< Mwanzo 24 >

1 Basi Abraham alikuwa mzee sana na Yahwe akawa amembariki katika mambo yote.
Og Abraham var gammel, vel ved Alder, og Herren havde velsignet Abraham i alting.
2 Abraham akamwambia mtumwa wake, ambaye alikuwa mkubwa kuliko wote wa nyumbani mwake na mkuu wa vyote alivyo kuwa navyo.”Weka mkono wako chini ya paja langu
Og Abraham sagde til sin ældste Svend i sit Hus, som raadede over alt hans Gods: Kære, læg din Haand under min Lænd,
3 na nitakufanya uape kwa Yahwe, Mungu wa Mbingu na nchi, kwamba hutampatia mwanangu mke kutoka kwa mabinti wa Wakanaani, miongoni mwao wale nikaao kati yao.
og jeg vil lade dig sværge ved Herren, Himmelens Gud og Jordens Gud, at du ikke skal tage min Søn en Hustru af Kananiternes Døtre, iblandt hvilke jeg bor;
4 Lakini utakwenda kwenye nchi yangu, na kwa ndugu zangu, na kumtafutia mwanangu Isaka mke.”
men du skal gaa til mit Land og til min Slægt og tage min Søn Isak en Hustru.
5 Yule mtumwa wake akamwambia, “Itakuwaje ikiwa mwanamke hatakuwa tayari kufuatana nami hadi katika nchi hii? Je nitamrudisha mwanao katika nchi ambayo ulitoka?”
Og Svenden sagde til ham: Maaske Kvinden ikke vil drage med mig til dette Land; skal jeg da vel føre din Søn tilbage til det Land, som du er kommen fra?
6 Abraham akamwambia, “Hakikisha kwamba hutamrudisha mwanangu kule!
Og Abraham sagde til ham: Forvar dig, at du ikke fører min Søn did igen.
7 Yahwe, Mungu wa mbingu, ambaye alinitoa mimi kutoka katika nyumba ya baba yangu na kutoka katika nchi ya ndugu zangu, na ambaye aliniahidia kwa kiapo maalumu akisema, 'Nitawapa uzao wako nchi hii,' atatuma malaika wake mbele yako, na utapata mke kwa ajili ya mwanangu kutoka huko.
Herren, Himmelens Gud, som tog mig fra min Faders Hus og fra min Slægts Land, og som talede med mig, og som tilsvor mig og sagde: dette Land vil jeg give din Sæd, han skal sende sin Engel for dig, at du skal tage min Søn en Hustru derfra.
8 Lakini ikiwa mwanamke hatakuwa tayari, ndipo utakuwa huru katika hiki kiapo changu. Cha muhimu tu ni kwamba usije ukamrudisha mwanangu huko.”
Men dersom Kvinden ikke vil følge dig, da skal du være fri for denne min Ed; ikkun min Søn skal du ikke føre derhen.
9 Kwa hiyo mtumwa akaweka mkono wake jini ya paja la Abraham bwana wake, na akaapa kuhusiana na jambo hili.
Da lagde Svenden sin Haand under Abrahams, sin Herres, Lænd og tilsvor ham om denne Sag.
10 Mtumwa akachukua ngamia kumi wa bwana wake na akaondoka. Akachukua pia aina zote za zawadi kutoka kwa bwana wake. Akaondoka na kwenda katika mkoa wa Aramu Naharaimu, mji wa Nahori.
Saa tog Svenden ti Kameler af sin Herres Kameler og for bort og havde alle Haande af sin Herres Gods med sig og gjorde sig rede og drog til Aram Naharaim, til Nakors Stad.
11 Akawapigisha magoti ngamia nje ya mji karibu na kisima cha maji. Ilikuwa jioni wakati ambao wanawake huenda kuchota maji.
Der lod han Kamelerne lægge sig uden for Staden ved en Vandbrønd mod Aftens Tid, mod den Tid da Kvinderne gaa ud at drage Vand.
12 Kisha akasema, “Yahwe, Mungu wa bwana wangu Abraham, anijalie kufanikiwa leo na aoneshe agano la uaminifu kwa bwana wangu Abraham.
Og han sagde: Herre, min Herre Abrahams Gud! Kære, lad det møde mig i Dag, og gør Miskundhed mod min Herre Abraham.
13 Tazama, nimesimama hapa karibu na chemchemi ya maji na binti za watu wa mji wanakuja kuteka maji.
Se, jeg staar ved denne Vandbrønd, og Byens Folks Døtre komme ud at drage Vand.
14 Na itokee hivi kwamba. Nikimwambia msichana, tafadhari tua mtungi wako ili niweze kunywa maji,' na akiniambia, 'Kunywa, na kwamba nitawanywesha ngamia wako pia,' huyo ndiye awe ambaye umemchagulia mtumwa wako Isaka. Kwa njia hii nitajua kuwa umeonesha agano la uaminifu kwa bwana wangu.”
Og naar det sker, at der kommer en Pige, til hvem jeg siger: Bøj nu din Krukke ned og lad mig drikke, og hun siger: Drik, og jeg vil ogsaa give dine Kameler at drikke, lad hende da være den, som du har udset til din Tjener Isak, saa jeg derpaa kan kende, at du har gjort Miskundhed mod min Herre.
15 Ikawa kwamba hata kabla hajamaliza kuzungumza, tazama, Rebeka akaja akiwa na mtungi wake wa maji begani mwake. Rebeka alizaliwa na Bethueli mwana wa Milka, mke wa Nahori, ndugu yake na Abraham.
Og det skete, før han havde endt at tale, se, da kom Rebekka ud, som var en Datter af Bethuel, som var en Søn af Milka, Nakors, Abrahams Broders, Hustru, og hendes Krukke var paa hendes Skulder.
16 Msichana huyu alikuwa mzuri na alikuwa bikira. Hapana mwanaume aliye kuwa amekwisha lala naye. Akashuka kisimani na kuujaza mtungi wake, na kupanda juu.
Og Pigen var meget smuk af Anseelse, en Jomfru, og ingen Mand havde kendt hende, og hun gik ned til Brønden og fyldte sin Krukke og gik op.
17 Kisha mtumwa yule akakimbia kumlaki yule msichana, na kusema, “Tafadhari nipatie maji kidogo ya kunywa kutoka katika mtungi wako.”
Da løb Svenden imod hende og sagde: Kære, lad mig drikke lidt Vand af din Krukke.
18 Akasema, “kunywa tafadhari bwana wangu,” na kwa haraka akatua mtungi wake juu ya mkono wake, na akampatia maji ya kunywa.
Og hun sagde: Drik, min Herre! og hun skyndte sig og tog sin Krukke ned i sin Haand og gav ham at drikke.
19 Alipokuwa amemaliza kumpatia maji, akasema, “Nitachota maji kwa ajili ya ngamia wako pia, mpaka watakapomaliza kunywa.”
Der hun havde givet ham at drikke, da sagde hun: Jeg vil og drage Vand til dine Kameler, til de have afdrukket.
20 Hivyo akaharakisha akamwaga maji yaliyokuwa mtungini kwenye chombo cha kunywshea mifugo, kisha akakimbia tena kisimani kuchota maji, na kuwanywesha ngamia wake wote.
Og hun skyndte sig og tømte sin Krukke i Truget og løb fremdeles til Brønden at øse, og hun drog til alle hans Kameler.
21 Yule mtu akamtazama msichana akiwa kimya kuona kama Yahwe amefanikisha njia yake au la.
Og Manden undrede sig over hende, tav dog stille for at faa at vide, om Herren havde ladet hans Rejse lykkes eller ej.
22 Ngamia walipomaliza kunywa maji, yule mtu akaleta pete ya pua ya dhahabu yenye uzito wa nusu shekeli, na bangili mbili za dhahabu kwa ajili ya mikono yake zenye uzito wa shekeli kumi,
Og det skete, der Kamelerne havde afdrukket, gav Manden hende en Guldring, som vejede en halv Sekel, og satte to Armbaand paa hendes Hænder, de vejede ti Guldsekler.
23 akamuuliza, “wewe ni binti wa nani? Niambie tafadhali, Je kuna nafasi nyumbani mwa baba yako kwa ajili yetu kupumzika usiku?”
Og han sagde: Hvis Datter er du? Kære, sig mig, monne der være Rum i din Faders Hus at give os Nattely?
24 Akamwambia, “Mimi ni binti wa Bethueli mwana wa Milka, ambaye alimzaa kwa Nahori.”
Og hun sagde til ham: Jeg er en Datter af Bethuel, som er en Søn af Milka, der fødte ham for Nakor.
25 Akasema pia, “Tunayo malisho tele na chakula, na iko nafasi kwa ajili yako kulala usiku.”
Og hun sagde til ham: Der er baade Straa og meget Foder hos os, ogsaa er der Rum til Herberge i Nat.
26 Kisha yume mtu akainama chini na kumwabudu Yahwe.
Og Manden bøjede sig og tilbad Herren.
27 Akasema, “Abarikiwe Yahwe, Mungu wa bwana wangu Abraham, ambaye hakuacha agano lake la uaminifu na kweli yake mbele ya bwana wangu. Kwa vile Yahwe ameniongoza moja kwa moja kwenye nyumba ya ndugu zake bwana wangu.”
Og han sagde: Lovet være Herren, min Herre Abrahams Gud, som ikke har afladt med sin Miskundhed og sin Trofasthed mod min Herre! mig, ja, mig har Herren ført paa Vejen til min Herres Broders Hus.
28 Kisha yule msichana akakimbia na kwenda kuwaeleza watu wa nyumba ya mama yake juu ya mambo yote haya.
Og Pigen løb og kundgjorde i sin Moders Hus disse Ting.
29 Na sasa Rebeka alikuwa na kaka yake, jina lake aliitwa Labani. Labani akakimbia kwa yule mtu aliye kuwa nje barabarani karibu na kisima.
Og Rebekka havde en Broder, og hans Navn var Laban, og Laban løb ud til Manden, til Brønden.
30 Akisha kuona hereni ya puani pamoja na zile bangili kwenye mikono ya dada yake, na kusikia maneno ya Rebeka dada yake, “Hivi ndivyo yule mtu alicho niambia,” alikwenda kwa yule mtu, na, Tazama, alikuwa amesimama karibu na ngamia pale kisimani.
Og det skete, der han saa Ringen og Armbaandene paa sin Søsters Hænder, og der han hørte Rebekkas, sin Søsters, Ord, at hun sagde: Saaledes har Manden sagt til mig, da kom han til Manden, og se, han stod hos Kamelerne ved Brønden.
31 Labani akasema, “Njoo, wewe uliye barikiwa na Yahwe. Kwa nini umesimama nje? nimekwisha andaa nyumba, pamoja na mahali kwa ajili ya ngamia.”
Og han sagde: Kom ind, du Herrens Velsignede, hvi staar du herude? thi jeg har beredt Huset, og der er Rum for Kamelerne.
32 Kwa hiyo yule mtu akaingia ndani ya nyumba na akashusha mizigo kutoka kwa wale ngamia. Ngamia wakapatiwa malisho na chakula, na maji yakatolewa kuosha miguu yake pamoja na miguu ya wale watu aliokuwa pamoja nao.
Saa kom Manden i Huset og løste Kamelerne, og han gav Straa og Foder til Kamelerne, og Vand til at to hans Fødder og de Mænds Fødder, som vare med ham.
33 Wakaandaa chakula mbele yake ale, lakini akasema, “Sitakula mpaka niseme kile ninacho paswa kusema.” Kwa hiyo Labani akmwambia, “Sema.”
Og der blev sat Mad for ham; men han sagde: Jeg vil ikke æde, før jeg har udsagt mit Ærinde; og han sagde: Tal!
34 Akasema, “Mimi ni mtumwa wa Abraham.
Og han sagde: Jeg er Abrahams Svend.
35 Yahwe amembariki sana bwana wangu na amekuwa mtu mkuu. Amempatia mifugo na makundi ya wanyama, fedha, dhahabu, watumwa wa kiume na watumwa wa kike, pamoja na ngamia na punda.
Og Herren har velsignet min Herre meget, at han er bleven mægtig; og han har givet ham Faar og Kvæg og Sølv og Guld og Svende og Tjenestepiger og Kameler og Asener.
36 Sara, mke wa bwana wangu, alimzalia mwana bwana wangu alipokuwa mzee, na amempatia mwanawe kila kitu anachomiliki.
Og Sara, min Herres Hustru, har født min Herre en Søn, efter at hun var gammel, og denne har han givet alt det, han ejer.
37 Bwana wangu aliniapisha, akisema, “Usije ukampatia mwanangu mke kutoka kwa mabinti wa Wakanaani, ambao kwao nimefanya makazi.
Og min Herre har taget en Ed af mig og sagt: Du skal ikke tage min Søn en Hustru af Kananiternes Døtre, i hvis Land jeg bor.
38 Badala yake, lazima uende kwa familia ya baba yangu, na kwa ndugu zangu, na kupata mke kwa ajili ya mwanangu.'
Men du skal fare hen til min Faders Hus og til min Slægt og tage min Søn en Hustru.
39 Nikamwambia bwana wangu, pengine mwanamke huyo asikubali kufuatana nami.'
Og jeg sagde til min Herre: Maaske Kvinden ikke vil drage med mig.
40 Lakini akaniambia, Yahwe, ambaye ninakwenda mbele yake, atatuma malaika wake pamoja nawe na atakufanikisha njia yako, kwamba utapata mke kwa ajili ya mwangu kutoka miongoni mwa ndugu zangu na kutoka katika ukoo wa baba yangu.
Og han sagde til mig: Herren, for hvis Ansigt jeg har vandret, skal sende sin Engel med dig og give dig en lyksalig Rejse, og du skal tage min Søn en Hustru af min Slægt og af min Faders Hus.
41 Lakini utakuwa huru katika kiapo changu ikiwa utafika kwa ndugu zangu na wasikuruhusu kuja naye. Ndipo utakuwa huru katika kiapo changu.
Da skal du være fri for min Ed, naar du kommer til min Slægt; og om de ikke ville give dig hende, saa er du fri for min Ed.
42 Hivyo nimefika leo kisimani, na nikasema, 'O Yahwe, Mungu wa bwana wangu Abraham, tafadhari, ikiwa kweli umekusudia kuifanya safari yangu kuwa yenye kufanikiwa -
Saa kom jeg i Dag til Brønden og sagde: Herre, min Herre Abrahams Gud! Kære, dersom du har givet Lykke paa min Rejse, paa hvilken jeg har vandret,
43 tazama niko hapa nimesimama karibu na kisima cha maji - na iwe kwamba binti ajaye kuchota maji, nitakaye mwambia, “Tafadhari unipatie maji kidoka kutoka kwenye mtungi wako ninywe,” mwanamke atakaye niabia,
se, jeg staar ved denne Vandbrønd, og naar det sker, der kommer en Jomfru ud at drage Vand, og jeg siger til hende: Giv mig nu lidet Vand at drikke af din Krukke;
44 “Kunywa, na nitakuchotea pia maji kwa ajili ya ngamia wako” - na awe ndiye ambaye wewe Yahwe, umemchagulia mtoto wa bwana wangu.”
og hun siger mig: Baade maa du drikke, og jeg vil ogsaa øse til dine Kameler, lad hende være den Kvinde, som Herren har udset til min Herres Søn.
45 Ikawa hata kabla sijamaliza kuzungumza moyoni mwangu, Tazama, Rebeka akaja na mtungi wake juu ya bega lake akashuka chini kisimani akachota maji. Hivyo nikamwambia, 'Tafadhari nipatie maji ninywe.'
Førend jeg havde udtalet i mit Hjerte, se, da kom Rebekka ud, og hendes Krukke var paa hendes Skulder, og hun gik ned til Brønden og drog Vand! da sagde jeg til hende: Kære, giv mig at drikke.
46 Ndipo kwa haraka alipoushusha mtungi wake begani mwake na akasema, 'Kunywa, na pia nitawapatia maji ngamia wak.' Kwa hiyo nikanywa, na akawanywesha ngamia pia.
Saa skyndte hun sig og tog sin Krukke ned ad sig og sagde: Drik, og jeg vil ogsaa give dine Kameler at drikke; og jeg drak, og hun gav ogsaa Kamelerne at drikke.
47 Nikamuuliza na kusema, 'Wewe ni binti wa nani?' Akasema, 'Binti wa Bethueli, Mwana wa Nahori, ambaye Milka alizaa kwake.' Kisha nikamwekea pete puani mwake pamoja na bangili mikononi mwake.
Og jeg spurgte hende og sagde: Hvis Datter er du? og hun sagde: Jeg er en Datter af Bethuel, Nakors Søn, som Milka fødte ham. Saa hængte jeg en Ring i hendes Næse og Armbaand paa hendes Hænder.
48 Kisha nikainama chini nikamwabudu Yahwe, na kumbariki Yahwe, Mungu wa bwana wangu Abraham, ambaye ameniongoza katika njia sahihi kumpata binti wa ndugu za bwana wangu kwa ajili ya mwanawe.
Og jeg bøjede mig og tilbad Herren og lovede Herren, min Herre Abrahams Gud, som havde ledet mig paa den rette Vej at tage min Herres Broders Datter til hans Søn.
49 Kwa hiyo, ikiwa mko tayari kumfanyia rehema na kweli, niambieni. Lakini kama sivyo, niambieni, ili kwamba niweze kwenda upande wa kulia, au kushoto.”
Og nu, dersom I ville vise Miskundhed og Trofasthed mod min Herre, siger mig det; men dersom I ikke ville det, da siger mig det, at jeg kan vende mig til den højre eller til den venstre Side.
50 Ndipo Labani na Bethueli wakajibu na kusema, “Jambo hili limetoka kwa Yahwe; hatuwezi kusema kwako aidha neno baya au zuri.
Da svarede Laban og Bethuel og sagde: Denne Sag er kommen fra Herren, vi kunne hverken tale til dig ondt eller godt.
51 Tazama, Rebeka yu mbele yako. Mchukue na uende, ili awe mke wa mtoto wa bwana wako, kama Yahwe alivyosema.”
Se, der er Rebekka for dig, tag hende og gak, at hmi bliver din Herres Søns Hustru, som Herren har sagt.
52 Mtumwa wa Abraham aliposikia maneno yao, akainama mwenyewe chini ardhini kwa Yahwe.
Og det skete, der Abrahams Svend hørte deres Ord, da bøjede han sig til Jorden for Herren.
53 Mtumwa akaleta vipande vya fedha na vipande vya dhahabu, na nguo, akampatia Rebeka. Akampatia pia kaka yake na mama yake zawadi zenye thamani.
Og Svenden udtog Sølvtøj og Guldtøj og Klæder og gav Rebekka; men hendes Broder og hendes Moder gav han dyrebar Skænk.
54 Kisha yeye na watu aliokuwa nao wakala na kunywa. wakakaa pale mpaka usiku, na walipoamka asubuhi, akasema, Niruhusuni niende kwa bwana wangu.”
Saa aade de og drak, han og de Mænd, som vare med ham, og bleve der om Natten, og de stode op om Morgenen, og han sagde: Lader mig fare til min Herre!
55 Kaka yake na mama yake wakasema, mwache binti abaki nasi kwa siku chache zingine, angalau siku kumi. baada ya hapo anaweza kwenda.”
Da sagde hendes Broder og hendes Moder: Lad Pigen blive hos os nogle Dage eller ti, siden maa du fare.
56 Lakini akawambia, msinizuie, kwa kuwa Yahwe amefanikisha njia yangu. Niruhusuni niende kwa bwana wangu.”
Og han sagde til dem: Holder mig ikke op, thi Herren har givet Lykke paa min Rejse; lader mig fare, og jeg vil vandre til min Herre.
57 Wakasema, “Tutamwita binti na kumuuliza.”
Og de sagde: Lader os kalde Pigen og spørge, hvad hun siger.
58 Kwa hiyo wakamwita Rebeka na kumuuliza, “Je utakwenda na mtu huyu?” Akajibu, “Nitakwenda.”
Saa kaldte de ad Rebekka og sagde til hende: Vil du fare med denne Mand? og hun sagde: Jeg vil fare.
59 Kwa hiyo wakampeleka dada yao Rebeka, pamoja na watumishi wake wa kike, kwenda njiani pamoja na mtumishi wa Abraham na watu wake.
Saa lode de deres Søster Rebekka og hendes Amme og Abrahams Svend og hans Mænd fare.
60 Wakambarikia Rebeka, na wakamwambia, “Ndugu yetu, na uwe mama wa maelfu na wa makumi elfu, uzao wako upate kumiliki lango la wale wanao wachukia.”
Og de velsignede Rebekka og sagde til hende: Vor Søster! bliv du til tusinde Gange Titusinde, og din Sæd skal eje sine Fjenders Port.
61 Kisha Rebeka akasimama, yeye na watumishi wake kwa hesabu ya ngamia, na wakamfuata yule mtu. Hivyo watumishi wakamchukua Rebeka, na wakaenda zao.
Saa stod Rebekka op og hendes Piger, og de satte sig paa Kameler og fore med Manden, og Svenden annammede Rebekka og for bort.
62 Nyakati hizo Isaka alikuwa anakaa katika Negebu, na alikuwa tu amerejea kutoka Beerlahairoi.
Og Isak kom gaaende fra den Brønd, som kaldes Beer Lakai Roi; thi han boede i Landet imod Sønden.
63 Isaka akaenda kutafakari shambani jioni. Alipotazama akaona, natazama, kulikuwa na ngamia wakija!
Og Isak var udgangen til at gøre Bøn paa Marken mod Aften, og han opløftede sine Øjne og saa, og se, Kamelerne kom.
64 Rebeka akatazama na alipomwona Isaka, akaruka kutoka kwenye ngamia.
Og Rebekka opløftede sine Øjne og saa Isak og steg hastig ned ad Kamelen.
65 Akamwambia mtumwa, “mtu huyo ni nani anaye tembea shambani akija kutupokea?” Mtumwa akasema, “Ni bwana wangu.” Hivyo Rebeka akachukua shela yake akajifunika.
Og hun sagde til Svenden: Hvo er den Mand, som gaar paa Marken imod os? og Svenden sagde: Det er min Herre; saa tog hun et Slør og skjulte sig.
66 Mtumwa akamwambia Isaka mambo yote ambayo amefanya.
Og Svenden fortalte Isak hele Sagen, som han havde udrettet.
67 Kisha Isaka akamleta katika hema ya Sara mama yake na akamchukua Rebeka, na akawa mke wake, na akampenda. Kwa hiyo Isaka akafarijika baada ya kifo cha mama yake.
Saa ledte Isak hende til sin Moder Saras Telt, og han tog Rebekka, og hun blev hans Hustru, og han elskede hende; og Isak blev trøstet efter sin Moder.

< Mwanzo 24 >