< Mwanzo 28 >

1 Isaka akamwita Yakobo, akambariki, na kumwagiza, “Usichukuwe mwanamke katika wanawake wa Kikanaani.
Than Isaac called Iacob his sonne and blessed him ad charged him and sayde vnto him: se thou take not a wife of the doughters of Canaan
2 Inuka, nenda Padani Aramu, katika nyumba ya Bethueli baba wa mama yako, na uchukue mwanamke pale, mmojawapo wa binti za Labani, kaka wa mama yako.
but aryse ad gett the to Mesopotamia to the house of Bethuel thy mothers father: and there take the a wife of the doughters of Laban thi mothers brother.
3 Mungu Mwenyezi na akubariki, akupe uzao na akuzidishe, hata uwe wingi wa watu.
And God allmightie blesse the increase the and multiplie the that thou mayst be a nombre of people
4 Na akupe baraka ya Ibrahimu, wewe, na uzao wako baada yako, kwamba uweze kumilki nchi ambapo umekuwa ukiishi, ambayo Mungu alimpa Ibrahimu.”
and geue the the blessynge of Abraham: both to the and to thy seed with the that thou mayst possesse the lade (wherein thou art a strangere) which God gaue vnto Abraham.
5 Hivyo Isaka akamwondoa Yakobo. Yakobo akaenda Padani Aramu, kwa Labani mwana wa Bethueli Mwaramu, kaka wa Rebeka, mama yao Yakobo na Esau.
Thus Isaac sent forth Iacob to goo to Mesopotamia vnto Laban sonne of Bethuel the Sirien and brother to Rebecca Iacobs and Esaus mother.
6 Basi Esau alipoona kwamba Isaka amembariki Yakobo na kumpeleka Padani Aramu, kuchukua mke kutoka pale. Lakini pia akaona kwamba Isaka alikuwa amembariki na kumwagiza, akisema, “Usichukue mke katika wanawake wa Kanaani.”
When Esau sawe that Isaac had blessed Iacob and sent him to Mesopotamia to fett him a wife thence and that as he blessed him he gaue him a charge saynge: se thou take not a wife of the doughters of Canaan:
7 Esau pia akaona kwamba Yakobo alikuwa amemtii baba yake na mama yake, na alikuwa amekwenda Padani Aramu.
and that Iacob had obeyed his father and mother and was gone vnto Mesopotamia:
8 Esau akaona kwamba wanawake wa Kanaani hawakumpendeza Isaka baba yake.
and seynge also that the doughters of Canaan pleased not Isaac his father:
9 Hivyo akaenda kwa Ishmaeli, na kuchukua, mbali na wake aliokuwa nao, Mahalathi binti Ishmaeli, mwana wa Ibrahimu, dada wa Nebayothi, kuwa mke wake.
Then went he vnto Ismael and toke vnto the wiues which he had Mahala the doughter of Ismael Abrahams sonne the sister of Nabaioth to be his wife.
10 Yakobo akatoka Beersheba na akaelekea Harani.
Iacob departed from Berseba and went toward Haran
11 Akaja mahali fulani na akakaa pale usiku kucha, kwa kuwa jua lilikuwa limekuchwa. Akachukua mojawapo ya mawe katika eneo hilo, akaliweka chini ya kichwa chake, na akalala usingizi katika eneo hilo.
and came vnto a place and taried there all nyghte because the sonne was downe. And toke a stone of the place and put it vnder his heade and layde him downe in the same place to slepe.
12 Akaota na kuona ngazi imewekwa juu ya nchi. Ncha yake ilifika hata mbinguni na malaika wa Mungu walikuwa wakishuka na kupanda juu yake.
And he dreamed: and beholde there stode a ladder apon the erth and the topp of it reached vpp to heaue. And se the angells of God went vp and downe apon it
13 Tazama, Yahwe amesimama juu yake na kusema, “Mimi ni Yahwe, Mungu wa Ibrahimu baba yako, na Mungu wa Isaka. Nchi uliyolala juu yake, nitakupa wewe na uzao wako.
yee ad the LORde stode apon it and sayde. I am the LORde God of Abraham thi father and the God of Isaac: The londe which thou slepest apon will I geue the and thy seed.
14 Uzao wako utakuwa kama mavumbi ya ardhi, na utaenea mbali kuelekea magharibi, mashariki, kaskazini, na kusini. Kupitia kwako na kupitia uzao wako familia zote za dunia zitabarikiwa.
And thy seed shalbe as the dust of the erth: And thou shalt spreade abrode: west east north and south. And thorow the and thy seed shall all the kynreddes of the erth be blessed.
15 Tazama, mimi nipo nawe, na nitakulinda kila uendako, Nitakurudisha katika nchi hii tena; kwani sitakuacha. Nitafanya kila nililokuahidi.”
And se I am with the and wylbe thy keper in all places whother thou goost and wyll brynge ye agayne in to this lande: Nether will I leaue the vntill I haue made good all that I haue promysed the.
16 Yakobo akaamka katika usingizi, na akasema, “Hakika Yahwe yupo mahali hapa, sikujua hili.”
When Iacob was awaked out of his slepe he sayde: surely the LORde is in this place ad I was not aware.
17 Akaogopa na kusema, “Eneo hili linatisha kama nini! Hili sio kingine zaidi ya nyumba ya Mungu. Hili ni lango la mbinguni.”
And he was afrayde and sayde how fearfull is this place? it is none other but euen the house of God and the gate of heaue.
18 Yakobo akaamka mapema asubuhi na akachukua jiwe alilokuwa ameliweka chini ya kichwa chake. Akaliweka kama nguzo na kumimina mafuta juu yake.
And Iacob stode vp early in the mornynge and toke the stone that he had layde vnder his heade and pitched it vp an ende and poured oyle on the topp of it.
19 Akapaita pale Betheli, lakini jina la kawaida la mji lilikuwa Luzu.
And he called the name of the place Bethell for in dede the name of the citie was called Lus before tyme.
20 Yakobo akatoa nadhiri, kusema, “Ikiwa Mungu atakuwa nami na atanilinda katika njia nipitayo, na atanipa mkate wa kula, na mavazi ya kuvaa,
And Iacob vowed a vowe saynge: Yf God will be with me and wyll kepe me in this iourney which I goo and will geue me bread to eate and cloothes to put on
21 hata nikarudi salama katika nyumba ya baba yangu, ndipo Yahwe atakapokuwa Mungu wangu.
so that I come agayne vnto my fathers house in saftie: then shall the LORde be my God
22 Kisha jiwe hili nililoliweka kama nguzo litakuwa jiwe takatifu. Kutoka katika kila utakachonipa, kwa hakika nitakupa tena sehemu ya kumi.”
and this stone which I haue sett vp an ende shalbe godes house And of all that thou shalt geue me will I geue the tenth vnto the.

< Mwanzo 28 >