< Mwanzo 30 >
1 Raheli alipoona kwamba hamzalii Yakobo watoto, Raheli akamwonea wivu dada yake. Akamwambia Yakobo, “Nipe watoto, sivyo nitakufa.”
And when Rachel saw that she bore Jacob no children, Rachel envied her sister; and said to Jacob, Give me children, or else I die.
2 Hasira ya Yakobo ikawaka juu ya Raheli. Akasema, “Mimi ni badala ya Mungu, aliyekuzuilia usipate watoto?
And Jacob's anger was kindled against Rachel; and he said, [Am] I in God's stead, who hath withheld from thee the fruit of the womb?
3 Akasema, “Tazama, kuna mjakazi wangu Bilha. Lala naye, hivyo aweze kuzaa watoto magotini pangu, nami nitapata watoto kwake.
And she said, Behold, my maid Bilhah, go in to her; and she shall bear upon my knees, that I may also have children by her.
4 Hivyo akampa Bilha mjakazi kama mke wake, na Yakobo akalala naye.
And she gave him Bilhah, her handmaid, for a wife: and Jacob went in to her.
5 Bilha akashika mimba na kumzalia Yakobo mwana.
And Bilhah conceived, and bore Jacob a son.
6 Kisha Raheli akasema, “Mungu ameamua kwa faida yangu. Ameyasikiliza maombi yangu na kunipa mwana.” Kwa sababu hiyo akamwita jina lake Dani
And Rachel said, God hath judged me, and hath also heard my voice, and hath given me a son: therefore she called his name Dan.
7 Bilha, mjakazi wa Raheli, akashika mimba tena na kumzalia Yakobo mwana wa pili.
And Bilhah, Rachel's maid, conceived again, and bore Jacob a second son.
8 Raheli akasema, “Kwa mashindano yenye nguvu nimeshindana na dada yangu na kushinda.” Akamwita jina lake Naftali.
And Rachel said, With great wrestlings have I wrestled with my sister, and I have prevailed: and she called his name Naphtali.
9 Lea alipoona kwamba ameacha kuzaa, akamchukua Zilpa, mjakazi wake, na kumpa Yakobo kama mke wake.
When Leah saw that she had left bearing, she took Zilpah, her maid, and gave her Jacob for a wife.
10 Zilpa, mjakazi wa Lea, akamzalia Yakobo mwana.
And Zilpah, Leah's maid, bore Jacob a son.
11 Lea akasema, “Hii ni bahati njema!” Hivyo akamwita jina lake Gadi.
And Leah said, A troop cometh: and she called his name Gad.
12 Kisha Zilpa, mjakazi wa Lea, akamzalia Yakobo mwana wa pili.
And Zilpah, Leah's maid, bore Jacob a second son.
13 Lea akasema, “Nina furaha! Kwa maana mabinti wataniita furaha.” Hivyo akamwita jina lake Asheri.
And Leah said, Happy am I, for the daughters will call me blessed: and she called his name Asher.
14 Siku za mavuno ya ngano Rubeni akaenda shambani na kuona tunguja. Akazileta kwa mama yake. Kisha Raheli akamwambia Lea, “Nipe baadhi ya tunguja za mwanao.”
And Reuben went, in the days of wheat-harvest, and found mandrakes in the field, and brought them to his mother Leah. Then Rachel said to Leah, Give me, I pray thee, of thy son's mandrakes.
15 Lea akamwambia, “Je ni jambo dogo kwako, kumchukua mme wangu? Je na sasa unataka kuchukua tunguja za mwanangu pia? Raheli akasema, “Kisha atalala nawe leo usiku, kwa kubadilishana na tunguja za mwanao.
And she said to her, [Is it] a small matter that thou hast taken my husband? and wouldest thou take away my son's mandrakes also? And Rachel said, Therefore he shall lie with thee to-night for thy son's mandrakes.
16 Jioni Yakobo akaja kutoka uwandani. Lea akaenda kumlaki na kusema, “Leo usiku utalala nami, kwani nimekuajiri kwa tunguja za mwanangu.” Hivyo Yakobo akalala na Lea usiku huo.
And Jacob came from the field in the evening, and Leah went out to meet him, and said, Thou must come in to me; for surely I have hired thee with my son's mandrakes. And he lay with her that night.
17 Mungu akamsikia Lea, na akashika mimba na kumzalia Yakobo mwana wa tano.
And God hearkened to Leah, and she conceived, and bore Jacob the fifth son.
18 Lea akasema, “Mungu amenipa ujira wangu, kwa sababu nilimpa mme wangu mjakazi wangu.” Akamwita jina lake Isakari.
And Leah said, God hath given me my hire, because I have given my maiden to my husband: and she called his name Issachar.
19 Lea akashika mimba tena na kuzaa mwana wa tano kwa Yakobo.
And Leah conceived again, and bore Jacob the sixth son.
20 Lea akasema, “Mungu amenipa zawadi njema. Sasa mme wangu ataniheshimu, kwa sababu nimemzalia wana sita.” Akamwita jina lake Zabuloni.
And Leah said, God hath endowed me [with] a good dower; now will my husband dwell with me, because I have borne him six sons: and she called his name Zebulun.
21 Baadaye akazaa binti na kumwita jina lake Dina.
And afterwards she bore a daughter, and called her name Dinah.
22 Mungu akamkumbuka Raheli na kumsikiliza. Akampa kushika mimba.
And God remembered Rachel, and God hearkened to her, and rendered her fruitful.
23 Akashika mimba na kuzaa mwana. Akasema, “Mungu ameiondoa aibu yangu.”
And she conceived, and bore a son; and said, God hath taken away my reproach:
24 Akamwita jina lake Yusufu, akisema, Yahwe ameniongeza mwana mwingine.”
And she called his name Joseph; and said, The LORD will add to me another son.
25 Baada ya Raheli kumzaa Yusufu, Yakobo akamwambia Labani, “Niache niande, ili kwamba niende nyumbani kwetu na katika nchi yangu.
And it came to pass, when Rachel had borne Joseph, that Jacob said to Laban, Send me away, that I may go to my own place, and to my country.
26 Nipe wake zangu na watoto wangu niliokutumikia kwa ajili yao, na uniache niondoke, kwani unafahamu nilivyokutumikia.
Give [me] my wives and my children, for whom I have served thee, and let me go: for thou knowest my service which I have done thee.
27 Labani akamwambia, “Ikiwa nimepata kibali machoni pako, subiri, kwa sababu nimejifunza kwa kutumia uaguzi kwamba Yahwe amenibariki kwa ajili yako.”
And Laban said to him, I pray thee, if I have found favor in thine eyes, [tarry: for] I have learned by experience, that the LORD hath blessed me for thy sake.
28 Kisha akasema, “Taja ujira wako, nami nitalipa.”
And he said, Appoint me thy wages, and I will give [it].
29 Yakobo akamwambia, “Unajua nilivyokutumikia, na jinsi ambavyo mifugo wako wamekuwa nami.
And he said to him, Thou knowest how I have served thee, and how thy cattle were with me.
30 Kwani walikuwa wachache kabla sijaja, na wameongezeka kwa wingi. Popote nilipokutumikia Mungu amekubariki. Je ni lini mimi nitaandaa kwa ajili ya nyumba yangu pia?”
For [it was] little which thou hadst before I [came], and it is [now] increased to a multitude; and the Lord hath blessed thee since my coming: and now when shall I provide for my own house also?
31 Hivyo Labani akasema, “Je nikulipe nini? Yakobo akasema, 'Usinipe chochote. Ikiwa utafanya jambo hili kwa ajili yangu, nitawalisha tena kondoo wako na kuwatunza.
And he said, What shall I give thee? And Jacob said, Thou shalt not give me any thing; if thou wilt do this thing for me, I will again feed [and] keep thy flock:
32 Niache nipite kati ya kundi lako lote leo, kwa kuondoa kila kondoo mwenye milia na mabaka, na kila kondoo mweusi kati yao, na kati ya wenye mabaka na milia katika mbuzi. Hawa watakuwa ujira wangu.
I will pass through all thy flock to-day, removing from thence all the speckled and spotted cattle, and all the brown cattle among the sheep, and the spotted and speckled among the goats: and [of such] shall be my hire.
33 Uadilifu wangu utashuhudia kwa ajili yangu hapo baadaye, utakapokuja kuangalia ujira wangu. Kila ambaye hana milia na hana madoa miongoni mwa mbuzi, na mweusi kati ya kondoo, ikiwa wataonekana kwangu, watahesabiwa kuwa wameibwa.”
So shall my righteousness answer for me in time to come, when it shall come for my hire before thy face: every one that [is] not speckled and spotted among the goats, and brown among the sheep, that shall be accounted stolen with me.
34 Labani akasema, “Nakubali. Na iwe kama yalivyo maneno yako.”
And Laban said, Behold, I would it might be according to thy word.
35 Siku hiyo Labani akaondoa mabeberu yaliyokuwa na milia na madoa, na majike ya mbuzi yaliyokuwa na milia na madoa, kila aliyekuwa mweupe, na weusi wote katika mbuzi, akawakabidhi katika mikono ya wanaye.
And he removed that day the he-goats that were ring-streaked and spotted, and all the she-goats that were speckled and spotted; every one that had [some] white in it, and all the brown among the sheep, and gave [them] into the hands of his sons.
36 Pia Labani akaweka safari ya siku tatu kati yake na Yakobo. Hivyo Yakobo akabaki kuchunga wale kondoo wa Labani waliosalia.
And he set three days' journey between himself and Jacob: and Jacob fed the rest of Laban's flocks.
37 Yakobo akachukua matawi mabichi yaliyokatwa ya mipopla, mlozi na mwaramoni mbichi akatoa maganda ili michilizi myeupe ionekane, na akaifanya sehemu nyeupe ya ndani ya mti iliyokuwa ndani ya fito ionekane.
And Jacob took to him rods of green poplar, and of the hazel and chesnut-tree; and peeled white streaks in them, and made the white appear which [was] in the rods.
38 Kisha akaziweka fito alizokuwa amezibambua mbele ya makundi ya kondoo, mbele ya mabirika yakunyweshea walipokuja kunywa maji. Wakashika mimba walipokuja kunywa maji.
And he set the rods, which he had peeled, before the flocks in the gutters in the watering-troughs, when the flocks came to drink, that they should conceive when they came to drink.
39 Wanyama wakapandana mbele ya fito; nao wakazaa watoto wenye milia, mabaka na wenye madoa.
And the flocks conceived before the rods, and brought forth cattle ring-streaked, speckled, and spotted.
40 Yakobo akawatenga hawa wanakondoo, lakini akawafanya waliosalia kuelekea wanyama wenye milia na kondoo weusi wote katika kundi la Labani. Kisha akayatenga makundi yake mwenyewe pekee na hakuwaweka pamoja na wale wa Labani.
And Jacob separated the lambs, and set the faces of the flocks towards the ring-streaked, and all the brown in the flock of Laban: and he put his own flocks by themselves, and put them not with Laban's cattle.
41 Pindi kondoo wenye nguvu katika kundi walipopandana, Yakobo alilaza fito katika mabirika ya maji mbele ya macho ya kundi, ili kwamba washike mimba kati ya fito.
And it came to pass, whenever the stronger cattle conceived, that Jacob laid the rods before the eyes of the cattle in the gutters, that they might conceive among the rods.
42 Lakini wakati waliodhaifu walipokuja, hakuweka fito mbele yao. Hivyo wanyama dhaifu wakawa wa Labani, na wenye nguvu wakawa wa Yakobo.
But when the cattle were feeble, he put [them] not in: so the feebler were Laban's, and the stronger Jacob's.
43 Mtu huyo akastawi sana. Akawa na kundi kubwa la kondoo, wajakazi na wajoli, ngamia na punda.
And the man increased exceedingly, and had many cattle, and maid-servants, and men-servants, and camels, and asses.