< Mwanzo 31 >

1 Basi Yakobo akasikia maneno ya wana wa Labani, wakisema, “Yakobo amechukuwa yote yaliyokuwa ya baba yetu, na ni kutoka katika mali ya baba yetu amepata utajiri wake.”
Jacob entendit les propos des fils de Laban, qui disaient: « Jacob a pris tout ce qui était à notre père, et c’est avec le bien de notre père qu’il s’est fait toute cette richesse. »
2 Yakobo akaona mwonekano katika uso wa Labani. Akaona kwamba nia yake imebadilika.
Jacob remarqua aussi le visage de Laban, et voici, il n’était plus à son égard comme auparavant.
3 Kisha Yahwe akamwambia Yakobo, “Rudi katika nchi ya baba zako na ya ndugu zako, nami nitakuwa nawe.”
Et Yahweh dit à Jacob: « Retourne au pays de tes pères et au lieu de ta naissance, et je serai avec toi. »
4 Yakobo akatuma kuwaita Raheli na Lea uwandani katika kundi lake la kondoo
Alors Jacob fit dire à Rachel et à Lia de venir le trouver aux champs, où il faisait paître son troupeau.
5 naye akawambia, “Naona nia ya baba yenu kwangu imebadilika, lakini Mungu wa baba yangu amekuwa nami.
Il leur dit: « Je vois que le visage de votre père n’est plus le même envers moi qu’auparavant; or le Dieu de mon père a été avec moi.
6 Nanyi mnajua kwamba ni kwa nguvu zangu zote nimemtumikia baba yenu.
Vous savez vous-mêmes que j’ai servi votre père de tout mon pouvoir;
7 Baba yenu amenidanganya na amebadilisha ujira wangu mara kumi, lakini Mungu hakumruhusu kunidhuru.
et votre père s’est joué de moi, changeant dix fois mon salaire; mais Dieu ne lui a pas permis de me causer du préjudice.
8 Ikiwa alisema, 'Wanyama wenye mabaka watakuwa ujira wako,' ndipo kondoo wote walipozaa watoto wenye mabaka. Na aliposema, wenye milia watakuwa ujira wako,' ndipo kundi lote lilipozaa watoto wenye milia.
Quand il disait: Les bêtes tachetées seront ton salaire, toutes les brebis faisaient des agneaux tachetés. Et s’il disait: Les bêtes rayées seront ton salaire, toutes les brebis faisaient des agneaux rayés.
9 Kwa njia hii Mungu amemnyang'anya mifugo baba yenu na kunipa mimi.
Dieu a donc pris le bétail de votre père et me l’a donné.
10 Wakati fulani wa majira ya kupandana, niliona katika ndoto mabeberu yaliyowapanda kundi. Mabeberu yalikuwa ya milia, mabaka na madoa.
Au temps où les brebis entrent en chaleur, je levai les yeux et je vis en songe que les béliers qui couvraient les brebis étaient rayés, tachetés et marquetés.
11 Malaika wa Mungu akaniambia katika ndoto, 'Yakobo.' Nikasema, 'Mimi hapa.'
Et un ange de Dieu me dit en songe: Jacob! Je répondis: Me voici.
12 Akasema, 'Inua macho yako uone mabeberu wanaolipanda kundi. Wana milia, madoa na na mabaka, kwani nimeona kila jambo Labani analokutendea.
Et il dit: « Lève les yeux et regarde: tous les béliers qui couvrent les brebis sont rayés, tachetés et marquetés; car j’ai vu tout ce que t’a fait Laban.
13 Mimi ni Mungu wa Betheli, mahali ulipoitia nguzo mafuta, mahali uliponitolea nadhiri. Basi sasa inuka na uondoke katika nchi hii na kurudi katika nchi uliyozaliwa.
Je suis le Dieu de Béthel, où tu as oint un monument, où tu m’as fait un vœu. Maintenant lève-toi, sors de ce pays et retourne au pays de ta naissance. »
14 Raheli na Lea wakajibu na kumwambia, “Je kuna sehemu yoyote au urithi wetu katika nyumba ya baba yetu?
Rachel et Lia répondirent en disant: « Est-ce que nous avons encore une part et un héritage dans la maison de notre père?
15 Je hatutendei kama wageni? Kwa maana ametuuza na kwa ujumla ametapanya pesa zetu.
Ne sommes-nous pas regardées par lui comme des étrangères, puisqu’il nous a vendues et qu’il mange notre argent?
16 Mali zote ambazo sasa Mungu amemnyang'anya baba yetu ni zetu na watoto wetu. Sasa basi, lolote Mungu alilokuambia, fanya.
D’ailleurs tout le bien que Dieu a enlevé à notre père, nous l’avons, nous et nos enfants. Fais donc maintenant ce que Dieu t’a ordonné ».
17 Kisha Yakobo akainuka na kuwapandisha wanawe na wakeze kwenye ngamia.
Jacob se leva et fit monter ses enfants et ses femmes sur les chameaux.
18 Akawaongoza mifugo wake wote mbele yake, pamoja na mali zake zote, wakiwemo wanyama aliowapata huko Padani Aramu. Kisha akaenda kuelekea kwa Isaka baba yake katika nchi ya Kanaani.
Il emmena tout son troupeau et tout le bien qu’il avait acquis, le troupeau qu’il possédait, qu’il avait acquis à Paddan-Aram; et il s’en alla vers Isaac, son père, au pays de Chanaan.
19 Labani alipokuwa amekwenda kuwakata manyoya kondoo wake, Raheli akaiba miungu ya nyumba ya baba yake.
Comme Laban était allé tondre ses brebis, Rachel déroba les théraphim de son père.
20 Yakobo pia akamdanganya Labani Mwarami, kwa kutomtaarifu kwamba anaondoka.
Et Jacob trompa Laban, l’Araméen, en ne l’informant pas de sa fuite.
21 Hivyo akaondoka na vyote alivyokuwa navyo na kwa haraka akavuka mto, na akaenda kuelekea nchi ya vilima ya Gileadi.
Il s’enfuit, lui et tout ce qui lui appartenait et, s’étant levé, il traversa le fleuve et se dirigea vers la montagne de Galaad.
22 Siku ya tatu Labani akaambiwa kwamba Yakobo amekimbia.
Le troisième jour, on annonça à Laban que Jacob s’était enfui.
23 Hivyo akawachukua ndugu zake pamoja naye na kumfuatia kwa safari ya siku saba. Akampata katika nchi ya vilima ya Gileadi.
Il prit avec lui ses frères et le poursuivit pendant sept journées de chemin; il l’atteignit à la montagne de Galaad.
24 Basi Mungu akaja kwa Labani Mwarami katika ndoto usiku na kumwambia, “Ujiadhari kumwambia Yakobo jambo lolote liwe jema au baya.”
Et Dieu vint en songe, de nuit, vers Laban l’Araméen, et il lui dit: « Garde-toi de rien dire à Jacob, ni en bien ni en mal. »
25 Labani akampata Yakobo. Basi Yakobo alikuwa amepiga hema yake katika nchi ya vilima. Labani pia akapiga kambi pamoja na ndugu zake katika nchi ya kilima ya Gileadi.
Laban atteignit donc Jacob. — Jacob avait dressé sa tente sur la montagne, et Laban avait aussi dressé la sienne, avec ses frères, sur la montagne de Galaad.
26 Labani akamwambia Yakobo, “Umefanya nini, kwamba umewachukua binti zangu kama mateka wa vita?
Laban dit à Jacob: « Qu’as-tu fait? tu as abusé mon esprit et tu as emmené mes filles comme des captives prises par l’épée?
27 Kwa nini umekimbia kwa siri na kunihadaa kwa kutokuniambia? Ningekuruhusu uondoke kwa sherehe na kwa nyimbo, kwa matari na vinubi.
Pourquoi as-tu pris secrètement la fuite et m’as-tu trompé, au lieu de m’avertir, moi qui t’aurais laissé aller dans l’allégresse des chants, au son du tambourin et de la harpe?
28 Haukuniacha niwabusu wajukuu wangu na binti zangu kwa kuwaaga. Basi umefanya upumbavu.
Tu ne m’as pas laissé embrasser mes fils et mes filles! Vraiment tu as agi en insensé.
29 Iko katika uwezo wangu kukudhuru, lakini Mungu wa baba yako alisema nami usiku wa leo na kuniambia, 'Jiadhari usimwambie Yakobo neno la heri wala shari.'
Ma main est assez forte pour vous faire du mal; mais le Dieu de votre père m’a parlé cette nuit en disant: Garde-toi de rien dire à Jacob, ni en bien ni en mal.
30 Na sasa, umeondoka kwa sababu umeitamani sana nyumba ya baba yako. Lakini kwa nini umeiba miungu yangu?
Et maintenant, tu es parti parce que tu languissais après la maison de ton père; mais, pourquoi as-tu dérobé mes dieux? »
31 Yakobo akajibu na kumwambia Labani, “Ni kwa sababu niliogopa na kudhani kuwa ungeninyang'anya binti zako kwa nguvu ndiyo maana nikaondoka kwa siri.
Jacob répondit et dit à Laban: « C’est que j’avais de la crainte, en me disant que peut-être tu m’enlèverais tes filles.
32 Yeyote aliyeiiba miungu yako hataendelea kuishi. Mbele ya ndugu zetu, onesha chochote kilichochako nilichonacho na uchukue.” Kwa maana Yakobo hakujua kwamba Raheli alikuwa ameviiba.
Quant à celui chez qui tu trouveras tes dieux, il ne vivra pas! En présence de nos frères, reconnais ce qui t’appartient chez moi et prends-le. » — Or Jacob ignorait que Rachel les eût dérobés. —
33 Labani akaingia katika hema ya Yakobo, katika hema ya Lea, na katika hema za wale wajakazi wawili, lakini hakuviona. Akatoka katika hema ya Lea na kuingia katika hema ya Raheli.
Laban entra dans la tente de Jacob, dans la tente de Lia et dans la tente des deux servantes, et il ne trouva rien. Puis il sortit de la tente de Lia et entra dans la tente de Rachel.
34 Basi Raheli alikuwa ameichukua miungu ya nyumbani, na kuiweka katika ngozi ya ngamia, na kukaa juu yake. Labani akatafuta katika hema yote, lakini hakuiona.
Rachel avait pris les théraphim, les avait mis dans la selle du chameau et s’était assise dessus. Laban fouilla toute la tente, sans rien trouver.
35 Akamwambia baba yake, “Usikasirike, bwana wangu, kwamba siwezi kusimama mbele yako, kwani nipo katika kipindi changu.” Hivyo akatafuta lakini hakuiona miungu ya nyumbani mwake.
Et Rachel dit à son père: « Que mon seigneur ne s’irrite point de ce que je ne puis me lever devant toi, car j’ai ce qui est ordinaire aux femmes. » Il chercha, mais ne trouva pas les théraphim.
36 Yakobo akakasirika na kuojiana na Labani. Akamwambia, “Kosa langu ni nini? Dhambi yangu ni ipi, hata ukanifuatia kwa ukali?
Jacob se mit en colère et adressa des reproches à Laban; et Jacob prit la parole et dit à Laban: « Quel est mon crime, quelle est ma faute, que tu t’acharnes après moi?
37 Kwa maana umechunguza mali zangu zote. Umeona nini kati ya kitu chochote cha nyumbani mwako? Viweke hapa mbele ya ndugu zetu, ili waamue kati yetu wawili.
Quand tu as fouillé tous mes effets, qu’as-tu trouvé des effets de ta maison? Produis-le ici devant mes frères et tes frères, et qu’ils soient juges entre nous deux.
38 Kwa miaka ishirini nimekuwa nawe. Kondoo wako na mbuzi wako hawakutoa mimba, wala sikula dume lolote la kondoo katika wanyama wako.
Voilà vingt ans que j’ai passés chez toi; tes brebis et tes chèvres n’ont pas avorté, et je n’ai pas mangé les béliers de ton troupeau.
39 Kilichoraruliwa na hayawani sikukuletea. Badala yake, nilichukua upotevu huo, kwamba wameibwa mchana au usiku.
Ce qui était déchiré par les bêtes sauvages, je ne te l’ai pas rapporté; c’est moi qui en ai supporté la perte. Tu me réclamais ce qui avait été dérobé de jour et ce qui avait été dérobé de nuit.
40 Nilikuwepo wakati wote; mchana joto lilinipata, na baridi wakati wa usiku; na sikupata usingizi.
J’étais dévoré le jour par la chaleur, et la nuit par le froid, et mon sommeil fuyait de mes yeux.
41 Miaka hii ishirini nimekuwa katika nyumba yako. Nilikufanyia kazi miaka kumi na nne kwa ajili ya binti zako wawili, na miaka sita kwa ajili ya wanyama wako. Umebadili ujira wangu mara kumi.
Voilà vingt ans que je suis dans ta maison; je t’ai servi quatorze ans pour tes deux filles et six ans pour ton bétail, et tu as changé mon salaire dix fois.
42 Isipokuwa Mungu wa baba yangu, Mungu wa Ibrahimu, yule Isaka anayemwofu, amekuwa nami, bila shaka sasa ungenipeleka mikono mitupu. Mungu ameliona teso langu na jinsi nilivyofanya kazi kwa bidii, na hivyo akakukemea usiku wa leo.
Si le Dieu de mon père, le Dieu d’Abraham et la Terreur d’Isaac n’eût pas été pour moi, tu m’aurais maintenant laissé partir à vide. Dieu a vu ma souffrance et le travail de mes mains, et cette nuit il a jugé entre nous. »
43 Labani akajibu na kumwambia Yakobo, “Mabinti hawa ni mabinti zangu, wajukuu ni wajukuu wangu, na wanyama ni wanyama wangu. Yote uyaonayo ni yangu. Lakini nitafanya nini leo kwa hawa binti zangu, au kwa watoto wao waliowazaa?
Laban répondit et dit à Jacob: « Ces filles sont mes filles, ces enfants mes enfants, ces troupeaux mes troupeaux, et tout ce que tu vois est à moi. Que ferais-je aujourd’hui à mes filles, à elles et aux fils qu’elles ont enfantés?
44 Hivyo sasa, na tufanye agano, wewe nami, na liwe shahidi kati yangu nawe.”
Maintenant donc, viens, faisons alliance, moi et toi, et qu’il y ait un témoin entre moi et toi. »
45 Hivyo Yakobo akachukua jiwe na kuliweka kama nguzo.
Jacob prit une pierre et la dressa pour monument.
46 Yakobo akawambia ndugu zake, “Kusanyeni mawe.” Hivyo wakachukua mawe na kufanya rundo. Kisha wakala pale kati ya lile rundo.
Et Jacob dit à ses frères: « Amassez des pierres. » Ils prirent des pierres et en firent un monceau, et ils mangèrent là sur le monceau.
47 Labani aliliita Yega Saha Dutha, lakini Yakobo akaiita Galeedi
Laban l’appela Yegar-Sahadutha, et Jacob l’appela Galaad.
48 Labani akasema, “Rundo hili ni shahidi kati yangu nawe leo.” Kwa hiyo jina lake likaitwa Galedi.
Et Laban dit: « Ce monceau est témoin entre moi et toi aujourd’hui. » C’est pourquoi on lui donna le nom de Galaad,
49 Inaitwa pia Mispa, kwa sababu Labani alisema, “Yahwe na atuangalie mimi nawe, tunapokuwa hatuonani.
et aussi celui de Mitspa, parce que Laban dit: « Que Yahweh nous surveille, moi et toi, quand nous serons séparés l’un de l’autre.
50 Ikiwa utawatesa binti zangu, au ikiwa utachukua wanawake wengine mbali na binti zangu, japokuwa hakuna mwingine yupo nasi, tazama, Mungu ni shahidi kati yangu nawe.”
Si tu maltraites mes filles et si tu prends d’autres femmes à côté de mes filles, ce n’est pas un homme qui sera avec nous; mais, prends-y garde, c’est Dieu qui sera témoin entre moi et toi. »
51 Labani akamwambia Yakobo, Tazama rundo hili, na tazama nguzo, nililoliweka kati yako nami.
Laban dit encore à Jacob: « Voici ce monceau et voici le monument que j’ai dressé entre moi et toi.
52 Rundo hili ni shahidi, na nguzo ni shahidi, kwamba sitapita rundo hili kuja kwako, na kwamba wewe hautapita rundo hili kuja kwangu, kwa madhara.
Ce monceau est témoin et ce monument est témoin que je n’avancerai pas vers toi au delà de ce monceau, et que tu n’avanceras pas vers moi au delà de ce monceau et de ce monument, pour faire du mal.
53 Mungu wa Ibrahimu, na mungu wa Nahori, miungu ya baba zao, waamue kati yetu.”Yakobo akaapa kwa Hofu ya Isaka baba yake.
Que le Dieu d’Abraham, le Dieu de Nachor et le Dieu de leurs pères soient juges entre nous! » Et Jacob jura par la Terreur d’Isaac.
54 Yakobo akatoa sadaka juu ya mlima na akawaita ndugu zake kula chakula. Walikula na kukaa usiku kucha juu ya mlima.
Et Jacob offrit un sacrifice sur la montagne, et il invita ses frères au repas. Ils mangèrent donc et passèrent la nuit sur la montagne.
55 Labani akaamka asubuhi na mapema, akawabusu wajuu zake na binti zake na kuwabariki. Kisha Labani akaondoka na kurudi kwake.
Laban se leva de bon matin; il baisa ses fils et ses filles et les bénit; puis il partit, pour retourner dans sa maison.

< Mwanzo 31 >