< Mwanzo 28 >
1 Isaka akamwita Yakobo, akambariki, na kumwagiza, “Usichukuwe mwanamke katika wanawake wa Kikanaani.
C’est pourquoi Isaac appela Jacob, le bénit et lui commanda, disant; Ne prends pas une femme de la race de Chanaan:
2 Inuka, nenda Padani Aramu, katika nyumba ya Bethueli baba wa mama yako, na uchukue mwanamke pale, mmojawapo wa binti za Labani, kaka wa mama yako.
Mais va, et pars pour la Mésopotamie de Syrie, dans la maison de Bathuel, père de ta mère, et prends de là une femme d’entre les filles de Laban ton oncle;
3 Mungu Mwenyezi na akubariki, akupe uzao na akuzidishe, hata uwe wingi wa watu.
Et que le Dieu tout-puissant te bénisse, qu’il te fasse croître et qu’il te multiplie, afin que tu sois le père d’un grand nombre de peuples;
4 Na akupe baraka ya Ibrahimu, wewe, na uzao wako baada yako, kwamba uweze kumilki nchi ambapo umekuwa ukiishi, ambayo Mungu alimpa Ibrahimu.”
Et qu’il te donne les bénédictions d’Abrabam, à toi et à ta postérité après toi, afin que tu possèdes la terre de ton pèlerinage qu’il a promise à ton aïeul.
5 Hivyo Isaka akamwondoa Yakobo. Yakobo akaenda Padani Aramu, kwa Labani mwana wa Bethueli Mwaramu, kaka wa Rebeka, mama yao Yakobo na Esau.
Lorsqu’Isaac eut renvoyé Jacob, celui-ci étant parti, vint en Mésopotamie de Syrie, chez Laban, fils de Bathuel, Syrien, frère de Rébecca sa mère.
6 Basi Esau alipoona kwamba Isaka amembariki Yakobo na kumpeleka Padani Aramu, kuchukua mke kutoka pale. Lakini pia akaona kwamba Isaka alikuwa amembariki na kumwagiza, akisema, “Usichukue mke katika wanawake wa Kanaani.”
Mais Esaü, voyant que son père avait béni Jacob, et qu’il l’avait envoyé en Mésopotamie de Syrie, pour en prendre une femme; et qu’après la bénédiction, il lui avait commandé, disant: Tu ne prendras point de femme d’entre les filles de Chanaan;
7 Esau pia akaona kwamba Yakobo alikuwa amemtii baba yake na mama yake, na alikuwa amekwenda Padani Aramu.
Et que Jacob, obéissant à ses parents, était allé en Syrie;
8 Esau akaona kwamba wanawake wa Kanaani hawakumpendeza Isaka baba yake.
Sachant aussi par expérience que son père ne voyait pas avec plaisir les filles de Chanaan,
9 Hivyo akaenda kwa Ishmaeli, na kuchukua, mbali na wake aliokuwa nao, Mahalathi binti Ishmaeli, mwana wa Ibrahimu, dada wa Nebayothi, kuwa mke wake.
Il alla vers Ismaël, et prit pour femme, outre celles qu’il avait déjà, Mahéleth, fille d’Ismaël fils d’Abraham, sœur de Nabaïoth.
10 Yakobo akatoka Beersheba na akaelekea Harani.
Jacob donc, sorti de Bersabée, poursuivait son chemin vers Haran.
11 Akaja mahali fulani na akakaa pale usiku kucha, kwa kuwa jua lilikuwa limekuchwa. Akachukua mojawapo ya mawe katika eneo hilo, akaliweka chini ya kichwa chake, na akalala usingizi katika eneo hilo.
Or, lorsqu’il fut venu en un certain lieu, et qu’il voulait s’y reposer, après le coucher du soleil, il prit une des pierres qui étaient là, et la mettant sous sa tête, il dormit en ce même lieu.
12 Akaota na kuona ngazi imewekwa juu ya nchi. Ncha yake ilifika hata mbinguni na malaika wa Mungu walikuwa wakishuka na kupanda juu yake.
Alors il vit en songe une échelle posée sur la terre, et dont le sommet touchait au ciel, les anges de Dieu aussi qui la montaient et la descendaient.
13 Tazama, Yahwe amesimama juu yake na kusema, “Mimi ni Yahwe, Mungu wa Ibrahimu baba yako, na Mungu wa Isaka. Nchi uliyolala juu yake, nitakupa wewe na uzao wako.
Et le Seigneur appuyé sur l’échelle, lui disant: Je suis le Seigneur, le Dieu d’Abraham ton père et le Dieu d’Isaac; la terre sur laquelle tu dors, je te la donnerai, à toi et à ta postérité.
14 Uzao wako utakuwa kama mavumbi ya ardhi, na utaenea mbali kuelekea magharibi, mashariki, kaskazini, na kusini. Kupitia kwako na kupitia uzao wako familia zote za dunia zitabarikiwa.
Et elle sera, ta postérité, comme la poussière de la terre, et tu t’étendras à l’occident et à l’orient, au septentrion et au midi; et seront bénies en toi et en ta postérité toutes les tribus de la terre.
15 Tazama, mimi nipo nawe, na nitakulinda kila uendako, Nitakurudisha katika nchi hii tena; kwani sitakuacha. Nitafanya kila nililokuahidi.”
Et je serai ton gardien partout où tu iras, et je te ramènerai dans ce pays, et je ne te quitterai point, que je n’aie accompli tout ce que j’ai dit.
16 Yakobo akaamka katika usingizi, na akasema, “Hakika Yahwe yupo mahali hapa, sikujua hili.”
Quand Jacob fut éveillé de son sommeil, il dit: Vraiment le Seigneur est en ce lieu, et moi je ne le savais pas.
17 Akaogopa na kusema, “Eneo hili linatisha kama nini! Hili sio kingine zaidi ya nyumba ya Mungu. Hili ni lango la mbinguni.”
Et, saisi d’effroi: Qu’il est terrible, dit-il, ce lieu-ci! Ce n’est autre chose que la maison de Dieu et la porte du ciel.
18 Yakobo akaamka mapema asubuhi na akachukua jiwe alilokuwa ameliweka chini ya kichwa chake. Akaliweka kama nguzo na kumimina mafuta juu yake.
Se levant donc le matin, Jacob prit la pierre qu’il avait mise sous sa tête, et l’érigea en monument, répandant de l’huile dessus,
19 Akapaita pale Betheli, lakini jina la kawaida la mji lilikuwa Luzu.
Et il appela du nom de Béthel la ville qui auparavant s’appelait Luza.
20 Yakobo akatoa nadhiri, kusema, “Ikiwa Mungu atakuwa nami na atanilinda katika njia nipitayo, na atanipa mkate wa kula, na mavazi ya kuvaa,
Il voua aussi un vœu, disant: Si le Seigneur Dieu est avec moi, s’il me garde dans le chemin par lequel je marche, et me donne du pain pour me nourrir et des vêtements pour me couvrir,
21 hata nikarudi salama katika nyumba ya baba yangu, ndipo Yahwe atakapokuwa Mungu wangu.
Et que je retourne heureusement à la maison de mon père, le Seigneur sera mon Dieu;
22 Kisha jiwe hili nililoliweka kama nguzo litakuwa jiwe takatifu. Kutoka katika kila utakachonipa, kwa hakika nitakupa tena sehemu ya kumi.”
Et cette pierre, que j’ai érigée en monument, sera appelée Maison de Dieu; et de tout ce que vous m’aurez donné, Seigneur, je vous offrirai la dîme.