< Mwanzo 23 >
1 Sara akaishi mika mia moja na ishirini na saba. Hii ndiyo ilikuwa ni miaka ya maisha ya Sara.
Sara lefde i hundrade sju och tjugu år:
2 Sara akafa katika Kiriathi Arba, ambayo ni Hebroni, katika nchi ya Kanaani. Abraham akaomboleza na kumlilia Sara.
Och blef död i den hufvudstaden, som kallas Hebron i Canaans lande. Då kom Abraham till att sörja och begråta henne.
3 Kisha Abraham akainuka na kutoka kwa mkewe aliye kufa, akanena na watoto wa kiume wa Hethi, akisema,
Sedan stod han upp ifrå hennes lik, och talade till Hets barn, och sade:
4 “Mimi ni mgeni kati yenu. Tafadhari nipatieni mahali pa kuzikia miongoni mwenu, ili kwamba niweze kuzika wafu wangu.”
Jag är en främling och en gäst när eder, gifver mig en arfrätt till begrafning när eder, att jag må begrafva min döda, som för mig ligger.
5 Wana wa Hethi wakamjibu Abraham, wakasema,
Då svarade Hets barn Abraham, och sade till honom:
6 “Tusikilize, bwana wangu. Wewe ni mwana wa Mungu miongoni mwetu. Zika wafu wako katika makaburi yetu utakayochagua. Hakuna miongoni mwetu atakaye kuzuilia kaburi lake, kwa ajili ya kuzikia wafu wako.”
Hör oss, käre herre, du äst en Guds förste när oss; begraf din döda uti våra bästa grifter; ingen menniska af oss skall förvägra dig, att du begrafver din döda i hans graf.
7 Abraham akainuka na kusujudu chini kwa watu wa nchi ile, kwa wana wa Hethi.
Då stod Abraham upp, och bugade sig för landsens folke, nemliga för Hets barnom.
8 Akawaambia, akisema, “ikiwa mmekubali mimi kuzika wafu wangu, ndipo nisikilizeni, msihini Efroni mwana wa Sohari kwa ajili yangu.
Och han talade med dem, och sade: Är det eder i sinnet, att jag begrafver min döda, som för mig ligger, så hörer mig, och beder för mig inför Ephron Zoars son,
9 Mwambieni aniuzie pango la Makpela, ambalo analimiliki, ambalo liko mwishoni mwa shamba lake. Kwa bei kamili aniuzie waziwazi mbele ya watu kama miliki ya kuzikia.”
Att han gifver mig sina dubbelkulo, den han hafver i andanom på sinom åker, för reda penningar; låter mig henne få när eder till en arfgrift.
10 Efroni alikuwa ameketi miongoni mwa wana wa Hethi, hivyo Efroni Mhiti akamjibu Abraham alipowasikia wana wa Hethi, wote ambao walikuwa wamekuja langoni mwa mji wake, akasema,
Ty Ephron bodde ibland Hets barn. Då svarade Ephron, den Hetheen, Abraham i Hets barns åhöro, för allom dem, som ut och in gingo genom hans stadsport, och sade:
11 “Hapana, bwana wangu, nisikilize. Ninakupatia shamba na pango ambalo limo ndani yake. Ninakupatia mbele ya wana wa watu wangu. Ninakupatia uzike wafu wako.”
Nej, min herre, utan hör till hvad jag säga vill: Jag gifver dig åkren, och den kulon med, som der inne är, och gifver dig honom för mitt folks barns åsyn, till att begrafva din döda.
12 Kisha Abraham akasujudu chini mbele ya watu wa nchi ile.
Då bugade sig Abraham för landsens folke,
13 Akamwambia Efroni watu wa nchi ile wakisikiliza, akasema, ikiwa uko radhi, tafadhari nisikilize. Nitalipia shamba. Chukua fedha kwangu, na nitazika wafu wangu pale.”
Och talade till Ephron i landsens folks åhöro, och sade: Vill du höra mig, så tag penningar af mig för åkren, de jag dig gifva vill; och så vill jag der begrafva min döda.
14 Efroni akamjibu Abraham, akisema,
Ephron svarade Abraham, och talade till honom:
15 “Tafadhari bwana wangu, nisikilize. Kipande cha ardhi kinathamani ya shekeli mia nne za fedha, na hiyo ni kitu gani kati yangu mimi na wewe? wazike wafu wako.”
Min herre, hör dock mig: Marken är värd fyrahundrade siklar silfver; men hvad kan det draga emellan mig och dig? Begraf man din döda.
16 Abraham akamsikiliza Efroni na akampimia Efroni kiwango cha fedha alizosema mbele ya wana wa Helthi wakisikiliza, shekeli mia nne za fedha, kwa mujibu wa viwango vya vipimo vya kibiashara.
Abraham hörde Ephron, och vog honom penningarna till, som han nämnt hade, hvilket Hets barn åhörde, nemliga fyrahundrade siklar silfver, som då gåfve och gängse voro.
17 Kwa hiyo shamba la Efroni, lililokuwa katika Makpela, mbele ya Mamre, shamba pamoja na pango lililokuwamo ndani yake na miti yote iliyokuwamo ndani ya shamba na iliyokuwa mpakani ikatolewa
Och så vardt Ephrons åker, der den dubbelkulan inne var, tvärs öfver Mamre, tillegnad Abraham till evärdeliga ägo, med kulone derinne, och med all trä omkring åkren,
18 kwa Abraham kwa njia ya manunuzi mbele ya wana wa Hethi, na mbele ya wote waliokuja malangoni pa mji wake.
I Hets barns och allas deras åsyn, som genom hans stadsport ut och in gingo.
19 Baada ya haya, Abraham akamzika Sara mkewe katika pango la shamba la Makpela, lililo mbele ya Mamre, ambayo ni Hebroni, katika nchi ya Kanaani.
Sedan begrof då Abraham Sara sina hustru uti kulone i åkrenom, den dubbel var, tvärs öfver ifrå Mamre, det är Hebron i Canaans lande.
20 Kwa hiyo shamba pamoja na pango likatolewa na wana wa Hethi kwa Abraham kama milki na eneo la kuzikia.
Och alltså vardt Abraham stadfäst den åkren, och kulan, till begrafnings egendom af Hets barnom.