< Mwanzo 3 >

1 Sasa nyoka alikuwa mwerevu kuliko myama mwingine yeyote wa kondeni ambaye Yahwe Mungu alikuwa amemuumba. Akamwambia mwanamke, “Je ni kweli Mungu amesema, 'Msile matunda kutoka kwenye mti wowote bustanini'?”
Or, le serpent était le plus rusé de tous les animaux qu'avait créés sur la terre le Seigneur Dieu. Et le serpent dit à la femme: Pourquoi Dieu a-t-il dit: Ne mangez pas de tous les arbres du paradis?
2 Mwanamke akamwambia nyoka, “Twaweza kula tunda kutoka kwenye miti ya bustani,
La femme dit au serpent: Nous pouvons manger des fruits des arbres du paradis.
3 lakini kuhusu tunda la mti ambao uko katikati ya bustani, Mungu alisema, 'msile, wala msiuguse, vinginevyo mtakufa.'”
Quant au fruit de l'arbre qui est au milieu du paradis, Dieu a dit: Vous n'en mangerez pas, vous n'y toucherez pas, afin que vous ne mouriez point.
4 Nyoka akamwambia mwanamke, “hakika hamtakufa.
Le serpent dit à la femme: Vous ne mourrez point de mort.
5 Kwasababu Mungu anajua kwamba siku mkila macho yenu yatafumbuliwa, na mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.”
Car le Seigneur Dieu sait, au contraire, que le jour où vous en mangerez, vos yeux s'ouvriront, et vous serez comme des dieux, connaissant le bien et le mal.
6 Na mwanamke alipoona kuwa mti ni mzuri kwa chakula, na kuwa unapendeza macho, na kwamba mti ulitamanika kwa kumfanya mtu awe mwerevu, alichukua sehemu ya tunda na akala. Na sehemu yake pia akampatia mumewe aliyekuwa naye, naye akala.
La femme vit que l'arbre était bon comme aliment qu'il était gracieux à l'œil, et magnifique à contempler. Et, ayant pris de son fruit, elle en mangea; de plus, elle en donna à son mari, et ils mangèrent.
7 Macho ya wote wawili yalifumbuliwa, na wakajua kuwa wako uchi. Wakashona majani ya miti pamoja na wakatengeneza vya kujifunika wao wenyewe.
Aussitôt leurs yeux à tous les deux s'ouvrirent; ils reconnurent qu'ils étaient nus; ils attachèrent les unes aux autres des feuilles de figuier, et ils s'en firent des ceintures.
8 Wakasikia sauti ya Yahwe Mungu akitembea bustanini majira ya kupoa kwa jua, kwa hiyo mwanaume na mke wake wakajificha wao wenyewe kwenye miti ya bustani kuepuka uwepo wa Yahwe Mungu.
Et ils entendirent la voix du Seigneur Dieu, se promenant l'après-midi dans le paradis, et Adam et sa femme se cachèrent de la face du Seigneur Dieu, dans l'ombrage des arbres du paradis.
9 Yahwe Mungu akamuita mwanaume na kumwambia, “uko wapi?”
Le Seigneur Dieu appela Adam, et il lui dit: Adam, où es-tu?
10 Mwanaume akasema, “nilikusikia bustanini, na nkaogopa, kwa sababu nilikuwa uchi. kwa hiyo nikajificha.”
Celui-ci répondit: J'ai entendu votre voix, comme vous vous promeniez dans le paradis, et j'ai eu peur parce que je suis nu, et je me suis caché.
11 Mungu akasema, “Ni nani alikwambia kuwa ulikuwa uchi? Je umekula kutoka mti ambao nilikuagiza usile matunda yake?”
Dieu lui dit: Qui t'a fait savoir que tu es nu, si tu n'as mangé de l'arbre, de celui-là seul dont je t'avais défendu de manger?
12 Mwanaume akasema, “Mwanamke uliyenipa kuwa na mimi, alinipatia tunda kutoka kwenye mti, na nikala.”
Adam reprit: La femme que vous m'avez donnée pour être avec moi m'a donné elle-même du fruit de l'arbre, et j'en ai mangé.
13 Yahwe Mungu akamwambia mwanamke, “Nini hiki ulichofanya?” mwanamke akasema, “nyoka alinidanganya, na nikala.”
Le Seigneur Dieu dit alors à la femme: Pourquoi as-tu fait cela? Et la femme dit: Le serpent m'a trompée, et j'ai mangé.
14 Yahwe Mungu akamwambia nyoka, “kwa sababu umefanya jambo hili, umelaaniwa wewe mwenyewe miongoni mwa wanyama wote wa kufugwa na wanyama wote wa mwituni. Itakuwa kwa tumbo lako utakwenda, na mavumbi utakula kwa siku zote za maisha yako.
Le Seigneur Dieu dit au serpent: Parce que tu as fait cela, maudit sois- tu parmi tous les bestiaux et les bêtes fauves de la terre; tu marcheras sur la poitrine et le ventre, et tu mangeras de la terre tous les jours de ta vie.
15 Nitaweka uadui kati yako na mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake. Atakujeruhi kichwa chako na utamjeruhi kisigino chake.”
J'établirai une haine entre toi et la femme, et entre ta race et sa race. Il surveillera ta tête, et tu guetteras son talon.
16 Kwa mwanamke akasema, nitaongeza uchungu wakati wa kuzaa watoto; itakuwa katika maumivu utazaa watoto. Tamaa yako itakua kwa mume wako, lakini atakutawala.”
Puis le Seigneur dit à la femme: Je multiplierai et multiplierai tes gémissements et tes douleurs; tu enfanteras dans les douleurs, tu attendras le commandement de ton époux, et il te maîtrisera.
17 Kwa Adam akasema, “kwa sababu umesikiliza sauti ya mke wako, na umekula kutoka katika mti, ambao nilikuagiza, nikisema, “usile matunda yake', ardhi imelaaniwa kwa sababu yako; kupitia kazi yenye maumivu utakula matunda ya ardhi kwa siku zote za maisha yako.
Quant à Adam, Dieu lui dit: Parce que tu as écouté la voix de ta femme, et que tu as mangé de l'arbre, du seul dont je t'avais défendu de manger, maudite sera ta terre en tes travaux. Tu t'en nourriras dans les douleurs tous les jours de ta vie.
18 Ardhi itazaa miiba na mbigili kwa ajili yako, na utakula mimea ya shambani.
Elle produira pour toi des épines et de l'ivraie, et tu mangeras l'herbe des champs.
19 Kwa jasho la uso wako utakula mkate, mpaka utakapo irudia ardhi, ambayo kwayo ulitwaliwa. kwa kuwa wewe ni mavumbi na kwenye mavumbi utarudi.”
C'est à la sueur de ton front que tu mangeras ton pain: jusqu'à ce que tu retournes dans la terre d'où tu as été tiré, parce que: Tu es terre, et tu t'en iras dans la terre.
20 Mwanaume akaita mke wake jina Hawa kwa sababu alikuwa mama wa wote wenye uhai.
Adam donna à la femme le nom d'Éve (vie), parce qu'elle-même est mère de tous les vivants.
21 Yahwe Mungu akatengeneza mavazi ya ngozi kwa ajili ya Adam na mke wake na akawavalisha.
Le Seigneur Dieu fit ensuite à Adam et à sa femme des tuniques de peau dont il les revêtit.
22 Yahwe Mungu akasema, “sasa mtu huyu amekuwa kama mmoja wetu, ajuaye mema na mabaya. Kwa hiyo sasa hataruhusiwa kugusa kwa mkono wake, na kuchukua tunda la mti wa uzima, na kula akaishi tena milele.”
Et Dieu dit: Voilà donc Adam devenu comme l'un de nous, pour connaître le bien et le mal; mais maintenant qu'il n'aille pas étendre la main et prendre encore de l'arbre de vie, et en manger, car il vivrait toujours.
23 Kwa hiyo Yahwe Mungu akamuondoa kutoka kwenye bustani ya Edeni, kwenda kulima ardhi ambayo kwahiyo alikuwa ametwaliwa.
Et le Seigneur Dieu le chassa du paradis de délices, pour qu'il travaillât à la terre de laquelle il avait été tiré.
24 Kwa hiyo Mungu akamfukuza mtu huyu nje ya bustani, na akaweka kerubi mashariki mwa bustani ya Edeni, na upanga wa moto ulio geuka geuka kila upande, ili kulinda njia ya kwenda kwenye mti wa uzima.
Il bannit Adam; il l'établit à l'opposé du paradis de délices, et il plaça des chérubins, armés d'épées flamboyantes qu'ils faisaient tournoyer, pour garder le chemin de l'arbre de vie.

< Mwanzo 3 >