< Mwanzo 32 >

1 Yakobo pia akaendelea na safari yake, na malaika wa Mungu wakakutana naye.
And Jacob went on his way, and the angels of God met him.
2 Yakobo alipowaona, akasema, “Hii ni kambi ya Mungu,” hivyo akapaita mahali pale Mahanaimu.
And Jacob said when he saw them: 'This is God's camp.' And he called the name of that place Mahanaim.
3 Yakobo akatuma wajumbe mbele yake waende kwa Esau ndugu yake katika nchi ya Seiri, katika eneo la Edomu.
And Jacob sent messengers before him to Esau his brother unto the land of Seir, the field of Edom.
4 Aliwaagiza, kusema, “Hivi ndivyo mtakavyosema kwa bwana wangu Esau: Hivi ndivyo mtumishi wako Yakobo asemavyo: 'Nimekuwa nikikaa na Labani, naye amekawilisha kurudi kwangu hata sasa.
And he commanded them, saying: 'Thus shall ye say unto my lord Esau: Thus saith thy servant Jacob: I have sojourned with Laban, and stayed until now.
5 Nina ng'ombe, punda, na kondoo, wajori na wajakazi. Nimetuma ujumbe huu kwa bwana wangu, ili kwamba nipate kibali mbele zako.”
And I have oxen, and asses and flocks, and men-servants and maid-servants; and I have sent to tell my lord, that I may find favour in thy sight.'
6 Wajumbe wakarudi kwa Yakobo na kusema, “Tulikwenda kwa Esau ndugu yako. Anakuja kukulaki, na watu mia nne pamoja naye.”
And the messengers returned to Jacob, saying: 'We came to thy brother Esau, and moreover he cometh to meet thee, and four hundred men with him.'
7 Ndipo Yakobo alipoogopa sana na kutaabika. Hivyo akagawanya watu aliokuwa nao katika kambi mbili, na kondoo pia, mbuzi na ngamia.
Then Jacob was greatly afraid and was distressed. And he divided the people that was with him, and the flocks, and the herds, and the camels, into two camps.
8 Akasema, “Ikiwa Esau ataishambulia kambi moja, ndipo kambi nyingine itakaposalimika.”
And he said: 'If Esau come to the one camp, and smite it, then the camp which is left shall escape.'
9 Yakobo akasema, “Mungu wa baba yangu Ibrahimu, na Mungu wa baba yangu Isaka, Yahwe, uliyeniambia, 'Rudi katika nchi yako na kwa jamaa yako, nami nitakustawisha,'
And Jacob said: 'O God of my father Abraham, and God of my father Isaac, O LORD, who saidst unto me: Return unto thy country, and to thy kindred, and I will do thee good;
10 Mimi sistahili matendo yako yote ya agano la uaminifu na ustahilifu wote uliomfanyia mtumishi wako. Kwa maana nilikuwa na fimbo tu nilipovuka mto huu wa Yordani, na sasa nimekuwa matuo mawili.
I am not worthy of all the mercies, and of all the truth, which Thou hast shown unto Thy servant; for with my staff I passed over this Jordan; and now I am become two camps.
11 Tafadhari niokoe kutoka katika mikono ya ndugu yangu, mikono ya Esau, kwa maana namwogopa, kwamba atakuja na kunishambulia mimi na wamama na watoto.
Deliver me, I pray Thee, from the hand of my brother, from the hand of Esau; for I fear him, lest he come and smite me, the mother with the children.
12 Lakini ulisema, 'hakika nitakufanya ufanikiwe. Nitaufanya uzao wako kuwa kama mchanga wa bahari, ambao hauwezi kuhesabika kwa hesabu yake.”
And Thou saidst: I will surely do thee good, and make thy seed as the sand of the sea, which cannot be numbered for multitude.'
13 Yakobo akakaa pale usiku huo. Akachukua baadhi ya alivyokuwa navyo kama zawadi kwa Esau, ndugu yake:
And he lodged there that night; and took of that which he had with him a present for Esau his brother:
14 mbuzi majike mia mbili na mabeberu ishirini, kondoo majike mia mbili na madume ya kondoo ishirini,
two hundred she-goats and twenty he-goats, two hundred ewes and twenty rams,
15 ngamia wakamwao thelathini na wana wao, ng'ombe madume arobaini na madume kumi ya ng'ombe, punda wa kike ishirini na madume yake ishirini.
thirty milch camels and their colts, forty kine and ten bulls, twenty she-asses and ten foals.
16 Akawaweka katika mikono ya watumishi wake, kila kundi peke yake. Akawambia watumishi, “Tangulieni mbele yangu na mwache nafasi kati ya makundi ya wanyama.”
And he delivered them into the hand of his servants, every drove by itself; and said unto his servants: 'Pass over before me, and put a space betwixt drove and drove.'
17 Akamwagiza mtumishi wa kwanza, akisema, “Ndugu yangu Esau atakapokutana nawe na kukuuliza, akasema, 'Ninyi ni wa nani? Mnakwenda wapi? Na wanyama hawa mbele yenu ni wa nani?
And he commanded the foremost, saying: 'When Esau my brother meeteth thee, and asketh thee, saying: Whose art thou? and whither goest thou? and whose are these before thee?
18 Ndipo umwambie, 'Ni wa mtumishi wako Yakobo. Ni zawadi wanaopelekwa kwa bwana wangu Esau. Na tazama, yeye pia anakuja nyuma yetu.”
then thou shalt say: They are thy servant Jacob's; it is a present sent unto my lord, even unto Esau; and, behold, he also is behind us.'
19 Yakobo akatoa maelekezo kwa kundi la pili pia, la tatu, na watu wote walioyafuata makundi ya wanyama. Akasema, mseme vilevile kwa Esau mtakapokutana naye.
And he commanded also the second, and the third, and all that followed the droves, saying: 'In this manner shall ye speak unto Esau, when ye find him;
20 Mnapaswa pia kusema, 'mtumwa wako Yakobo pia anakuja nyuma yetu.” Kwani alifikiri, “nitamtuliza Esau kwa zawadi nilizozituma mbele yangu. Kisha baadaye, nitakapomwona, bila shaka atanipokea.”
and ye shall say: Moreover, behold, thy servant Jacob is behind us.' For he said: 'I will appease him with the present that goeth before me, and afterward I will see his face; peradventure he will accept me.'
21 Hivyo zawadi zikatangulia mbele yake. Yeye mwenyewe akakaa kambini usiku huo
So the present passed over before him; and he himself lodged that night in the camp.
22 Yakobo akaamka wakati wa usiku, na akawachukua wakeze, wajakazi wake na wanaye kumi na wawili. Akawawavusha kijito cha Yaboki.
And he rose up that night, and took his two wives, and his two handmaids, and his eleven children, and passed over the ford of the Jabbok.
23 Kwa njia hii akawapeleka kupitia chemichemi pamoja na mali yake yote.
And he took them, and sent them over the stream, and sent over that which he had.
24 Yakobo akaachwa peke yake, na mtu akashindana naya mpaka alfajiri.
And Jacob was left alone; and there wrestled a man with him until the breaking of the day.
25 Mtu yule alipoona kwamba hawezi kumshinda, akalipiga paja lake. Paja la Yakobo likatenguka alipokuwa akishindana naye.
And when he saw that he prevailed not against him, he touched the hollow of his thigh; and the hollow of Jacob's thigh was strained, as he wrestled with him.
26 Yule mtu akasema, “Niache niende, kwani kunakucha.” Yakobo akasema, sitakuacha uende mpaka uwe umenibariki.”
And he said: 'Let me go, for the day breaketh.' And he said: 'I will not let thee go, except thou bless me.'
27 Yule mtu akamwuliza, “Jina lako ni nani?” Yakobo akasema, “Yakobo.” Yule mtu akasema,
And he said unto him: 'What is thy name?' And be said: 'Jacob.'
28 “Jina lako halitakuwa Yakobo tena, ila Israeli. Kwa kuwa umeshindana na Mungu na wanadamu na umeshinda.”
And he said: 'Thy name shall be called no more Jacob, but Israel; for thou hast striven with God and with men, and hast prevailed.'
29 Yakobo akamwambia, “Tafadhari niambie jina lako.” Akasema, “Kwa nini kuniuliza jina langu?” Kisha akambariki pale.
And Jacob asked him, and said: 'Tell me, I pray thee, thy name.' And he said: 'Wherefore is it that thou dost ask after my name?' And he blessed him there.
30 Yakobo akapaita mahali pale Penieli kwani alisema, “Nimemwona Mungu uso kwa uso, na maisha yangu yamesalimika.”
And Jacob called the name of the place Peniel: 'for I have seen God face to face, and my life is preserved.'
31 Jua likatoka wakati Yakobo anaipita Penieli. Alikuwa akichechemea kwa sababu ya paja lake.
And the sun rose upon him as he passed over Peniel, and he limped upon his thigh.
32 Ndiyo maana wana wa Israeli hawali kano ya paja iliyopo katika nyonga ya paja, kwa sababu yule mtu aliziumiza hizo kano alipotegua paja la Yakobo.
Therefore the children of Israel eat not the sinew of the thigh-vein which is upon the hollow of the thigh, unto this day; because he touched the hollow of Jacob's thigh, even in the sinew of the thigh-vein.

< Mwanzo 32 >