< Mwanzo 24 >

1 Basi Abraham alikuwa mzee sana na Yahwe akawa amembariki katika mambo yote.
And Abraham [is] old, he has entered into days, and YHWH has blessed Abraham in all [things];
2 Abraham akamwambia mtumwa wake, ambaye alikuwa mkubwa kuliko wote wa nyumbani mwake na mkuu wa vyote alivyo kuwa navyo.”Weka mkono wako chini ya paja langu
and Abraham says to his servant, the eldest of his house, who is ruling over all that he has, “Please put your hand under my thigh,
3 na nitakufanya uape kwa Yahwe, Mungu wa Mbingu na nchi, kwamba hutampatia mwanangu mke kutoka kwa mabinti wa Wakanaani, miongoni mwao wale nikaao kati yao.
and I cause you to swear by YHWH, God of the heavens and God of the earth, that you do not take a wife for my son from the daughters of the Canaanite, in the midst of whom I am dwelling;
4 Lakini utakwenda kwenye nchi yangu, na kwa ndugu zangu, na kumtafutia mwanangu Isaka mke.”
but to my land and to my family you go, and have taken a wife for my son, for Isaac.”
5 Yule mtumwa wake akamwambia, “Itakuwaje ikiwa mwanamke hatakuwa tayari kufuatana nami hadi katika nchi hii? Je nitamrudisha mwanao katika nchi ambayo ulitoka?”
And the servant says to him, “It may be the woman is not willing to come after me to this land; do I at all cause your son to return to the land from where you came out?”
6 Abraham akamwambia, “Hakikisha kwamba hutamrudisha mwanangu kule!
And Abraham says to him, “Take heed to yourself lest you cause my son to return there;
7 Yahwe, Mungu wa mbingu, ambaye alinitoa mimi kutoka katika nyumba ya baba yangu na kutoka katika nchi ya ndugu zangu, na ambaye aliniahidia kwa kiapo maalumu akisema, 'Nitawapa uzao wako nchi hii,' atatuma malaika wake mbele yako, na utapata mke kwa ajili ya mwanangu kutoka huko.
YHWH, God of the heavens, who has taken me from the house of my father, and from the land of my birth, and who has spoken to me, and who has sworn to me, saying, To your seed I give this land, He sends His messenger before you, and you have taken a wife for my son from there;
8 Lakini ikiwa mwanamke hatakuwa tayari, ndipo utakuwa huru katika hiki kiapo changu. Cha muhimu tu ni kwamba usije ukamrudisha mwanangu huko.”
and if the woman is not willing to come after you, then you have been acquitted from this my oath: only you do not cause my son to return there.”
9 Kwa hiyo mtumwa akaweka mkono wake jini ya paja la Abraham bwana wake, na akaapa kuhusiana na jambo hili.
And the servant puts his hand under the thigh of Abraham his lord, and swears to him concerning this matter.
10 Mtumwa akachukua ngamia kumi wa bwana wake na akaondoka. Akachukua pia aina zote za zawadi kutoka kwa bwana wake. Akaondoka na kwenda katika mkoa wa Aramu Naharaimu, mji wa Nahori.
And the servant takes ten camels of the camels of his lord and goes, also of all the goods of his lord in his hand, and he rises, and goes to Aram-Naharaim, to the city of Nahor;
11 Akawapigisha magoti ngamia nje ya mji karibu na kisima cha maji. Ilikuwa jioni wakati ambao wanawake huenda kuchota maji.
and he causes the camels to kneel at the outside of the city, at the well of water, at evening, at the time of the coming out of the women who draw water.
12 Kisha akasema, “Yahwe, Mungu wa bwana wangu Abraham, anijalie kufanikiwa leo na aoneshe agano la uaminifu kwa bwana wangu Abraham.
And he says, “YHWH, God of my lord Abraham, please cause to meet before me this day—(and do kindness with my lord Abraham;
13 Tazama, nimesimama hapa karibu na chemchemi ya maji na binti za watu wa mji wanakuja kuteka maji.
behold, I am standing by the fountain of water, and daughters of the men of the city are coming out to draw water;
14 Na itokee hivi kwamba. Nikimwambia msichana, tafadhari tua mtungi wako ili niweze kunywa maji,' na akiniambia, 'Kunywa, na kwamba nitawanywesha ngamia wako pia,' huyo ndiye awe ambaye umemchagulia mtumwa wako Isaka. Kwa njia hii nitajua kuwa umeonesha agano la uaminifu kwa bwana wangu.”
and it has been, the young person to whom I say, Please incline your pitcher and I drink, and she has said, Drink, and I also water your camels)—her [whom] You have decided for Your servant, for Isaac; and by it I know that You have done kindness with my lord.”
15 Ikawa kwamba hata kabla hajamaliza kuzungumza, tazama, Rebeka akaja akiwa na mtungi wake wa maji begani mwake. Rebeka alizaliwa na Bethueli mwana wa Milka, mke wa Nahori, ndugu yake na Abraham.
And it comes to pass, before he has finished speaking, that behold, Rebekah (who was born to Bethuel, son of Milcah, wife of Nahor, brother of Abraham) is coming out, and her pitcher on her shoulder,
16 Msichana huyu alikuwa mzuri na alikuwa bikira. Hapana mwanaume aliye kuwa amekwisha lala naye. Akashuka kisimani na kuujaza mtungi wake, na kupanda juu.
and the young person [is] of very good appearance, a virgin, and a man has not known her; and she goes down to the fountain, and fills her pitcher, and comes up.
17 Kisha mtumwa yule akakimbia kumlaki yule msichana, na kusema, “Tafadhari nipatie maji kidogo ya kunywa kutoka katika mtungi wako.”
And the servant runs to meet her and says, “Please let me swallow a little water from your pitcher”;
18 Akasema, “kunywa tafadhari bwana wangu,” na kwa haraka akatua mtungi wake juu ya mkono wake, na akampatia maji ya kunywa.
and she says, “Drink, my lord”; and she hurries, and lets down her pitcher on her hand, and gives him drink.
19 Alipokuwa amemaliza kumpatia maji, akasema, “Nitachota maji kwa ajili ya ngamia wako pia, mpaka watakapomaliza kunywa.”
And she finishes giving him drink and says, “Also for your camels I draw until they have finished drinking”;
20 Hivyo akaharakisha akamwaga maji yaliyokuwa mtungini kwenye chombo cha kunywshea mifugo, kisha akakimbia tena kisimani kuchota maji, na kuwanywesha ngamia wake wote.
and she hurries, and empties her pitcher into the drinking-trough, and runs again to the well to draw, and draws for all his camels.
21 Yule mtu akamtazama msichana akiwa kimya kuona kama Yahwe amefanikisha njia yake au la.
And the man, wondering at her, remains silent, to know whether YHWH has made his way prosperous or not.
22 Ngamia walipomaliza kunywa maji, yule mtu akaleta pete ya pua ya dhahabu yenye uzito wa nusu shekeli, na bangili mbili za dhahabu kwa ajili ya mikono yake zenye uzito wa shekeli kumi,
And it comes to pass, when the camels have finished drinking, that the man takes a golden ring (whose weight [is] a bekah), and two bracelets for her hands (whose weight [is] ten [bekahs] of gold),
23 akamuuliza, “wewe ni binti wa nani? Niambie tafadhali, Je kuna nafasi nyumbani mwa baba yako kwa ajili yetu kupumzika usiku?”
and says, “Whose daughter [are] you? Please declare to me, is the house of your father a place for us to lodge in?”
24 Akamwambia, “Mimi ni binti wa Bethueli mwana wa Milka, ambaye alimzaa kwa Nahori.”
And she says to him, “I [am] daughter of Bethuel, son of Milcah, whom she has borne to Nahor.”
25 Akasema pia, “Tunayo malisho tele na chakula, na iko nafasi kwa ajili yako kulala usiku.”
She also says to him, “Both straw and provender [are] abundant with us, also a place to lodge in.”
26 Kisha yume mtu akainama chini na kumwabudu Yahwe.
And the man bows, and pays respect to YHWH,
27 Akasema, “Abarikiwe Yahwe, Mungu wa bwana wangu Abraham, ambaye hakuacha agano lake la uaminifu na kweli yake mbele ya bwana wangu. Kwa vile Yahwe ameniongoza moja kwa moja kwenye nyumba ya ndugu zake bwana wangu.”
and says, “Blessed [is] YHWH, God of my lord Abraham, who has not left off His kindness and His truth with my lord—I [being] in the way, YHWH has led me to the house of my lord’s brothers.”
28 Kisha yule msichana akakimbia na kwenda kuwaeleza watu wa nyumba ya mama yake juu ya mambo yote haya.
And the young person runs, and declares to the house of her mother according to these words.
29 Na sasa Rebeka alikuwa na kaka yake, jina lake aliitwa Labani. Labani akakimbia kwa yule mtu aliye kuwa nje barabarani karibu na kisima.
And Rebekah has a brother, and his name [is] Laban, and Laban runs to the man who [is] outside, to the fountain;
30 Akisha kuona hereni ya puani pamoja na zile bangili kwenye mikono ya dada yake, na kusikia maneno ya Rebeka dada yake, “Hivi ndivyo yule mtu alicho niambia,” alikwenda kwa yule mtu, na, Tazama, alikuwa amesimama karibu na ngamia pale kisimani.
indeed, it comes to pass, when he sees the ring, and the bracelets on the hands of his sister, and when he hears the words of his sister Rebekah, saying, “Thus has the man spoken to me,” that he comes to the man, and behold, he is standing by the camels by the fountain.
31 Labani akasema, “Njoo, wewe uliye barikiwa na Yahwe. Kwa nini umesimama nje? nimekwisha andaa nyumba, pamoja na mahali kwa ajili ya ngamia.”
And he says, “Come in, O blessed one of YHWH! Why do you stand outside—and I have prepared the house and place for the camels?”
32 Kwa hiyo yule mtu akaingia ndani ya nyumba na akashusha mizigo kutoka kwa wale ngamia. Ngamia wakapatiwa malisho na chakula, na maji yakatolewa kuosha miguu yake pamoja na miguu ya wale watu aliokuwa pamoja nao.
And he brings in the man into the house, and looses the camels, and gives straw and provender for the camels, and water to wash his feet, and the feet of the men who [are] with him:
33 Wakaandaa chakula mbele yake ale, lakini akasema, “Sitakula mpaka niseme kile ninacho paswa kusema.” Kwa hiyo Labani akmwambia, “Sema.”
and sets before him to eat; but he says, “I do not eat until I have spoken my word”; and he says, “Speak.”
34 Akasema, “Mimi ni mtumwa wa Abraham.
And he says, “I [am] Abraham’s servant;
35 Yahwe amembariki sana bwana wangu na amekuwa mtu mkuu. Amempatia mifugo na makundi ya wanyama, fedha, dhahabu, watumwa wa kiume na watumwa wa kike, pamoja na ngamia na punda.
and YHWH has blessed my lord exceedingly, and he is great; and He gives to him flock, and herd, and silver, and gold, and menservants, and maidservants, and camels, and donkeys;
36 Sara, mke wa bwana wangu, alimzalia mwana bwana wangu alipokuwa mzee, na amempatia mwanawe kila kitu anachomiliki.
and Sarah, my lord’s wife, bears a son to my lord, after she has been aged, and he gives to him all that he has.
37 Bwana wangu aliniapisha, akisema, “Usije ukampatia mwanangu mke kutoka kwa mabinti wa Wakanaani, ambao kwao nimefanya makazi.
And my lord causes me to swear, saying, You do not take a wife to my son from the daughters of the Canaanite, in whose land I am dwelling.
38 Badala yake, lazima uende kwa familia ya baba yangu, na kwa ndugu zangu, na kupata mke kwa ajili ya mwanangu.'
If not—to the house of my father you go, and to my family, and you have taken a wife for my son.
39 Nikamwambia bwana wangu, pengine mwanamke huyo asikubali kufuatana nami.'
And I say to my lord, It may be the woman does not come after me;
40 Lakini akaniambia, Yahwe, ambaye ninakwenda mbele yake, atatuma malaika wake pamoja nawe na atakufanikisha njia yako, kwamba utapata mke kwa ajili ya mwangu kutoka miongoni mwa ndugu zangu na kutoka katika ukoo wa baba yangu.
and he says to me, YHWH, before whom I have habitually walked, sends His messenger with you, and has prospered your way, and you have taken a wife for my son from my family, and from the house of my father;
41 Lakini utakuwa huru katika kiapo changu ikiwa utafika kwa ndugu zangu na wasikuruhusu kuja naye. Ndipo utakuwa huru katika kiapo changu.
then you are acquitted from my oath, when you come to my family; and if they do not give [one] to you, then you have been acquitted from my oath.
42 Hivyo nimefika leo kisimani, na nikasema, 'O Yahwe, Mungu wa bwana wangu Abraham, tafadhari, ikiwa kweli umekusudia kuifanya safari yangu kuwa yenye kufanikiwa -
And I come to the fountain today, and I say, YHWH, God of my lord Abraham, now if You are making prosperous my way in which I am going—
43 tazama niko hapa nimesimama karibu na kisima cha maji - na iwe kwamba binti ajaye kuchota maji, nitakaye mwambia, “Tafadhari unipatie maji kidoka kutoka kwenye mtungi wako ninywe,” mwanamke atakaye niabia,
(behold, I am standing by the fountain of water), then the virgin is coming out to draw, and I have said to her, Please let me drink a little water from your pitcher,
44 “Kunywa, na nitakuchotea pia maji kwa ajili ya ngamia wako” - na awe ndiye ambaye wewe Yahwe, umemchagulia mtoto wa bwana wangu.”
and she has said to me, Both drink, and I also draw for your camels—she is the woman whom YHWH has decided for my lord’s son.
45 Ikawa hata kabla sijamaliza kuzungumza moyoni mwangu, Tazama, Rebeka akaja na mtungi wake juu ya bega lake akashuka chini kisimani akachota maji. Hivyo nikamwambia, 'Tafadhari nipatie maji ninywe.'
Before I finish speaking to my heart, then behold, Rebekah is coming out, and her pitcher [is] on her shoulder, and she goes down to the fountain and draws; and I say to her, Please let me drink,
46 Ndipo kwa haraka alipoushusha mtungi wake begani mwake na akasema, 'Kunywa, na pia nitawapatia maji ngamia wak.' Kwa hiyo nikanywa, na akawanywesha ngamia pia.
and she hurries and lets down her pitcher from off her and says, Drink, and I also water your camels; and I drink, and she has also watered the camels.
47 Nikamuuliza na kusema, 'Wewe ni binti wa nani?' Akasema, 'Binti wa Bethueli, Mwana wa Nahori, ambaye Milka alizaa kwake.' Kisha nikamwekea pete puani mwake pamoja na bangili mikononi mwake.
And I ask her, and say, Whose daughter [are] you? And she says, Daughter of Bethuel, son of Nahor, whom Milcah has borne to him, and I put the ring on her nose, and the bracelets on her hands,
48 Kisha nikainama chini nikamwabudu Yahwe, na kumbariki Yahwe, Mungu wa bwana wangu Abraham, ambaye ameniongoza katika njia sahihi kumpata binti wa ndugu za bwana wangu kwa ajili ya mwanawe.
and I bow, and pay respect before YHWH, and I bless YHWH, God of my lord Abraham, who has led me in the true way to receive the daughter of my lord’s brother for his son.
49 Kwa hiyo, ikiwa mko tayari kumfanyia rehema na kweli, niambieni. Lakini kama sivyo, niambieni, ili kwamba niweze kwenda upande wa kulia, au kushoto.”
And now, if you are dealing kindly and truly with my lord, declare to me; and if not, declare to me; and I turn to the right or to the left.”
50 Ndipo Labani na Bethueli wakajibu na kusema, “Jambo hili limetoka kwa Yahwe; hatuwezi kusema kwako aidha neno baya au zuri.
And Laban answers—Bethuel also—and they say, “The thing has gone out from YHWH; we are not able to speak to you bad or good;
51 Tazama, Rebeka yu mbele yako. Mchukue na uende, ili awe mke wa mtoto wa bwana wako, kama Yahwe alivyosema.”
behold, Rebekah [is] before you, take and go, and she is a wife to your lord’s son, as YHWH has spoken.”
52 Mtumwa wa Abraham aliposikia maneno yao, akainama mwenyewe chini ardhini kwa Yahwe.
And it comes to pass, when the servant of Abraham has heard their words, that he bows himself toward the earth before YHWH;
53 Mtumwa akaleta vipande vya fedha na vipande vya dhahabu, na nguo, akampatia Rebeka. Akampatia pia kaka yake na mama yake zawadi zenye thamani.
and the servant takes out vessels of silver, and vessels of gold, and garments, and gives to Rebekah; precious things also he has given to her brother and to her mother.
54 Kisha yeye na watu aliokuwa nao wakala na kunywa. wakakaa pale mpaka usiku, na walipoamka asubuhi, akasema, Niruhusuni niende kwa bwana wangu.”
And they eat and drink, he and the men who [are] with him, and lodge all night; and they rise in the morning, and he says, “Send me to my lord”;
55 Kaka yake na mama yake wakasema, mwache binti abaki nasi kwa siku chache zingine, angalau siku kumi. baada ya hapo anaweza kwenda.”
and her brother says—her mother also, “Let the young person abide with us a week or ten days, afterward she goes.”
56 Lakini akawambia, msinizuie, kwa kuwa Yahwe amefanikisha njia yangu. Niruhusuni niende kwa bwana wangu.”
And he says to them, “Do not delay me, seeing YHWH has prospered my way; send me away, and I go to my lord”;
57 Wakasema, “Tutamwita binti na kumuuliza.”
and they say, “Let us call for the young person, and inquire of her mouth”;
58 Kwa hiyo wakamwita Rebeka na kumuuliza, “Je utakwenda na mtu huyu?” Akajibu, “Nitakwenda.”
and they call for Rebekah, and say to her, “Do you go with this man?” And she says, “I go.”
59 Kwa hiyo wakampeleka dada yao Rebeka, pamoja na watumishi wake wa kike, kwenda njiani pamoja na mtumishi wa Abraham na watu wake.
And they send away their sister Rebekah, and her nurse, and Abraham’s servant, and his men;
60 Wakambarikia Rebeka, na wakamwambia, “Ndugu yetu, na uwe mama wa maelfu na wa makumi elfu, uzao wako upate kumiliki lango la wale wanao wachukia.”
and they bless Rebekah, and say to her, “You [are] our sister; become thousands of myriads, and your seed possesses the gate of those hating it.”
61 Kisha Rebeka akasimama, yeye na watumishi wake kwa hesabu ya ngamia, na wakamfuata yule mtu. Hivyo watumishi wakamchukua Rebeka, na wakaenda zao.
And Rebekah and her young women arise, and ride on the camels, and go after the man; and the servant takes Rebekah and goes.
62 Nyakati hizo Isaka alikuwa anakaa katika Negebu, na alikuwa tu amerejea kutoka Beerlahairoi.
And Isaac has come in from the entrance of the Well of the Living One, my Beholder; and he is dwelling in the land of the south,
63 Isaka akaenda kutafakari shambani jioni. Alipotazama akaona, natazama, kulikuwa na ngamia wakija!
and Isaac goes out to meditate in the field, at the turning of the evening, and he lifts up his eyes, and looks, and behold, camels are coming.
64 Rebeka akatazama na alipomwona Isaka, akaruka kutoka kwenye ngamia.
And Rebekah lifts up her eyes, and sees Isaac, and comes down off the camel;
65 Akamwambia mtumwa, “mtu huyo ni nani anaye tembea shambani akija kutupokea?” Mtumwa akasema, “Ni bwana wangu.” Hivyo Rebeka akachukua shela yake akajifunika.
and she says to the servant, “Who [is] this man who is walking in the field to meet us?” And the servant says, “It [is] my lord”; and she takes the veil, and covers herself.
66 Mtumwa akamwambia Isaka mambo yote ambayo amefanya.
And the servant recounts to Isaac all the things that he has done,
67 Kisha Isaka akamleta katika hema ya Sara mama yake na akamchukua Rebeka, na akawa mke wake, na akampenda. Kwa hiyo Isaka akafarijika baada ya kifo cha mama yake.
and Isaac brings her into the tent of his mother Sarah, and he takes Rebekah, and she becomes his wife, and he loves her, and Isaac is comforted after [the death of] his mother.

< Mwanzo 24 >