< Mwanzo 23 >
1 Sara akaishi mika mia moja na ishirini na saba. Hii ndiyo ilikuwa ni miaka ya maisha ya Sara.
Sara levede 127 Aar, saa mange var Saras Leveaar.
2 Sara akafa katika Kiriathi Arba, ambayo ni Hebroni, katika nchi ya Kanaani. Abraham akaomboleza na kumlilia Sara.
Sara døde i Kirjat-Arba, det er Hebron, i Kana'ans Land. Saa gik Abraham hen og holdt Klage over Sara og begræd hende.
3 Kisha Abraham akainuka na kutoka kwa mkewe aliye kufa, akanena na watoto wa kiume wa Hethi, akisema,
Og da han havde rejst sig fra sin døde, talte han saaledes til Hetiterne:
4 “Mimi ni mgeni kati yenu. Tafadhari nipatieni mahali pa kuzikia miongoni mwenu, ili kwamba niweze kuzika wafu wangu.”
»Jeg er Gæst og fremmed hos eder; men giv mig et Gravsted hos eder, saa jeg kan jorde min døde og bringe hende bort fra mit Ansigt!«
5 Wana wa Hethi wakamjibu Abraham, wakasema,
Da svarede Hetiterne Abraham:
6 “Tusikilize, bwana wangu. Wewe ni mwana wa Mungu miongoni mwetu. Zika wafu wako katika makaburi yetu utakayochagua. Hakuna miongoni mwetu atakaye kuzuilia kaburi lake, kwa ajili ya kuzikia wafu wako.”
»Hør os, Herre! En Guds Fyrste er du jo iblandt os; jord du din døde i en af vore bedste Grave! Ikke en af os vil nægte dig sin Grav og hindre dig i at jorde din døde.«
7 Abraham akainuka na kusujudu chini kwa watu wa nchi ile, kwa wana wa Hethi.
Men Abraham stod op og bøjede sig for Hetiterne, Folkene der paa Stedet,
8 Akawaambia, akisema, “ikiwa mmekubali mimi kuzika wafu wangu, ndipo nisikilizeni, msihini Efroni mwana wa Sohari kwa ajili yangu.
og sagde til dem: »Hvis I samtykker i, at jeg jorder min døde og bringer hende bort fra mit Ansigt, saa føj mig i at lægge et godt Ord ind for mig hos Efron, Zohars Søn,
9 Mwambieni aniuzie pango la Makpela, ambalo analimiliki, ambalo liko mwishoni mwa shamba lake. Kwa bei kamili aniuzie waziwazi mbele ya watu kama miliki ya kuzikia.”
saa han giver mig sin Klippehule i Makpela ved Udkanten af sin Mark; for fuld Betaling skal han i eders Nærværelse give mig den til Gravsted!«
10 Efroni alikuwa ameketi miongoni mwa wana wa Hethi, hivyo Efroni Mhiti akamjibu Abraham alipowasikia wana wa Hethi, wote ambao walikuwa wamekuja langoni mwa mji wake, akasema,
Men Efron sad blandt Hetiterne; og Hetiten Efron svarede Abraham i Hetiternes Paahør, saa mange som gik ind gennem hans Bys Port:
11 “Hapana, bwana wangu, nisikilize. Ninakupatia shamba na pango ambalo limo ndani yake. Ninakupatia mbele ya wana wa watu wangu. Ninakupatia uzike wafu wako.”
»Gid min Herre vilde høre mig! Marken giver jeg dig, og Hulen derpaa giver jeg dig; i mit Folks Nærværelse giver jeg dig den; jord du kun din døde!«
12 Kisha Abraham akasujudu chini mbele ya watu wa nchi ile.
Da bøjede Abraham sig for Folkene der paa Stedet
13 Akamwambia Efroni watu wa nchi ile wakisikiliza, akasema, ikiwa uko radhi, tafadhari nisikilize. Nitalipia shamba. Chukua fedha kwangu, na nitazika wafu wangu pale.”
og sagde til Efron i deres Paahør: »Om du blot — gid du dog vilde høre mig! Jeg giver dig, hvad Marken er værd; modtag det dog af mig, saa jeg kan jorde min døde der.«
14 Efroni akamjibu Abraham, akisema,
Da sagde Efron til Abraham:
15 “Tafadhari bwana wangu, nisikilize. Kipande cha ardhi kinathamani ya shekeli mia nne za fedha, na hiyo ni kitu gani kati yangu mimi na wewe? wazike wafu wako.”
»Gid min Herre vilde høre mig! Et Stykke Land til 400 Sekel Sølv, hvad har det at sige mellem mig og dig? Jord du kun din døde!«
16 Abraham akamsikiliza Efroni na akampimia Efroni kiwango cha fedha alizosema mbele ya wana wa Helthi wakisikiliza, shekeli mia nne za fedha, kwa mujibu wa viwango vya vipimo vya kibiashara.
Og Abraham forstod Efron og tilvejede ham den Sum, han havde nævnet i Hetiternes Paahør, 400 Sekel Sølv i gangbar Mønt.
17 Kwa hiyo shamba la Efroni, lililokuwa katika Makpela, mbele ya Mamre, shamba pamoja na pango lililokuwamo ndani yake na miti yote iliyokuwamo ndani ya shamba na iliyokuwa mpakani ikatolewa
Saaledes gik Efrons Mark i Makpela over for Mamre i hele sin Udstrækning tillige med Klippehulen og alle Træerne paa Marken
18 kwa Abraham kwa njia ya manunuzi mbele ya wana wa Hethi, na mbele ya wote waliokuja malangoni pa mji wake.
over i Abrahams Eje i Hetiternes Nærværelse, saa mange som gik ind gennem hans Bys Port.
19 Baada ya haya, Abraham akamzika Sara mkewe katika pango la shamba la Makpela, lililo mbele ya Mamre, ambayo ni Hebroni, katika nchi ya Kanaani.
Derefter jordede Abraham sin Hustru Sara i Klippehulen paa Makpelas Mark over for Mamre, det er Hebron, i Kana'ans Land.
20 Kwa hiyo shamba pamoja na pango likatolewa na wana wa Hethi kwa Abraham kama milki na eneo la kuzikia.
Og Marken med Klippehulen derpaa gik fra Hetiterne over til Abraham som Gravsted.