< Mwanzo 33 >
1 Yakobo akainua macho yake na, tazama, Esau alikuwa anakuja, na alikuwa na watu mia nne pamoja naye. Yakobo akawagawanya watoto kati ya Lea, Raheli, na wale wajakazi wawili.
Jacob saw Esau in the distance, coming towards him with four hundred men. So he split up the children between Leah, Rachel and the two personal maids.
2 Kisha akawaweka wajakazi na wanao mbele, wakifuatiwa na Lea na watoto wake, Raheli na Yusufu wakafuata mwisho wa wote.
He placed the two personal maids with their children first, then Leah and her children, and Rachel and Joseph last.
3 Yeye mwenyewe akatangulia mbele yao. Akasujudu mara saba kuelekea ardhi, hata alipomkaribia ndugu yake.
Then Jacob went ahead of them and bowed low to the ground seven times before approaching his brother.
4 Esau akakimbia kumlaki, akamkumbatia, akakumbatia shingo yake na kumbusu. Kisha wakalia.
Esau ran over to him and hugged him. He put his arms around his neck and kissed him. The two of them wept.
5 Esau alipoinua macho, aliona wanawake na watoto. Akauliza, “Hawa watu pamoja nawe ni kinanani?” Yakobo akasema, Ni watoto ambao Mungu amempa mtumishi wako kwa neema.”
Then Esau looked around at the women and children. “Who are these people with you?” he asked. “They are the children God graciously gave your servant,” Jacob replied.
6 Kisha wajakazi wakakaribia pamoja na watoto wao, nao wakasujudia.
The personal maids and their children came over and bowed down.
7 Akafuata Lea pia na watoto wake wakaja na kusujudia. Mwisho Yusufu na Raheli wakaja na kusujudia.
Then Leah and her children came over and bowed down. Lastly Joseph and Rachel came over and bowed down.
8 Esau akasema, Unamaanisha nini kwa makundi haya yote niliyokutana nayo?” Yakobo akasema, “Kutafuta kibali mbele za bwana wangu.
“What were all the livestock for that I met on the way?” Esau asked. “They're a gift to you my lord so you'd treat me well,” Jacob answered.
9 Esau akasema, “Ninayo ya kutosha, ndugu yangu. Tunza uliyonayo kwa ajili yako mwenyewe.”
“I have more than enough, my brother! You keep what you have,” said Esau.
10 Yakobo akasema, “Hapana, tafadhari, ikiwa nimeona kibali mbele zako, basi upokee zawadi yangu kutoka mkononi mwangu, na ni kama kuona uso wa Mungu, na umenipokea.
“No, please!” Jacob insisted. “If you're happy with me, then please accept the gift I'm giving you. Now I've seen your face again it's like seeing the face of God, and you have welcomed me so kindly!
11 Tafadhari pokea zawadi yangu uliyoletewa, kwa sababu Mungu amenitendea kwa neema, na kwa sababu ninavyo vya kutosha.” Hivyo Yakobo akamsihi, na Esau akamkubali.
Please take the gift I've brought to you because God has treated me so well and I have so much.” So Esau accepted it.
12 Kisha Esau akasema, “Haya na tuondoke. Nitakutangulia.”
“Let's get on our way,” Esau said. “I'll go ahead of you.”
13 Yakobo akamwambia, “Bwana wangu anajua kwamba watoto ni wadogo, na kwamba kondoo na ng'ombe wananyonyesha ndama wao. Ikiwa watapelekwa kwa haraka hata siku moja, wanyama wote watakufa.
“My lord can see that the children are weak,” Jacob responded. “Also, the goats, sheep, and cattle are nursing their young, and if I push them too hard, they'll all die.
14 Tafadhari bwana wangu na amtangulie mtumishi wake. Nitasafiri polopole, kwa kadili ya mifugo iliyo mbele yangu, na kadili ya watoto, hata nitakapofika kwa bwana wangu huko Seiri.”
You go on, my lord, and your servant will come along slowly, walking with the children, and I'll meet you at Seir.”
15 Esau akasema, haya nikuachie baadhi ya watu wangu waliopamoja nami.” Yakobo akasema, “Kwa nini kufanya hivyo? Bwana wangu amekuwa mkalimu kwangu kiasi cha kutosha.”
“Fine, but let me leave some of my men with you,” said Esau. “You're very kind, but there's no need to do that,” Jacob replied.
16 Hivyo Esau akaanza kurudi Seiri.
So Esau started on his way back to Seir that day.
17 Yakobo akasafiri kuelekea Sukothi, akajijengea nyumba, na akafanya mazizi kwa ajili ya mifugo wake. Hivyo jina la eneo linaitwa Sukothi.
But Jacob headed to Succoth, where he built himself a house and shelters for the livestock. That's why the place is called Succoth.
18 Yakobo alipokuja kutoka Padani Aramu, akafika salama katika mji wa Shekemu, uliyo katika nchi ya Kanaani. Akapiga kambi karibu na mji.
Later Jacob continued his journey from Paddan-aram. He arrived safely at Shechem in the country of Canaan where he camped outside the town.
19 Kisha akanunu sehemu ya ardhi alipokuwa ameweka hema yake kutoka kwa wana wa Hamori, baba wa Shekemu, kwa vipande mia vya fedha.
He bought the plot of ground where he was camping from the sons of Hamor, the founder of Shechem, for 100 pieces of money.
20 Akajenga madhabahu pale na kuiita El Elohe Israeli.
He built an altar there and called it El-Elohe-Israel.