< Mwanzo 29 >
1 Kisha Yakobo akaendelea na safari yake na akafika katika nchi ya watu wa mashariki.
Wtedy Jakub wyruszył w drogę i poszedł do ziemi ludów Wschodu.
2 Hata alipotazama, akaona kisima kondeni, na, tazama, makundi matatu ya kondoo yalikuwa yamelala kando yake. Kwani kutoka katika hicho wangeyanywesha makundi, na jiwe juu ya mdomo wa kisima lilikuwa kubwa.
I spojrzał, a oto w polu studnia i trzy stada owiec leżących przy niej. Z tej studni pojono bowiem stada, a wielki kamień [przykrywał] wierzch tej studni.
3 Wakati makundi yote yangekusanyika pale, wachungaji wangevingirisha jiwe kutoka katika mdomo wa kisima na kuwanywesha kondoo, na kisha kurudisha jiwe juu ya mdomo wa kisima, mahali pake.
A gdy schodziły się wszystkie stada, odsuwano kamień z wierzchu studni i pojono owce. Potem znów zasuwano kamień na wierzch studni na jego miejsce.
4 Yakobo akawambia, “Ndugu zangu, ninyi mnatokea wapi?” nao wakasema, “Tunatoka Harani.”
Jakub zapytał ich: Moi bracia, skąd jesteście? I odpowiedzieli: Jesteśmy z Charanu.
5 Akawambia, “Mnamfahamu Labani mwana wa Nahori?” Wakasema, “Tunamfahamu.”
Zapytał ich: Czy znacie Labana, syna Nachora? Odpowiedzieli: Znamy.
6 Akawambia, “Je hajambo?” Wakasema, “Hajambo, na, tazama pale, Raheli binti yake anakuja na kondoo.”
Potem zapytał: Czy dobrze się miewa? A oni odpowiedzieli: Dobrze. Oto właśnie jego córka Rachela nadchodzi ze stadem.
7 Yakobo akasema, “Tazama, ni mchana. Siyo wakati wa kukusanya kondoo pamoja. Mnapaswa kuwanywesha kondoo na kisha mkaenda na kuwaacha wachunge.”
Wtedy powiedział: Oto jeszcze jest jasny dzień i nie czas zganiać stada. Napójcie owce i idźcie, popaście je.
8 Wakamwambia, “Hatuwezi kuwanywesha mpaka makundi yote yakusanyike pamoja. Ndipo wanaume watakapovingirisha jiwe kutoka mlangoni mwa kisima, na ndipo tutakapowanywesha kondoo.”
Oni odpowiedzieli: Nie możemy, dopóki nie zbiorą się wszystkie stada i nie odsuną kamienia z wierzchu studni. Wtedy napoimy stada.
9 Wakati bado Yakobo anaongea nao, Raheli akaja pamoja na kondoo wa babaye, kwani alikuwa akiwachunga.
A gdy jeszcze tak z nimi rozmawiał, nadeszła Rachela z owcami swego ojca, bo [je] pasła.
10 Yakobo alipomwona Raheli, binti wa Labani, kaka wa mamaye, na kondoo wa Labani, kaka wa mama yake, Yakobo akaja juu, akalivingirisha jiwe kutoka mlangoni mwa kisima, na akawanywesha kondoo wa Labani, kaka wa mama yake.
I gdy Jakub ujrzał Rachelę, córkę Labana, brata swej matki, z owcami Labana, brata swej matki, podszedł, odsunął kamień z wierzchu studni i napoił owce Labana, brata swojej matki.
11 Yakobo akambusu Raheli na akalia kwa sauti.
Potem Jakub pocałował Rachelę i głośno zapłakał.
12 Yakobo akamwambia Raheli kwamba alikuwa ni ndugu wa baba yake, na kwamba alikuwa mwana wa Rebeka. Kisha yeye akakimbia kumwambia baba yake.
I Jakub powiedział Racheli, że jest bratem jej ojca i że jest synem Rebeki. Ona pobiegła więc i oznajmiła to swemu ojcu.
13 Labani aliposikia habari kuhusu Yakobo mwana wa dada yake, akaenda kukutana naye, akamkumbatia, akambusu, na kumleta nyumbani kwake. Yakobo akamwambia Labani mambo haya yote.
A gdy Laban usłyszał wieść o Jakubie, synu swojej siostry, wybiegł mu naprzeciw, objął go, ucałował i zaprowadził do swego domu. A [on] opowiedział Labanowi o wszystkim.
14 Labani akamwambia, “Kwa hakika wewe ni mfupa wangu na nyama yangu.” Kisha Yakobo akakaa naye kama mwezi mmoja.
Wtedy Laban powiedział mu: Ty naprawdę [jesteś] z moich kości i z mojego ciała. I [Jakub] mieszkał u niego przez cały miesiąc.
15 Kisha Labani akamwambia Yakobo, “Je unitumikie bure kwa kuwa wewe ni ndugu yangu? Niambie, ujira wako utakuwaje?
Potem Laban powiedział do Jakuba: Czyż dlatego, że jesteś moim bratem, będziesz mi służyć za darmo? Powiedz mi, jaka [ma być] twoja zapłata.
16 Basi Labani alikuwa na binti wawili. Jina la mkubwa lilikuwa ni Lea, na jina la mdogo lilikuwa Raheli.
A Laban miał dwie córki: starsza miała na imię Lea, młodsza zaś Rachela.
17 Macho ya Lea yalikuwa dhaifu, lakini Raheli alikuwa mzuri wa umbo na mwonekano.
Lea miała czułe oczy, Rachela zaś była piękna i miła dla oka.
18 Yakobo alimpenda Raheli, hivyo akasema, “Nitakutumikia miaka saba kwa ajili ya Raheli, binti yako mdogo.”
Jakub kochał Rachelę i powiedział: Będę ci służył siedem lat za twoją młodszą córkę Rachelę.
19 Labani akasema, Itakuwa vema kukupa wewe, kuliko kumpa mtu mwingine. Kaa nami.”
Laban odpowiedział: Lepiej mi ją dać tobie niż innemu mężczyźnie. Zamieszkaj ze mną.
20 Hivyo Yakobo akamtumikia kwa miaka saba kwa ajili ya Raheli; nayo ilionekana kwake kama siku chache tu, kwa ajili ya upendo aliokuwa nao kwake.
I Jakub służył za Rachelę siedem lat, które wydawały mu się jak kilka dni, bo ją kochał.
21 Kisha Yakobo akamwambia Labani, “Nipe mke wangu, kwani siku zangu zimetimia - ili kwamba nimwoe!
Potem Jakub powiedział do Labana: Daj mi moją żonę, bo wypełniły się moje dni, abym z nią obcował.
22 Hivyo Labani akawaalika watu wa mahali hapo na kuandaa sherehe.
Wtedy Laban zebrał wszystkich mężczyzn tego miejsca i wyprawił ucztę.
23 Wakati wa jioni, Labani akamchukua Lea binti yake mkubwa na kumleta kwa Yakobo, aliyelala naye.
A gdy nastał wieczór, wziął swoją córkę Leę i wprowadził ją do [Jakuba], a on obcował z nią.
24 Labani akampa mtumishi wake wakike Zilpa kuwa mjakazi wa Lea.
Laban dał też swoją służącą Zilpę swej córce Lei za służącą.
25 Ilipofika asubuhi, tazama, kumbe ni Lea! Yakobo akamwambia Labani, “Ni nini hiki ulichonifanyia? Je sikukutumikia kwa ajili ya Raheli? Kwa nini basi umenihadaa?
Rano okazało się, że to była Lea. Powiedział więc do Labana: Cóż mi zrobiłeś? Czy nie za Rachelę ci służyłem? Dlaczego mnie oszukałeś?
26 Labani akamwambia, “Siyo utamaduni wetu kumtoa bindi mdogo kabla ya mzaliwa wa kwanza.
Laban odpowiedział: Nie ma u nas zwyczaju, aby młodszą wydawać za mąż przed starszą.
27 Timiza juma la bibi arusi, na tutakupa yule mwingine pia kwa mbadala wa kunitumikia miaka mingine saba.”
Dopełnij jej tydzień, a dam ci i tę za służbę, którą mi odsłużysz drugie siedem lat.
28 Yakobo akafanya hivyo, na akatimiza juma la Lea. Kisha Labani akampa Raheli binti yake kuwa mke wake.
I Jakub tak zrobił, i dopełnił jej tydzień. Potem [Laban] dał mu swoją córkę Rachelę za żonę.
29 Lakini pia Labani akampa Raheli binti yake Bilha, kuwa mjakazi wake.
Laban dał też swoją służącą Bilhę swej córce Racheli za służącą.
30 Hivyo Yakobo akalala na Raheli, pia, lakini akampenda Raheli zaidi ya Lea. Hivyo Yakobo akamtumikia Labani kwa miaka saba mingine.
Wtedy [Jakub] obcował też z Rachelą i kochał Rachelę bardziej niż Leę, [i] służył mu jeszcze drugie siedem lat.
31 Yahwe akaona kwamba Lea hakupendwa, hivyo akalifungua tumbo lake, lakini Raheli hakuwa na mtoto.
A gdy PAN widział, że Lea była znienawidzona, otworzył jej łono. Rachela zaś [była] bezpłodna.
32 Lea akashika mimba na kuzaa mwana, naye akamwita Rubeni. Kwani alisema, “Kwa sababu Yahwe ameliangalia teso langu; bila shaka mme wangu sasa atanipenda.”
Lea poczęła więc i urodziła syna, i nadała mu imię Ruben. Powiedziała bowiem: PAN naprawdę wejrzał na moje utrapienie. Dlatego teraz mój mąż będzie mnie kochać.
33 Kisha akashika mimba tena na kuzaa mwana. Akasema, “Kwa sababu Yahwe amesikia kwamba sipendwi, kwa hiyo amenipa mwana mwingine,” na akamwita Simoni.
Gdy znów poczęła i urodziła syna, powiedziała: PAN usłyszał, że byłam znienawidzona. Dlatego dał mi także tego [syna]. I nadała mu imię Symeon.
34 Kisha akashika mimba tena na kuzaa mwana. Akasema, “Wakati huu mme wangu ataungana nami, kwa kuwa nimemzalia wana watatu.” Kwa hiyo akaitwa Lawi.
Potem znów poczęła i urodziła syna, i powiedziała: Tym razem mój mąż przywiąże się do mnie, bo urodziłam mu trzech synów. Dlatego nadała mu imię Lewi.
35 Akashika mimba tena na kuzaa mwana. Akasema, “Wakati huu nitamsifu Yahwe.” Kwa hiyo akamwita jina lake Yuda; kisha akaacha kuzaa watoto.
Gdy jeszcze raz poczęła i urodziła syna, powiedziała: Teraz już będę chwalić PANA. Dlatego nadała mu imię Juda. I przestała rodzić.