< Mwanzo 33 >
1 Yakobo akainua macho yake na, tazama, Esau alikuwa anakuja, na alikuwa na watu mia nne pamoja naye. Yakobo akawagawanya watoto kati ya Lea, Raheli, na wale wajakazi wawili.
Then Jacob lifted up his eyes and looked, and lo! Esau, coming in, —and with him, four hundred men. So he divided the children—unto Leah and unto Rachel, and unto the two handmaids;
2 Kisha akawaweka wajakazi na wanao mbele, wakifuatiwa na Lea na watoto wake, Raheli na Yusufu wakafuata mwisho wa wote.
and put the handmaids and their children first, —and Leah and her children next, and Rachel and Joseph next;
3 Yeye mwenyewe akatangulia mbele yao. Akasujudu mara saba kuelekea ardhi, hata alipomkaribia ndugu yake.
but he himself, passed over before them, and bowed himself to the earth seven times, until he had come near unto his brother.
4 Esau akakimbia kumlaki, akamkumbatia, akakumbatia shingo yake na kumbusu. Kisha wakalia.
Then ran Esau to meet him, and embraced him, and fell on his neck, —and they wept.
5 Esau alipoinua macho, aliona wanawake na watoto. Akauliza, “Hawa watu pamoja nawe ni kinanani?” Yakobo akasema, Ni watoto ambao Mungu amempa mtumishi wako kwa neema.”
Then lifted he up his eyes, and beheld the women and the children, and said What are these to thee? And he said—The children wherewith God hath favoured thy servant,
6 Kisha wajakazi wakakaribia pamoja na watoto wao, nao wakasujudia.
Then came near the handmaids, they—and their children, —and bowed themselves.
7 Akafuata Lea pia na watoto wake wakaja na kusujudia. Mwisho Yusufu na Raheli wakaja na kusujudia.
Then came near Leah also with her children, —and they bowed themselves. And afterwards, came near Joseph with Rachel, and they bowed themselves,
8 Esau akasema, Unamaanisha nini kwa makundi haya yote niliyokutana nayo?” Yakobo akasema, “Kutafuta kibali mbele za bwana wangu.
Then said he, What to thee is all this camp, which I have fallen in with? And he said, —To find favour in the eyes of my lord.
9 Esau akasema, “Ninayo ya kutosha, ndugu yangu. Tunza uliyonayo kwa ajili yako mwenyewe.”
Then said Esau, I have an abundance, —my brother, be thine what thou hast!
10 Yakobo akasema, “Hapana, tafadhari, ikiwa nimeona kibali mbele zako, basi upokee zawadi yangu kutoka mkononi mwangu, na ni kama kuona uso wa Mungu, na umenipokea.
Then said Jacob, Nay, I pray thee, if, I pray thee, I have found favour in thine eyes, then thou wilt take my present at my hand, —For on this account, hath my seeing thy face been like seeing the face of God in that thou wast well-pleased with me.
11 Tafadhari pokea zawadi yangu uliyoletewa, kwa sababu Mungu amenitendea kwa neema, na kwa sababu ninavyo vya kutosha.” Hivyo Yakobo akamsihi, na Esau akamkubali.
Take, I pray thee my blessing which hath been brought in to thee, because God hath shewed me favour and because I have everything. So he was urgent with him and he took it.
12 Kisha Esau akasema, “Haya na tuondoke. Nitakutangulia.”
Then he said, Let us break up and go, and let me go on before thee.
13 Yakobo akamwambia, “Bwana wangu anajua kwamba watoto ni wadogo, na kwamba kondoo na ng'ombe wananyonyesha ndama wao. Ikiwa watapelekwa kwa haraka hata siku moja, wanyama wote watakufa.
And he said unto him, My lord, is taking note, that, the children are tender, —and the flocks and the herds are giving suck with me, —and, should I overdrive them a single day, then would all the flocks die.
14 Tafadhari bwana wangu na amtangulie mtumishi wake. Nitasafiri polopole, kwa kadili ya mifugo iliyo mbele yangu, na kadili ya watoto, hata nitakapofika kwa bwana wangu huko Seiri.”
Let my lord, I pray thee pass over before his servant, and let, me, lead on in my own easy way, at the pace of the cattle that are before me, and at the pace of the children, until that I come in unto my lord, towards Seir.
15 Esau akasema, haya nikuachie baadhi ya watu wangu waliopamoja nami.” Yakobo akasema, “Kwa nini kufanya hivyo? Bwana wangu amekuwa mkalimu kwangu kiasi cha kutosha.”
Then said Esau: Let me leave, I pray thee, along with thee, some of the people who are with me! And he said—Why so? let me find favour in the eyes of my lord!
16 Hivyo Esau akaanza kurudi Seiri.
So Esau returned, that day, to his journey towards Mount Seir.
17 Yakobo akasafiri kuelekea Sukothi, akajijengea nyumba, na akafanya mazizi kwa ajili ya mifugo wake. Hivyo jina la eneo linaitwa Sukothi.
But, Jacob, brake up towards Succoth, and built for himself a house, for his cattle, made he places of shelter, for which cause, the name of the place was called, Succoth.
18 Yakobo alipokuja kutoka Padani Aramu, akafika salama katika mji wa Shekemu, uliyo katika nchi ya Kanaani. Akapiga kambi karibu na mji.
And Jacob came in peace to the city of Shechem, which is in the land of Canaan, —when he came in from Padan-aram, —and he encamped before the city.
19 Kisha akanunu sehemu ya ardhi alipokuwa ameweka hema yake kutoka kwa wana wa Hamori, baba wa Shekemu, kwa vipande mia vya fedha.
And he bought the portion of the field where he had spread out his tent, at the hand of the sons of Hamor, father of Shechem, —for a hundred kesitahs.
20 Akajenga madhabahu pale na kuiita El Elohe Israeli.
And he set up there an altar, —and called it, El-elohe-Israel.