< Mwanzo 24 >

1 Basi Abraham alikuwa mzee sana na Yahwe akawa amembariki katika mambo yote.
And Abraham he was old he had come in days and Yahweh he had blessed Abraham in everything.
2 Abraham akamwambia mtumwa wake, ambaye alikuwa mkubwa kuliko wote wa nyumbani mwake na mkuu wa vyote alivyo kuwa navyo.”Weka mkono wako chini ya paja langu
And he said Abraham to servant his old of household his who was ruling over all that [belonged] to him put please hand your under thigh my.
3 na nitakufanya uape kwa Yahwe, Mungu wa Mbingu na nchi, kwamba hutampatia mwanangu mke kutoka kwa mabinti wa Wakanaani, miongoni mwao wale nikaao kati yao.
So I may make swear you by Yahweh [the] God of the heavens and [the] God of the earth that not you will take a wife for son my from [the] daughters of the Canaanite[s] whom I [am] dwelling in midst its.
4 Lakini utakwenda kwenye nchi yangu, na kwa ndugu zangu, na kumtafutia mwanangu Isaka mke.”
For to land my and to kindred my you will go and you will take a wife for son my for Isaac.
5 Yule mtumwa wake akamwambia, “Itakuwaje ikiwa mwanamke hatakuwa tayari kufuatana nami hadi katika nchi hii? Je nitamrudisha mwanao katika nchi ambayo ulitoka?”
And he said to him the servant perhaps not she will be willing the woman to go after me to the land this ¿ really will I take back son your to the land where you came out from there.
6 Abraham akamwambia, “Hakikisha kwamba hutamrudisha mwanangu kule!
And he said to him Abraham take heed to yourself lest you should take back son my there towards.
7 Yahwe, Mungu wa mbingu, ambaye alinitoa mimi kutoka katika nyumba ya baba yangu na kutoka katika nchi ya ndugu zangu, na ambaye aliniahidia kwa kiapo maalumu akisema, 'Nitawapa uzao wako nchi hii,' atatuma malaika wake mbele yako, na utapata mke kwa ajili ya mwanangu kutoka huko.
Yahweh - [the] God of the heavens who he took me from [the] household of father my and from [the] land of kindred my and who he spoke to me and who he swore an oath to me saying to offspring your I will give the land this he he will send angel his before you and you will take a wife for son my from there.
8 Lakini ikiwa mwanamke hatakuwa tayari, ndipo utakuwa huru katika hiki kiapo changu. Cha muhimu tu ni kwamba usije ukamrudisha mwanangu huko.”
And if not she will be willing the woman to go after you and you will be free from oath my this only son my not you must take back there towards.
9 Kwa hiyo mtumwa akaweka mkono wake jini ya paja la Abraham bwana wake, na akaapa kuhusiana na jambo hili.
And he put the servant hand his under [the] thigh of Abraham master his and he swore an oath to him on the matter this.
10 Mtumwa akachukua ngamia kumi wa bwana wake na akaondoka. Akachukua pia aina zote za zawadi kutoka kwa bwana wake. Akaondoka na kwenda katika mkoa wa Aramu Naharaimu, mji wa Nahori.
And he took the servant ten camels from [the] camels of master his and he went and every good thing of master his [was] in hand his and he arose and he went to Aram Naharaim to [the] city of Nahor.
11 Akawapigisha magoti ngamia nje ya mji karibu na kisima cha maji. Ilikuwa jioni wakati ambao wanawake huenda kuchota maji.
And he made kneel the camels from [the] outside of the city to [the] well of the water to [the] time of evening to [the] time of [the] going out of the [women who] draw water.
12 Kisha akasema, “Yahwe, Mungu wa bwana wangu Abraham, anijalie kufanikiwa leo na aoneshe agano la uaminifu kwa bwana wangu Abraham.
And he said - O Yahweh [the] God of master my Abraham make happen please before me this day and do covenant loyalty with master my Abraham.
13 Tazama, nimesimama hapa karibu na chemchemi ya maji na binti za watu wa mji wanakuja kuteka maji.
Here! I [am] standing at [the] spring of the water and [the] daughters of [the] people of the city [are] coming out to draw water.
14 Na itokee hivi kwamba. Nikimwambia msichana, tafadhari tua mtungi wako ili niweze kunywa maji,' na akiniambia, 'Kunywa, na kwamba nitawanywesha ngamia wako pia,' huyo ndiye awe ambaye umemchagulia mtumwa wako Isaka. Kwa njia hii nitajua kuwa umeonesha agano la uaminifu kwa bwana wangu.”
And it will be the young woman whom I will say to her bend down please jar your so I may drink and she will say drink and also camels your I will give a drink to her you have appointed for servant your for Isaac and by it I will know that you have done covenant loyalty with master my.
15 Ikawa kwamba hata kabla hajamaliza kuzungumza, tazama, Rebeka akaja akiwa na mtungi wake wa maji begani mwake. Rebeka alizaliwa na Bethueli mwana wa Milka, mke wa Nahori, ndugu yake na Abraham.
And it was he not yet he had finished to speak and there! Rebekah [was] coming out who she had been born to Bethuel [the] son of Milcah [the] wife of Nahor [the] brother of Abraham and jar her [was] on shoulder her.
16 Msichana huyu alikuwa mzuri na alikuwa bikira. Hapana mwanaume aliye kuwa amekwisha lala naye. Akashuka kisimani na kuujaza mtungi wake, na kupanda juu.
And the young woman [was] good of appearance exceedingly a virgin and a man not he had known her and she went down the spring towards and she filled jar her and she came up.
17 Kisha mtumwa yule akakimbia kumlaki yule msichana, na kusema, “Tafadhari nipatie maji kidogo ya kunywa kutoka katika mtungi wako.”
And he ran the servant to meet her and he said give to drink me please a little of water from jar your.
18 Akasema, “kunywa tafadhari bwana wangu,” na kwa haraka akatua mtungi wake juu ya mkono wake, na akampatia maji ya kunywa.
And she said drink O lord my and she hurried and she put down jar her on hand her and she gave a drink him.
19 Alipokuwa amemaliza kumpatia maji, akasema, “Nitachota maji kwa ajili ya ngamia wako pia, mpaka watakapomaliza kunywa.”
And she finished to give a drink him and she said also for camels your I will draw water until they have finished to drink.
20 Hivyo akaharakisha akamwaga maji yaliyokuwa mtungini kwenye chombo cha kunywshea mifugo, kisha akakimbia tena kisimani kuchota maji, na kuwanywesha ngamia wake wote.
And she hurried and she emptied jar her into the watering channel and she ran again to the well to draw water and she drew water for all camels his.
21 Yule mtu akamtazama msichana akiwa kimya kuona kama Yahwe amefanikisha njia yake au la.
And the man [was] gazing to her being silent to know ¿ had he made successful Yahweh journey his or? not.
22 Ngamia walipomaliza kunywa maji, yule mtu akaleta pete ya pua ya dhahabu yenye uzito wa nusu shekeli, na bangili mbili za dhahabu kwa ajili ya mikono yake zenye uzito wa shekeli kumi,
And it was just as they had finished the camels to drink and he took the man a ring of gold [was] a beka weight its and two bracelets on hands her [was] ten of gold weight their.
23 akamuuliza, “wewe ni binti wa nani? Niambie tafadhali, Je kuna nafasi nyumbani mwa baba yako kwa ajili yetu kupumzika usiku?”
And he said daughter of whom? [are] you tell please to me ¿ [is] there [the] house of father your room for us to stay [the] night.
24 Akamwambia, “Mimi ni binti wa Bethueli mwana wa Milka, ambaye alimzaa kwa Nahori.”
And she said to him [am] [the] daughter of Bethuel I [the] son of Milcah whom she bore to Nahor.
25 Akasema pia, “Tunayo malisho tele na chakula, na iko nafasi kwa ajili yako kulala usiku.”
And she said to him both straw as well as fodder much which [is] with us also room to stay [the] night.
26 Kisha yume mtu akainama chini na kumwabudu Yahwe.
And he bowed low the man and he bowed down to Yahweh.
27 Akasema, “Abarikiwe Yahwe, Mungu wa bwana wangu Abraham, ambaye hakuacha agano lake la uaminifu na kweli yake mbele ya bwana wangu. Kwa vile Yahwe ameniongoza moja kwa moja kwenye nyumba ya ndugu zake bwana wangu.”
And he said [be] blessed Yahweh [the] God of master my Abraham who not he has left covenant loyalty his and faithfulness his from with master my I on the journey he has led me Yahweh [the] house of [the] relatives of master my.
28 Kisha yule msichana akakimbia na kwenda kuwaeleza watu wa nyumba ya mama yake juu ya mambo yote haya.
And she ran the young woman and she told to [the] household of mother her according to the things these.
29 Na sasa Rebeka alikuwa na kaka yake, jina lake aliitwa Labani. Labani akakimbia kwa yule mtu aliye kuwa nje barabarani karibu na kisima.
And [belonged] to Rebekah a brother and name his [was] Laban and he ran Laban to the man the outside towards to the spring.
30 Akisha kuona hereni ya puani pamoja na zile bangili kwenye mikono ya dada yake, na kusikia maneno ya Rebeka dada yake, “Hivi ndivyo yule mtu alicho niambia,” alikwenda kwa yule mtu, na, Tazama, alikuwa amesimama karibu na ngamia pale kisimani.
And it was - when saw the ring and the bracelets on [the] hands of sister his and just as heard he [the] words of Rebekah sister his saying thus he spoke to me the man and he went to the man and there! [he was] standing with the camels at the spring.
31 Labani akasema, “Njoo, wewe uliye barikiwa na Yahwe. Kwa nini umesimama nje? nimekwisha andaa nyumba, pamoja na mahali kwa ajili ya ngamia.”
And he said come O [one] blessed of Yahweh why? are you standing on the outside and I I have made clear the house and a place for the camels.
32 Kwa hiyo yule mtu akaingia ndani ya nyumba na akashusha mizigo kutoka kwa wale ngamia. Ngamia wakapatiwa malisho na chakula, na maji yakatolewa kuosha miguu yake pamoja na miguu ya wale watu aliokuwa pamoja nao.
And he went the man the house towards and he unharnessed the camels and he gave straw and fodder to the camels and water to wash feet his and [the] feet of the men who [were] with him.
33 Wakaandaa chakula mbele yake ale, lakini akasema, “Sitakula mpaka niseme kile ninacho paswa kusema.” Kwa hiyo Labani akmwambia, “Sema.”
(And it was put *Q(K)*) before him to eat and he said not I will eat until I have spoken words my and he said speak.
34 Akasema, “Mimi ni mtumwa wa Abraham.
And he said [am] [the] servant of Abraham I.
35 Yahwe amembariki sana bwana wangu na amekuwa mtu mkuu. Amempatia mifugo na makundi ya wanyama, fedha, dhahabu, watumwa wa kiume na watumwa wa kike, pamoja na ngamia na punda.
And Yahweh he has blessed master my exceedingly and he has become great and he has given to him sheep and cattle and silver and gold and [male] servants and female servants and camels and donkeys.
36 Sara, mke wa bwana wangu, alimzalia mwana bwana wangu alipokuwa mzee, na amempatia mwanawe kila kitu anachomiliki.
And she has borne Sarah [the] wife of master my a son to master my after old age her and he has given to him all that [belongs] to him.
37 Bwana wangu aliniapisha, akisema, “Usije ukampatia mwanangu mke kutoka kwa mabinti wa Wakanaani, ambao kwao nimefanya makazi.
And he made swear an oath me master my saying not (you must take *LA(bh)*) a wife for son my from [the] daughters of the Canaanite[s] whom I [am] dwelling in land its.
38 Badala yake, lazima uende kwa familia ya baba yangu, na kwa ndugu zangu, na kupata mke kwa ajili ya mwanangu.'
If not to [the] house of father my you will go and to family my and you will take a wife for son my.
39 Nikamwambia bwana wangu, pengine mwanamke huyo asikubali kufuatana nami.'
And I said to master my perhaps not she will go the woman after me.
40 Lakini akaniambia, Yahwe, ambaye ninakwenda mbele yake, atatuma malaika wake pamoja nawe na atakufanikisha njia yako, kwamba utapata mke kwa ajili ya mwangu kutoka miongoni mwa ndugu zangu na kutoka katika ukoo wa baba yangu.
And he said to me Yahweh whom I have walked about before him he will send angel his with you and he will make successful journey your and you will take a wife for son my from family my and from [the] household of father my.
41 Lakini utakuwa huru katika kiapo changu ikiwa utafika kwa ndugu zangu na wasikuruhusu kuja naye. Ndipo utakuwa huru katika kiapo changu.
Then you will be free from oath my for you will go to family my and if not they will give [her] to you and you will be free from oath my.
42 Hivyo nimefika leo kisimani, na nikasema, 'O Yahwe, Mungu wa bwana wangu Abraham, tafadhari, ikiwa kweli umekusudia kuifanya safari yangu kuwa yenye kufanikiwa -
And I came this day to the spring and I said O Yahweh [the] God of master my Abraham if [are] there you please [are] making successful journey my which I [am] going on it.
43 tazama niko hapa nimesimama karibu na kisima cha maji - na iwe kwamba binti ajaye kuchota maji, nitakaye mwambia, “Tafadhari unipatie maji kidoka kutoka kwenye mtungi wako ninywe,” mwanamke atakaye niabia,
Here! I [am] standing at [the] spring of the water and it will be the young woman who will come out to draw water and I will say to her give to drink me please a little of water from jar your.
44 “Kunywa, na nitakuchotea pia maji kwa ajili ya ngamia wako” - na awe ndiye ambaye wewe Yahwe, umemchagulia mtoto wa bwana wangu.”
And she will say to me both you drink and also for camels your I will draw water she [be] the woman whom he has appointed Yahweh for [the] son of master my.
45 Ikawa hata kabla sijamaliza kuzungumza moyoni mwangu, Tazama, Rebeka akaja na mtungi wake juu ya bega lake akashuka chini kisimani akachota maji. Hivyo nikamwambia, 'Tafadhari nipatie maji ninywe.'
I not yet I had finished to speak to heart my and there! Rebekah [was] coming out and jar her [was] on shoulder her and she went down the spring towards and she drew water and I said to her give a drink me please.
46 Ndipo kwa haraka alipoushusha mtungi wake begani mwake na akasema, 'Kunywa, na pia nitawapatia maji ngamia wak.' Kwa hiyo nikanywa, na akawanywesha ngamia pia.
And she hurried and she put down jar her from on her and she said drink and also camels your I will give a drink to and I drank and also the camels she gave a drink.
47 Nikamuuliza na kusema, 'Wewe ni binti wa nani?' Akasema, 'Binti wa Bethueli, Mwana wa Nahori, ambaye Milka alizaa kwake.' Kisha nikamwekea pete puani mwake pamoja na bangili mikononi mwake.
And I asked her and I said daughter of whom? [are] you and she said [the] daughter of Bethuel [the] son of Nahor whom she bore to him Milcah and I put the ring on nose her and the bracelets on hands her.
48 Kisha nikainama chini nikamwabudu Yahwe, na kumbariki Yahwe, Mungu wa bwana wangu Abraham, ambaye ameniongoza katika njia sahihi kumpata binti wa ndugu za bwana wangu kwa ajili ya mwanawe.
And I bowed low and I bowed down to Yahweh and I blessed Yahweh [the] God of master my Abraham who he had led me in [the] way of truth to take [the] daughter of [the] brother of master my for son his.
49 Kwa hiyo, ikiwa mko tayari kumfanyia rehema na kweli, niambieni. Lakini kama sivyo, niambieni, ili kwamba niweze kwenda upande wa kulia, au kushoto.”
And now if [are] there you doing loyalty and faithfulness with master my tell to me and if not tell to me so I may turn to right or to left.
50 Ndipo Labani na Bethueli wakajibu na kusema, “Jambo hili limetoka kwa Yahwe; hatuwezi kusema kwako aidha neno baya au zuri.
And he answered Laban and Bethuel and they said from Yahweh it has come out the matter not we are able to speak to you evil or good.
51 Tazama, Rebeka yu mbele yako. Mchukue na uende, ili awe mke wa mtoto wa bwana wako, kama Yahwe alivyosema.”
Here! Rebekah [is] before you take [her] and go so may she be a wife for [the] son of master your just as he has spoken Yahweh.
52 Mtumwa wa Abraham aliposikia maneno yao, akainama mwenyewe chini ardhini kwa Yahwe.
And it was just as he heard [the] servant of Abraham words their and he bowed down [the] ground towards to Yahweh.
53 Mtumwa akaleta vipande vya fedha na vipande vya dhahabu, na nguo, akampatia Rebeka. Akampatia pia kaka yake na mama yake zawadi zenye thamani.
And he brought out the servant articles of silver and articles of gold and garments and he gave [them] to Rebekah and precious gifts he gave to brother her and to mother her.
54 Kisha yeye na watu aliokuwa nao wakala na kunywa. wakakaa pale mpaka usiku, na walipoamka asubuhi, akasema, Niruhusuni niende kwa bwana wangu.”
And they ate and they drank he and the men who [were] with him and they stayed [the] night and they arose in the morning and he said send away me to master my.
55 Kaka yake na mama yake wakasema, mwache binti abaki nasi kwa siku chache zingine, angalau siku kumi. baada ya hapo anaweza kwenda.”
And he said brother her and mother her let her remain the young woman with us days or ten (after *L(S)*) she will go.
56 Lakini akawambia, msinizuie, kwa kuwa Yahwe amefanikisha njia yangu. Niruhusuni niende kwa bwana wangu.”
And he said to them may not you delay me and Yahweh he has made successful journey my send away me so let me go to master my.
57 Wakasema, “Tutamwita binti na kumuuliza.”
And they said let us summon the young woman and let us ask mouth her.
58 Kwa hiyo wakamwita Rebeka na kumuuliza, “Je utakwenda na mtu huyu?” Akajibu, “Nitakwenda.”
And they summoned Rebekah and they said to her ¿ will you go with the man this and she said I will go.
59 Kwa hiyo wakampeleka dada yao Rebeka, pamoja na watumishi wake wa kike, kwenda njiani pamoja na mtumishi wa Abraham na watu wake.
And they sent away Rebekah sister their and suckling-nurse her and [the] servant of Abraham and men his.
60 Wakambarikia Rebeka, na wakamwambia, “Ndugu yetu, na uwe mama wa maelfu na wa makumi elfu, uzao wako upate kumiliki lango la wale wanao wachukia.”
And they blessed Rebekah and they said to her O sister our you become thousands of ten thousand so may it take possession of offspring your [the] gate of [those who] hate it.
61 Kisha Rebeka akasimama, yeye na watumishi wake kwa hesabu ya ngamia, na wakamfuata yule mtu. Hivyo watumishi wakamchukua Rebeka, na wakaenda zao.
And she arose Rebekah and maids her and they rode on the camels and they went after the man and he took the servant Rebekah and he went.
62 Nyakati hizo Isaka alikuwa anakaa katika Negebu, na alikuwa tu amerejea kutoka Beerlahairoi.
And Isaac he came from going Beer Lahai Roi and he [was] dwelling in [the] land of the Negev.
63 Isaka akaenda kutafakari shambani jioni. Alipotazama akaona, natazama, kulikuwa na ngamia wakija!
And he went out Isaac to meditate in the field to [the] turning of evening and he lifted up eyes his and he saw and there! camels [were] coming.
64 Rebeka akatazama na alipomwona Isaka, akaruka kutoka kwenye ngamia.
And she lifted up Rebekah eyes her and she saw Isaac and she fell from on the camel.
65 Akamwambia mtumwa, “mtu huyo ni nani anaye tembea shambani akija kutupokea?” Mtumwa akasema, “Ni bwana wangu.” Hivyo Rebeka akachukua shela yake akajifunika.
And she said to the servant who? [is] the man this who is walking in the field to meet us and he said the servant it [is] master my and she took the veil and she covered herself.
66 Mtumwa akamwambia Isaka mambo yote ambayo amefanya.
And he recounted the servant to Isaac all the things which he had done.
67 Kisha Isaka akamleta katika hema ya Sara mama yake na akamchukua Rebeka, na akawa mke wake, na akampenda. Kwa hiyo Isaka akafarijika baada ya kifo cha mama yake.
And he brought her Isaac the tent of towards Sarah mother his and he took Rebekah and she became of him a wife and he loved her and he was comforted Isaac after mother his.

< Mwanzo 24 >