< Mwanzo 24 >

1 Basi Abraham alikuwa mzee sana na Yahwe akawa amembariki katika mambo yote.
and Abraham be old to come (in): advanced in/on/with day: year and LORD to bless [obj] Abraham in/on/with all
2 Abraham akamwambia mtumwa wake, ambaye alikuwa mkubwa kuliko wote wa nyumbani mwake na mkuu wa vyote alivyo kuwa navyo.”Weka mkono wako chini ya paja langu
and to say Abraham to(wards) servant/slave his old house: household his [the] to rule in/on/with all which to/for him to set: put please hand: swear your underneath: swear thigh my
3 na nitakufanya uape kwa Yahwe, Mungu wa Mbingu na nchi, kwamba hutampatia mwanangu mke kutoka kwa mabinti wa Wakanaani, miongoni mwao wale nikaao kati yao.
and to swear you in/on/with LORD God [the] heaven and God [the] land: country/planet which not to take: take woman: wife to/for son: child my from daughter [the] Canaanite which I to dwell in/on/with entrails: among his
4 Lakini utakwenda kwenye nchi yangu, na kwa ndugu zangu, na kumtafutia mwanangu Isaka mke.”
for to(wards) land: country/planet my and to(wards) relatives my to go: went and to take: take woman: wife to/for son: child my to/for Isaac
5 Yule mtumwa wake akamwambia, “Itakuwaje ikiwa mwanamke hatakuwa tayari kufuatana nami hadi katika nchi hii? Je nitamrudisha mwanao katika nchi ambayo ulitoka?”
and to say to(wards) him [the] servant/slave perhaps not be willing [the] woman to/for to go: follow after me to(wards) [the] land: country/planet [the] this to return: return to return: return [obj] son: child your to(wards) [the] land: country/planet which to come out: come from there
6 Abraham akamwambia, “Hakikisha kwamba hutamrudisha mwanangu kule!
and to say to(wards) him Abraham to keep: careful to/for you lest to return: return [obj] son: child my there [to]
7 Yahwe, Mungu wa mbingu, ambaye alinitoa mimi kutoka katika nyumba ya baba yangu na kutoka katika nchi ya ndugu zangu, na ambaye aliniahidia kwa kiapo maalumu akisema, 'Nitawapa uzao wako nchi hii,' atatuma malaika wake mbele yako, na utapata mke kwa ajili ya mwanangu kutoka huko.
LORD God [the] heaven which to take: take me from house: household father my and from land: country/planet relatives my and which to speak: speak to/for me and which to swear to/for me to/for to say to/for seed: children your to give: give [obj] [the] land: country/planet [the] this he/she/it to send: depart messenger: angel his to/for face: before your and to take: take woman: wife to/for son: child my from there
8 Lakini ikiwa mwanamke hatakuwa tayari, ndipo utakuwa huru katika hiki kiapo changu. Cha muhimu tu ni kwamba usije ukamrudisha mwanangu huko.”
and if not be willing [the] woman to/for to go: follow after you and to clear from oath my this except [obj] son: child my not to return: return there [to]
9 Kwa hiyo mtumwa akaweka mkono wake jini ya paja la Abraham bwana wake, na akaapa kuhusiana na jambo hili.
and to set: put [the] servant/slave [obj] hand: swear his underneath: swear thigh Abraham lord his and to swear to/for him upon [the] word: thing [the] this
10 Mtumwa akachukua ngamia kumi wa bwana wake na akaondoka. Akachukua pia aina zote za zawadi kutoka kwa bwana wake. Akaondoka na kwenda katika mkoa wa Aramu Naharaimu, mji wa Nahori.
and to take: take [the] servant/slave ten camel from camel lord his and to go: went and all goodness lord his in/on/with hand: to his and to arise: rise and to go: went to(wards) Mesopotamia Mesopotamia to(wards) city Nahor
11 Akawapigisha magoti ngamia nje ya mji karibu na kisima cha maji. Ilikuwa jioni wakati ambao wanawake huenda kuchota maji.
and to bless [the] camel from outside to/for city to(wards) well [the] water to/for time evening to/for time to come out: come [the] to draw
12 Kisha akasema, “Yahwe, Mungu wa bwana wangu Abraham, anijalie kufanikiwa leo na aoneshe agano la uaminifu kwa bwana wangu Abraham.
and to say LORD God lord my Abraham to meet please to/for face of my [the] day and to make: do kindness with lord my Abraham
13 Tazama, nimesimama hapa karibu na chemchemi ya maji na binti za watu wa mji wanakuja kuteka maji.
behold I to stand upon spring [the] water and daughter human [the] city to come out: come to/for to draw water
14 Na itokee hivi kwamba. Nikimwambia msichana, tafadhari tua mtungi wako ili niweze kunywa maji,' na akiniambia, 'Kunywa, na kwamba nitawanywesha ngamia wako pia,' huyo ndiye awe ambaye umemchagulia mtumwa wako Isaka. Kwa njia hii nitajua kuwa umeonesha agano la uaminifu kwa bwana wangu.”
and to be [the] maiden which to say to(wards) her to stretch please jar your and to drink and to say to drink and also camel your to water: watering [obj] her to rebuke to/for servant/slave your to/for Isaac and in/on/with her to know for to make: do kindness with lord my
15 Ikawa kwamba hata kabla hajamaliza kuzungumza, tazama, Rebeka akaja akiwa na mtungi wake wa maji begani mwake. Rebeka alizaliwa na Bethueli mwana wa Milka, mke wa Nahori, ndugu yake na Abraham.
and to be he/she/it before to end: finish to/for to speak: speak and behold Rebekah to come out: come which to beget to/for Bethuel son: child Milcah woman: wife Nahor brother: male-sibling Abraham and jar her upon shoulder her
16 Msichana huyu alikuwa mzuri na alikuwa bikira. Hapana mwanaume aliye kuwa amekwisha lala naye. Akashuka kisimani na kuujaza mtungi wake, na kupanda juu.
and [the] maiden pleasant appearance much virgin and man not to know her and to go down [the] spring [to] and to fill jar her and to ascend: rise
17 Kisha mtumwa yule akakimbia kumlaki yule msichana, na kusema, “Tafadhari nipatie maji kidogo ya kunywa kutoka katika mtungi wako.”
and to run: run [the] servant/slave to/for to encounter: meet her and to say to swallow me please little water from jar your
18 Akasema, “kunywa tafadhari bwana wangu,” na kwa haraka akatua mtungi wake juu ya mkono wake, na akampatia maji ya kunywa.
and to say to drink lord my and to hasten and to go down jar her upon hand her and to water: drink him
19 Alipokuwa amemaliza kumpatia maji, akasema, “Nitachota maji kwa ajili ya ngamia wako pia, mpaka watakapomaliza kunywa.”
and to end: finish to/for to water: drink him and to say also to/for camel your to draw till if: until to end: finish to/for to drink
20 Hivyo akaharakisha akamwaga maji yaliyokuwa mtungini kwenye chombo cha kunywshea mifugo, kisha akakimbia tena kisimani kuchota maji, na kuwanywesha ngamia wake wote.
and to hasten and to uncover jar her to(wards) [the] trough and to run: run still to(wards) [the] well to/for to draw and to draw to/for all camel his
21 Yule mtu akamtazama msichana akiwa kimya kuona kama Yahwe amefanikisha njia yake au la.
and [the] man to gaze to/for her be quiet to/for to know to prosper LORD way: journey his if not
22 Ngamia walipomaliza kunywa maji, yule mtu akaleta pete ya pua ya dhahabu yenye uzito wa nusu shekeli, na bangili mbili za dhahabu kwa ajili ya mikono yake zenye uzito wa shekeli kumi,
and to be like/as as which to end: finish [the] camel to/for to drink and to take: take [the] man ring gold bekah weight his and two bracelet upon hand: swear her ten gold weight their
23 akamuuliza, “wewe ni binti wa nani? Niambie tafadhali, Je kuna nafasi nyumbani mwa baba yako kwa ajili yetu kupumzika usiku?”
and to say daughter who? you(f. s.) to tell please to/for me there house: home father your place to/for us to/for to lodge
24 Akamwambia, “Mimi ni binti wa Bethueli mwana wa Milka, ambaye alimzaa kwa Nahori.”
and to say to(wards) him daughter Bethuel I son: child Milcah which to beget to/for Nahor
25 Akasema pia, “Tunayo malisho tele na chakula, na iko nafasi kwa ajili yako kulala usiku.”
and to say to(wards) him also straw also fodder many with us also place to/for to lodge
26 Kisha yume mtu akainama chini na kumwabudu Yahwe.
and to bow [the] man and to bow to/for LORD
27 Akasema, “Abarikiwe Yahwe, Mungu wa bwana wangu Abraham, ambaye hakuacha agano lake la uaminifu na kweli yake mbele ya bwana wangu. Kwa vile Yahwe ameniongoza moja kwa moja kwenye nyumba ya ndugu zake bwana wangu.”
and to say to bless LORD God lord my Abraham which not to leave: forsake kindness his and truth: faithful his from from with lord my I in/on/with way: journey to lead me LORD house: home brother: male-relative lord my
28 Kisha yule msichana akakimbia na kwenda kuwaeleza watu wa nyumba ya mama yake juu ya mambo yote haya.
and to run: run [the] maiden and to tell to/for house: household mother her like/as word: thing [the] these
29 Na sasa Rebeka alikuwa na kaka yake, jina lake aliitwa Labani. Labani akakimbia kwa yule mtu aliye kuwa nje barabarani karibu na kisima.
and to/for Rebekah brother: male-sibling and name his Laban and to run: run Laban to(wards) [the] man [the] outside [to] to(wards) [the] spring
30 Akisha kuona hereni ya puani pamoja na zile bangili kwenye mikono ya dada yake, na kusikia maneno ya Rebeka dada yake, “Hivi ndivyo yule mtu alicho niambia,” alikwenda kwa yule mtu, na, Tazama, alikuwa amesimama karibu na ngamia pale kisimani.
and to be like/as to see: see [obj] [the] ring and [obj] [the] bracelet upon hand sister his and like/as to hear: hear he [obj] word Rebekah sister his to/for to say thus to speak: speak to(wards) me [the] man and to come (in): come to(wards) [the] man and behold to stand: stand upon [the] camel upon [the] spring
31 Labani akasema, “Njoo, wewe uliye barikiwa na Yahwe. Kwa nini umesimama nje? nimekwisha andaa nyumba, pamoja na mahali kwa ajili ya ngamia.”
and to say to come (in): come to bless LORD to/for what? to stand: stand in/on/with outside and I to turn [the] house: home and place to/for camel
32 Kwa hiyo yule mtu akaingia ndani ya nyumba na akashusha mizigo kutoka kwa wale ngamia. Ngamia wakapatiwa malisho na chakula, na maji yakatolewa kuosha miguu yake pamoja na miguu ya wale watu aliokuwa pamoja nao.
and to come (in): come [the] man [the] house: home [to] and to open [the] camel and to give: give straw and fodder to/for camel and water to/for to wash: wash foot his and foot [the] human which with him
33 Wakaandaa chakula mbele yake ale, lakini akasema, “Sitakula mpaka niseme kile ninacho paswa kusema.” Kwa hiyo Labani akmwambia, “Sema.”
(and to set: put *Q(K)*) to/for face: before his to/for to eat and to say not to eat till if: surely no to speak: speak word: speaking my and to say to speak: speak
34 Akasema, “Mimi ni mtumwa wa Abraham.
and to say servant/slave Abraham I
35 Yahwe amembariki sana bwana wangu na amekuwa mtu mkuu. Amempatia mifugo na makundi ya wanyama, fedha, dhahabu, watumwa wa kiume na watumwa wa kike, pamoja na ngamia na punda.
and LORD to bless [obj] lord my much and to magnify and to give: give to/for him flock and cattle and silver: money and gold and servant/slave and maidservant and camel and donkey
36 Sara, mke wa bwana wangu, alimzalia mwana bwana wangu alipokuwa mzee, na amempatia mwanawe kila kitu anachomiliki.
and to beget Sarah woman: wife lord my son: child to/for lord my after old age her and to give: give to/for him [obj] all which to/for him
37 Bwana wangu aliniapisha, akisema, “Usije ukampatia mwanangu mke kutoka kwa mabinti wa Wakanaani, ambao kwao nimefanya makazi.
and to swear me lord my to/for to say not (to take: take *LA(bh)*) woman: wife to/for son: child my from daughter [the] Canaanite which I to dwell in/on/with land: country/planet his
38 Badala yake, lazima uende kwa familia ya baba yangu, na kwa ndugu zangu, na kupata mke kwa ajili ya mwanangu.'
if: surely yes not to(wards) house: household father my to go: went and to(wards) family my and to take: take woman: wife to/for son: child my
39 Nikamwambia bwana wangu, pengine mwanamke huyo asikubali kufuatana nami.'
and to say to(wards) lord my perhaps not to go: follow [the] woman after me
40 Lakini akaniambia, Yahwe, ambaye ninakwenda mbele yake, atatuma malaika wake pamoja nawe na atakufanikisha njia yako, kwamba utapata mke kwa ajili ya mwangu kutoka miongoni mwa ndugu zangu na kutoka katika ukoo wa baba yangu.
and to say to(wards) me LORD which to go: walk to/for face: before his to send: depart messenger: angel his with you and to prosper way: journey your and to take: take woman: wife to/for son: child my from family my and from house: household father my
41 Lakini utakuwa huru katika kiapo changu ikiwa utafika kwa ndugu zangu na wasikuruhusu kuja naye. Ndipo utakuwa huru katika kiapo changu.
then to clear from oath my for to come (in): come to(wards) family my and if not to give: give to/for you and to be innocent from oath my
42 Hivyo nimefika leo kisimani, na nikasema, 'O Yahwe, Mungu wa bwana wangu Abraham, tafadhari, ikiwa kweli umekusudia kuifanya safari yangu kuwa yenye kufanikiwa -
and to come (in): come [the] day to(wards) [the] spring and to say LORD God lord my Abraham if there you please to prosper way: journey my which I to go: went upon her
43 tazama niko hapa nimesimama karibu na kisima cha maji - na iwe kwamba binti ajaye kuchota maji, nitakaye mwambia, “Tafadhari unipatie maji kidoka kutoka kwenye mtungi wako ninywe,” mwanamke atakaye niabia,
behold I to stand upon spring [the] water and to be [the] maiden [the] to come out: come to/for to draw and to say to(wards) her to water: drink me please little water from jar your
44 “Kunywa, na nitakuchotea pia maji kwa ajili ya ngamia wako” - na awe ndiye ambaye wewe Yahwe, umemchagulia mtoto wa bwana wangu.”
and to say to(wards) me also you(m. s.) to drink and also to/for camel your to draw he/she/it [the] woman which to rebuke LORD to/for son: child lord my
45 Ikawa hata kabla sijamaliza kuzungumza moyoni mwangu, Tazama, Rebeka akaja na mtungi wake juu ya bega lake akashuka chini kisimani akachota maji. Hivyo nikamwambia, 'Tafadhari nipatie maji ninywe.'
I before to end: finish to/for to speak: speak to(wards) heart my and behold Rebekah to come out: come and jar her upon shoulder her and to go down [the] spring [to] and to draw and to say to(wards) her to water: drink me please
46 Ndipo kwa haraka alipoushusha mtungi wake begani mwake na akasema, 'Kunywa, na pia nitawapatia maji ngamia wak.' Kwa hiyo nikanywa, na akawanywesha ngamia pia.
and to hasten and to go down jar her from upon her and to say to drink and also camel your to water: watering and to drink and also [the] camel to water: watering
47 Nikamuuliza na kusema, 'Wewe ni binti wa nani?' Akasema, 'Binti wa Bethueli, Mwana wa Nahori, ambaye Milka alizaa kwake.' Kisha nikamwekea pete puani mwake pamoja na bangili mikononi mwake.
and to ask [obj] her and to say daughter who? you(f. s.) and to say daughter Bethuel son: child Nahor which to beget to/for him Milcah and to set: put [the] ring upon face: nose her and [the] bracelet upon hand her
48 Kisha nikainama chini nikamwabudu Yahwe, na kumbariki Yahwe, Mungu wa bwana wangu Abraham, ambaye ameniongoza katika njia sahihi kumpata binti wa ndugu za bwana wangu kwa ajili ya mwanawe.
and to bow and to bow to/for LORD and to bless [obj] LORD God lord my Abraham which to lead me in/on/with way: journey truth: true to/for to take: take [obj] daughter brother: male-relative lord my to/for son: child his
49 Kwa hiyo, ikiwa mko tayari kumfanyia rehema na kweli, niambieni. Lakini kama sivyo, niambieni, ili kwamba niweze kwenda upande wa kulia, au kushoto.”
and now if there you to make: do kindness and truth: faithful with lord my to tell to/for me and if not to tell to/for me and to turn upon right or upon left
50 Ndipo Labani na Bethueli wakajibu na kusema, “Jambo hili limetoka kwa Yahwe; hatuwezi kusema kwako aidha neno baya au zuri.
and to answer Laban and Bethuel and to say from LORD to come out: come [the] word: thing not be able to speak: speak to(wards) you bad: harmful or pleasant
51 Tazama, Rebeka yu mbele yako. Mchukue na uende, ili awe mke wa mtoto wa bwana wako, kama Yahwe alivyosema.”
behold Rebekah to/for face: before your to take: take and to go: went and to be woman: wife to/for son: child lord your like/as as which to speak: speak LORD
52 Mtumwa wa Abraham aliposikia maneno yao, akainama mwenyewe chini ardhini kwa Yahwe.
and to be like/as as which to hear: hear servant/slave Abraham [obj] word their and to bow land: soil [to] to/for LORD
53 Mtumwa akaleta vipande vya fedha na vipande vya dhahabu, na nguo, akampatia Rebeka. Akampatia pia kaka yake na mama yake zawadi zenye thamani.
and to come out: send [the] servant/slave article/utensil silver: money and article/utensil gold and garment and to give: give to/for Rebekah and precious thing to give: give to/for brother: male-sibling her and to/for mother her
54 Kisha yeye na watu aliokuwa nao wakala na kunywa. wakakaa pale mpaka usiku, na walipoamka asubuhi, akasema, Niruhusuni niende kwa bwana wangu.”
and to eat and to drink he/she/it and [the] human which with him and to lodge and to arise: rise in/on/with morning and to say to send: depart me to/for lord my
55 Kaka yake na mama yake wakasema, mwache binti abaki nasi kwa siku chache zingine, angalau siku kumi. baada ya hapo anaweza kwenda.”
and to say brother: male-sibling her and mother her to dwell [the] maiden with us day or ten (after *L(S)*) to go: went
56 Lakini akawambia, msinizuie, kwa kuwa Yahwe amefanikisha njia yangu. Niruhusuni niende kwa bwana wangu.”
and to say to(wards) them not to delay [obj] me and LORD to prosper way: journey my to send: depart me and to go: went to/for lord my
57 Wakasema, “Tutamwita binti na kumuuliza.”
and to say to call: call to to/for maiden and to ask [obj] lip her
58 Kwa hiyo wakamwita Rebeka na kumuuliza, “Je utakwenda na mtu huyu?” Akajibu, “Nitakwenda.”
and to call: call to to/for Rebekah and to say to(wards) her to go: went with [the] man [the] this and to say to go: went
59 Kwa hiyo wakampeleka dada yao Rebeka, pamoja na watumishi wake wa kike, kwenda njiani pamoja na mtumishi wa Abraham na watu wake.
and to send: depart [obj] Rebekah sister their and [obj] to suckle her and [obj] servant/slave Abraham and [obj] human his
60 Wakambarikia Rebeka, na wakamwambia, “Ndugu yetu, na uwe mama wa maelfu na wa makumi elfu, uzao wako upate kumiliki lango la wale wanao wachukia.”
and to bless [obj] Rebekah and to say to/for her sister our you(f. s.) to be to/for thousand myriad and to possess: take seed: children your [obj] gate to hate him
61 Kisha Rebeka akasimama, yeye na watumishi wake kwa hesabu ya ngamia, na wakamfuata yule mtu. Hivyo watumishi wakamchukua Rebeka, na wakaenda zao.
and to arise: rise Rebekah and maiden her and to ride upon [the] camel and to go: follow after [the] man and to take: take [the] servant/slave [obj] Rebekah and to go: journey
62 Nyakati hizo Isaka alikuwa anakaa katika Negebu, na alikuwa tu amerejea kutoka Beerlahairoi.
and Isaac to come (in): come from to come (in): come Beer-lahai-roi Beer-lahai-roi Beer-lahai-roi and he/she/it to dwell in/on/with land: country/planet [the] Negeb
63 Isaka akaenda kutafakari shambani jioni. Alipotazama akaona, natazama, kulikuwa na ngamia wakija!
and to come out: come Isaac to/for to meditate in/on/with land: country to/for to turn evening and to lift: look eye his and to see: see and behold camel to come (in): come
64 Rebeka akatazama na alipomwona Isaka, akaruka kutoka kwenye ngamia.
and to lift: look Rebekah [obj] eye her and to see: see [obj] Isaac and to fall: fall from upon [the] camel
65 Akamwambia mtumwa, “mtu huyo ni nani anaye tembea shambani akija kutupokea?” Mtumwa akasema, “Ni bwana wangu.” Hivyo Rebeka akachukua shela yake akajifunika.
and to say to(wards) [the] servant/slave who? [the] man this [the] to go: walk in/on/with land: country to/for to encounter: meet us and to say [the] servant/slave he/she/it lord my and to take: take [the] shawl and to cover
66 Mtumwa akamwambia Isaka mambo yote ambayo amefanya.
and to recount [the] servant/slave to/for Isaac [obj] all [the] word: thing which to make: do
67 Kisha Isaka akamleta katika hema ya Sara mama yake na akamchukua Rebeka, na akawa mke wake, na akampenda. Kwa hiyo Isaka akafarijika baada ya kifo cha mama yake.
and to come (in): bring her Isaac [the] tent [to] Sarah mother his and to take: marry [obj] Rebekah and to be to/for him to/for woman: wife and to love: lover her and to be sorry: comfort Isaac after mother his

< Mwanzo 24 >