< Mwanzo 28 >

1 Isaka akamwita Yakobo, akambariki, na kumwagiza, “Usichukuwe mwanamke katika wanawake wa Kikanaani.
Izak je poklical Jakoba, ga blagoslovil, mu naročil ter mu rekel: »Ne boš si vzel žene izmed Kánaanovih hčera.
2 Inuka, nenda Padani Aramu, katika nyumba ya Bethueli baba wa mama yako, na uchukue mwanamke pale, mmojawapo wa binti za Labani, kaka wa mama yako.
Vstani, pojdi v Padan–aram, k hiši Betuéla, očeta tvoje matere in od tam si vzemi ženo izmed hčera Labána, brata tvoje matere.
3 Mungu Mwenyezi na akubariki, akupe uzao na akuzidishe, hata uwe wingi wa watu.
Bog Vsemogočni naj te blagoslovi in te naredi rodovitnega in te namnoži, da boš lahko postal množica ljudstva
4 Na akupe baraka ya Ibrahimu, wewe, na uzao wako baada yako, kwamba uweze kumilki nchi ambapo umekuwa ukiishi, ambayo Mungu alimpa Ibrahimu.”
in ti da Abrahamov blagoslov, tebi in tvojemu semenu s teboj, da boš lahko podedoval deželo, v kateri si tujec, ki jo je Bog dal Abrahamu.«
5 Hivyo Isaka akamwondoa Yakobo. Yakobo akaenda Padani Aramu, kwa Labani mwana wa Bethueli Mwaramu, kaka wa Rebeka, mama yao Yakobo na Esau.
Izak je odposlal Jakoba in ta je odšel v Padan–aram, k Labánu, sinu Sirca Betuéla, brata Jakobove in Ezavove matere Rebeke.
6 Basi Esau alipoona kwamba Isaka amembariki Yakobo na kumpeleka Padani Aramu, kuchukua mke kutoka pale. Lakini pia akaona kwamba Isaka alikuwa amembariki na kumwagiza, akisema, “Usichukue mke katika wanawake wa Kanaani.”
Ko je Ezav videl, da je Izak blagoslovil Jakoba in ga odposlal v Padan–aram, da si od tam vzame ženo in da mu je med blagoslovom dal naročilo, rekoč: »Ne boš si vzel žene izmed Kánaanovih hčera, «
7 Esau pia akaona kwamba Yakobo alikuwa amemtii baba yake na mama yake, na alikuwa amekwenda Padani Aramu.
in da je Jakob ubogal svojega očeta in svojo mater ter odšel v Padan–aram,
8 Esau akaona kwamba wanawake wa Kanaani hawakumpendeza Isaka baba yake.
je Ezav videl, da Kánaanove hčere njegovemu očetu Izaku niso ugajale
9 Hivyo akaenda kwa Ishmaeli, na kuchukua, mbali na wake aliokuwa nao, Mahalathi binti Ishmaeli, mwana wa Ibrahimu, dada wa Nebayothi, kuwa mke wake.
in je Ezav potem odšel k Izmaelu in si k ženama, ki ju je imel, vzel Mahaláto, hčer Abrahamovega sina Izmaela, Nebajótovo sestro, da postane njegova žena.
10 Yakobo akatoka Beersheba na akaelekea Harani.
Jakob pa je odšel iz Beeršébe in odšel proti Haránu.
11 Akaja mahali fulani na akakaa pale usiku kucha, kwa kuwa jua lilikuwa limekuchwa. Akachukua mojawapo ya mawe katika eneo hilo, akaliweka chini ya kichwa chake, na akalala usingizi katika eneo hilo.
Ker pa je sonce zašlo, se je spustil na nek kraj in se tam vso noč zadrževal in vzel je kamne tega kraja in jih položil za svoje blazine in se ulegel na ta kraj, da zaspi.
12 Akaota na kuona ngazi imewekwa juu ya nchi. Ncha yake ilifika hata mbinguni na malaika wa Mungu walikuwa wakishuka na kupanda juu yake.
Sanjal je in glej lestev, postavljeno na zemljo in njen vrh je segal do nebes. In glej, Božji angeli so se vzpenjali in spuščali po njej.
13 Tazama, Yahwe amesimama juu yake na kusema, “Mimi ni Yahwe, Mungu wa Ibrahimu baba yako, na Mungu wa Isaka. Nchi uliyolala juu yake, nitakupa wewe na uzao wako.
In glej, Gospod je stal nad njo ter rekel: »Jaz sem Gospod, Bog tvojega očeta Abrahama in Izakov Bog. Deželo, na kateri ležiš, bom dal tebi in tvojemu semenu.
14 Uzao wako utakuwa kama mavumbi ya ardhi, na utaenea mbali kuelekea magharibi, mashariki, kaskazini, na kusini. Kupitia kwako na kupitia uzao wako familia zote za dunia zitabarikiwa.
Tvojega semena bo kakor zemeljskega prahu in razširjen boš na zahod, na vzhod, na sever in na jug. In v tebi in v tvojem semenu bodo blagoslovljene vse družine zemlje.
15 Tazama, mimi nipo nawe, na nitakulinda kila uendako, Nitakurudisha katika nchi hii tena; kwani sitakuacha. Nitafanya kila nililokuahidi.”
Glej, jaz sem s teboj in varoval te bom na vseh krajih, kamor greš in ponovno te bom privedel v to deželo, kajti ne bom te zapustil, dokler ne storim tega, o čemer sem ti govoril.«
16 Yakobo akaamka katika usingizi, na akasema, “Hakika Yahwe yupo mahali hapa, sikujua hili.”
Jakob se je zbudil iz svojega spanja in rekel: »Zagotovo je na tem kraju Gospod, jaz pa tega nisem vedel.«
17 Akaogopa na kusema, “Eneo hili linatisha kama nini! Hili sio kingine zaidi ya nyumba ya Mungu. Hili ni lango la mbinguni.”
Bil je prestrašen in rekel: »Kako grozen je ta kraj! To ni nič drugega kakor Božja hiša in to so velika nebeška vrata.«
18 Yakobo akaamka mapema asubuhi na akachukua jiwe alilokuwa ameliweka chini ya kichwa chake. Akaliweka kama nguzo na kumimina mafuta juu yake.
Jakob je zgodaj zjutraj vstal in vzel kamen, ki ga je podstavil za svoje blazine in ga postavil za steber in nanj, na njegov vrh, izlil olje.
19 Akapaita pale Betheli, lakini jina la kawaida la mji lilikuwa Luzu.
Ime tega kraja je imenoval Betel, toda ime tega kraja je bilo najprej imenovano Luz.
20 Yakobo akatoa nadhiri, kusema, “Ikiwa Mungu atakuwa nami na atanilinda katika njia nipitayo, na atanipa mkate wa kula, na mavazi ya kuvaa,
Jakob se je zaobljubil, rekoč: »Če bo Bog z menoj in me bo varoval na tej poti, ki jo hodim in mi bo dal za jesti kruha in oblačilo, da ga oblečem,
21 hata nikarudi salama katika nyumba ya baba yangu, ndipo Yahwe atakapokuwa Mungu wangu.
tako da ponovno v miru pridem k hiši svojega očeta, potem bo Gospod moj Bog.
22 Kisha jiwe hili nililoliweka kama nguzo litakuwa jiwe takatifu. Kutoka katika kila utakachonipa, kwa hakika nitakupa tena sehemu ya kumi.”
In ta kamen, ki sem ga postavil za steber, bo Božja hiša. Od vsega, kar mi boš dal, ti bom zagotovo dajal desetino.«

< Mwanzo 28 >