< Mwanzo 29 >

1 Kisha Yakobo akaendelea na safari yake na akafika katika nchi ya watu wa mashariki.
雅各起行,到了东方人之地,
2 Hata alipotazama, akaona kisima kondeni, na, tazama, makundi matatu ya kondoo yalikuwa yamelala kando yake. Kwani kutoka katika hicho wangeyanywesha makundi, na jiwe juu ya mdomo wa kisima lilikuwa kubwa.
看见田间有一口井,有三群羊卧在井旁;因为人饮羊群都是用那井里的水。井口上的石头是大的。
3 Wakati makundi yote yangekusanyika pale, wachungaji wangevingirisha jiwe kutoka katika mdomo wa kisima na kuwanywesha kondoo, na kisha kurudisha jiwe juu ya mdomo wa kisima, mahali pake.
常有羊群在那里聚集,牧人把石头转离井口饮羊,随后又把石头放在井口的原处。
4 Yakobo akawambia, “Ndugu zangu, ninyi mnatokea wapi?” nao wakasema, “Tunatoka Harani.”
雅各对牧人说:“弟兄们,你们是哪里来的?”他们说:“我们是哈兰来的。”
5 Akawambia, “Mnamfahamu Labani mwana wa Nahori?” Wakasema, “Tunamfahamu.”
他问他们说:“拿鹤的孙子拉班,你们认识吗?”他们说:“我们认识。”
6 Akawambia, “Je hajambo?” Wakasema, “Hajambo, na, tazama pale, Raheli binti yake anakuja na kondoo.”
雅各说:“他平安吗?”他们说:“平安。看哪,他女儿拉结领着羊来了。”
7 Yakobo akasema, “Tazama, ni mchana. Siyo wakati wa kukusanya kondoo pamoja. Mnapaswa kuwanywesha kondoo na kisha mkaenda na kuwaacha wachunge.”
雅各说:“日头还高,不是羊群聚集的时候,你们不如饮羊,再去放一放。”
8 Wakamwambia, “Hatuwezi kuwanywesha mpaka makundi yote yakusanyike pamoja. Ndipo wanaume watakapovingirisha jiwe kutoka mlangoni mwa kisima, na ndipo tutakapowanywesha kondoo.”
他们说:“我们不能,必等羊群聚齐,人把石头转离井口才可饮羊。”
9 Wakati bado Yakobo anaongea nao, Raheli akaja pamoja na kondoo wa babaye, kwani alikuwa akiwachunga.
雅各正和他们说话的时候,拉结领着她父亲的羊来了,因为那些羊是她牧放的。
10 Yakobo alipomwona Raheli, binti wa Labani, kaka wa mamaye, na kondoo wa Labani, kaka wa mama yake, Yakobo akaja juu, akalivingirisha jiwe kutoka mlangoni mwa kisima, na akawanywesha kondoo wa Labani, kaka wa mama yake.
雅各看见母舅拉班的女儿拉结和母舅拉班的羊群,就上前把石头转离井口,饮他母舅拉班的羊群。
11 Yakobo akambusu Raheli na akalia kwa sauti.
雅各与拉结亲嘴,就放声而哭。
12 Yakobo akamwambia Raheli kwamba alikuwa ni ndugu wa baba yake, na kwamba alikuwa mwana wa Rebeka. Kisha yeye akakimbia kumwambia baba yake.
雅各告诉拉结,自己是她父亲的外甥,是利百加的儿子,拉结就跑去告诉她父亲。
13 Labani aliposikia habari kuhusu Yakobo mwana wa dada yake, akaenda kukutana naye, akamkumbatia, akambusu, na kumleta nyumbani kwake. Yakobo akamwambia Labani mambo haya yote.
拉班听见外甥雅各的信息,就跑去迎接,抱着他,与他亲嘴,领他到自己的家。雅各将一切的情由告诉拉班。
14 Labani akamwambia, “Kwa hakika wewe ni mfupa wangu na nyama yangu.” Kisha Yakobo akakaa naye kama mwezi mmoja.
拉班对他说:“你实在是我的骨肉。”雅各就和他同住了一个月。
15 Kisha Labani akamwambia Yakobo, “Je unitumikie bure kwa kuwa wewe ni ndugu yangu? Niambie, ujira wako utakuwaje?
拉班对雅各说:“你虽是我的骨肉,岂可白白地服事我?请告诉我,你要什么为工价?”
16 Basi Labani alikuwa na binti wawili. Jina la mkubwa lilikuwa ni Lea, na jina la mdogo lilikuwa Raheli.
拉班有两个女儿,大的名叫利亚,小的名叫拉结。
17 Macho ya Lea yalikuwa dhaifu, lakini Raheli alikuwa mzuri wa umbo na mwonekano.
利亚的眼睛没有神气,拉结却生得美貌俊秀。
18 Yakobo alimpenda Raheli, hivyo akasema, “Nitakutumikia miaka saba kwa ajili ya Raheli, binti yako mdogo.”
雅各爱拉结,就说:“我愿为你小女儿拉结服事你七年。”
19 Labani akasema, Itakuwa vema kukupa wewe, kuliko kumpa mtu mwingine. Kaa nami.”
拉班说:“我把她给你,胜似给别人,你与我同住吧!”
20 Hivyo Yakobo akamtumikia kwa miaka saba kwa ajili ya Raheli; nayo ilionekana kwake kama siku chache tu, kwa ajili ya upendo aliokuwa nao kwake.
雅各就为拉结服事了七年;他因为深爱拉结,就看这七年如同几天。
21 Kisha Yakobo akamwambia Labani, “Nipe mke wangu, kwani siku zangu zimetimia - ili kwamba nimwoe!
雅各对拉班说:“日期已经满了,求你把我的妻子给我,我好与她同房。”
22 Hivyo Labani akawaalika watu wa mahali hapo na kuandaa sherehe.
拉班就摆设筵席,请齐了那地方的众人。
23 Wakati wa jioni, Labani akamchukua Lea binti yake mkubwa na kumleta kwa Yakobo, aliyelala naye.
到晚上,拉班将女儿利亚送来给雅各,雅各就与她同房。
24 Labani akampa mtumishi wake wakike Zilpa kuwa mjakazi wa Lea.
拉班又将婢女悉帕给女儿利亚作使女。
25 Ilipofika asubuhi, tazama, kumbe ni Lea! Yakobo akamwambia Labani, “Ni nini hiki ulichonifanyia? Je sikukutumikia kwa ajili ya Raheli? Kwa nini basi umenihadaa?
到了早晨,雅各一看是利亚,就对拉班说:“你向我做的是什么事呢?我服事你,不是为拉结吗?你为什么欺哄我呢?”
26 Labani akamwambia, “Siyo utamaduni wetu kumtoa bindi mdogo kabla ya mzaliwa wa kwanza.
拉班说:“大女儿还没有给人,先把小女儿给人,在我们这地方没有这规矩。
27 Timiza juma la bibi arusi, na tutakupa yule mwingine pia kwa mbadala wa kunitumikia miaka mingine saba.”
你为这个满了七日,我就把那个也给你,你再为她服事我七年。”
28 Yakobo akafanya hivyo, na akatimiza juma la Lea. Kisha Labani akampa Raheli binti yake kuwa mke wake.
雅各就如此行。满了利亚的七日,拉班便将女儿拉结给雅各为妻。
29 Lakini pia Labani akampa Raheli binti yake Bilha, kuwa mjakazi wake.
拉班又将婢女辟拉给女儿拉结作使女。
30 Hivyo Yakobo akalala na Raheli, pia, lakini akampenda Raheli zaidi ya Lea. Hivyo Yakobo akamtumikia Labani kwa miaka saba mingine.
雅各也与拉结同房,并且爱拉结胜似爱利亚,于是又服事了拉班七年。
31 Yahwe akaona kwamba Lea hakupendwa, hivyo akalifungua tumbo lake, lakini Raheli hakuwa na mtoto.
耶和华见利亚失宠,就使她生育,拉结却不生育。
32 Lea akashika mimba na kuzaa mwana, naye akamwita Rubeni. Kwani alisema, “Kwa sababu Yahwe ameliangalia teso langu; bila shaka mme wangu sasa atanipenda.”
利亚怀孕生子,就给他起名叫吕便,因而说:“耶和华看见我的苦情,如今我的丈夫必爱我。”
33 Kisha akashika mimba tena na kuzaa mwana. Akasema, “Kwa sababu Yahwe amesikia kwamba sipendwi, kwa hiyo amenipa mwana mwingine,” na akamwita Simoni.
她又怀孕生子,就说:“耶和华因为听见我失宠,所以又赐给我这个儿子”,于是给他起名叫西缅。
34 Kisha akashika mimba tena na kuzaa mwana. Akasema, “Wakati huu mme wangu ataungana nami, kwa kuwa nimemzalia wana watatu.” Kwa hiyo akaitwa Lawi.
她又怀孕生子,起名叫利未,说:“我给丈夫生了三个儿子,他必与我联合。”
35 Akashika mimba tena na kuzaa mwana. Akasema, “Wakati huu nitamsifu Yahwe.” Kwa hiyo akamwita jina lake Yuda; kisha akaacha kuzaa watoto.
她又怀孕生子,说:“这回我要赞美耶和华”,因此给他起名叫犹大。这才停了生育。

< Mwanzo 29 >