< Mwanzo 33 >
1 Yakobo akainua macho yake na, tazama, Esau alikuwa anakuja, na alikuwa na watu mia nne pamoja naye. Yakobo akawagawanya watoto kati ya Lea, Raheli, na wale wajakazi wawili.
And Jacob lifted up his eyes and looked, and behold, Esau was coming, and with him four hundred men. And he distributed the children to Leah, and to Rachel, and to the two maidservants:
2 Kisha akawaweka wajakazi na wanao mbele, wakifuatiwa na Lea na watoto wake, Raheli na Yusufu wakafuata mwisho wa wote.
and he put the maidservants and their children foremost, and Leah and her children after, and Rachel and Joseph hindmost.
3 Yeye mwenyewe akatangulia mbele yao. Akasujudu mara saba kuelekea ardhi, hata alipomkaribia ndugu yake.
And he passed on before them, and bowed to the earth seven times, until he came near to his brother.
4 Esau akakimbia kumlaki, akamkumbatia, akakumbatia shingo yake na kumbusu. Kisha wakalia.
And Esau ran to meet him, and embraced him, and fell on his neck, and kissed him; and they wept.
5 Esau alipoinua macho, aliona wanawake na watoto. Akauliza, “Hawa watu pamoja nawe ni kinanani?” Yakobo akasema, Ni watoto ambao Mungu amempa mtumishi wako kwa neema.”
And he lifted up his eyes and saw the women and the children, and said, Who are these with thee? And he said, The children that God has graciously given thy servant.
6 Kisha wajakazi wakakaribia pamoja na watoto wao, nao wakasujudia.
And the maidservants drew near, they and their children, and they bowed.
7 Akafuata Lea pia na watoto wake wakaja na kusujudia. Mwisho Yusufu na Raheli wakaja na kusujudia.
And Leah also, with her children, drew near, and they bowed. And lastly Joseph drew near, and Rachel, and they bowed.
8 Esau akasema, Unamaanisha nini kwa makundi haya yote niliyokutana nayo?” Yakobo akasema, “Kutafuta kibali mbele za bwana wangu.
And he said, What [meanest] thou by all the drove which I met? And he said, To find favour in the eyes of my lord.
9 Esau akasema, “Ninayo ya kutosha, ndugu yangu. Tunza uliyonayo kwa ajili yako mwenyewe.”
And Esau said, I have enough, my brother; let what thou hast be thine.
10 Yakobo akasema, “Hapana, tafadhari, ikiwa nimeona kibali mbele zako, basi upokee zawadi yangu kutoka mkononi mwangu, na ni kama kuona uso wa Mungu, na umenipokea.
And Jacob said, No, I pray thee; if now I have found favour in thine eyes, then receive my gift from my hand; for therefore have I seen thy face, as though I had seen the face of God, and thou hast received me with pleasure.
11 Tafadhari pokea zawadi yangu uliyoletewa, kwa sababu Mungu amenitendea kwa neema, na kwa sababu ninavyo vya kutosha.” Hivyo Yakobo akamsihi, na Esau akamkubali.
Take, I pray thee, my blessing which has been brought to thee; because God has been gracious to me, and because I have everything. And he urged him, and he took [it].
12 Kisha Esau akasema, “Haya na tuondoke. Nitakutangulia.”
And he said, Let us take our journey, and go on, and I will go before thee.
13 Yakobo akamwambia, “Bwana wangu anajua kwamba watoto ni wadogo, na kwamba kondoo na ng'ombe wananyonyesha ndama wao. Ikiwa watapelekwa kwa haraka hata siku moja, wanyama wote watakufa.
And he said to him, My lord knows that the children are tender, and the suckling sheep and kine are with me; and if they should overdrive them only one day, all the flock would die.
14 Tafadhari bwana wangu na amtangulie mtumishi wake. Nitasafiri polopole, kwa kadili ya mifugo iliyo mbele yangu, na kadili ya watoto, hata nitakapofika kwa bwana wangu huko Seiri.”
Let my lord, I pray thee, pass on before his servant, and I will drive on at my ease according to the pace of the cattle that is before me, and according to the pace of the children, until I come to my lord, to Seir.
15 Esau akasema, haya nikuachie baadhi ya watu wangu waliopamoja nami.” Yakobo akasema, “Kwa nini kufanya hivyo? Bwana wangu amekuwa mkalimu kwangu kiasi cha kutosha.”
And Esau said, Let me now leave with thee [some] of the people that are with me. And he said, What need? Let me find favour in the eyes of my lord.
16 Hivyo Esau akaanza kurudi Seiri.
And Esau returned that day on his way to Seir.
17 Yakobo akasafiri kuelekea Sukothi, akajijengea nyumba, na akafanya mazizi kwa ajili ya mifugo wake. Hivyo jina la eneo linaitwa Sukothi.
And Jacob journeyed to Succoth, and built himself a house, and for his cattle he made booths. Therefore the name of the place was called Succoth.
18 Yakobo alipokuja kutoka Padani Aramu, akafika salama katika mji wa Shekemu, uliyo katika nchi ya Kanaani. Akapiga kambi karibu na mji.
And Jacob came safely [to the] city Shechem, which is in the land of Canaan, when he came from Padan-Aram; and he encamped before the city.
19 Kisha akanunu sehemu ya ardhi alipokuwa ameweka hema yake kutoka kwa wana wa Hamori, baba wa Shekemu, kwa vipande mia vya fedha.
And he bought the portion of the field where he had spread his tent, of the hand of the sons of Hamor, Shechem's father, for a hundred kesitahs.
20 Akajenga madhabahu pale na kuiita El Elohe Israeli.
And there he set up an altar, and called it El-Elohe-Israel.