< Mwanzo 30 >
1 Raheli alipoona kwamba hamzalii Yakobo watoto, Raheli akamwonea wivu dada yake. Akamwambia Yakobo, “Nipe watoto, sivyo nitakufa.”
And Rachel saw she had borne no children unto Jacob, so Rachel became envious of her sister, —and said unto Jacob, Come! give me children, or else, I die.
2 Hasira ya Yakobo ikawaka juu ya Raheli. Akasema, “Mimi ni badala ya Mungu, aliyekuzuilia usipate watoto?
Then kindled the anger of Jacob with Rachel, —and he said, Am I, in the place of God, who hath withheld from thee the fruit of the womb?
3 Akasema, “Tazama, kuna mjakazi wangu Bilha. Lala naye, hivyo aweze kuzaa watoto magotini pangu, nami nitapata watoto kwake.
And she said, Lo! my handmaid, Bilhah. Go in unto her, —that she may bear upon my knees, so that, I also, may be builded up by her!
4 Hivyo akampa Bilha mjakazi kama mke wake, na Yakobo akalala naye.
And she gave him Bilhah her handmaid, to wife, —and Jacob went in unto her;
5 Bilha akashika mimba na kumzalia Yakobo mwana.
and Bilhah conceived, and bare unto Jacob a son;
6 Kisha Raheli akasema, “Mungu ameamua kwa faida yangu. Ameyasikiliza maombi yangu na kunipa mwana.” Kwa sababu hiyo akamwita jina lake Dani
and Rachel said God hath vindicated me. Moreover also he hath hearkened unto my voice, and hath given me a son. For this cause, called she his name Dan.
7 Bilha, mjakazi wa Raheli, akashika mimba tena na kumzalia Yakobo mwana wa pili.
And Bilhah, Rachel’s handmaid conceived again, and bare a second son to Jacob.
8 Raheli akasema, “Kwa mashindano yenye nguvu nimeshindana na dada yangu na kushinda.” Akamwita jina lake Naftali.
Then said Rachel With wrestlings of God, have I wrestled with my sister Yea I have prevailed. So she called his name, Naphtali.
9 Lea alipoona kwamba ameacha kuzaa, akamchukua Zilpa, mjakazi wake, na kumpa Yakobo kama mke wake.
Then saw Leah, that she had left off bearing, —so she took Zilpah, her handmaid, and gave her to Jacob to wife.
10 Zilpa, mjakazi wa Lea, akamzalia Yakobo mwana.
And Zilpah, Leah’s handmaid, bare to Jacob a son:
11 Lea akasema, “Hii ni bahati njema!” Hivyo akamwita jina lake Gadi.
and Leah said, Victory hath come! So she called his name Gad.
12 Kisha Zilpa, mjakazi wa Lea, akamzalia Yakobo mwana wa pili.
And Zilpah, Leah’s handmaid bare a second son to Jacob;
13 Lea akasema, “Nina furaha! Kwa maana mabinti wataniita furaha.” Hivyo akamwita jina lake Asheri.
and Leah said, For my happiness, surely happy have daughters pronounced me. So she called his name, Asher.
14 Siku za mavuno ya ngano Rubeni akaenda shambani na kuona tunguja. Akazileta kwa mama yake. Kisha Raheli akamwambia Lea, “Nipe baadhi ya tunguja za mwanao.”
Then went Reuben, in the days of the wheat harvest, and found mandrakes, in the field, and brought them in unto Leah his mother, and Rachel said unto Leah, Pray give me, some of the mandrakes of thy son
15 Lea akamwambia, “Je ni jambo dogo kwako, kumchukua mme wangu? Je na sasa unataka kuchukua tunguja za mwanangu pia? Raheli akasema, “Kisha atalala nawe leo usiku, kwa kubadilishana na tunguja za mwanao.
And she said to her, Is it, a small thing, that thou hast taken away my husband? And wouldst thou take away, even the mandrakes of my son? Then said Rachel, Therefore, shall he lie with thee to-night, for the mandrakes of thy son.
16 Jioni Yakobo akaja kutoka uwandani. Lea akaenda kumlaki na kusema, “Leo usiku utalala nami, kwani nimekuajiri kwa tunguja za mwanangu.” Hivyo Yakobo akalala na Lea usiku huo.
And Jacob came in from the field, in the evening, so Leah went out to meet him and said: Unto me, shalt thou come in, for I have hired, thee, even with the mandrakes of my son. And he lay with her that night,
17 Mungu akamsikia Lea, na akashika mimba na kumzalia Yakobo mwana wa tano.
And God hearkened unto Leah, —and she conceived and bare to Jacob a fifth son.
18 Lea akasema, “Mungu amenipa ujira wangu, kwa sababu nilimpa mme wangu mjakazi wangu.” Akamwita jina lake Isakari.
Then said Leah. God hath given my hire, in that I gave my handmaid to my husband. So she called his name, Issachar.
19 Lea akashika mimba tena na kuzaa mwana wa tano kwa Yakobo.
And Leah conceived again and bare a sixth son to Jacob.
20 Lea akasema, “Mungu amenipa zawadi njema. Sasa mme wangu ataniheshimu, kwa sababu nimemzalia wana sita.” Akamwita jina lake Zabuloni.
Then said Leah, God hath dowered me even me with a hand-some dowry, Now! will my husband dwell with me, for I have borne him six sons. So she called his name, Zebulon.
21 Baadaye akazaa binti na kumwita jina lake Dina.
And afterwards she bare a daughter, —so she called her name, Dinah.
22 Mungu akamkumbuka Raheli na kumsikiliza. Akampa kushika mimba.
Then God remembered Rachel, —and God hearkened unto her, and granted her to bear.
23 Akashika mimba na kuzaa mwana. Akasema, “Mungu ameiondoa aibu yangu.”
So she conceived and bare a son, —and said, God hath taken away my reproach;
24 Akamwita jina lake Yusufu, akisema, Yahwe ameniongeza mwana mwingine.”
So she called his name Joseph, saying, Yahweh is adding unto me another son.
25 Baada ya Raheli kumzaa Yusufu, Yakobo akamwambia Labani, “Niache niande, ili kwamba niende nyumbani kwetu na katika nchi yangu.
And it came to pass, when Rachel had borne Joseph, that Jacob said unto Laban, Let me go that I may take my journey, unto my place, and to my land.
26 Nipe wake zangu na watoto wangu niliokutumikia kwa ajili yao, na uniache niondoke, kwani unafahamu nilivyokutumikia.
Come, give me my wives and my children for whom I have served thee and let me take my journey, —for, thou, knowest my service wherewith I have served thee.
27 Labani akamwambia, “Ikiwa nimepata kibali machoni pako, subiri, kwa sababu nimejifunza kwa kutumia uaguzi kwamba Yahwe amenibariki kwa ajili yako.”
And Laban said unto him, If, I pray thee, I have found favour in thine eyes, …I have divined that Yahweh hath blessed me for thy sake.
28 Kisha akasema, “Taja ujira wako, nami nitalipa.”
And he said, —Come, fix thy wages for me, that I may give it!
29 Yakobo akamwambia, “Unajua nilivyokutumikia, na jinsi ambavyo mifugo wako wamekuwa nami.
And he said unto him, Thou, knowest how I have served thee, —and how thy cattle have fared, with me.
30 Kwani walikuwa wachache kabla sijaja, na wameongezeka kwa wingi. Popote nilipokutumikia Mungu amekubariki. Je ni lini mimi nitaandaa kwa ajili ya nyumba yangu pia?”
For it was, little, that thou hadst—before I came and then it brake forth into multitude, and Yahweh blessed thee at my every step. Now, therefore, when am, I, also to do something for my own house?
31 Hivyo Labani akasema, “Je nikulipe nini? Yakobo akasema, 'Usinipe chochote. Ikiwa utafanya jambo hili kwa ajili yangu, nitawalisha tena kondoo wako na kuwatunza.
And he said, What shall I give thee? And Jacob said: Thou shall give me, nothing at all, If thou wilt do for me this thing, I will return, I will shepherd thy flock I will keep it:
32 Niache nipite kati ya kundi lako lote leo, kwa kuondoa kila kondoo mwenye milia na mabaka, na kila kondoo mweusi kati yao, na kati ya wenye mabaka na milia katika mbuzi. Hawa watakuwa ujira wangu.
Let me pass through all thy flock to-day, removing from thence every young one that is speckled and spotted and every young one that is dark-coloured among the young sheep, and spotted and speckled among the goats, and they shall be my wages.
33 Uadilifu wangu utashuhudia kwa ajili yangu hapo baadaye, utakapokuja kuangalia ujira wangu. Kila ambaye hana milia na hana madoa miongoni mwa mbuzi, na mweusi kati ya kondoo, ikiwa wataonekana kwangu, watahesabiwa kuwa wameibwa.”
And my righteousness shall answer for me on a future day, when thou shall come in respecting my hire that is before thee, Every one that is not speckled and spotted among the goats and dark-coloured among the young sheep, stolen, shall it be accounted, if found with me.
34 Labani akasema, “Nakubali. Na iwe kama yalivyo maneno yako.”
Then said Laban, Lo! would it might be according to thy word!
35 Siku hiyo Labani akaondoa mabeberu yaliyokuwa na milia na madoa, na majike ya mbuzi yaliyokuwa na milia na madoa, kila aliyekuwa mweupe, na weusi wote katika mbuzi, akawakabidhi katika mikono ya wanaye.
So he removed, on that day, the he-goats that were striped and spotted and all the she-goats that were speckled and spotted, every one that had white in it, and every dark-coloured one among the young sheep, —and delivered them into the hand of his sons;
36 Pia Labani akaweka safari ya siku tatu kati yake na Yakobo. Hivyo Yakobo akabaki kuchunga wale kondoo wa Labani waliosalia.
then put he a journey of three days between himself and Jacob, —but, Jacob himself, continued tending the flocks of Laban that were left.
37 Yakobo akachukua matawi mabichi yaliyokatwa ya mipopla, mlozi na mwaramoni mbichi akatoa maganda ili michilizi myeupe ionekane, na akaifanya sehemu nyeupe ya ndani ya mti iliyokuwa ndani ya fito ionekane.
So then Jacob took him rods of young storax, and hazel and maple, —and peeled in them white stripes, laying bare the white which was on the rods.
38 Kisha akaziweka fito alizokuwa amezibambua mbele ya makundi ya kondoo, mbele ya mabirika yakunyweshea walipokuja kunywa maji. Wakashika mimba walipokuja kunywa maji.
And he set the rods which he had peeled, in the channels in the troughs of water, —where the flocks came in to drink straight before the flocks, and the females of the flock used to be in heat when they came in to drink;
39 Wanyama wakapandana mbele ya fito; nao wakazaa watoto wenye milia, mabaka na wenye madoa.
and the males of the flock were in heat before the rods, —so the flocks brought forth ring-straked, speckled, and spotted.
40 Yakobo akawatenga hawa wanakondoo, lakini akawafanya waliosalia kuelekea wanyama wenye milia na kondoo weusi wote katika kundi la Labani. Kisha akayatenga makundi yake mwenyewe pekee na hakuwaweka pamoja na wale wa Labani.
The rams also, did Jacob separate, and then set the faces of the flocks towards the ring-straked and all the dark-coloured, among the flocks of Laban, —and he put his own droves by themselves, and put them not with the flocks of Laban.
41 Pindi kondoo wenye nguvu katika kundi walipopandana, Yakobo alilaza fito katika mabirika ya maji mbele ya macho ya kundi, ili kwamba washike mimba kati ya fito.
So it came to pass whensoever the stronger of the flocks were in heat, that Jacob set the rods before the eyes of the flocks in the channels, —that the females might be in heat among the rods;
42 Lakini wakati waliodhaifu walipokuja, hakuweka fito mbele yao. Hivyo wanyama dhaifu wakawa wa Labani, na wenye nguvu wakawa wa Yakobo.
but, when the flocks were late in bearing, he did not set them, —and so the late-born were Laban’s, but the strong ones Jacob’s.
43 Mtu huyo akastawi sana. Akawa na kundi kubwa la kondoo, wajakazi na wajoli, ngamia na punda.
Thus did the man break forth, exceedingly, —thus came he to have flocks in abundance, and maid-servants, and men-servants and camels and asses.