< Mwanzo 24 >

1 Basi Abraham alikuwa mzee sana na Yahwe akawa amembariki katika mambo yote.
Och Abraham var gammal och väl ålderstigen: Och Herren hade välsignat honom i all stycke.
2 Abraham akamwambia mtumwa wake, ambaye alikuwa mkubwa kuliko wote wa nyumbani mwake na mkuu wa vyote alivyo kuwa navyo.”Weka mkono wako chini ya paja langu
Då sade han till sin äldsta hustjenare, den all hans tingest förestod: Lägg dina hand under mina länd;
3 na nitakufanya uape kwa Yahwe, Mungu wa Mbingu na nchi, kwamba hutampatia mwanangu mke kutoka kwa mabinti wa Wakanaani, miongoni mwao wale nikaao kati yao.
Och svär mig vid Herran, himmelens och jordenes Gud, att du icke tager minom sone hustru af Canaans döttrar, ibland hvilka jag bor:
4 Lakini utakwenda kwenye nchi yangu, na kwa ndugu zangu, na kumtafutia mwanangu Isaka mke.”
Utan far in uti mitt fädernesland, och till mina slägt, och tag minom sone Isaac hustru.
5 Yule mtumwa wake akamwambia, “Itakuwaje ikiwa mwanamke hatakuwa tayari kufuatana nami hadi katika nchi hii? Je nitamrudisha mwanao katika nchi ambayo ulitoka?”
Tjenaren sade: Om så hände, att qvinnan icke ville komma med mig in i detta land, skall jag då låta din son komma dit i landet igen, dädan du kommen äst?
6 Abraham akamwambia, “Hakikisha kwamba hutamrudisha mwanangu kule!
Abraham sade till honom: Vakta dig derföre, att du icke förer min son dit igen.
7 Yahwe, Mungu wa mbingu, ambaye alinitoa mimi kutoka katika nyumba ya baba yangu na kutoka katika nchi ya ndugu zangu, na ambaye aliniahidia kwa kiapo maalumu akisema, 'Nitawapa uzao wako nchi hii,' atatuma malaika wake mbele yako, na utapata mke kwa ajili ya mwanangu kutoka huko.
Herren himmelens Gud, som mig tog utu mins faders huse, och utu mitt födsloland, den med mig talat, och desslikes svurit och sagt hafver: Detta landet vill jag gifva dine säd; han skall sända sin Ängel framför dig, att du skall taga minom sone der hustru.
8 Lakini ikiwa mwanamke hatakuwa tayari, ndipo utakuwa huru katika hiki kiapo changu. Cha muhimu tu ni kwamba usije ukamrudisha mwanangu huko.”
Hvar nu qvinnan dig icke följa vill; så äst du qvitt denna ed: Allenast låt icke min son komma dit igen.
9 Kwa hiyo mtumwa akaweka mkono wake jini ya paja la Abraham bwana wake, na akaapa kuhusiana na jambo hili.
Då lade tjenaren sina hand under Abrahams sins herras länd, och svor honom här uppå.
10 Mtumwa akachukua ngamia kumi wa bwana wake na akaondoka. Akachukua pia aina zote za zawadi kutoka kwa bwana wake. Akaondoka na kwenda katika mkoa wa Aramu Naharaimu, mji wa Nahori.
Så tog tjenaren tio camelar, af sins herras camelar, och drog åstad, och hade med sig af allahanda sins herras håfvor, och var uppe, och for till Mesopotamien till Nahors stad.
11 Akawapigisha magoti ngamia nje ya mji karibu na kisima cha maji. Ilikuwa jioni wakati ambao wanawake huenda kuchota maji.
Der lät han camelarna blifva utanför stadenom, vid en vattubrunn, om aftonen då qvinfolken plägade der komma och taga vatten,
12 Kisha akasema, “Yahwe, Mungu wa bwana wangu Abraham, anijalie kufanikiwa leo na aoneshe agano la uaminifu kwa bwana wangu Abraham.
Och sade: Herre, mins herras Abrahams Gud, kom i dag emot mig, och gör barmhertighet med minom herra Abraham.
13 Tazama, nimesimama hapa karibu na chemchemi ya maji na binti za watu wa mji wanakuja kuteka maji.
Si, jag står här när vattubrunnenom, och deras döttrar, som bo i denna stad, varda här utkommande till att taga vatten.
14 Na itokee hivi kwamba. Nikimwambia msichana, tafadhari tua mtungi wako ili niweze kunywa maji,' na akiniambia, 'Kunywa, na kwamba nitawanywesha ngamia wako pia,' huyo ndiye awe ambaye umemchagulia mtumwa wako Isaka. Kwa njia hii nitajua kuwa umeonesha agano la uaminifu kwa bwana wangu.”
Hvar nu någon piga kommer, och jag säger till henne: Håll hit dina kruko, och låt mig dricka, och hon säger: Drick, jag vill ock gifva dina camelar dricka, att hon är den samma, som du hafver beskärt dinom tjenare Isaac, och att jag derpå må förstå, att du hafver gjort barmhertighet med minom herra.
15 Ikawa kwamba hata kabla hajamaliza kuzungumza, tazama, Rebeka akaja akiwa na mtungi wake wa maji begani mwake. Rebeka alizaliwa na Bethueli mwana wa Milka, mke wa Nahori, ndugu yake na Abraham.
Och förra än han uttalat hade, si, Rebecka Bethuels dotter kom ut, hvilken är Milcas son, den Nahors Abrahams broders hustru var; hon bar ena kruko på axlarna.
16 Msichana huyu alikuwa mzuri na alikuwa bikira. Hapana mwanaume aliye kuwa amekwisha lala naye. Akashuka kisimani na kuujaza mtungi wake, na kupanda juu.
Och hon var en ganska dägelig piga under ansigtet, och var ännu jungfru, och ingen man hade känt henne: Hon kom ned till brunnen, och fyllde krukona, och ville gå hem igen.
17 Kisha mtumwa yule akakimbia kumlaki yule msichana, na kusema, “Tafadhari nipatie maji kidogo ya kunywa kutoka katika mtungi wako.”
Då lopp tjenaren emot henne, och sade: Låt mig dricka något litet vatten af dine kruko.
18 Akasema, “kunywa tafadhari bwana wangu,” na kwa haraka akatua mtungi wake juu ya mkono wake, na akampatia maji ya kunywa.
Och hon sade: Drick, min herre; och strax tog hon krukona ned på sina hand, och gaf honom dricka.
19 Alipokuwa amemaliza kumpatia maji, akasema, “Nitachota maji kwa ajili ya ngamia wako pia, mpaka watakapomaliza kunywa.”
Och då hon hade gifvit honom dricka, sade hon: Jag vill ock ösa vatten åt dina camelar, till dess att de få alle dricka.
20 Hivyo akaharakisha akamwaga maji yaliyokuwa mtungini kwenye chombo cha kunywshea mifugo, kisha akakimbia tena kisimani kuchota maji, na kuwanywesha ngamia wake wote.
Och hon slog straxt vattnet utu krukone i hoen, och lopp åter till brunnen till att ösa, och vattnade alla hans camelar.
21 Yule mtu akamtazama msichana akiwa kimya kuona kama Yahwe amefanikisha njia yake au la.
Men mannen undrade på henne, och var stilla, till dess han kunde få veta, om Herren hade gjort hans resa lyckosam, eller ej.
22 Ngamia walipomaliza kunywa maji, yule mtu akaleta pete ya pua ya dhahabu yenye uzito wa nusu shekeli, na bangili mbili za dhahabu kwa ajili ya mikono yake zenye uzito wa shekeli kumi,
Då nu alle camelarne hade druckit, tog han fram ett gyldene ännespann, vägandes en half sikel, och två armringar till hennes händer, vägande tio siklar guld;
23 akamuuliza, “wewe ni binti wa nani? Niambie tafadhali, Je kuna nafasi nyumbani mwa baba yako kwa ajili yetu kupumzika usiku?”
Och sade: Min dotter, hvem hörer du till? Säg mig dock det. Hafve vi ock rum till att få herberge i dins faders huse?
24 Akamwambia, “Mimi ni binti wa Bethueli mwana wa Milka, ambaye alimzaa kwa Nahori.”
Hon sade till honom: Jag är Bethuels dotter, Milcas sons, som hon hafver födt Nahor.
25 Akasema pia, “Tunayo malisho tele na chakula, na iko nafasi kwa ajili yako kulala usiku.”
Och hon sade ytterligare till honom: Är ock så mycket halm och foder när oss, och rum nog till herberge.
26 Kisha yume mtu akainama chini na kumwabudu Yahwe.
Då böjde mannen sig ned, och bad till Herran.
27 Akasema, “Abarikiwe Yahwe, Mungu wa bwana wangu Abraham, ambaye hakuacha agano lake la uaminifu na kweli yake mbele ya bwana wangu. Kwa vile Yahwe ameniongoza moja kwa moja kwenye nyumba ya ndugu zake bwana wangu.”
Och sade: Lofvad vare Herren, mins herras Abrahams Gud, som icke hafver tagit sina barmhertighet och sina sanning ifrå minom herra; förty Herren hafver fört mig den rätta vägen till mins herras broders hus.
28 Kisha yule msichana akakimbia na kwenda kuwaeleza watu wa nyumba ya mama yake juu ya mambo yote haya.
Och pigan lopp, och sade allt detta i sins moders huse.
29 Na sasa Rebeka alikuwa na kaka yake, jina lake aliitwa Labani. Labani akakimbia kwa yule mtu aliye kuwa nje barabarani karibu na kisima.
Och Rebecka hade en broder, som het Laban: Och Laban lopp ut till mannen vid brunnen.
30 Akisha kuona hereni ya puani pamoja na zile bangili kwenye mikono ya dada yake, na kusikia maneno ya Rebeka dada yake, “Hivi ndivyo yule mtu alicho niambia,” alikwenda kwa yule mtu, na, Tazama, alikuwa amesimama karibu na ngamia pale kisimani.
Och när han såg ännespannet och armringarna i sine systers händer, och hörde Rebeckas sine systers ord, att hon sade: Så hafver mannen sagt mig; kom han till mannen: Och si, han stod när camelarna vid brunnen:
31 Labani akasema, “Njoo, wewe uliye barikiwa na Yahwe. Kwa nini umesimama nje? nimekwisha andaa nyumba, pamoja na mahali kwa ajili ya ngamia.”
Och sade: Kom här in, du Herrans välsignade, hvi står du här ute? Jag hafver rymt huset, och gjort rum för camelarna.
32 Kwa hiyo yule mtu akaingia ndani ya nyumba na akashusha mizigo kutoka kwa wale ngamia. Ngamia wakapatiwa malisho na chakula, na maji yakatolewa kuosha miguu yake pamoja na miguu ya wale watu aliokuwa pamoja nao.
Så hade han mannen in i huset, och lade af camelarna, och gaf dem halm och foder, och vatten till att två hans fötter, och männernas, som med honom voro.
33 Wakaandaa chakula mbele yake ale, lakini akasema, “Sitakula mpaka niseme kile ninacho paswa kusema.” Kwa hiyo Labani akmwambia, “Sema.”
Och satte mat för honom. Då sade han: Jag vill icke äta, förra än jag hafver värfvat mitt ärende. De svarade: Säg.
34 Akasema, “Mimi ni mtumwa wa Abraham.
Han sade: Jag är Abrahams tjenare.
35 Yahwe amembariki sana bwana wangu na amekuwa mtu mkuu. Amempatia mifugo na makundi ya wanyama, fedha, dhahabu, watumwa wa kiume na watumwa wa kike, pamoja na ngamia na punda.
Och Herren hafver rikeliga välsignat min herra, och han är stor vorden, och han hafver gifvit honom får och fä, silfver och guld, tjenare och tjenarinnor, camelar och åsnar.
36 Sara, mke wa bwana wangu, alimzalia mwana bwana wangu alipokuwa mzee, na amempatia mwanawe kila kitu anachomiliki.
Dertill hafver Sara, mins herras hustru, födt minom herra en son i sinom ålderdom, honom hafver han gifvit allt det han hafver.
37 Bwana wangu aliniapisha, akisema, “Usije ukampatia mwanangu mke kutoka kwa mabinti wa Wakanaani, ambao kwao nimefanya makazi.
Och min herre hafver tagit en ed af mig, och sagt: Du skall icke taga minom sone någon hustru af de Cananeers döttrar, i hvilkas land jag bor;
38 Badala yake, lazima uende kwa familia ya baba yangu, na kwa ndugu zangu, na kupata mke kwa ajili ya mwanangu.'
Utan far bort till mins faders hus, och till mina slägt, tag der minom sone hustru.
39 Nikamwambia bwana wangu, pengine mwanamke huyo asikubali kufuatana nami.'
Men jag sade till min herra: Huru? Om qvinnan icke vill följa mig?
40 Lakini akaniambia, Yahwe, ambaye ninakwenda mbele yake, atatuma malaika wake pamoja nawe na atakufanikisha njia yako, kwamba utapata mke kwa ajili ya mwangu kutoka miongoni mwa ndugu zangu na kutoka katika ukoo wa baba yangu.
Då sade han till mig: Herren, för hvilkom jag vandrar, varder sändandes sin Ängel med dig, och skall göra din väg lyckosam, så att du skall taga minom sone hustru af mine slägt och mins faders huse.
41 Lakini utakuwa huru katika kiapo changu ikiwa utafika kwa ndugu zangu na wasikuruhusu kuja naye. Ndipo utakuwa huru katika kiapo changu.
Då skall du vara min ed qvitt, när du kommer till mina slägt; gifva de dig icke, så äst du min ed qvitt.
42 Hivyo nimefika leo kisimani, na nikasema, 'O Yahwe, Mungu wa bwana wangu Abraham, tafadhari, ikiwa kweli umekusudia kuifanya safari yangu kuwa yenye kufanikiwa -
Så kom jag i dag till brunnen, och sade: Herre, mins herras Abrahams Gud, hafver du gjort min väg lyckosam, den jag nu reser:
43 tazama niko hapa nimesimama karibu na kisima cha maji - na iwe kwamba binti ajaye kuchota maji, nitakaye mwambia, “Tafadhari unipatie maji kidoka kutoka kwenye mtungi wako ninywe,” mwanamke atakaye niabia,
Si, så står jag här vid vattubrunnen. När nu en jungfru kommer här ut till att taga vatten, och jag säger till henne: Gif mig litet vatten att dricka af dine kruko;
44 “Kunywa, na nitakuchotea pia maji kwa ajili ya ngamia wako” - na awe ndiye ambaye wewe Yahwe, umemchagulia mtoto wa bwana wangu.”
Och hon varder sägandes: Drick du; jag vill ock vattna dina camelar: det är den qvinna, som Herren hafver beskärt mins herras sone.
45 Ikawa hata kabla sijamaliza kuzungumza moyoni mwangu, Tazama, Rebeka akaja na mtungi wake juu ya bega lake akashuka chini kisimani akachota maji. Hivyo nikamwambia, 'Tafadhari nipatie maji ninywe.'
Förra än jag nu sådan ord utsagt hade i mino hjerta, si, då kom Rebecka ut med ene kruko på sine axel, och gick ned åt brunnen till att taga vatten. Då sade jag till henne: Gif mig dricka.
46 Ndipo kwa haraka alipoushusha mtungi wake begani mwake na akasema, 'Kunywa, na pia nitawapatia maji ngamia wak.' Kwa hiyo nikanywa, na akawanywesha ngamia pia.
Och hon tog snarliga krukona af sin axel, och sade: Drick; dina camelar vill jag ock vattna. Så drack jag, och hon vattnade också camelarna.
47 Nikamuuliza na kusema, 'Wewe ni binti wa nani?' Akasema, 'Binti wa Bethueli, Mwana wa Nahori, ambaye Milka alizaa kwake.' Kisha nikamwekea pete puani mwake pamoja na bangili mikononi mwake.
Och jag frågade henne, och sade: Hvars dotter äst du? Hon svarade: Jag är Bethuels dotter, Nahors sons, som Milca honom födt hafver. Då hängde jag ett ännespann på hennes anlete, och armringar öfver hennes händer:
48 Kisha nikainama chini nikamwabudu Yahwe, na kumbariki Yahwe, Mungu wa bwana wangu Abraham, ambaye ameniongoza katika njia sahihi kumpata binti wa ndugu za bwana wangu kwa ajili ya mwanawe.
Och böjde mig neder, och bad till Herran, och lofvade Herran, mins herras Abrahams Gud, som mig hade fört rätta vägen, att jag skulle taga till hans son mins herras broders dotter.
49 Kwa hiyo, ikiwa mko tayari kumfanyia rehema na kweli, niambieni. Lakini kama sivyo, niambieni, ili kwamba niweze kwenda upande wa kulia, au kushoto.”
Om I nu ären de, som bevisen minom herra barmhertighet och sanning, så säger mig det; hvar ock icke, så säger mig ock det; att jag vänder mig antingen till den högra sidona, eller till den venstra.
50 Ndipo Labani na Bethueli wakajibu na kusema, “Jambo hili limetoka kwa Yahwe; hatuwezi kusema kwako aidha neno baya au zuri.
Då svarade Laban och Bethuel, och sade: Det är utgånget af Herranom, derföre kunne vi intet säga dig emot, hvarken ondt eller godt.
51 Tazama, Rebeka yu mbele yako. Mchukue na uende, ili awe mke wa mtoto wa bwana wako, kama Yahwe alivyosema.”
Der är Rebecka för dig, tag henne, och far din väg, att hon blifver dins herras sons hustru, som Herren sagt hafver.
52 Mtumwa wa Abraham aliposikia maneno yao, akainama mwenyewe chini ardhini kwa Yahwe.
Då Abrahams tjenare hörde dessa ord, bugade han sig till jordena för Herranom.
53 Mtumwa akaleta vipande vya fedha na vipande vya dhahabu, na nguo, akampatia Rebeka. Akampatia pia kaka yake na mama yake zawadi zenye thamani.
Och tog fram silfver och gyldene klenodier och kläder, och gaf dem Rebecka; men hennes broder och moder gaf han örter.
54 Kisha yeye na watu aliokuwa nao wakala na kunywa. wakakaa pale mpaka usiku, na walipoamka asubuhi, akasema, Niruhusuni niende kwa bwana wangu.”
Då åt han och drack samt med männerne, som med honom voro, och blefvo der öfver nattena. Om morgonen stod han upp, och sade: Låter mig fara till min herra.
55 Kaka yake na mama yake wakasema, mwache binti abaki nasi kwa siku chache zingine, angalau siku kumi. baada ya hapo anaweza kwenda.”
Men hennes broder och moder sade: Låt dock blifva pigona vid tio dagar när oss; sedan skall du fara.
56 Lakini akawambia, msinizuie, kwa kuwa Yahwe amefanikisha njia yangu. Niruhusuni niende kwa bwana wangu.”
Då sade han till dem: Förhåller mig icke, förty Herren hafver gjort min väg lyckosam; släpper mig, att jag far till min herra.
57 Wakasema, “Tutamwita binti na kumuuliza.”
Då sade de: Låter oss kalla pigona, och fråga hvad hon säger dertill.
58 Kwa hiyo wakamwita Rebeka na kumuuliza, “Je utakwenda na mtu huyu?” Akajibu, “Nitakwenda.”
Och de kallade Rebecka, och sade till henne: Vill du fara med denne mannenom? Hon svarade: Ja, jag vill med honom.
59 Kwa hiyo wakampeleka dada yao Rebeka, pamoja na watumishi wake wa kike, kwenda njiani pamoja na mtumishi wa Abraham na watu wake.
Så läto de Rebecka sina syster fara med hennes ammo, och Abrahams tjenare, och hans följare.
60 Wakambarikia Rebeka, na wakamwambia, “Ndugu yetu, na uwe mama wa maelfu na wa makumi elfu, uzao wako upate kumiliki lango la wale wanao wachukia.”
Och de välsignade Rebecka, och sade till henne: Du äst vår syster, förkofra dig till tusende tusend, och din säd besitte sina fienders portar.
61 Kisha Rebeka akasimama, yeye na watumishi wake kwa hesabu ya ngamia, na wakamfuata yule mtu. Hivyo watumishi wakamchukua Rebeka, na wakaenda zao.
Så redde Rebecka sig till med sina pigor, och satte sig på camelarna, och följde mannen efter. Och tjenaren tog Rebecka till sig, och for sin väg.
62 Nyakati hizo Isaka alikuwa anakaa katika Negebu, na alikuwa tu amerejea kutoka Beerlahairoi.
Men Isaac kom ifrå den brunnen, som kallades dens lefvandes och seendes; ty han bodde i det landet söder ut.
63 Isaka akaenda kutafakari shambani jioni. Alipotazama akaona, natazama, kulikuwa na ngamia wakija!
Och var utgången till att bedja i markene om aftonen; och hof upp sin ögon, och såg att camelarne kommo der.
64 Rebeka akatazama na alipomwona Isaka, akaruka kutoka kwenye ngamia.
Och Rebecka hof upp sin ögon, och såg Isaac; då steg hon af camelen,
65 Akamwambia mtumwa, “mtu huyo ni nani anaye tembea shambani akija kutupokea?” Mtumwa akasema, “Ni bwana wangu.” Hivyo Rebeka akachukua shela yake akajifunika.
Och sade till tjenaren: Hvad man är det, som kommer emot oss på markene? Tjenaren sade: Det är min herre. Då tog hon mantelen och höljde sig.
66 Mtumwa akamwambia Isaka mambo yote ambayo amefanya.
Och tjenaren förtäljde Isaac allt, huru han sakena uträttat hade.
67 Kisha Isaka akamleta katika hema ya Sara mama yake na akamchukua Rebeka, na akawa mke wake, na akampenda. Kwa hiyo Isaka akafarijika baada ya kifo cha mama yake.
Då förde Isaac henne in i sins moders Saras hyddo, och tog Rebecka, och hon vardt hans hustru, och han vardt kär åt henne: Och så vardt Isaac hugsvalad öfver sina moder.

< Mwanzo 24 >