke either of them his sworde and went into the citie boldly, and slue euery male.
26 Wakamwua Hamori na Shekemu kwa makali ya upanga. Wakamchukua Dina kutoka nyumba ya Shekemu na kuondoka.
They slewe also Hamor and Shechem his sonne with the edge of the sword, and tooke Dinah out of Shechems house, and went their way.
27 Wale wana wengine wa Yakobo wakaja kwa maiti na kuuteka nyara mji, kwa sababu watu wale walikuwa wamemnajisi dada yao.
Againe the other sonnes of Iaakob came vpon the dead, and spoyled the citie, because they had defiled their sister.
28 Wakachukua makundi yao ya kondoo, mbuzi, punda, na kila kitu ndani ya mji na viunga vyake
They tooke their sheepe and their beeues, and their asses, and whatsoeuer was in the citie, and in the fieldes.
29 utajiri wote. Watoto na wake zao wote, wakawachukua. Hata wakachukua kila kitu kilichokua katika nyumba.
Also they caryed away captiue and spoyled all their goods, and all their children and their wiues, and all that was in the houses.
30 Yakobo akawambia Simoni na Lawi, “Mmeleta shida juu yangu, kunifanya ninuke kwa wenyeji wa nchi, Wakanaani na Waperizi. Mimi nina watu wachache. Ikiwa watajikusanya pamoja kinyume changu na kunishambulia.”
Then Iaakob said to Simeon and Leui, Ye haue troubled me, and made me stinke among the inhabitats of the land, aswell the Canaanites, as the Perizzites, and and I being few in nomber, they shall gather theselues together against me, and slay me, and so shall I, and my house be destroied.
31 Lakini Simoni na Lawi wakasema, “Je Shekemu alipaswa kumtendea dada yetu kama kahaba?”
And they answered, Shoulde hee abuse our sister as a whore?

< Mwanzo 34 >