< Mwanzo 34 >
1 Basi Dina, Binti wa Lea aliyemzalia Yakobo, akaenda kuwaona wasichana wa nchi.
Then Dinah, the daughter of Leah, went out to see the women of that region.
2 Shekemu mwana wa Hamori Mhivi, mwana mfalme wa nchi, akamwona na akamkamata kwa nguvu na kulala naye.
And when Shechem, the son of Hamor the Hivite, the leader of that land, had seen her, he fell in love with her. And so he seized her and slept with her, overwhelming the virgin by force.
3 Akavutiwa na Dina, binti Yakobo. Akampenda msichana na kuongea naye kwa upole.
And his soul was closely bound to her, and, since she was sorrowful, he soothed her with flattery.
4 Shekemu akamwambia Hamori baba yeke, kusema, “Nipe msichana huyu kuwa mke wangu.”
And going on to Hamor, his father, he said, “Obtain this girl for me as a mate.”
5 Basi Yakobo akasikia kwamba alikuwa amemchafua Dina binti yake. Wanawe walikuwa pamoja na wanyama uwandani, hivyo Yakaobo akawangoja hata walipokuja.
But when Jacob had heard this, since his sons were absent and he was occupied in pasturing the cattle, he remained silent until they came back.
6 Hamori baba wa Shekemu akaenda kuongea na Yakobo.
Then, when Hamor, the father of Shechem, had gone out to speak to Jacob,
7 Wana wa Yakobo waliposikia neno hili wakaja kutoka uwandani. Watu hawa walichukizwa sana. Walikasirika sana kwa sababu alikuwa amemwaibisha Israeli kwa kumlazimisha binti wa Yakobo, kwa maana jambo kama hilo halikupasa kutendeka.
behold, his sons arrived from the field. And hearing what had happened, they were very angry, because he had done a filthy thing in Israel and, in violating a daughter of Jacob, had perpetrated an unlawful act.
8 Hamori akaongea nao, akisema, “Shekemu mwanangu anampenda binti yenu. Tafadhari mpeni kuwa mke wake.
And so Hamor spoke to them: “The soul of my son Shechem has become attached to your daughter. Give her to him as a wife.
9 Mwoane nasi, tupeni binti zenu, na mjichukulie binti zetu kwa ajili yenu wenyewe.
And let us celebrate marriages with one with another. Give us your daughters, and receive our daughters.
10 Mtaishi nasi, na nchi itakuwa wazi kwa ajili yenu kufanya biashara humo, na kupata mali.”
And live with us. The land is in your power: cultivate, trade, and possess it.”
11 Shekemu akamwambia baba yake na ndugu zake, “Na nione kibari machoni penu, na chochote mtakachoniambia nitatoa.
And Shechem even said to her father and to her brothers: “May I find favor in your sight, and whatever you will appoint, I will give.
12 Niambieni kiasi kikubwa chochote cha mahari na zawadi kama mtakavyo, nami nitatoa chochote msemacho, lakini mnipe msichana kuwa mke wangu.”
Increase the dowry, and request gifts, and I will freely bestow what you will ask. Only give me this girl as a wife.”
13 Wana wa Yakobo wakamjibu Shekemu na Hamori baba yake kwa hila, kwa sababu Shekemu alikuwa amemnajisi Dina dada yao.
The sons of Jacob answered Shechem and his father with deceit, being enraged at the rape of their sister:
14 Wakawambia, “Hatuwezi kufanya jambo hili, kumpa dada yetu mtu yeyote ambaye hajatailiwa; kwani hiyo ni aibu kwetu.
“We are not able to do what you ask, nor to give our sister to an uncircumcised man. For us, this is unlawful and abominable.
15 Kwa sharti hili peke yake tutakubaliana nanyi: iwapo mtatailiwa kama sisi, ikiwa kila mtu mme miongoni mwenu atatailiwa.
But we may succeed in this, so as to be allied with you, if you are willing to become like us, and if all the male sex among you will be circumcised.
16 Ndipo tutakapowapa binti zetu, nasi tutachukua binti zenu kwetu sisi wenyewe, na tutaishi nanyi na kuwa wamoja.
Then we will mutually give and receive your daughters as well as ours; and we will live with you, and we will become one people.
17 Lakini kama hamtusikilizi na kutailiwa, ndipo tutakapomchukua dada yetu na kuondoka.
But if you will not be circumcised, we will take our daughter and withdraw.”
18 Maneno yao yakawafurahisha Hamori na Shekemu mwanaye.
Their offer pleased Hamor and his son Shechem.
19 Kijana hakukawia kufanya walichokisema, kwa maana alipendezwa na binti Yakobo, na kwa sababu alikuwa mtu aliyeheshimiwa sana katika nyumba ya babaye.
Neither did the young man cause any delay; in fact he immediately fulfilled what was requested. For he loved the girl very much, and he was well-known throughout his father’s house.
20 Hamori na Shekemu mwanaye wakaenda katika lango la mji wao na kuongea na watu wa mji, kusema,
And entering at the gate of the city, they spoke to the people:
21 “Watu hawa wanaamani nasi, hivyo na waishi katika nchi na kufanya biashara humo kwa maana, kweli, nchi ni kubwa ya kuwatosha. Haya na tuwachukue binti zao kuwa wake, nasi tuwape binti zetu.
“These men are peaceful, and they want to live among us. Let them trade in the land and cultivate it, for, being spacious and broad, it is in need of cultivation. We will receive their daughters as wives, and we will give them ours.
22 Kwa shariti hili pekee watu hawa wanakubali kuishi nasi na kuwa wamoja: ikiwa kila mwanamme miongoni mwetu atatailiwa, kama wao.
There is one thing that prevents so great a good: whether we will circumcise our males, imitating the ritual of their nation.
23 Je wanyama wao na vitu vyao - wanyama wao wote kuwa wetu? Haya na tukubaliane nao, nao wataishi kati yetu.”
And their substance, and cattle, and all that they possess, will be ours, if only we will acquiesce to this, and so, in living together, will form one people.”
24 Watu wote wa mji wakamsikiliza Hamori na Shekemu, mwanaye. Kila mwanamme akatailiwa.
And they all agreed to circumcise every one of the males.
25 Katika siku ya tatu, walipokuwa katika maumivu bado, wawili wa wana wa Yakobo (Simoni na Lawi, kaka zake Dina), wakachukua kila mmoja upanga wake na kuushambulia mji ambao ulikuwa na uhakika wa ulinzi wake, nao wakauwa wanamme wote.
And behold, on the third day, when the pain of the wound was greatest, two of the sons of Jacob, Simeon and Levi, the brothers of Dinah, boldly entered the city with swords. And they put to death all of the males.
26 Wakamwua Hamori na Shekemu kwa makali ya upanga. Wakamchukua Dina kutoka nyumba ya Shekemu na kuondoka.
They killed Hamor and Shechem together, taking their sister Dinah from the house of Shechem.
27 Wale wana wengine wa Yakobo wakaja kwa maiti na kuuteka nyara mji, kwa sababu watu wale walikuwa wamemnajisi dada yao.
And when they had departed, the other sons of Jacob rushed over the slain, and they plundered the city in vengeance for the rape.
28 Wakachukua makundi yao ya kondoo, mbuzi, punda, na kila kitu ndani ya mji na viunga vyake
Taking their sheep, and herds, and donkeys, and laying waste to everything else that was in their houses and in their fields,
29 utajiri wote. Watoto na wake zao wote, wakawachukua. Hata wakachukua kila kitu kilichokua katika nyumba.
they also took their little ones and their wives captive.
30 Yakobo akawambia Simoni na Lawi, “Mmeleta shida juu yangu, kunifanya ninuke kwa wenyeji wa nchi, Wakanaani na Waperizi. Mimi nina watu wachache. Ikiwa watajikusanya pamoja kinyume changu na kunishambulia.”
When they had boldly completed these acts, Jacob said to Simeon and Levi: “You have troubled me, and you have made me hateful to the Canaanites and the Perizzites, the inhabitants of this land. We are few. They, gathering themselves together, may strike me down, and then both I and my house will be wiped away.”
31 Lakini Simoni na Lawi wakasema, “Je Shekemu alipaswa kumtendea dada yetu kama kahaba?”
They responded, “Should they abuse our sister like a prostitute?”