< Mwanzo 29 >
1 Kisha Yakobo akaendelea na safari yake na akafika katika nchi ya watu wa mashariki.
Tada se podiže Jakov i otide u zemlju istoènu.
2 Hata alipotazama, akaona kisima kondeni, na, tazama, makundi matatu ya kondoo yalikuwa yamelala kando yake. Kwani kutoka katika hicho wangeyanywesha makundi, na jiwe juu ya mdomo wa kisima lilikuwa kubwa.
I obziruæi se ugleda studenac u polju; i gle, tri stada ovaca ležahu kod njega, jer se na onom studencu pojahu stada, a veliki kamen bijaše studencu na vratima.
3 Wakati makundi yote yangekusanyika pale, wachungaji wangevingirisha jiwe kutoka katika mdomo wa kisima na kuwanywesha kondoo, na kisha kurudisha jiwe juu ya mdomo wa kisima, mahali pake.
Ondje se skupljahu sva stada, te pastiri odvaljivahu kamen s vrata studencu i pojahu stada, i poslije opet privaljivahu kamen na vrata studencu na njegovo mjesto.
4 Yakobo akawambia, “Ndugu zangu, ninyi mnatokea wapi?” nao wakasema, “Tunatoka Harani.”
I Jakov im reèe: braæo, odakle ste? Rekoše: iz Harana smo.
5 Akawambia, “Mnamfahamu Labani mwana wa Nahori?” Wakasema, “Tunamfahamu.”
A on im reèe: poznajete li Lavana sina Nahorova? Oni rekoše: poznajemo.
6 Akawambia, “Je hajambo?” Wakasema, “Hajambo, na, tazama pale, Raheli binti yake anakuja na kondoo.”
On im reèe: je li zdrav? Rekoše: jest, i evo Rahilje kæeri njegove, gdje ide sa stadom.
7 Yakobo akasema, “Tazama, ni mchana. Siyo wakati wa kukusanya kondoo pamoja. Mnapaswa kuwanywesha kondoo na kisha mkaenda na kuwaacha wachunge.”
I on reèe: eto još je rano, niti je vrijeme vraæati stoku; napojte stoku pa idite i pasite je.
8 Wakamwambia, “Hatuwezi kuwanywesha mpaka makundi yote yakusanyike pamoja. Ndipo wanaume watakapovingirisha jiwe kutoka mlangoni mwa kisima, na ndipo tutakapowanywesha kondoo.”
A oni rekoše: ne možemo, dokle se ne skupe sva stada, da odvalimo kamen s vrata studencu, onda æemo napojiti stoku.
9 Wakati bado Yakobo anaongea nao, Raheli akaja pamoja na kondoo wa babaye, kwani alikuwa akiwachunga.
Dok on još govoraše s njima, doðe Rahilja sa stadom oca svojega, jer ona pasijaše ovce.
10 Yakobo alipomwona Raheli, binti wa Labani, kaka wa mamaye, na kondoo wa Labani, kaka wa mama yake, Yakobo akaja juu, akalivingirisha jiwe kutoka mlangoni mwa kisima, na akawanywesha kondoo wa Labani, kaka wa mama yake.
A kad Jakov vidje Rahilju kæer Lavana ujaka svojega, i stado Lavana ujaka svojega, pristupi Jakov i odvali kamen studencu s vrata, i napoji stado Lavana ujaka svojega.
11 Yakobo akambusu Raheli na akalia kwa sauti.
I poljubi Jakov Rahilju, i povikavši zaplaka se.
12 Yakobo akamwambia Raheli kwamba alikuwa ni ndugu wa baba yake, na kwamba alikuwa mwana wa Rebeka. Kisha yeye akakimbia kumwambia baba yake.
I kaza se Jakov Rahilji da je rod ocu njezinu i da je sin Reveèin; a ona otrèa te javi ocu svojemu.
13 Labani aliposikia habari kuhusu Yakobo mwana wa dada yake, akaenda kukutana naye, akamkumbatia, akambusu, na kumleta nyumbani kwake. Yakobo akamwambia Labani mambo haya yote.
A kad Lavan èu za Jakova sina sestre svoje, istrèa mu na susret, i zagrli ga i poljubi, i uvede u svoju kuæu. I on pripovjedi Lavanu sve ovo.
14 Labani akamwambia, “Kwa hakika wewe ni mfupa wangu na nyama yangu.” Kisha Yakobo akakaa naye kama mwezi mmoja.
A Lavan mu reèe: ta ti si kost moja i tijelo moje. I osta kod njega cio mjesec dana.
15 Kisha Labani akamwambia Yakobo, “Je unitumikie bure kwa kuwa wewe ni ndugu yangu? Niambie, ujira wako utakuwaje?
Tada reèe Lavan Jakovu: zar badava da mi služiš, što si mi rod? Kaži mi šta æe ti biti plata?
16 Basi Labani alikuwa na binti wawili. Jina la mkubwa lilikuwa ni Lea, na jina la mdogo lilikuwa Raheli.
A Lavan imaše dvije kæeri: starijoj bješe ime Lija, a mlaðoj Rahilja.
17 Macho ya Lea yalikuwa dhaifu, lakini Raheli alikuwa mzuri wa umbo na mwonekano.
I u Lije bjehu kvarne oèi, a Rahilja bješe lijepa stasa i lijepa lica.
18 Yakobo alimpenda Raheli, hivyo akasema, “Nitakutumikia miaka saba kwa ajili ya Raheli, binti yako mdogo.”
I Jakovu omilje Rahilja, te reèe: služiæu ti sedam godina za Rahilju, mlaðu kæer tvoju.
19 Labani akasema, Itakuwa vema kukupa wewe, kuliko kumpa mtu mwingine. Kaa nami.”
A Lavan mu reèe: bolje tebi da je dam nego drugom; ostani kod mene.
20 Hivyo Yakobo akamtumikia kwa miaka saba kwa ajili ya Raheli; nayo ilionekana kwake kama siku chache tu, kwa ajili ya upendo aliokuwa nao kwake.
I otsluži Jakov za Rahilju sedam godina, i uèiniše mu se kao nekoliko dana, jer je ljubljaše.
21 Kisha Yakobo akamwambia Labani, “Nipe mke wangu, kwani siku zangu zimetimia - ili kwamba nimwoe!
I reèe Jakov Lavanu: daj mi ženu, jer mi se navrši vrijeme, da legnem s njom.
22 Hivyo Labani akawaalika watu wa mahali hapo na kuandaa sherehe.
I sazva Lavan sve ljude iz onoga mjesta i uèini gozbu.
23 Wakati wa jioni, Labani akamchukua Lea binti yake mkubwa na kumleta kwa Yakobo, aliyelala naye.
A uveèe uze Liju kæer svoju i uvede je k Jakovu, i on leže s njom.
24 Labani akampa mtumishi wake wakike Zilpa kuwa mjakazi wa Lea.
I Lavan dade Zelfu robinju svoju Liji kæeri svojoj da joj bude robinja.
25 Ilipofika asubuhi, tazama, kumbe ni Lea! Yakobo akamwambia Labani, “Ni nini hiki ulichonifanyia? Je sikukutumikia kwa ajili ya Raheli? Kwa nini basi umenihadaa?
A kad bi ujutru, gle, ono bješe Lija; te reèe Jakov Lavanu: šta si mi to uèinio? ne služim li za Rahilju kod tebe? zašto si me prevario?
26 Labani akamwambia, “Siyo utamaduni wetu kumtoa bindi mdogo kabla ya mzaliwa wa kwanza.
A Lavan mu reèe: ne biva u našem mjestu da se uda mlaða prije starije.
27 Timiza juma la bibi arusi, na tutakupa yule mwingine pia kwa mbadala wa kunitumikia miaka mingine saba.”
Navrši nedjelju dana s tom, pa æemo ti dati i drugu za službu što æeš služiti kod mene još sedam godina drugih.
28 Yakobo akafanya hivyo, na akatimiza juma la Lea. Kisha Labani akampa Raheli binti yake kuwa mke wake.
Jakov uèini tako, i navrši s njom nedjelju dana, pa mu dade Lavan Rahilju kæer svoju za ženu.
29 Lakini pia Labani akampa Raheli binti yake Bilha, kuwa mjakazi wake.
I dade Lavan Rahilji kæeri svojoj robinju svoju Valu da joj bude robinja.
30 Hivyo Yakobo akalala na Raheli, pia, lakini akampenda Raheli zaidi ya Lea. Hivyo Yakobo akamtumikia Labani kwa miaka saba mingine.
I tako leže Jakov s Rahiljom; i voljaše Rahilju nego Liju, i stade služiti kod Lavana još sedam drugih godina.
31 Yahwe akaona kwamba Lea hakupendwa, hivyo akalifungua tumbo lake, lakini Raheli hakuwa na mtoto.
A Gospod videæi da Jakov ne mari za Liju, otvori njojzi matericu, a Rahilja osta nerotkinja.
32 Lea akashika mimba na kuzaa mwana, naye akamwita Rubeni. Kwani alisema, “Kwa sababu Yahwe ameliangalia teso langu; bila shaka mme wangu sasa atanipenda.”
I Lija zatrudnje, i rodi sina, i nadjede mu ime Ruvim, govoreæi: Gospod pogleda na jade moje, sada æe me ljubiti muž moj.
33 Kisha akashika mimba tena na kuzaa mwana. Akasema, “Kwa sababu Yahwe amesikia kwamba sipendwi, kwa hiyo amenipa mwana mwingine,” na akamwita Simoni.
I opet zatrudnje, i rodi sina, i reèe: Gospod èu da sam prezrena, pa mi dade i ovoga. I nadjede mu ime Simeun.
34 Kisha akashika mimba tena na kuzaa mwana. Akasema, “Wakati huu mme wangu ataungana nami, kwa kuwa nimemzalia wana watatu.” Kwa hiyo akaitwa Lawi.
I opet zatrudnje, i rodi sina, i reèe: da ako se sada veæ priljubi k meni muž moj, kad mu rodih tri sina. Zato mu nadješe ime Levije.
35 Akashika mimba tena na kuzaa mwana. Akasema, “Wakati huu nitamsifu Yahwe.” Kwa hiyo akamwita jina lake Yuda; kisha akaacha kuzaa watoto.
I zatrudnje opet, i rodi sina, i reèe: sada æu hvaliti Gospoda. Zato mu nadjede ime Juda; i presta raðati.