< Mwanzo 31 >
1 Basi Yakobo akasikia maneno ya wana wa Labani, wakisema, “Yakobo amechukuwa yote yaliyokuwa ya baba yetu, na ni kutoka katika mali ya baba yetu amepata utajiri wake.”
And he hears the words of Laban’s sons, saying, “Jacob has taken all that our father has; indeed, from that which our father has, he has made all this glory”;
2 Yakobo akaona mwonekano katika uso wa Labani. Akaona kwamba nia yake imebadilika.
and Jacob sees the face of Laban, and behold, it is not with him as before.
3 Kisha Yahwe akamwambia Yakobo, “Rudi katika nchi ya baba zako na ya ndugu zako, nami nitakuwa nawe.”
And YHWH says to Jacob, “Return to the land of your fathers, and to your family, and I am with you.”
4 Yakobo akatuma kuwaita Raheli na Lea uwandani katika kundi lake la kondoo
And Jacob sends and calls for Rachel and for Leah to the field to his flock;
5 naye akawambia, “Naona nia ya baba yenu kwangu imebadilika, lakini Mungu wa baba yangu amekuwa nami.
and says to them, “I am beholding your father’s face—that it is not toward me as before, and the God of my father has been with me,
6 Nanyi mnajua kwamba ni kwa nguvu zangu zote nimemtumikia baba yenu.
and you have known that with all my power I have served your father,
7 Baba yenu amenidanganya na amebadilisha ujira wangu mara kumi, lakini Mungu hakumruhusu kunidhuru.
and your father has played on me, and has changed my hire ten times; and God has not permitted him to do evil with me.
8 Ikiwa alisema, 'Wanyama wenye mabaka watakuwa ujira wako,' ndipo kondoo wote walipozaa watoto wenye mabaka. Na aliposema, wenye milia watakuwa ujira wako,' ndipo kundi lote lilipozaa watoto wenye milia.
If he says thus: The speckled are your hire, then all the flock bore speckled ones; and if he says thus: The striped are your hire, then all the flock bore striped;
9 Kwa njia hii Mungu amemnyang'anya mifugo baba yenu na kunipa mimi.
and God takes away the substance of your father, and gives to me.
10 Wakati fulani wa majira ya kupandana, niliona katika ndoto mabeberu yaliyowapanda kundi. Mabeberu yalikuwa ya milia, mabaka na madoa.
And it comes to pass at the time of the flock conceiving, that I lift up my eyes and see in a dream, and behold, the male goats, which are going up on the flock, [are] striped, speckled, and spotted;
11 Malaika wa Mungu akaniambia katika ndoto, 'Yakobo.' Nikasema, 'Mimi hapa.'
and the Messenger of God says to me in the dream, Jacob, and I say, Here I [am].
12 Akasema, 'Inua macho yako uone mabeberu wanaolipanda kundi. Wana milia, madoa na na mabaka, kwani nimeona kila jambo Labani analokutendea.
And He says, Now lift up your eyes and see [that] all the male goats which are going up on the flock [are] striped, speckled, and spotted, for I have seen all that Laban is doing to you;
13 Mimi ni Mungu wa Betheli, mahali ulipoitia nguzo mafuta, mahali uliponitolea nadhiri. Basi sasa inuka na uondoke katika nchi hii na kurudi katika nchi uliyozaliwa.
I [am] the God of Bethel where you have anointed a standing pillar, where you have vowed a vow to me; now, arise, go out from this land, and return to the land of your birth.”
14 Raheli na Lea wakajibu na kumwambia, “Je kuna sehemu yoyote au urithi wetu katika nyumba ya baba yetu?
And Rachel answers—Leah also—and says to him, “Have we yet a portion and inheritance in the house of our father?
15 Je hatutendei kama wageni? Kwa maana ametuuza na kwa ujumla ametapanya pesa zetu.
Have we not been reckoned strangers to him? For he has sold us, and he also utterly consumes our money;
16 Mali zote ambazo sasa Mungu amemnyang'anya baba yetu ni zetu na watoto wetu. Sasa basi, lolote Mungu alilokuambia, fanya.
for all the wealth which God has taken away from our father, it [is] ours, and our children’s; and now, all that God has said to you—do.”
17 Kisha Yakobo akainuka na kuwapandisha wanawe na wakeze kwenye ngamia.
And Jacob rises, and lifts up his sons and his wives on the camels,
18 Akawaongoza mifugo wake wote mbele yake, pamoja na mali zake zote, wakiwemo wanyama aliowapata huko Padani Aramu. Kisha akaenda kuelekea kwa Isaka baba yake katika nchi ya Kanaani.
and leads all his livestock, and all his substance which he has acquired, the livestock of his getting, which he has acquired in Padan-Aram, to go to his father Isaac, to the land of Canaan.
19 Labani alipokuwa amekwenda kuwakata manyoya kondoo wake, Raheli akaiba miungu ya nyumba ya baba yake.
And Laban has gone to shear his flock, and Rachel steals the teraphim which her father has;
20 Yakobo pia akamdanganya Labani Mwarami, kwa kutomtaarifu kwamba anaondoka.
and Jacob deceives the heart of Laban the Aramean, because he has not declared to him that he is fleeing;
21 Hivyo akaondoka na vyote alivyokuwa navyo na kwa haraka akavuka mto, na akaenda kuelekea nchi ya vilima ya Gileadi.
and he flees, he and all that he has, and rises, and passes over the River, and sets his face [toward] the Mount of Gilead.
22 Siku ya tatu Labani akaambiwa kwamba Yakobo amekimbia.
And it is told to Laban on the third day that Jacob has fled,
23 Hivyo akawachukua ndugu zake pamoja naye na kumfuatia kwa safari ya siku saba. Akampata katika nchi ya vilima ya Gileadi.
and he takes his brothers with him, and pursues after him a journey of seven days, and overtakes him in the Mount of Gilead.
24 Basi Mungu akaja kwa Labani Mwarami katika ndoto usiku na kumwambia, “Ujiadhari kumwambia Yakobo jambo lolote liwe jema au baya.”
And God comes to Laban the Aramean in a dream of the night and says to him, “Take heed to yourself lest you speak with Jacob from good to evil.”
25 Labani akampata Yakobo. Basi Yakobo alikuwa amepiga hema yake katika nchi ya vilima. Labani pia akapiga kambi pamoja na ndugu zake katika nchi ya kilima ya Gileadi.
And Laban overtakes Jacob; and Jacob has fixed his tent in the mountain; and Laban with his brothers have fixed [theirs] in the Mount of Gilead.
26 Labani akamwambia Yakobo, “Umefanya nini, kwamba umewachukua binti zangu kama mateka wa vita?
And Laban says to Jacob, “What have you done that you deceive my heart, and lead away my daughters as captives of the sword?
27 Kwa nini umekimbia kwa siri na kunihadaa kwa kutokuniambia? Ningekuruhusu uondoke kwa sherehe na kwa nyimbo, kwa matari na vinubi.
Why have you hidden yourself to flee, and deceive me, and have not declared to me, and I send you away with joy and with songs, with tambourine and with harp,
28 Haukuniacha niwabusu wajukuu wangu na binti zangu kwa kuwaaga. Basi umefanya upumbavu.
and have not permitted me to kiss my sons and my daughters? Now you have acted foolishly in doing [so];
29 Iko katika uwezo wangu kukudhuru, lakini Mungu wa baba yako alisema nami usiku wa leo na kuniambia, 'Jiadhari usimwambie Yakobo neno la heri wala shari.'
my hand is to God to do evil with you, but the God of your father last night has spoken to me, saying, Take heed to yourself from speaking with Jacob from good to evil.
30 Na sasa, umeondoka kwa sababu umeitamani sana nyumba ya baba yako. Lakini kwa nini umeiba miungu yangu?
And now, you have certainly gone, because you have been very desirous for the house of your father; why have you stolen my gods?”
31 Yakobo akajibu na kumwambia Labani, “Ni kwa sababu niliogopa na kudhani kuwa ungeninyang'anya binti zako kwa nguvu ndiyo maana nikaondoka kwa siri.
And Jacob answers and says to Laban, “Because I was afraid, for I said, Lest you violently take away your daughters from me;
32 Yeyote aliyeiiba miungu yako hataendelea kuishi. Mbele ya ndugu zetu, onesha chochote kilichochako nilichonacho na uchukue.” Kwa maana Yakobo hakujua kwamba Raheli alikuwa ameviiba.
with whomsoever you find your gods—he must not live; before our brothers discern for yourself what [is] with me, and take to yourself”: and Jacob has not known that Rachel has stolen them.
33 Labani akaingia katika hema ya Yakobo, katika hema ya Lea, na katika hema za wale wajakazi wawili, lakini hakuviona. Akatoka katika hema ya Lea na kuingia katika hema ya Raheli.
And Laban goes into the tent of Jacob, and into the tent of Leah, and into the tent of the two handmaidens, and has not found; and he goes out from the tent of Leah, and goes into the tent of Rachel.
34 Basi Raheli alikuwa ameichukua miungu ya nyumbani, na kuiweka katika ngozi ya ngamia, na kukaa juu yake. Labani akatafuta katika hema yote, lakini hakuiona.
And Rachel has taken the teraphim, and puts them in the furniture of the camel, and sits on them; and Laban feels all the tent, and has not found;
35 Akamwambia baba yake, “Usikasirike, bwana wangu, kwamba siwezi kusimama mbele yako, kwani nipo katika kipindi changu.” Hivyo akatafuta lakini hakuiona miungu ya nyumbani mwake.
and she says to her father, “Let it not be displeasing in the eyes of my lord that I am not able to rise at your presence, for the way of women [is] on me”; and he searches, and has not found the teraphim.
36 Yakobo akakasirika na kuojiana na Labani. Akamwambia, “Kosa langu ni nini? Dhambi yangu ni ipi, hata ukanifuatia kwa ukali?
And it is displeasing to Jacob, and he strives with Laban; and Jacob answers and says to Laban, “What [is] my transgression? What my sin, that you have burned after me?
37 Kwa maana umechunguza mali zangu zote. Umeona nini kati ya kitu chochote cha nyumbani mwako? Viweke hapa mbele ya ndugu zetu, ili waamue kati yetu wawili.
For you have felt all my vessels: what have you found of all the vessels of your house? Set here before my brothers, and your brothers, and they decide between us both.
38 Kwa miaka ishirini nimekuwa nawe. Kondoo wako na mbuzi wako hawakutoa mimba, wala sikula dume lolote la kondoo katika wanyama wako.
These twenty years I [am] with you: your ewes and your female goats have not miscarried, and the rams of your flock I have not eaten;
39 Kilichoraruliwa na hayawani sikukuletea. Badala yake, nilichukua upotevu huo, kwamba wameibwa mchana au usiku.
the torn I have not brought to you—I repay it—from my hand you seek it; I have been deceived by day, and I have been deceived by night;
40 Nilikuwepo wakati wote; mchana joto lilinipata, na baridi wakati wa usiku; na sikupata usingizi.
I have been [thus]: drought has consumed me in the day, and frost by night, and my sleep wanders from my eyes.
41 Miaka hii ishirini nimekuwa katika nyumba yako. Nilikufanyia kazi miaka kumi na nne kwa ajili ya binti zako wawili, na miaka sita kwa ajili ya wanyama wako. Umebadili ujira wangu mara kumi.
This [is] to me twenty years in your house: I have served you fourteen years for your two daughters, and six years for your flock; and you change my hire ten times;
42 Isipokuwa Mungu wa baba yangu, Mungu wa Ibrahimu, yule Isaka anayemwofu, amekuwa nami, bila shaka sasa ungenipeleka mikono mitupu. Mungu ameliona teso langu na jinsi nilivyofanya kazi kwa bidii, na hivyo akakukemea usiku wa leo.
unless the God of my father, the God of Abraham, and the Fear of Isaac, had been for me, surely now you had sent me away empty; God has seen my affliction and the labor of my hands, and reproves last night.”
43 Labani akajibu na kumwambia Yakobo, “Mabinti hawa ni mabinti zangu, wajukuu ni wajukuu wangu, na wanyama ni wanyama wangu. Yote uyaonayo ni yangu. Lakini nitafanya nini leo kwa hawa binti zangu, au kwa watoto wao waliowazaa?
And Laban answers and says to Jacob, “The daughters [are] my daughters, and the sons my sons, and the flock my flock, and all that you are seeing [is] mine; and to my daughters—what do I to these today, or to their sons whom they have born?
44 Hivyo sasa, na tufanye agano, wewe nami, na liwe shahidi kati yangu nawe.”
And now, come, let us make a covenant, I and you, and it has been for a witness between me and you.”
45 Hivyo Yakobo akachukua jiwe na kuliweka kama nguzo.
And Jacob takes a stone, and lifts it up [for] a standing pillar;
46 Yakobo akawambia ndugu zake, “Kusanyeni mawe.” Hivyo wakachukua mawe na kufanya rundo. Kisha wakala pale kati ya lile rundo.
and Jacob says to his brothers, “Gather stones,” and they take stones, and make a heap; and they eat there on the heap;
47 Labani aliliita Yega Saha Dutha, lakini Yakobo akaiita Galeedi
and Laban calls it Jegar-Sahadutha; and Jacob has called it Galeed.
48 Labani akasema, “Rundo hili ni shahidi kati yangu nawe leo.” Kwa hiyo jina lake likaitwa Galedi.
And Laban says, “This heap [is] witness between me and you today”; therefore has he called its name Galeed;
49 Inaitwa pia Mispa, kwa sababu Labani alisema, “Yahwe na atuangalie mimi nawe, tunapokuwa hatuonani.
Mizpah also, for he said, “YHWH watches between me and you, for we are hidden from one another;
50 Ikiwa utawatesa binti zangu, au ikiwa utachukua wanawake wengine mbali na binti zangu, japokuwa hakuna mwingine yupo nasi, tazama, Mungu ni shahidi kati yangu nawe.”
if you afflict my daughters, or take wives beside my daughters—there is no man with us—see, God [is] witness between me and you.”
51 Labani akamwambia Yakobo, Tazama rundo hili, na tazama nguzo, nililoliweka kati yako nami.
And Laban says to Jacob, “Behold, this heap, and behold, the standing pillar which I have cast between me and you;
52 Rundo hili ni shahidi, na nguzo ni shahidi, kwamba sitapita rundo hili kuja kwako, na kwamba wewe hautapita rundo hili kuja kwangu, kwa madhara.
this heap [is] witness, and the standing pillar [is] witness, that I do not pass over this heap to you, and that you do not pass over this heap and this standing pillar to me—for evil;
53 Mungu wa Ibrahimu, na mungu wa Nahori, miungu ya baba zao, waamue kati yetu.”Yakobo akaapa kwa Hofu ya Isaka baba yake.
the God of Abraham and the God of Nahor, judges between us—the God of their father,” and Jacob swears by the Fear of his father Isaac.
54 Yakobo akatoa sadaka juu ya mlima na akawaita ndugu zake kula chakula. Walikula na kukaa usiku kucha juu ya mlima.
And Jacob sacrifices a sacrifice on the mountain, and calls to his brothers to eat bread, and they eat bread, and lodge on the mountain;
55 Labani akaamka asubuhi na mapema, akawabusu wajuu zake na binti zake na kuwabariki. Kisha Labani akaondoka na kurudi kwake.
and Laban rises early in the morning, and kisses his sons and his daughters, and blesses them; and Laban goes on, and turns back to his place.