< Mwanzo 23 >

1 Sara akaishi mika mia moja na ishirini na saba. Hii ndiyo ilikuwa ni miaka ya maisha ya Sara.
Sara was an hundred and. xxvij. yere olde (for so longe lyued she)
2 Sara akafa katika Kiriathi Arba, ambayo ni Hebroni, katika nchi ya Kanaani. Abraham akaomboleza na kumlilia Sara.
and than dyed in a heade cyte called Hebron in the londe of Canaan. Than Abraham came to morne Sara and to wepe for her.
3 Kisha Abraham akainuka na kutoka kwa mkewe aliye kufa, akanena na watoto wa kiume wa Hethi, akisema,
And Abraham stode vp from the coorse and talked with the sonnes of heth saynge:
4 “Mimi ni mgeni kati yenu. Tafadhari nipatieni mahali pa kuzikia miongoni mwenu, ili kwamba niweze kuzika wafu wangu.”
I am a straunger ad a foryner amonge yow geue me a possession to bury in with you that I may bury my dead oute of my sighte.
5 Wana wa Hethi wakamjibu Abraham, wakasema,
And the children of heth answered Abraham saynge vnto him:
6 “Tusikilize, bwana wangu. Wewe ni mwana wa Mungu miongoni mwetu. Zika wafu wako katika makaburi yetu utakayochagua. Hakuna miongoni mwetu atakaye kuzuilia kaburi lake, kwa ajili ya kuzikia wafu wako.”
heare vs lorde thou art a prynce of God amonge vs. In the chefest of oure sepulchres bury thy dead: None of vs shall forbydd ye his sepulchre yt thou shuldest not bury thy deade therein.
7 Abraham akainuka na kusujudu chini kwa watu wa nchi ile, kwa wana wa Hethi.
Abraha stode vp and bowed hi selfe before ye people of ye lade ye childre of heth.
8 Akawaambia, akisema, “ikiwa mmekubali mimi kuzika wafu wangu, ndipo nisikilizeni, msihini Efroni mwana wa Sohari kwa ajili yangu.
And he comoned with them saynge: Yf it be youre myndes yt I shall bury my deade oute of my sighte heare me ad speke for me to Ephron the sonne of Zoar:
9 Mwambieni aniuzie pango la Makpela, ambalo analimiliki, ambalo liko mwishoni mwa shamba lake. Kwa bei kamili aniuzie waziwazi mbele ya watu kama miliki ya kuzikia.”
and let him geue me the dubill caue which he hath in the end of his felde for as moch money as it is worth let him geue it me in the presence of you for a possession to bury in.
10 Efroni alikuwa ameketi miongoni mwa wana wa Hethi, hivyo Efroni Mhiti akamjibu Abraham alipowasikia wana wa Hethi, wote ambao walikuwa wamekuja langoni mwa mji wake, akasema,
For Hephron dwelled amoge ye childern of heth. Than Ephron the Hethite answered Abraham in the audyece of the childern of Heth and of all that went in at the gates of his cyte saynge:
11 “Hapana, bwana wangu, nisikilize. Ninakupatia shamba na pango ambalo limo ndani yake. Ninakupatia mbele ya wana wa watu wangu. Ninakupatia uzike wafu wako.”
Not so my lorde but heare me: The felde geue I the and the caue that therein is geue I the also And even in the presence of the sonnes of my people geve I it the to bury thy deede in.
12 Kisha Abraham akasujudu chini mbele ya watu wa nchi ile.
Than Abraham bowed himselfe before the people of the lade
13 Akamwambia Efroni watu wa nchi ile wakisikiliza, akasema, ikiwa uko radhi, tafadhari nisikilize. Nitalipia shamba. Chukua fedha kwangu, na nitazika wafu wangu pale.”
and spake vnto Ephro in the audyence of the people of the contre saynge: I praye the heare me I will geue sylver for the felde take it of me ad so will I bury my deed there.
14 Efroni akamjibu Abraham, akisema,
Ephron answered Abraha saynge vnto him
15 “Tafadhari bwana wangu, nisikilize. Kipande cha ardhi kinathamani ya shekeli mia nne za fedha, na hiyo ni kitu gani kati yangu mimi na wewe? wazike wafu wako.”
My lorde harken vnto me. The lande is worth iiij. hundreth sycles of syluer: But what is that betwixte the and me? bury thy deede.
16 Abraham akamsikiliza Efroni na akampimia Efroni kiwango cha fedha alizosema mbele ya wana wa Helthi wakisikiliza, shekeli mia nne za fedha, kwa mujibu wa viwango vya vipimo vya kibiashara.
And Abraham harkened vnto Ephron and weyde him the sylver which he had sayde in the audyence of the sonnes of Heth. Euen. iiij. hudred syluer sycles of currant money amonge marchauntes
17 Kwa hiyo shamba la Efroni, lililokuwa katika Makpela, mbele ya Mamre, shamba pamoja na pango lililokuwamo ndani yake na miti yote iliyokuwamo ndani ya shamba na iliyokuwa mpakani ikatolewa
Thus was the felde of Ephron where in the dubbill caue is before Mamre: euen the felde and the caue that is therein and all the trees of the felde which growe in all the borders rounde aboute made sure
18 kwa Abraham kwa njia ya manunuzi mbele ya wana wa Hethi, na mbele ya wote waliokuja malangoni pa mji wake.
vnto Abraham for a possession in the syghte of the childern of Heth and of all that went in at the gates of the cyte.
19 Baada ya haya, Abraham akamzika Sara mkewe katika pango la shamba la Makpela, lililo mbele ya Mamre, ambayo ni Hebroni, katika nchi ya Kanaani.
And then Abraham buried Sara his wyfe in the double caue of the felde that lyeth before Mare otherwise called Ebron in the lande of Canaan.
20 Kwa hiyo shamba pamoja na pango likatolewa na wana wa Hethi kwa Abraham kama milki na eneo la kuzikia.
And so both the felde ad the caue that is therein was made vnto Abraham a sure possession to bury in of the sonnes of Heth.

< Mwanzo 23 >