< Mwanzo 30 >

1 Raheli alipoona kwamba hamzalii Yakobo watoto, Raheli akamwonea wivu dada yake. Akamwambia Yakobo, “Nipe watoto, sivyo nitakufa.”
And Rachel sees that she has not borne to Jacob, and Rachel is envious of her sister, and says to Jacob, “Give me sons, and if there is none—I die.”
2 Hasira ya Yakobo ikawaka juu ya Raheli. Akasema, “Mimi ni badala ya Mungu, aliyekuzuilia usipate watoto?
And Jacob’s anger burns against Rachel, and he says, “Am I in stead of God who has withheld from you the fruit of the womb?”
3 Akasema, “Tazama, kuna mjakazi wangu Bilha. Lala naye, hivyo aweze kuzaa watoto magotini pangu, nami nitapata watoto kwake.
And she says, “Behold, my handmaid Bilhah, go in to her, and she bears on my knees, and I am built up, even I, from her”;
4 Hivyo akampa Bilha mjakazi kama mke wake, na Yakobo akalala naye.
and she gives Bilhah her maidservant to him for a wife, and Jacob goes in to her;
5 Bilha akashika mimba na kumzalia Yakobo mwana.
and Bilhah conceives, and bears a son to Jacob,
6 Kisha Raheli akasema, “Mungu ameamua kwa faida yangu. Ameyasikiliza maombi yangu na kunipa mwana.” Kwa sababu hiyo akamwita jina lake Dani
and Rachel says, “God has decided for me, and has also listened to my voice, and gives a son to me”; therefore she has called his name Dan.
7 Bilha, mjakazi wa Raheli, akashika mimba tena na kumzalia Yakobo mwana wa pili.
And Bilhah, Rachel’s maidservant, conceives again, and bears a second son to Jacob,
8 Raheli akasema, “Kwa mashindano yenye nguvu nimeshindana na dada yangu na kushinda.” Akamwita jina lake Naftali.
and Rachel says, “With wrestlings of God I have wrestled with my sister, indeed, I have prevailed”; and she calls his name Napthali.
9 Lea alipoona kwamba ameacha kuzaa, akamchukua Zilpa, mjakazi wake, na kumpa Yakobo kama mke wake.
And Leah sees that she has ceased from bearing, and she takes Zilpah her maidservant, and gives her to Jacob for a wife;
10 Zilpa, mjakazi wa Lea, akamzalia Yakobo mwana.
and Zilpah, Leah’s maidservant, bears a son to Jacob,
11 Lea akasema, “Hii ni bahati njema!” Hivyo akamwita jina lake Gadi.
and Leah says, “A troop is coming”; and she calls his name Gad.
12 Kisha Zilpa, mjakazi wa Lea, akamzalia Yakobo mwana wa pili.
And Zilpah, Leah’s maidservant, bears a second son to Jacob,
13 Lea akasema, “Nina furaha! Kwa maana mabinti wataniita furaha.” Hivyo akamwita jina lake Asheri.
and Leah says, “Because of my happiness, for daughters have pronounced me blessed”; and she calls his name Asher.
14 Siku za mavuno ya ngano Rubeni akaenda shambani na kuona tunguja. Akazileta kwa mama yake. Kisha Raheli akamwambia Lea, “Nipe baadhi ya tunguja za mwanao.”
And Reuben goes in the days of wheat-harvest, and finds love-apples in the field, and brings them to his mother Leah, and Rachel says to Leah, “Please give to me of the love-apples of your son.”
15 Lea akamwambia, “Je ni jambo dogo kwako, kumchukua mme wangu? Je na sasa unataka kuchukua tunguja za mwanangu pia? Raheli akasema, “Kisha atalala nawe leo usiku, kwa kubadilishana na tunguja za mwanao.
And she says to her, “Is your taking my husband a little thing, that you have also taken the love-apples of my son?” And Rachel says, “He therefore lies with you tonight, for your son’s love-apples.”
16 Jioni Yakobo akaja kutoka uwandani. Lea akaenda kumlaki na kusema, “Leo usiku utalala nami, kwani nimekuajiri kwa tunguja za mwanangu.” Hivyo Yakobo akalala na Lea usiku huo.
And Jacob comes in from the field at evening; and Leah goes to meet him and says, “You come in to me, for [in] hiring I have hired you with my son’s love-apples”; and he lies with her during that night.
17 Mungu akamsikia Lea, na akashika mimba na kumzalia Yakobo mwana wa tano.
And God listens to Leah, and she conceives, and bears a son to Jacob, a fifth,
18 Lea akasema, “Mungu amenipa ujira wangu, kwa sababu nilimpa mme wangu mjakazi wangu.” Akamwita jina lake Isakari.
and Leah says, “God has given my hire, because I have given my maidservant to my husband”; and she calls his name Issachar.
19 Lea akashika mimba tena na kuzaa mwana wa tano kwa Yakobo.
And Leah conceives again, and she bears a sixth son to Jacob,
20 Lea akasema, “Mungu amenipa zawadi njema. Sasa mme wangu ataniheshimu, kwa sababu nimemzalia wana sita.” Akamwita jina lake Zabuloni.
and Leah says, “God has endowed me—a good dowry; this time my husband dwells with me, for I have borne six sons to him”; and she calls his name Zebulun;
21 Baadaye akazaa binti na kumwita jina lake Dina.
and afterward she has borne a daughter, and calls her name Dinah.
22 Mungu akamkumbuka Raheli na kumsikiliza. Akampa kushika mimba.
And God remembers Rachel, and God listens to her, and opens her womb,
23 Akashika mimba na kuzaa mwana. Akasema, “Mungu ameiondoa aibu yangu.”
and she conceives and bears a son, and says, “God has gathered up my reproach”;
24 Akamwita jina lake Yusufu, akisema, Yahwe ameniongeza mwana mwingine.”
and she calls his name Joseph, saying, “YHWH is adding to me another son.”
25 Baada ya Raheli kumzaa Yusufu, Yakobo akamwambia Labani, “Niache niande, ili kwamba niende nyumbani kwetu na katika nchi yangu.
And it comes to pass, when Rachel has borne Joseph, that Jacob says to Laban, “Send me away, and I go to my place, and to my land;
26 Nipe wake zangu na watoto wangu niliokutumikia kwa ajili yao, na uniache niondoke, kwani unafahamu nilivyokutumikia.
give up my wives and my children, for whom I have served you, and I go; for you have known my service which I have served you.”
27 Labani akamwambia, “Ikiwa nimepata kibali machoni pako, subiri, kwa sababu nimejifunza kwa kutumia uaguzi kwamba Yahwe amenibariki kwa ajili yako.”
And Laban says to him, “Now if I have found grace in your eyes—I have observed diligently that YHWH blesses me for your sake.”
28 Kisha akasema, “Taja ujira wako, nami nitalipa.”
He also says, “Define your hire to me, and I give.”
29 Yakobo akamwambia, “Unajua nilivyokutumikia, na jinsi ambavyo mifugo wako wamekuwa nami.
And he says to him, “You have known that which I have served you [in], and that which your substance was with me;
30 Kwani walikuwa wachache kabla sijaja, na wameongezeka kwa wingi. Popote nilipokutumikia Mungu amekubariki. Je ni lini mimi nitaandaa kwa ajili ya nyumba yangu pia?”
for [it is] little which you have had at my appearance, and it breaks forth into a multitude, and YHWH blesses you at my coming; and now, when do I make, I also, for my own house?”
31 Hivyo Labani akasema, “Je nikulipe nini? Yakobo akasema, 'Usinipe chochote. Ikiwa utafanya jambo hili kwa ajili yangu, nitawalisha tena kondoo wako na kuwatunza.
And he says, “What do I give to you?” And Jacob says, “You do not give me anything; if you do this thing for me, I turn back; I have delight; I watch your flock;
32 Niache nipite kati ya kundi lako lote leo, kwa kuondoa kila kondoo mwenye milia na mabaka, na kila kondoo mweusi kati yao, na kati ya wenye mabaka na milia katika mbuzi. Hawa watakuwa ujira wangu.
I pass through all your flock today to turn aside every speckled and spotted sheep from there, and every brown sheep among the lambs, and speckled and spotted among the goats—and it has been my hire;
33 Uadilifu wangu utashuhudia kwa ajili yangu hapo baadaye, utakapokuja kuangalia ujira wangu. Kila ambaye hana milia na hana madoa miongoni mwa mbuzi, na mweusi kati ya kondoo, ikiwa wataonekana kwangu, watahesabiwa kuwa wameibwa.”
and my righteousness has answered for me in the day to come, when it comes in for my hire before your face—everyone which is not speckled and spotted among [my] goats, and brown among [my] lambs—it is stolen with me.”
34 Labani akasema, “Nakubali. Na iwe kama yalivyo maneno yako.”
And Laban says, “Behold, O that it were according to your word”;
35 Siku hiyo Labani akaondoa mabeberu yaliyokuwa na milia na madoa, na majike ya mbuzi yaliyokuwa na milia na madoa, kila aliyekuwa mweupe, na weusi wote katika mbuzi, akawakabidhi katika mikono ya wanaye.
and he turns aside during that day the striped and the spotted male goats, and all the speckled and the spotted female goats, everyone that [has] white in it, and every brown one among the lambs, and he gives into the hand of his sons,
36 Pia Labani akaweka safari ya siku tatu kati yake na Yakobo. Hivyo Yakobo akabaki kuchunga wale kondoo wa Labani waliosalia.
and sets a journey of three days between himself and Jacob; and Jacob is feeding the rest of the flock of Laban.
37 Yakobo akachukua matawi mabichi yaliyokatwa ya mipopla, mlozi na mwaramoni mbichi akatoa maganda ili michilizi myeupe ionekane, na akaifanya sehemu nyeupe ya ndani ya mti iliyokuwa ndani ya fito ionekane.
And Jacob takes to himself a rod of fresh poplar and almond and plane-tree, and peels in them white peelings, making bare the white that [is] on the rods,
38 Kisha akaziweka fito alizokuwa amezibambua mbele ya makundi ya kondoo, mbele ya mabirika yakunyweshea walipokuja kunywa maji. Wakashika mimba walipokuja kunywa maji.
and sets up the rods which he has peeled in the gutters in the watering troughs (where the flock comes to drink), in front of the flock, that they may conceive in their coming to drink;
39 Wanyama wakapandana mbele ya fito; nao wakazaa watoto wenye milia, mabaka na wenye madoa.
and the flocks conceive at the rods, and the flock bears striped, speckled, and spotted ones.
40 Yakobo akawatenga hawa wanakondoo, lakini akawafanya waliosalia kuelekea wanyama wenye milia na kondoo weusi wote katika kundi la Labani. Kisha akayatenga makundi yake mwenyewe pekee na hakuwaweka pamoja na wale wa Labani.
And Jacob has parted the lambs, and he puts the face of the flock toward the striped, also all the brown in the flock of Laban, and he sets his own droves by themselves, and has not set them near Laban’s flock.
41 Pindi kondoo wenye nguvu katika kundi walipopandana, Yakobo alilaza fito katika mabirika ya maji mbele ya macho ya kundi, ili kwamba washike mimba kati ya fito.
And it has come to pass, whenever the strong ones of the flock conceive, that Jacob sets the rods before the eyes of the flock in the gutters, to cause them to conceive by the rods,
42 Lakini wakati waliodhaifu walipokuja, hakuweka fito mbele yao. Hivyo wanyama dhaifu wakawa wa Labani, na wenye nguvu wakawa wa Yakobo.
and when the flock is feeble, he does not set [them]; and the feeble ones have been Laban’s, and the strong ones Jacob’s.
43 Mtu huyo akastawi sana. Akawa na kundi kubwa la kondoo, wajakazi na wajoli, ngamia na punda.
And the man increases very exceedingly, and has many flocks, and maidservants, and menservants, and camels, and donkeys.

< Mwanzo 30 >